Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Februari 10, 2012

AMRI YA JUMAPILI KWA TAIFA ZIMA

1.     Biblia yasemaje juu ya Amerika ya Kiprotestanti itakavyoisujudu Mamlaka ile ya Kikatoliki ya Roma? Ufu.13:11-17.

Photo Credit By: temcat.com

2. Je, unabii huo utatimizwa lini?

a. "Unabii wa Ufunuo 13 unatangaza kwamba mamlaka ile iliyowakilishwa na mnyama aliye na pembe kama za mwana-kondoo ita"ifanya dunia na wote wakaao ndani yake wausujudu upapa -----ulioonyeshwa hapo kama mnyama "mfano wa chui."... Unabii huo utatimizwa wakati ule Marekani itakapotunga amri ya kuitunza Jumapili, tendo ambalo Roma inadai kuwa ni kuutambua ukuu wake kwa namna ya pekee." GC 578,579.

b. "Kulazimisha utunzaji wa Jumapili kwa upande wa Uprotestanti ni sawa na kulazimisha ibada ya upapa." GC 448.

3. Shinikizo la kuitungia amri [sheria] Jumapili litatoka wapi?

a. "Viongozi wakuu wa kanisa na serikali wataungana ili kuwahonga, kuwashawishi, au kuwalazimisha watu wa tabaka zote wapate kuiheshimu Jumapili. Kule kukosekana kwa mamlaka ya Mungu [katika Biblia] kutafanya zipate kutungwa amri kali za ukandamizaji. Rushwa katika ngazi za kisiasa inaharibu moyo ule wa kupenda haki na kuijali kweli; hata katika Amerika iliyo huru, watawala na watunga sheria, ili kupata upendeleo wa umma, watakubali madai ya wengi wanaopendelea iwepo amri [sheria] ya kulazimisha utunzaji wa Jumapili." GC 592 (Angalia pia 4SP 410).

b. "Ili kujipatia hali ile ya kupendwa na watu wengi na haki ya kuweza kuteuliwa, watunga sheria watakubaliana na madai ya kuwapo kwa amri ya Jumapili." 5T 451.

c. "Watunga sheria watakubaliana na madai ya kuwapo kwa amri za Jumapili." PK 606.

d. "Waprotestanti wa Marekani watakuwa mstari wa mbele katika kuinyosha mikono yao juu ya ghuba ili kuushika mkono wa Imani ya Mizimu; tena, watainyosha juu ya shimo kubwa lenye kilindi kirefu kushikana mikono na Mamlaka ile ya Roma; hapo ndipo, chini ya uongozi wa muungano huo wa utatu, nchi hii itafuata katika nyayo za Roma kwa kuikanyaga chini ya miguu yake haki ya mtu kuamini kama dhamiri yake inavyotaka." GC 588.

e. "Iwapo watu wanaweza kushawishika kupendelea iwepo amri ya Jumapili, basi, wachungaji na mapadre wanakusudia kutumia nguvu ya mvuto wao wa pamoja katika kujipatia marekebisho ya dini katika Katiba ya nchi, na kulilazimisha Taifa zima [la Marekani] kuitunza Jumapili." RH, Extra 12-24-1889, uk.2.

4. Je! hao wanaoitetea Amri ya Jumapili wanatambua wanalolitenda?

a. "Pana watu wengi, hata miongoni mwa wale walio katika shughuli hiyo ya kutaka itungwe Amri ya Jumapili, ambao wamepofushwa macho yao wasiweze kuona matokeo yatakayofuata baada ya kitendo hicho kutekelezwa. Hawaoni ya kwamba wanaupiga rungu uhuru wa dini moja kwa moja. Wako wengi ambao hawajapata kuyaelewa kamwe madai ya Sabato ya Biblia na msingi wa uongo ambao Amri ya Jumapili inaukalia." 5T 711. b. "Wanafanya kazi hiyo wakiwa vipofu. Hawaoni ya kwamba kama Serikali yao ya Kiprotestanti inaziachilia mbali kanuni zilizowafanya kuwa Taifa huru, linalojitegemea, na kwa njia ya kutunga sheria wanaingiza katika Katiba ya Nchi, kanuni ambazo zitatangaza uongo wa upapa na madanganyo ya upapa, watakuwa wanajitumbukiza katika utawala wa hofu wa Roma wa Zama zile za Giza." RH, Extra 12-11-1888, uk.4.

c. "Kuna nguvu ya Kishetani inayoliendesha tapo [kundi] hilo la Jumapili, ila imejificha. Hata watu wale waliojiingiza katika kazi hiyo, wamepofushwa macho yao wasiweze kuona matokeo yatakayofuata baada ya kazi ya tapo lao kukamilika." RH 1-1-1889, uk.1; 7BC 975.

5. Ni nani hasa aliye mwanzilishi mwamba mkuu wa kuitungia amri Jumapili?

a. "Hakuna hatua yo yote iliyochukuliwa katika kuitukuza Sabato hiyo ya sanamu, na kuileta Jumapili ipate kutunzwa kwa kuitungia amri [sheria], isipokuwa ni yule Shetani aliye nyuma yake, na ndiye amekuwa mtendaji mkuu." 7BC 977.

b. "Bunge litakapotunga sheria ambazo zinaitukuza siku ya kwanza ya juma, na kuiweka mahali pa siku ile ya saba, hapo ndipo hila ya Shetani itakuwa imekamilika." 7BC 976.

c. "Sabato hiyo ya uongo [Jumapili] italazimishwa kwa njia ya kuitungia sheria [amri] ya ukandamizaji. Shetani na malaika zake wako macho sana, nao wanashughulika vibaya sana, wakifanya kazi kwa nguvu na ustahimilivu kupitia kwa wakala wao wa kibinadamu ili kulitimiza kusudi lake la kufutilia mbali katika mioyo ya watu maarifa ya kumjua Mungu." 7BC 985; RH 12- 13-1892.

6. Je, Amri hiyo ya Jumapili inaonyesha dharau juu ya nani?

"Juhudi zaidi ya wazi itafanyika kuitukuza sabato hiyo ya uongo, na kumwonyesha dharau Mungu Mwenyewe kwa kuibadili siku ile aliyoibariki na kuitakasa. Sabato hiyo ya uongo [Jumapili] italazimishwa kwa sheria ya ukandamizaji." 7BC 985.

7. Je, tutazamie kuziona sheria za Jumapili katika majimbo yanayojitawala (states) fulani fulani tu au Bunge la Marekani litachukua hatua ya kuitunga sheria hiyo[kwa Taifa zima]?

a. "Nchi yetu [ya Marekani] imeingia hatarini. Wakati unakaribia ambapo watunga sheria [Wabunge] wake watakapozikataa kabisa kanuni zile za Uprotestanti na kuunga mkono uasi wa Kanisa Katoliki. Watu hao ambao Mungu amewatendea maajabu makubwa sana, akiwatia nguvu kulitupilia mbali lile kongwa linaloumiza sana la upapa, kwa njia ya sheria ya taifa zima wataitia nguvu nyingi imani potofu ya Roma, na kwa njia hiyo kuuamsha utawala ule wa mabavu ambao unangojea tu uguswe ili uanze tena ukatili wake na udikteta." 4SP 410 (1884); ST, 7-17-1907, uk.1907, uk.7.

b. "Tunaona ya kwamba juhudi zinafanywa ili kutuwekea vizuizi katika uhuru wetu wa dini. Hoja ya Jumapili sasa inafikia viwango vikubwa. Marekebisho ya Katiba yetu ya nchi yanasisitizwa katika Bunge la Marekani, na mara yatakapopatikana, basi, ni lazima ukandamizaji utafuata." RH, 12-18-1888, uk.786 (Angalia pia 5T 711).

c. "Hivi karibuni kitatokea kipindi cha kusisimua sana kwa wote walio hai. Malumbano ya zamani yataanza tena; malumbano mapya yatazuka. Mandhari [picha] ya mambo yale yatakayotendwa kama maigizo katika dunia yetu bado hata hayajapata kuingia katika mawazo yetu. Shetani yuko kazini kupitia kwa mawakala wake wa kibinadamu. Wale wanaofanya juhudi ya kuibadilisha Katiba ya Nchi na kujipatia nafasi ya kutunga sheria inayolazimisha utunzaji wa Jumapili hawatambui hata kidogo matokeo yake yatakavyokuwa. Hatari kubwa imetukabili hivi sasa." 5T 753.

d. "Taifa letu litakapozikataa kabisa kanuni za Serikali yake hata kutunga sheria ya Jumapili, katika kitendo hicho Uprotestanti utakuwa umeshikana mikono na upapa." 5T 712.

e. "Hatari kubwa inawangojea watu wa Mungu. Karibu sana Taifa letu litajaribu kuwalazimisha wote kuitunza siku ya kwanza ya juma kama siku takatifu. Kwa kufanya hivyo, hawatakuwa na haya [aibu] kuwalazimisha wanadamu kinyume cha sauti ya dhamiri zao wenyewe ili kuitunza siku ambayo Taifa linaitangaza kuwa ndiyo Sabato." RH, Extra 12-ll-1888, uk. 4.

e. "Sheria ya Mungu itakapobatilishwa, na uasi kuwa dhambi ya Taifa hili, hapo ndipo Bwana atakapotenda kazi kwa ajili ya watu wake." RH, Extra 12-11-1888, uk.3.

g. "Kwa agizo lile linalolazimisha [utunzaji wa] siku ile iliyowekwa na upapa kwa kukiuka sheria ya Mungu, Taifa letu litajitenga kabisa mbali na haki." 5T 451.


Photo Credit By: Yusuph Mcharia

8. Je, Marekani litaendelea kuwa Taifa lililopata upendeleo wa Mungu baada ya kuchukua hatua ya kisheria na kuiweka kando Sheria ya Mungu?

a. "Watu wa Marekani ni watu waliopata upendeleo; lakini watakapouwekea vizuizi uhuru wa dini, kuachilia mbali Uprotestanti, na kuunga mkono upapa, hapo ndipo kikombe chao cha maovu kitakuwa kimejaa, na 'uasi wa Taifa' hili utaandikwa katika vitabu vile vya mbinguni." RH, 5-2- 1893, uk.274.

b. "...Kwa hiyo, uasi huo na uwe ishara kwetu sisi ya kwamba kikomo cha uvumilivu wa Mungu kimefikiwa, ya kwamba kikombe cha maovu ya Taifa letu kimejaa...." 5T 451.

9. Je, matokeo ya uasi wa Taifa letu hili yatakuwaje?

a. "Wakati unakuja ambapo sheria ya Mungu, kwa maana ya pekee, itabatilishwa katika nchi yetu. Watawala wa Taifa letu, kwa njia ya kutunga sheria Bungeni, wataitia nguvu sheria hiyo ya Jumapili, na kwa njia hiyo watu wa Mungu wataingia katika hatari kubwa sana. Taifa letu, katika vikao vyake vya Bunge, litakapotunga sheria za kuzibana dhamiri za watu kuhusu haki zao za kidini, likilazimisha utunzaji wa Jumapili, na kutumia nguvu ya ukandamizaji dhidi ya wale wanaoitunza Sabato ya Siku ya Saba, hapo ndipo sheria ya Mungu, kwa makusudi na nia kamili, itakuwa imebatilishwa katika nchi yetu; na uasi wa Taifa hili utafuatiwa na maangamizi yaTaifa hili." RH, 12-18-1888, uk. 785; 7BC 977.

b. "Ni katika wakati ule wa uasi wa Taifa hili, wakiwa wanazitekeleza sera za Shetani, watawala wa nchi hii watakapojipanga wenyewe upande wa mtu yule wa dhambi, ----- hapo ndipo, kikombe chao cha maovu kitakuwa kimejaa; uasi wa taifa hili ni ishara ya maangamizi ya Taifa hili." GCB 1891, uk.259.


c. "Matokeo ya uasi huu yatakuwa ni maangamizi ya Taifa hili." RH, 5-2-1893, uk. 274.

d. "Waprotestanti watashughulika sana na watawala wa nchi hii kutunga sheria zitakazourejesha ukuu alioupoteza mtu yule wa dhambi, anayeketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu. Kanuni za Ukatoliki wa Roma zitahifadhiwa na kulindwa na Serikali hii. Uasi huo wa Taifa hili utafuatiwa kwa haraka sana na maangamizi ya Taifa hili.... Serikali za Kiprotestanti zitaifikia njia ngeni, nyembamba ipitayo katikati ya milima. Wataongolewa na dunia. Pia, katika kujitenga kwao na Mungu, watafanya kazi kuufanya uongo na uasi wao kwa Mungu viwe ndiyo sheria ya Taifa." RH, 6-15-1897, uk.370.

e. "Makanisa ya Kiprotestanti yatakapoungana na mamlaka za kidunia kuiimarisha dini hiyo ya uongo, ambayo kwa kuipinga mababu zao walistahimili mateso makali sana, hapo ndipo sabato ya papa itakapolazimishwa kwa mamlaka iliyoungana ya kanisa na serikali [dola]. Patakuwa na uasi wa Taifa, ambao utaishia tu katika maangamizi ya Taifa hili. Ev 235 (1899).

f. "Makanisa ya Kiprotestanti yatakapotafuta msaada kutoka kwa mamlaka za kidunia, hivyo kuiga mfano wa kanisa lile asi, ambalo kwa kulipinga babu zao walistahimili mateso makali sana, hapo ndipo patakuwa na uasi wa Taifa ambao utaishia tu katika maangamizi ya Taifa hili." 4SP 410 (1884); ST 7-17-1907, uk. 7.

g. "Makanisa ya Kiprotestanti yatakapoungana na mamlaka za kidunia kuiimarisha dini hiyo ya uongo,... dola hii itakapotumia mamlaka yake kulazimisha amri hizo na kutoa ruzuku kwa taasisi za kanisa ----- hapo ndipo Amerika ya Kiprotestanti itakuwa imeunda sanamu ya upapa, na kutakuwa na uasi wa Taifa ambao utaishia tu katika maangamizi ya Taifa hili." ST, 3-22-1910; 7BC 976.

10. Je, Amerika ya Kiprotestanti itaiundaje sanamu ya mnyama?

a. "Makanisa makuu ya Marekani yatakapoungana katika mafundisho yale wanayoshirikiana pamoja, watakapoishawishi serikali kuyatia nguvu maagizo yao kisheria na kuzipa ruzuku taasisi zao, hapo ndipo Amerika ya Kiprotestanti itakuwa imeunda sanamu ya utawala [wa kidini] wa Roma, na adhabu ya serikali haitaweza kuepukwa kutolewa juu ya wale wasioafiki." GC 445 (Angalia pia 4SP 278).

b. "Katika tendo lile lile la kulazimisha wajibu wa kidini kwa kutumia mamlaka ya kidunia, makanisa yenyewe yangeunda sanamu ya mnyama; kwa hiyo, kulazimisha utunzaji wa Jumapili kule Marekani kungekuwa ndiko kulazimisha ibada ya mnyama na sanamu yake." GC 449.

11. Je, kulazimisha utunzaji wa Jumapili (kuunda sanamu ya mnyama) kule Marekani kutakuja baada au kabla ya kufungwa kwa mlango wa rehema?

a. "Bwana amenionyesha waziwazi ya kwamba sanamu ya mnyama itaundwa kabla ya mlango wa rehema kufungwa; maana hiyo ndiyo itakuwa jaribio kubwa kwa watu wake Mungu.... Hilo ndilo jaribio ambalo watu wa Mungu hawana budi kuwa nalo kabla hawajatiwa muhuri." 7BC 976.

b. "Kwa agizo lile linalolazimisha siku iliyowekwa na upapa, Taifa letu litajitenga kabisa mbali na haki. Uprotestanti utakapounyosha mkono wake ng'ambo ya ghuba kuushika mkono wa Mamlaka ya Roma, utakapounyosha juu ya shimo kubwa lenye kilindi kirefu kushikana mikono na Imani ya Mizimu, nchi yetu, chini ya uongozi wa muungano huo wa utatu, itakapokuwa imeikataa kila kanuni ya Katiba yake kama Serikali ya Kiprotestanti na ya Jamhuri, na kutunga sheria inayotangaza uongo na madanganyo ya upapa, hapo ndipo tunaweza kujua kwamba wakati umewadia kwa utendaji wa miujiza ya ajabu ya Shetani na ya kwamba mwisho u karibu.

Kama vile kukaribia kwa majeshi yale ya Kirumi kulivyokuwa ishara ya maangamizi ya Yerusalemu yaliyokuwa karibu sana kwa wanafunzi wake wale, hivyo ndivyo uasi huo unavyoweza kuwa ishara kwetu kwamba kikomo cha uvumilivu wa Mungu kimefikiwa, na ya kwamba kikombe cha maovu ya Taifa letu kimejaa, na ya kwamba malaika yule wa rehema karibu ataruka kwenda zake, asirudi tena kamwe." 5T 451.

c. "Njozi za Anna zinaweka kuundwa kwa sanamu ya mnyama baada ya kufungwa kwa mlango wa rehema. Hivyo sivyo mambo yalivyo. Unajidai kuziamini shuhuda; hebu na zikuweke sawa katika suala hili. Bwana amenionyesha mimi waziwazi kwamba sanamu ya mnyama itaundwa kabla ya mlango wa rehema kufungwa; maana hiyo ndiyo itakuwa jaribio kuu kwa watu wa Mungu, ambalo kwalo umilele wao utaamuliwa." 2SM 81.

12. Kwa kuzingatia matarajio ya kutungwa kwa Amri ya Jumapili, Waadventista wanaokaa katika miji mikubwa wanasihiwa kufanya nini upesi iwezekanavyo?

a. "Anataka sisi tuishi mahali palipo na nafasi ya kutosha. Watu wake hawapaswi kusongamana katika miji mikubwa. Anawataka kwenda na familia zao nje ya miji mikubwa, ili wapate kujiandaa vizuri kwa uzima ule wa milele. Kitambo kidogo tu watatakiwa kuiacha miji mikubwa.... Tokeni katika miji mikubwa upesi iwezekanavyo...." 2SM 356.

b. "Hatari kubwa inakuja haraka kuhusiana na utunzaji wa Jumapili.... Kama kwa mpango wa Mungu tunaweza kujipatia mahali palipo mbali kutoka katika miji mikubwa, basi, Bwana atatutaka sisi kufanya hivyo. Kuna nyakati za taabu mbele yetu.... Nauona umuhimu upo wa kuharakisha kuyaweka mambo yote tayari kwa hatari hiyo." 2SM 359.
 
Photo Credit By: Morning Star Radio 105.3 fm

13. Sheria za Jumapili zitatoa onyo gani kwa Waadventista ambao bado wanaendelea kukaa katika miji mikubwa?

"Kama kuzingirwa kwa Yerusalemu na majeshi ya Warumi kulivyokuwa ishara ya kukimbia kwa Wakristo wale wa Yudea, ndivyo kutwaa madaraka kwa upande wa Taifa letu katika kutoa amri iie inayolazimisha sabato ya papa kutakavyokuwa onyo kwetu. Basi huo utakuwa ndio wakati wa kuondoka kwenye miji midogo kwenda kwenye makazi ya upweke mahali pa faragha miongoni mwa milima." 5T 464,465.

14. Je, tutazitumiaje siku za Jumapili baada ya Amri za Jumapili kupitishwa?

a. "Waadventista Wasabato walitakiwa kuonyesha hekima yao kwa kujizuia kufanya kazi zao za kawaida katika siku ile, wakiitumia kwa shughuli za kimishonari. "Kuzipinga Amri za Jumapili kutawaimarisha tu washupavu wa dini wanaojaribu kuzilazimisha kwao ili kuongeza mateso yao. Msiwape nafasi yo yote kuwaita ninyi kuwa wavunjaji wa sheria hizo.... Mtu hapokei alama ya mnyama kwa sababu anaonyesha kwamba anatambua hekima ya kutunza amani kwa kujizuia kufanya kazi inayoleta uvunjaji wa sheria hizo.... "Wakati wo wote inapowezekana, endesheni huduma za kidini katika siku hiyo ya Jumapili.... Waalimu wetu katika shule zetu waitumie Jumapili kwa shughuli za kimishonari." 9T 232,233.

b. "Msifanye maandamano yo yote siku ya Jumapili kupinga sheria hiyo." 9T 235.

c. "Wakati mmoja wale waliokuwa wasimamizi wa shule yetu ya Avondale waliniuliza mimi wakisema: 'Tufanye nini? Mapolisi wanaoilinda sheria hiyo wameagizwa kuwakamata wale wanaofanya kazi siku ya Jumapili.' Mimi niliwajibu hivi: 'Litakuwa ni jambo rahisi sana kuliepuka tatizo hilo. Itoeni siku ya Jumapili kwa Bwana kama siku ya kufanya kazi ya kimishonari. Nendeni nje na wanafunzi wenu kuendesha mikutano mahali mbalimbali, na kufanya kazi ya uganga. Watawakuta watu majumbani mwao, nao watakuwa na wakati mzuri sana wa kuifundisha ile kweli. Njia hii ya kuitumia Jumapili sikuzote inakubaliwa na Bwana." 9T 238.

d. "Tulipokuwa tunaishi mahali paitwapo Cooranbong, ambapo shule yetu ya Avondale imejengwa,... Hoja ya kufanya kazi Jumapili ilikuja kwetu kwa ajili ya kuitafakari. Ilionekana kana kwamba punde kamba zingetufunga sana kila upande hata tusiweze kufanya kazi yo yote siku ya Jumapili. Shule yetu ilikuwa katikati ya misitu, mbali na kijiji cho chote au kituo cha reli.

Hakuna ye yote aliyekuwa anaishi karibu kiasi cha kutosha kutufanya tuingiwe na wasiwasi kwa njia iwayo yote kwa jambo lo lote ambalo tungeweza kulifanya. Hata hivyo, tulikuwa tunachunguzwa. Maofisa wa polisi walishurutishwa kuja kuangalia tulichokuwa tukifanya katika eneo lile la shule; nao walikuja hakika, lakini hawakuweza kuwaona wale waliokuwa wanafanya kazi. Imani yao na heshima yao kwa watu wetu ilikuwa imepatikana kutokana na kazi ile tuliyokuwa tumeifanya kwa wagonjwa katika jumuia ile kiasi kwamba awakutaka kuingilia kati kazi yetu isiyokuwa na madhara yo yote ambayo sisi tuliifanya katika siku ya Jumapili.

"Wakati mwingine ndugu zetu walipotishiwa kuteswa, tena wakawa wanauliza kile ambacho wangeweza kufanya, niliwapa ushauri uo huo niliokuwa nimeutoa kujibu hoja ya kuitumia Jumapili kwa michezo. Niliwaambia, "Itumieni Jumapili kwa kufanya kazi ya kimishonari kwa ajili yake Mungu. Waalimu, nendeni pamoja na wanafunzi wenu.'... "Waalimu katika shule zetu na waitumie Jumapili kwa shughuli za kimishionari." CT 459-551.

15. Je, mtazamo wetu leo uweje? Twawezaje kufanya kazi na kuomba?

a. "Hatufanyi mapenzi ya Mungu tunapokaa kimya tu, bila kufanya kitu cho chote kuuhifadhi uhuru wa dhamiri zetu. Maombi ya bidii, yenye kuleta matokeo yangekuwa yakipanda mbinguni ili janga hilo lipate kuahirishwa mpaka hapo tutakapoweza kuimaliza kazi ambayo imeachwa kwa muda mrefu sana. Hebu na pawe na maombi yanayotolewa kwa bidii sana, kisha na tufanye kazi kulingana na maombi yetu. Yaweza kuonekana kwamba Shetani anashinda na ya kwamba kweli imeshindwa na makosa [mafundisho potofu] na uongo;... Lakini Mungu angetutaka sisi kukumbuka alivyowatendea watu wake wa zamani kuwaokoa kutoka kwa maadui wao. Sikuzote amechagua upeo wa matatizo ili kuonyesha uweza wake, yaani, wakati ule ilipoonekana ya kuwa hakuna uwezekano wo wote wa kuokoka kutoka katika utendaji wa Shetani. Shida ya mwanadamu ni nafasi ya Mungu ya kutenda kazi yake." 5T 714.

b. "Tungejifunza kwa bidii Neno la Mungu, na kuomba kwa imani ili Mungu apate kuzizuia nguvu za giza; maana mpaka sasa ujumbe umekwenda karibu kwa watu wachache mno, na ulimwengu huu unapaswa kuangazwa kwa utukufu wake. Ukweli wa leo ----- amri za Mungu [kumi] na Imani ya Yesu ----- bado haujatangazwa kama unavyopaswa kutangazwa.... Yatupasa kuwa na msimamo thabiti ya kwamba sisi hatutaiheshimu siku ya kwanza ya juma kama sabato...." RH, Extra 12-24-1889, uk.2.

c. "Kwa miaka mingi tumekuwa tukiitazamia Amri ya Jumapili kutungwa katika nchi yetu; na sasa kwa vile tapo hilo liko juu yetu, tunauliza hivi, Watu wetu watafanya nini katika suala hili?...

Tungemtafuta Mungu hasa ili watu wake wapewe neema na nguvu sasa. Mungu wetu yu hai; wala hatuamini kwamba wakati umefika kabisa ambao angeruhusu uhuru wetu uwekewe vizuizi. Nabii aliwaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wo wote. Malaika mwingine akipanda kutoka maawio ya jua, akawapigia kelele, akisema, 'Msiidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao.' Hii inaonyesha kazi tunayopaswa kuifanya sasa, ambayo ni kumlilia Mungu wetu ili malaika wale waendelee kuzizuia pepo zile nne mpaka Wamishonari wapate kutumwa sehemu zote za dunia, na mpaka watakapokuwa wamelitangaza lile onyo juu ya wale wanaoivunja Sheria ya Yehova." RH, Extra 12-11-1888, uk.4,5.

d. "Jukumu zito limekabidhiwa kwa wanaume na wanawake wenye maombi katika nchi nzima, kupeleka dua ili Mungu alifagilie nyuma wingu hili la maovu, na kutupatia miaka michache zaidi ya kufanya kazi kwa ajili ya Bwana." RH, Extra 12-11-1888, uk.4.

e. "Twaona ya kwamba wale ambao sasa wanazishika amri zake Mungu wanahitaji kujishughulisha ili waweze kupata msaada maalum ambao ni Mungu peke yake awezaye kuwapa. Wangefanya kazi kwa bidii zaidi ili kuchelewesha kwa muda mrefu iwezekanavyo janga hilo linalotishia. RH 12-18-1888, uk. 785.

f. "Iwapo hawafanyi lo lote kuielimisha mioyo ya watu, na kwa njia ya ujinga wa kutoijua kweli Mabunge yetu yangeweza kuzikataa kanuni za Uprotestanti, na kuunga mkono na kulitia nguvu kosa la Roma, yaani, sabato ya bandia [Jumapili], basi, Mungu atawashikilia watu wake waliopokea nuru kubwa kuwa wanawajibika kwa utovu wao wa juhudi na uaminifu. Lakini kama suala hili la kutunga sheria ya dini linawekwa mbele ya watu kwa busara na kwa akili, nao wanaona ya kwamba kwa njia hiyo ya kuilazimisha Jumapili uasi wa Roma ulitokea, ya kwamba ulimwengu wa Kikristo ungeweza kuigiza tena kitendo kama hicho, na ya kwamba utawala wa mabavu wa vizazi vile vilivyopita ungerudiwa tena, basi, lo lote lijalo na lije, sisi tutakuwa tumefanya wajibu wetu." RH Extra 12-24-1889, uk.3.

g. "Hebu watu wa Mungu wanaozishika amri zake [kumi] wasinyamaze wakati kama huu, kana kwamba tulikuwa tunaikubali hali hii na kuipenda. Kuna matarajio mbele yetu ya kupigana vita ya kudumu, kwa hasara ya kufungwa, kupoteza mali zetu na hata maisha yenyewe katika kuitetea Sheria ya Mungu [Amri Kumi], ambayo inabatilishwa kwa sheria za wanadamu." RH 1-1-1889, uk.1; 7BC 975.

h. "Ni matumaini yangu kuwa tarumbeta itatoa sauti ya hakika kuhusu tapo [kundi] hili linalotaka kuiweka Amri ya Jumapili. Nadhani kwamba ingekuwa bora sana kama katika magazeti yetu somo la umilele wa Sheria ya Mungu [Amri Kumi] lingetolewa kama somo maalum.... Hivi sasa tungekuwa tunafanya kila tuwezalo kuishinda sheria hiyo ya Jumapili." CW 97,98 (1906).

j. "Wale waliokwisha kuonywa juu ya matukio yaliyo mbele yao hawapaswi kukaa wakiwa wanaingojea kimya kimya dhoruba ile inayokuja, wakijifariji wenyewe kwamba Bwana atawalinda wale walio waaminifu katika siku ile ya taabu. Yatupasa sisi kuwa kama watu wanaomngojea Bwana wao, si kwa kukaa bila kazi, bali kwa kufanya kazi kwa juhudi nyingi, kwa imani isiyotikisika. Huu sasa sio wakati wa kuiacha mioyo yetu kujazwa na mambo yale yasiyo na maana...

Tapo hilo la Jumapili hivi sasa linasonga mbele gizani. Viongozi wake wanaficha hoja halisi, na wengi wanaojiunga na tapo hilo wao wenyewe hawaoni ni wapi mkondo wake wa chini unakokwenda. Itikadi zake ni laini, na mwonekano wake ni wa Kikristo; lakini litakaponena, litaifunua roho ile ya joka. Ni jukumu letu kufanya yote yaliyo katika uwezo wetu kuiepusha hatari hii inayotishia. Tungejitahidi kuzizima hisia za chuki kwa kujiweka wenyewe katika nuru ile inayofaa mbele ya watu. Tungeweka mbele yao hoja halisi ya jambo hilo, hivyo kuingilia kati kwa kupinga kunakofaa dhidi ya hatua za kuuwekea kizuizi uhuru wa dhamiri zetu. Yatupasa kuyachunguza Maandiko, na kuweza kutoa sababu kwa imani yetu." RH Extra 12-11-1888, uk. 4.

k. "Vitabu vya 'Patriarchs and Prophets, Daniel and Revelation, na The Great Controversy' vinahitajika sana sasa kuliko vilivyopata kuhitajika huko nyuma. Vingetawanywa kwa wingi sana kwa sababu kweli zile vinazozisisitizia zitayafungua macho mengi yaliyopofuka.... Wengi miongoni mwa watu wetu wamekuwa vipofu kwa umuhimu wa vitabu vile vile hasa vinavyohitajika sana. Kama busara na ustadi vingekuwa vimeonyeshwa kwa wakati ule katika kuviuza vitabu hivyo, basi, tapo hilo la Sheria ya Jumapili lisingefika hapo lilipo leo." CM 123; RH 12-16-1905.

l. "Hatuwezi kufanya kazi ili kuwafurahisha watu wale watakaoutumia mvuto wao kuukandamiza uhuru wa dini, na kuanzisha hatua za ukandamizaji ili kuwaongoza au kuwalazimisha wanadamu wenzao kuitunza Jumapili kama Sabato. Siku ya kwanza ya juma sio siku ya kuiheshimu. Ni sabato ya bandia, na washiriki wa familia yake Bwana hawawezi kushirikiana na watu hao wanaoitukuza siku hiyo, na kuivunja Sheria ya Mungu [Amri Kumi] kwa kuikanyaga chini ya miguu yao Sabato yake. Watu wa Mungu hawapaswi kupiga kura ili kuwaweka watu kama hao katika ofisi; maana wanapofanya hivyo, wanashiriki pamoja nao dhambi zile watakazozitenda wakiwa ofisini." FE 475; GW 39l,392.

********************

UNA MAONI AU USHAURI WOWOTE?

USISITE KUACHA KTK KIBOSKI CHA MAONI MTAA FLANI HAPO CHINI.

********************

Alhamisi, Februari 09, 2012

HATARI KUBWA MBELE YETU



Bibi White anakielezaje kipindi kile cha dhiki kinachoujia ulimwengu wetu?







(1) "Hatari Kubwa ya Kuogofya."

 "Kazi ambayo kanisa limeshindwa kufanya katika kipindi hiki cha amani na usitawi, litapaswa kuifanya katika kipindi cha hatari kubwa ya kuogofya, chini ya mazingira ya kukatisha tamaa sana, yaani, ya kuogofya sana." Ev.31; 5T 463.






(2) "Hatari Kubwa ya Mwisho."


a. "Katika kipindi hiki cha maovu yanayotapakaa kila mahali tunaweza kujua ya kwamba hatari kubwa ya mwisho imekaribia. Wakati uasi juu ya Sheria ya Mungu utakapokuwa umeenea karibu katika ulimwengu wote, watu wake watakapokuwa wanakandamizwa na kuteswa na wanadamu wenzao hapo ndipo Bwana atakapoingilia kati." COL 178.


b. "Maafa katika nchi kavu na baharini, hali ya kutotulia ya jamii, tetesi za vita, hutuonya juu ya mambo mabaya yatakayotokea mbele. Hubashiri matukio yanayokuja ya kiwango kikubwa mno. "Mawakala wa uovu wanayaunganisha majeshi yao na kuyaimarisha. Wanajizatiti kwa hatari kubwa ile ya mwisho. Mabadiliko makubwa yatatokea mara moja katika ulimwengu wetu, na mabadiliko yale ya mwisho yatakuwa ya haraka-haraka." 9T 11.






(3) "Pambano la maana sana" la vizazi."

 "Hatari kubwa inawangojea watu wa Mungu. Hatari inawangojea walimwengu. Pambano la maana sana la vizazi vyote ndio kwanza liko mbele yetu." 5T 711.






(4) "Hatari ya Vizazi Vyote.

" Tunasimama mlangoni mwa hatari ya vizazi vyote. Kwa mfuatano wa haraka hukumu za Mungu zitakuja moja baada ya nyingine ----- moto, na mafuriko, na tetemeko la nchi, pamoja na vita na umwagaji wa damu. Hatupaswi kushangazwa wakati huu na matukio makuu na ya kukata maneno; maana malaika wa rehema hawezi kuendelea kwa muda mwingi zaidi kuwakinga wale wasiotaka kutubu." PK 278.






(5) Hatari kubwa sana tangu wakati ulipoanza kuwako.

"Tunaukaribia wakati ambao, zaidi ya wakati mwingine wo wote uliopita tangu kuwako kwa ulimwengu huu, utataka kujitoa wakf kikamilifu kwa kila mmoja aliyepata kulitaja jina lake Kristo." GW 323.






(6) "Hatari Kubwa Sana."

"Wakati huu wa sasa ni wakati wa kusisimua mno kwa wote wenye uhai. Watawala na viongozi wa siasa, watu wanaovikalia vyeo vyenye dhamana na mamlaka, wanaume na wanawake wanaotafakari sana wa tabaka zote, mawazo yao wameyakaza juu ya matukio yanayotokea kutuzunguka. Wanaangalia uhusiano uliopo miongoni mwa mataifa. Wanachunguza nguvu inayoingia katika kila kitu cha asili [ardhi, hewa, moto, maji], nao wanatambua ya kwamba jambo fulani kubwa na la kukata maneno li karibu kutokea, ----- ya kwamba ulimwengu huu umefikia ukingoni mwa hatari kubwa sana." PK 537; Ev 703,704, Ed 179.






(7) "Dhoruba."


a. "Dhoruba inaanza kuja ambayo itaupotosha na kuujaribu msingi wa kiroho wa kila mmoja wetu kufikia upeo wake." 5T 129.


b. "Dhoruba inakuja, ina ghadhabu isiyo na huruma. Je! tumejiweka tayari kukabiliana nayo?" 8T 315.



(8) "Tufani."


a. "Mungu amefunua kile kitakachotokea katika siku zile za mwisho, ili watu wake waweze kujiweka tayari kusimama dhidi ya tufani hiyo ya upinzani na ghadhabu." 5T 452.


b. "Tufani inakuja, nasi yatupasa kuwa tayari kukabiliana na ghadhabu yake kwa njia ya kuwa na toba kwa Mungu na imani kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Bwana tasimama kuitetemesha sana dunia hii. Tutaona dhiki pande zote. Maelfu ya meli yatazamishwa chini ya vilindi vya bahari. Majeshi ya wanamaji yatazama chini, na maisha ya wanadamu yatatolewa mhanga kwa mamilioni. Mioto itawaka bila kutazamia, wala hakuna juhudi iwayo yote ya kibinadamu itakayoweza kuizima. Majumba ya kifalme ya duniani humu yatafagiliwa mbali katika ukali wa ndimi za mioto hiyo. Ajali katika njia za reli zitazidi kuongezeka mara kwa mara; kiwewe, migongano, na vifo bila hata taarifa ya dakika moja vitatokea katika njia zote kuu za usafiri. Mwisho umekaribia, mlango wa rehema [karibu] unafungwa. Hebu na tumtafute Mungu maadamu anapatikana, tumwite maadamu yu karibu!" MYP 89,90.



(9) "Pambano la Kuogofya Mno ambalo Halijapata Kushuhudiwa."

 "Pambano ambalo limetufikia sisi litakuwa la kuogofya mno ambalo halijapata kushuhudiwa." 7T 407.



(10) "Pambano la Kutisha."

"Shetani anayakusanya majeshi yake; je! sisi kila mmoja peke yake tumejiweka tayari kukabiliana na pambano la kutisha ambalo li mbele yetu sasa? Je! tunawatayarisha watoto wetu kwa hatari hiyo kubwa?" AH 186.



(11) "Jaribio Kuu."

"Endapo waumini wa ile kweli hawategemezwi na imani yao katika siku hizi za amani linganifu, ni kitu gani, basi, kitakachowainua juu wakati ule wa jaribio kuu utakapokuja na amri kutangazwa dhidi ya wale wote ambao watakataa kuiabudu sanamu ile ya mnyama, wala kuipokea alama yake juu ya vipaji vya nyuso zao au katika mikono yao? Kipindi hicho cha kutisha hakiko mbali. Badala ya kuwa dhaifu na kusitasita, watu wa Mungu wangekuwa wanakusanya nguvu zao na ujasiri kwa ajili ya wakati huo wa taabu." 4T 251.



(12) "Hofu Kuu."

"Uasi karibu sana umefikia kipeo chake. Machafuko yamejaa duniani, na hofu kuu karibu sana itawajia wanadamu. Mwisho umekaribia sana." 8T 28.



3. Je, wakazi wa mbinguni wana habari kuhusu pambano letu linalokuja?

"Malimwengu yote yanaangalia kwa shauku isiyoelezeka kuiona kazi hii ya mwisho ya kufungia pambano kuu kati ya Kristo na Shetani." 5T 526.






4. Je, sehemu kubwa ya wakazi wa dunia hii wana habari juu ya matukio yaliyo karibu kutokea?


a. "Sisi tunaoijua kweli tungekuwa tunajiweka tayari kwa kile kitakachoupata ulimwengu huu hivi karibuni kama mshangao mkubwa mno kwao." 8T 28; 7BC 911.


b. "Wakristo wangekuwa wanajiandaa kwa kile kitakachoupata ulimwengu huu hivi karibuni kama mshangao mkubwa mno kwao, na maandalizi hayo wangeyafanya kwa njia ya kujifunza Neno la Mungu kwa bidii na kujitahidi kuyafanya maisha yao kupatana na amri zake [kumi].... Mungu anataka pawepo na uamsho na matengenezo." PK 626.






5. Je, sisi kama Waadventista Wasabato tunaitambua kweli kweli hatari iliyo mbele yetu?






a. " 'Wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo,' hivi punde utakuja juu yetu; tutahitaji uzoefu ambao hatunao sasa, na ambao wengi ni wavivu mno kuupata. Mara nyingi ndivyo mambo yalivyo ya kwamba taabu inayotarajiwa huonekana kuwa ni kubwa kuliko ilivyo hasa; lakini jambo hilo si kweli kuhusu hatari kubwa iliyo mbele yetu. Maelezo ya wazi kabisa hayawezi kukifafanua kiwango cha ukubwa wa mateso hayo." GC 622.






b. "Sisi tuko ukingoni kabisa mwa wakati ule wa taabu, na mifadhaiko ambayo haijapata kuingia katika mawazo yetu i mbele yetu." 9T 43.






6. Je, yawezekana kwa Wakristo kutojiweka tayari kwa taabu ile inayokuja, ijapokuwa wao wamepata maonyo ya nyuma?

Marko 8:31,32; 9:31; 10:32-34; Mathayo 26:56; Luka 24:6-8.






7. Kwa nini wanafunzi wake walikuwa hawajajiweka tayari kabisa?


A. "Hawakuweza kulistahimili wazo la kwamba yeye ambaye matumaini yao yote yalikuwa yamejengwa juu yake angeweza kuteseka na kufa kifo cha aibu sana. Maneno ambayo walihitaji kuyakumbuka yalikuwa yamefutika katika mawazo yao; na wakati wa kujaribiwa ulipofika, uliwakuta hawajawa tayari. Kifo cha Yesu kikayavunjilia mbali matumaini yao yote kana kwamba alikuwa hajawaonya mapema." GC 594.


B. "Petro hakuwa na hamu ya kuuona msalaba katika kazi yake Kristo." DA 415.






8. Je, Bwana ametupa muhtasari ulio wazi wa matukio yanayoambatana na kufungwa kwa mlango wa rehema?



A "Matukio yale yanayoambatana na kufungwa kwa mlango wa rehema na kazi ile ya maandalizi kwa ajili ya wakati wa taabu, vimeonyeshwa kwa wazi. Makundi na makundi ya watu hawana ufahamu wo wote [hawajui] kuhusu kweli hizi za maana sawa na vile ambavyo zingekuwa hazijapata kufunuliwa kwao kamwe." GC 594.



B "Amepewa ramani inayoonyesha kila alama ya njia katika safari yake ya kwenda mbinguni, wala isingempasa kukisia kitu cho chote." GC 98.




C "Katika historia tunapaswa kuona utimilizo wa unabii,kujifunza mkono wa Mungu unavyofanya kazi katika matapo (movements) makubwa ya matengenezo, na kuelewa maendeleo ya matukio katika kuyakusanya mataifa kwa vita ile ya mwisho katika pambano lile kuu." MH 442; 8T 307.






9. Je, hii ina maana kwamba tunaweza kuelewa kwa undani elezo moja moja la matukio hayo yanayotarajiwa kabla hayajatokea?


a. "Alama ya Mnyama ni sawa kabisa na vile ilivyobainishwa tayari. Si yote kuhusu suala hilo yamefahamika, wala yataweza kufahamika mpaka hapo mbingu zitakapokunjwa kama ukurasa." 6T 17; 8T 159.


b. "Mengi juu ya mambo hayo yameonyeshwa kwangu, lakini mimi naweza kutoa maelezo machache tu kwenu. Enendeni kwa Mungu ninyi wenyewe, ombeni mwelimishwe na mbingu, ili mpate kujua ya kwamba mnaijua hasa kweli ni nini, ili uwezo ule wa Shetani ufanyao miujiza utakapodhihirishwa, kisha yule adui akawajia kama malaika wa nuru, mpate kupambanua kati ya miujiza ya kweli ya Mungu na miujiza ya bandia [uongo] ya mamlaka zile za giza." RH, 12-24- 1889, uk.3.


 



10. Je, ni muhimu jinsi gani kwetu kujifunza unabii ule unaohusu siku hizi za mwisho?


a. "Tunapokaribia mwisho wa kufungwa kwa historia ya ulimwengu huu, unabii ule unaohusu siku hizi za mwisho unataka hasa tuufanyie utafiti wetu." COL 133.


b. "Wangepaswa kuyajua mambo yale ambayo hayana budi kutokea kabla ya kuifunga historia ya ulimwengu huu. Mambo hayo yanahusika na usitawi wetu wa milele, na waalimu pamoja na wanafunzi wao wangeyaangalia kwa makini zaidi." 6T 129.


c. "Kisha mimi nikamwona malaika yule wa tatu. Malaika aliyeandamana nami akasema, 'Kazi yake ni ya kutisha. Ujumbe wake ni wa kuogofya. Huyo ndiye malaika anayechagua ngano kutoka katika magugu, na kuitia muhuri, au kuifunga, ngano hiyo tayari kwa kuwekwa katika ghala ile ya mbinguni. Mambo hayo yangejaa katika mawazo yetu yote, yaani, yangeyavuta mawazo yetu yote.' " EW 118.

d. "Katika majira ya usiku maneno haya yalinenwa kwangu: 'Waagize waalimu katika shule zetu kuwatayarisha wanafunzi wao kwa kile kinachoujia ulimwengu.' " FE 526,527.


e. "Lakini iko siku aliyoiweka Mungu kwa ajili ya kufungwa kwa historia ya ulimwengu huu: 'Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.' Unabii huo unatimia haraka sana. Mengi, mengi sana yangeweza kusemwa juu ya masomo haya ya maana sana." FE 335.



f. "Walinzi na wapaze sauti zao na kutoa ujumbe huu ambao ndio ukweli wa leo. Hebu na tuwaonyeshe watu mahali tulipofikia katika historia ya unabii." 5T 516.


g. "Jitihada kubwa zingefanyika kuliweka somo hili mbele ya watu. Ukweli huu wa kutisha unapaswa kuwekwa sio tu mbele ya watu wa ulimwengu huu, bali pia mbele ya makanisa yetu , ya kwamba siku ya Bwana itakuja ghafula, bila kutazamia. Onyo la kutisha la unabii huu ni kwa kila mtu. Asiwepo hata mmoja anayejisikia kuwa yu salama mbali na hatari ile ya kugutushwa. Tafsiri ya unabii ya mtu awaye yote [isiyopatana na Maandiko] isiwanyang'anye uhakika wa kuyajua matukio ambayo yanaonyesha kwamba tukio hilo kuu limekaribia sana." FE 336.






11. Sisi tumeonywa tusifanye kitu gani hasa?




a. "Uko wakati wa taabu unaowajia watu wa Mungu, lakini hatupaswi kuuweka mbele ya watu daima, na kuwafanya [kusababisha] waweze kupata wakati wao wa taabu mapema. Kupepetwa kuko miongoni mwa watu wa Mungu, lakini huo sio ukweli wa leo wa kuyapelekea makanisa yetu." 1SM 180; 2SM 13.


b. "Ziko nyakati za dhoruba mbele yetu, lakini tusitamke neno hata moja liletalo mashaka au kukatisha tamaa [kwa waumini]." ChS 136.



12. Tukiwa tumeizingatia hatari kubwa inayokuja, tungekuwa tunafanya nini hivi sasa?


"Kama Mungu amepata kunena kupitia kwangu, basi, wakati utakuja mtakapopelekwa mbele ya mabaraza, na kila msimamo wa ile kweli mnayoishikilia utakosolewa kwa ukali sana. Muda ambao wengi sana wanauacha kupotea bure ungetumika kulitii agizo ambalo Bwana ametupa la kujiweka tayari kwa hatari kubwa inayokuja." 5T 717.





13. Ni akina nani pekee watakaosimama imara katika Pambano Kuu la mwisho?


a. "Hakuna watakaoweza kusimama katika Pambano lile Kuu la mwisho isipokuwa wale walioiimarisha mioyo yao kwa zile kweli za Biblia." GC 593.


b. "Jifunzeni Biblia zenu kwa namna ambayo hamjapata kamwe kujifunza kwa siku za nyuma. Msipoinuka na kukifikia kiwango kile cha juu cha utakatifu katika maisha yenu ya kidini, hamtakuwa tayari kwa kufunuliwa [kuja] kwake Bwana wetu." 5T 717.



c. "Tunazikaribia nyakati zile za dhoruba.... Kila msimamo wa imani yetu utachunguzwa; na kama sisi si wanafunzi wakamilifu wa Biblia, tulioimarishwa, tuliotiwa nguvu, na kutulia [katika kweli], basi, hekima ya wakuu wa ulimwengu huu itatufanya sisi tupotee." 5T 546.



d. "Ni wale tu ambao wamekuwa wanafunzi wenye bidii wa Maandiko, na ambao wameipenda hiyo kweli [wameishi kulingana na hiyo kweli], watakaolindwa kutokana na madanganyo yenye nguvu yatakayouteka ulimwengu wote." GC 625.






Jumatano, Februari 08, 2012

MUUNGANO WA MAKANISA



1. Je, kila dhehebu la Kiprotestanti katika nchi ya Amerika litaingia katika Muungano wa Makanisa unaokuja?

"Makanisa Makuu ya Marekani, yatakapoungana katika mafundisho yale wanayoshirikiana pamoja, watakapoishawishi serikali yao kuyatia nguvu kisheria maagizo yao na kuzipa ruzuku taasisi zao, hapo ndipo Amerika ya Kiprotestanti itakuwa imeunda sanamu ya utawala wa kidini wa Roma, na adhabu ya serikali haitaweza kuepukwa kutolewa juu ya wale wasioafiki." GC 445.



2. Kwa msingi gani makanisa ya Kiprotestanti hatimaye yataweza kuungana?

"Tofauti kubwa ya imani inayojitokeza katika makanisa ya Kiprotestanti inaangaliwa na wengine kama ni ushahidi wa kutosha kuonyesha kwamba hakuna juhudi yo yote inayoweza kufanywa ili kupata umoja utakaolazimishwa. Lakini kwa miaka mingi, katika makanisa yenye imani ya Kiprotestanti, pamekuwa na maoni yenye nguvu, yanayoendelea kukua ambayo yanapendelea muungano uwepo uliojengwa juu ya mafundisho yale wanayoshirikiana pamoja. Kuupata muungano kama huo, mjadala wa mafundisho yale ambayo wote walikuwa hawaafikiani ----- haidhuru yawe ya maana jinsi gani kutokana na msimamo wa Biblia ----- itabidi utupiliwe mbali." GC 444.



3. Ni mafundisho gani makuu mawili yenye makosa ambayo makanisa hayo yameyashikilia kwa pamoja?

"Kwa njia ya makosa makuu mawili ----- imani kwamba roho haifi, na utakatifu wa Jumapili ----- Shetani atawaleta watu chini ya madanganyo yake. Wakati lile la kwanza linaweka msingi wa imani ya mizimu (spiritualism), lile la pili linaleta mapatano ya kushirikiana na Roma." GC 588.



4. Je, Uprotestanti hatimaye utaweza kuungana na Ukatoliki?

a. "Neno la Mungu linafundisha kwamba matukio hayo [ya kuikandamiza Sabato] yatarudiwa wakati ule Wakatoliki wa Roma na Waprotestanti watakapoungana kwa lengo la kuitukuza Jumapili." GC 578.



b. "Kwa jinsi gani Kanisa la Roma linaweza kujinasua kutokana na shtaka la kuabudu sanamu hatuwezi kuelewa.... Na hiyo ndiyo dini ambayo Waprotestanti wanaanza kuiangalia kwa upendeleo mkubwa sana, na ambayo hatimaye itaungana na Uprotestanti." RH, 6-1-1886, uk.338.



c. "Maadam muda wa majaribio bado ungalipo, itapatikana nafasi kwa mwinjilisti wa vitabu kufanya kazi yake. Madhehebu za dini zitakapoungana na upapa ili kuwatesa watu wa Mungu, basi, mahali pale ambapo uhuru wa dini utakuwapo patafunguliwa kwa uinjilisti wa vitabu." 6T 478.



5. Je, kutakuwa na muungano wa makanisa au muungano katika utendaji wake?

a. "Ulimwengu unaojidai kuwa ni wa Kiprotestanti utaungana kwa mapatano na yule mtu wa dhambi (kuasi), hapo ndipo kanisa na ulimwengu vitakuwa katika mwafaka potovu." 7BC 975.



b. "Uroma katika Ulimwengu ule wa Zamani [Ulaya], na Uprotestanti Asi katika ule Mpya [Marekani], watafuata njia ile ile moja katika kuwashughulikia wale wanaoziheshimu amri zote [kumi] za Mungu." GC 616.



6. Je, Roma itabadilika au Uprotestanti ndio utakaobadilika ili kufanya kuunganika tena kuwezekane?

a. "Muungano huo, kwa hali yo yote, hautafanyika kutokana na badiliko katika Ukatoliki; kwa maana Roma haibadiliki kamwe. Inadai kwamba haiwezi kukosea. Ni Uprotestanti, basi, utakaobadilika. Kupokea mawazo mapana yaliyo huru kwa upande wake [Uprotestanti] kutauleta mahali ambapo utaushika kwa nguvu mkono wa Ukatoliki. 'Biblia, Biblia, ndiyo msingi wa imani yetu,' kilikuwa ndicho kilio cha Waprotestanti katika siku zile za Luther, wakati Wakatoliki walipopaza sauti zao, wakisema, 'Mababa, Desturi, Mapokeo.' Siku hizi Waprotestanti wanaona ni vigumu kuyathibitisha mafundisho yao kutoka katika Biblia, hata hivyo, hawana ujasiri wa kimaadili kuweza kuipokea kweli ambayo inaambatana na msalaba; kwa hiyo, kwa kasi wanaufuata msimamo wa Ukatoliki.... Naam, Waprotestanti wa karne ya kumi na tisa wanakaribia kwa kasi kwa Wakatoliki katika kukosa uaminifu wao kuhusu Maandiko." RH, 6-1-1886, uk.338.



b. "Waprotestanti wa Marekani watakuwa mstari wa mbele katika kuinyosha mikono yao juu ya ghuba ili kuushika mkono ule wa Imani ya Mizimu; kisha watainyosha juu ya shimo kubwa lenye kilindi kirefu [bahari] kushikana mikono na Mamlaka ile ya Roma; hapo ndipo, chini ya uongozi wa muungano huo wa utatu [Uprotestanti, Umizimu, na Ukatoliki], nchi hii [ya Marekani] itafuata katika nyayo za Roma kwa kuikanyaga chini ya miguu yake haki ya mtu ya kuamini kama dhamiri yake inavyotaka." GC 588.



c. "Uprotestanti utakapounyosha mkono wake ng'ambo ya ghuba kuushika mkono wa Mamlaka ya Roma, utakapounyosha juu ya shimo kubwa lenye kilindi kirefu kushikana mikono na Imani ya Mizimu [toka Mashariki ya Mbali - India, China, n.k.], hapo ndipo nchi yetu [Marekani], chini ya uongozi wa muungano huo wa utatu, itakapokuwa imeikataa kila kanuni ya Katiba yake kama Serikali ya Kiprotestanti na ya Jamhuri, na kuiweka sheria inayotangaza uongo na adanganyo ya upapa, ndipo sisi tutaweza kujua ya kwamba wakati umewadia kwa utendaji wa miujiza ya ajabu ya Shetani na ya kwamba mwisho u karibu." 5T 451.



d. "Uprotestanti utaipa mkono wa ushirika Mamlaka ile ya Roma. Ndipo itapitishwa sheria dhidi ya Sabato ya Uumbaji wa Mungu, kisha ndipo Mungu naye atafanya 'kazi yake ya ajabu' katika nchi [ulimwengu]." 7BC 910.



e. "Taifa letu [la Marekani] litakapozikataa kanuni za serikali yake hata kuweza kutunga Amri ya Jumapili, kwa tendo hilo Uprotestanti utakuwa umeshikana mikono na Upapa...." 5T 712.



7. Je, Upapa hatimaye utakuwa na nguvu kiasi gani hapa Amerika?

"Waprotestanti... wanafungua mlango kwa upapa katika Amerika ya Kiprotestanti ili upate kushika tena hatamu zake za utawala ambazo umezipoteza katika Ulimwengu ule wa Zamani [Ulaya - tangu 1798]." GC 573.



8. Ni nani atakayewaongoza watu hao watakapoungana ili kuwapinga wafuasi wa Mungu?

"Tunapoikaribia hatari kubwa ile ya mwisho, ni jambo la maana sana kwetu sisi kwamba amani na umoja viwepo miongoni mwa vyombo vya Bwana. Ulimwengu umejawa na dhoruba na vita na ugomvi. Hata hivyo, chini ya kiongozi mmoja ---- Mamlaka ya Kipapa ----- watu wataungana kumpinga Mungu kwa njia ya mashahidi wake. Muungano huo umeimarishwa kabisa na yule
Mwasi Mkuu [Shetani]." 7T 182.



9. Kusema kweli, ni nani hasa anayesimama nyuma ya Papa?

"Mmoja amesondwa kidole katika unabii kuwa ni mtu wa dhambi (kuasi). Yeye ndiye mwakilishi wa Shetani.... Hapa yupo mtu aliye msaidizi mkuu wa Shetani, aliye tayari kutekeleza kazi ile aliyoianzisha Shetani kule mbinguni, ya kujaribu kuirekebisha sheria ya Mungu [AmriKumi]. Na ulimwengu huo wa Kikristo umeziunga mkono juhudi zake kwa kumpokea mtoto huyo wa Upapa ----- yaani, amri hiyo ya Jumapili." 7BC 910; RH, 3-9-1886, uk. 146.



10. Je, tungekuwa tukifanya nini sasa, ili kukabiliana kwa ufanisi na upinzani wa jamii hiyo iliyoungana pamoja ya Mataifa hayo ya Kikristo?

"Ulimwengu wote uko kinyume nasi, makanisa yale yanayopendwa sana na watu yako kinyume nasi, sheria za nchi hivi punde zitakuwa kinyume nasi. Kama ulipata kuwako wakati ambapo watu wa Mungu wangeshikamana kwa karibu sana, ni sasa." 5T 236.




USTAARABU NA USHENZI

DO NOT GIVE UP.
THE BIGINNING IS ALWAYS THE H a r D e s t.


Hamuwezi kupata mnayoyataka mpaka muache mnayotamani,
wala kupata mnayotarajia mpaka muwe na subira ktk vile mnavyovichukia.

Jumanne, Februari 07, 2012

UTIMILIZO HALISI



Sasa mbele yetu tunayo orodha ya tabia maalum tisa, ambazo zimetolewa toka katika sura ya saba ya Danieli, ili kuifafanua pembe ile ndogo. Kuna mamlaka moja tu katika historia yote ambayo inapatana kabisa na maelezo yaliyotolewa hapa. Kwa shida mno ishara yo yote katika hizo inaweza kutumika kwa mamlaka nyingine, isipokuwa ni UPAPA peke yake. Kanisa Katoliki peke yake linatimiza mambo yote yanayoitambulisha pembe hiyo ndogo ambayo yametajwa katika Danieli 7. Hebu na tuangalie kwa haraka na kuona kwa wazi jinsi jambo hilo linavyotekelezwa.



KWANZA kabisa, UPAPA ulitokea katika eneo la Ulaya Magharibi, katikati kabisa ya eneo la Dola ya Rumi ya Kipagani ----- katika RUMI yenyewe.



PILI, ulizuka baada ya mwaka 476
B.K. wakati Mfalme Justinian alipomteua Papa kuwa mtawala wa KISIASA na wa KIROHO wa ulimwengu wote. Haya ni mambo ya kweli ya historia ambayo yanaweza kuhakikishwa Kutoka katika chimbuko la mamlaka yo yote ile ya kihistoria.



TATU, Upapa ulipotokea ulipingwa na makabila matatu ambayo yalikuwa yametawala baada ya kuangushwa kwa Dola ya Kirumi. Wavandali (Vandals), Waostrogothi (Ostrogoths), na Waheruli (Heruli) walikuwa ni mamlaka zenye imani ya Arius (Arian powers) ambao kwa Nguvu zao zote walipinga kuzuka kwa Kanisa Katoliki. Majeshi ya Warumi yakayang'oa kabisa na kuyaangamiza makabila hayo matatu. La mwisho katika hayo matatu liliangamizwa katika mwaka ule ule wa 538 B.K., wakati RUMI YA KIPAPA ilipoanza kutawala dunia.



NNE, Katika mfumo wake, Kanisa Katoliki lilikuwa na MTU akiliongoza.



TANO, Upapa ulikuwa ni UFALME ULIO TOFAUTI na falme zile nyingine za kisiasa zilizoutangulia. Ulikuwa ni MAMLAKA YA KIDINI NA KISERIKALI ambayo iliitawala dunia yote. Hakuna mamlaka iliyofanana kabisa na hiyo ambayo ilipata kuonekana ulimwenguni kabla ya wakati ule.



Sasa tunaiangalia tabia yake ya SITA ----- ile ya kunena maneno makuu na makufuru dhidi yake Aliye juu. Je, Upapa unatimiza maelezo hayo? Tunahitaji tu kukumbushwa Kwamba Kanisa Katoliki limejitwalia lenyewe UWEZO WA KUSAMEHE DHAMBI. Kuhusu maneno yake makuu, hebu ninukuu kutoka katika makala ya F. Lucii Ferraris, iliyo katika kitabu cha PROMPTA BIBLIOTHECA CANONICA JURIDICA MORALIS THEOLOGICA. Kitabu hiki kilichapishwa mjini Roma, na kimeidhinishwa na ensaiklopidia ya Kikatoliki. Sikiliza madai haya: "Papa ni mkuu mno, naye ametukuzwa sana, kiasi kwamba yeye si mtu tu, bali kama ilivyo, yeye ni Mungu na Aliye Badala ya Mungu (Vicar of God). Kama ilivyo, PAPA NI MUNGU DUNIANI. Mfalme mkuu wa wafalme, mwenye uwezo mwingi." Gombo la VI, uk.25-29. Haya ni maneno machache tu ambayo Biblia inasema kuwa ni makufuru. UPAPA unatimiza ishara zote za utambulisho na
hivyo kuwa ile PEMBE NDOGO.



Sasa tunakuja kwenye kitambulisho cha SABA, tunaona ya kwamba HISTORIA inaunga mkono unabii huu kuhusu MATESO YA PAPA. Kila mmoja anayejua habari za Kizazi kile cha Kati (Middle Ages) Zama za Giza anafahamu fika ukweli kwamba mamilioni ya watu waliteswa kikatili mno na kuuawa na Mahakama Maalum za Kikatoliki (Inquisitions). Kutoka katika kitabu kilichoandikwa na Kadinali wa Kikatoliki, ambacho pia kimeidhinishwa na Kanisa Katoliki, tunasoma hivi: "Kanisa Katoliki... lina hofu kuu ya kumwaga damu. Hata hivyo, linapokabiliwa na UZUSHI HERESY... LINALAZIMIKA KUTUMIA NGUVU, kutoa adhabu ya kupigwa viboko mwilini, na KUTESA. Linaunda mahakama kama ile ya Inkwizisheni (Inquisition).



Linatumia SHERIA ZA SERIKALI kulisaidia... Lilifanya hivyo hasa katika karne ile ya 16 kuhusiana na WAPROTESTANTI... Katika nchi ya Ufaransa, chini ya wafalme Francis I na Henry II, katika nchi ya Uingereza chini ya Malkia Mary Tudor, Kanisa Katoliki liliwatesa wazushi." Maneno haya yamenukuliwa kutoka katika kitabu cha 'THE CATHOLIC CHURCH, THE RENAISSANCE AND PROTESTANTISM', uk.182-184. Tunaweza kuongeza semi nyingi kama hiyo kutoka kwa wanahistoria, Wakatoliki na Waprotestanti, zinazoelezea MATESO YA KUTISHA ya mamlaka ya kipapa juu ya Waprotestanti. Kwa njia hiyo tunaweza kuona utimilizo kamili wa maelezo haya ya pembe ndogo. 

Ishara ya NANE, kama ilivyotolewa katika fungu la ishirini na tano, inahusu jaribio lile la kubadili Sheria ya Mungu Amri Kumi. Je, jambo hilo linahusika na Upapa?



Tafadhali zingatia haya: Kanisa Katoliki limeondoa Amri ya Pili kutoka katika vitabu vyake vya mafundisho ya dini na Katekisimu zake, kwa sababu inashutumu IBADA YA SANAMU. Kisha Amri ya Kumi imegawanywa sehemu mbili ili waendelee kuwa na Amri Kumi. Walakini mbili zinakataza KUTAMANI, na hakuna hata moja inayokataza IBADA YA SANAMU. Kwa njia hii, Upapa UMEAZIMU UMEFIKIRIA kubadili Sheria ya Mungu, lakini bila mafanikio. SHERIA YA MUNGU HAIWEZI KUBADILISHWA

Mwishowe, tunakuja kwenye ishara ile ya TISA ya kitambulisho chake, ambayo inatuambia hasa muda ambao mamlaka hii ya Upapa ingeyatumia mamlaka yake juu ya dunia hii. Tuligundua kwamba ingetawala kwa miaka 1260.



Je, jambo hilo linakubaliana na kumbukumbu za historia? Kumbuka, ya kwamba tumeona jinsi Upapa ulivyoanza utawala wake, kwa amri ya Justinian, katika mwaka wa 538 B.K.. Tukihesabu kuja upande wetu miaka 1260 kuanzia mwaka huo tunaletwa kwenye mwaka wa 1798. Katika mwaka uo huo Jenerali wa Kifaransa, Berthier, aliongoza majeshi yake kuingia mjini Roma na kumng'oa Papa Pius wa VI Kutoka kwenye kiti chake cha enzi. Alichukuliwa uhamishoni, na mali zote za Kanisa zikataifishwa zikanyang'anywa. Uongozi wa Serikali ya Kifaransa ulitoa amri kwamba pasingekuwa na Askofu mwingine wa Roma kamwe. Kwa kadiri ulimwengu ulivyohusika, na kwa mwonekano wa nje, Kanisa Katoliki lilikuwa limekufa. Baada ya miaka 1260 kamili, kwa kutimiza unabii huu, likapoteza utawala wake juu ya dunia hii. Hivyo pointi hii ya mwisho imetimizwa kwa wazi kabisa katika Upapa, na katika Upapa peke yake.

Kuthibitisha na kujionea maelezo zaidi ya haya click HAPA

Jumatatu, Februari 06, 2012

YALIYOJIRI WEEKEND HII 105.3 FM

 USHINDI SDA YOUTH CHOIR - HAWA VIJANA NINAWAPENDA SANA.

UMOJA NA NIDHAMU NI NGUZO YA KUFIKIA MALENGO KWA USHINDI SDA YOUTH CHOIR

MTANGAZAJI MADUHU NA MTAYARISHAJI YUSUPH MCHARIA

MTANGAZAJI MADUHU NA MTAYARISHAJI YUSUPH MCHARIA

TEMEKE SDA CHOIR LIVE 105.3 FM

ILIKUWA NI SIKU YA PEKEE HASA TEMEKE SDA CHOIR WALIPOKUWA LIVE 105.3 FM

TEMEKE SDA CHOIR - WAKIFANYA VITU LIVE 105.3 FM

NINAWAPONGEZA TEMEKE SDA CHOIR KWA MAAMUZI YA KUTUMIA ACAPPELLA TU.

TEMEKE SDA CHOIR LIVE 105.3 FM


MTAYARISHAJI YUSUPH MCHARIA

BUSY BEE QUARTET - ACAPPELLA SINGING GROUP LIVE 105.3 FM

MTAYARISHAJI



********************


JAPO PICHA HAZINA UBORA, HATA HIVYO NIA YANGU NI KUKUFAHAMISHA KUWA:

Waimbaji wa Wyimbo za Injili Wanatakiwa Kujitambua Kwamba Wao ni Watumishi wa MUNGU na Kazi Kubwa Waliyonayo ni Kuhakikisha Kuwa Jamii Inabadilika na sio Kuiburudisha.









Jumamosi, Februari 04, 2012

MAJIBU YAFANYANYAYO KAZI....MIBARAKA YA KUTUCHANGAMSHA







Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako ulizowawekea wakuchao; 
Ulizowatendea wakukimbiliao mbele ya wanadamu! Zaburi 31:19.



 
Mungu anaimwaga mibaraka yake katika njia yetu yote ili kuifanya safari yetu iwe ya
furaha na kuiongoza mioyo yetu kumpenda na kumsifu, Naye anatutaka sisi kuteka maji
yetu katika visima vya wokovu ili mioyo yetu ipate kuburudika. Twaweza kuimba
nyimbo za Sayuni, twaweza kuichangamsha mioyo yetu sisi wenyewe, tena twaweza
kuichangamsha mioyo ya wengine; tumaini letu laweza kuimarishwa, na giza kugeuzwa
kuwa nuru. Mungu hajatuacha sisi katika ulimwengu huu wa giza ----- kama wasafiri na
wageni watafutao nchi iliyo bora, ile ya mbinguni ----- pasipo kutupa sisi ahadi zake za
thamani ili kuufanya kila mzigo mzito tuliobeba kuwa mwepesi. Kingo za njia yetu
zimepambwa kwa maua mazuri ya ahadi zake. Yanachipua pande zote yakitoa harufu
nzuri sana. ----- Letter 27, 1886.

Ni mibaraka mingapi tunayoipoteza kwa sababu tunaidharau na kuipuuza kutoitilia
maanani mibaraka tunayopokea kila siku, tukiitamani sana ile ambayo hatunayo kwa
sasa. Fadhili za kawaida ambazo zinamwagwa huku na huko katika njia yetu
zinasahaulika na kuthaminiwa kidogo tu. Twaweza kujifunza mengi kutoka kwa vitu vya
kawaida katika viumbe vya asili. Ua lililo mahali penye giza na palipo duni hupokea
mwanga wote linaoweza kuupata, na kutoa majani yake. Ndege aliyefungiwa katika
kitundu anaimba katika kitundu cha gereza lake, ndani
ya nyumba zisizopata mwanga wa jua, kana kwamba yuko katika jengo la kimwinyi,
lenye mwanga wa jua. Mungu anajua iwapo sisi tutaitumia mibaraka yake kwa hekima na
kwa vizuri; kamwe hataweza kutupatia mibaraka hiyo ili tupate kuitumia vibaya.
Mungu anaupenda moyo wenye shukrani, unaoyasadiki kabisa maneno yake yenye ahadi,
ukijikusanyia faraja na tumaini na amani kutokana nayo; Naye atatufunulia sisi vina
virefu zaidi vya upendo wake. ----- RH, Aprili l2, 1887.
  
  

Endapo tungelisifu jina takatifu la Mungu kama ipasavyo, basi, mwali wa moto wa
upendo ungewashwa ndani ya mioyo mingi.... Sifa kwa Mungu inapaswa kuwa mioyoni
mwetu daima na vinywani mwetu. Hii ndiyo njia iliyo bora sana ya kulipinga jaribu lile
la kushiriki katika maongezi yasiyofaa na ya upuuzi. ----- Letter 42, 1900.

Bwana angependa sisi tuwe tunatazama juu, na kuwa na shukrani kwake kwamba
mbingu iko.... Hebu na tuzishikilie sana kwa imani hai ahadi nyingi sana za Mungu, na
kuwa na shukrani kuanzia asubuhi mpaka usiku. ----- RH, Aprili 12, 1887.

********************************
Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...
(Namaanisha JumaMosi)

Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo

Miami Temple Seventh-day Adventist Church

Inapotuletea: Divine Service - Sermon 10-22-11





SABATO NJEMA MKUU



Jumatano, Februari 01, 2012

Katika historia zilitokea.

Tufahamu kwamba, utumwa ni mfumo unaotoa fursa kwa binadamu kummiliki binadamu mwenzake kama mali yake. Binadamu anayemilikiwa anakuwa na hadhi sawa na chombo au kifaa chochote kinachoweza kuuzwa. Mfumo huu ulikuwa maarufu kabla ya harakati za ukoloni duniani mathalani karne ya 15 ambapo watumwa walihitajika katika shughuli za kilimo na uchimbaji madini katika sehemu mbalimbali za ulimwengu. Mfumo huu huunda matabaka ya "mabwana" ambao humiliki watumwa na "watwana" ambao ni watumwa wenyewe. Kwa nini nakwambia haya? Hebu endelea kusoma hapo chini

Kuna utumwa tofautitofauti, kivipi:


Katika historia zilitokea. Kulikuwa na utumwa wa muda (yaani mtu huwa mtumwa kwa miaka kadhaa) au kwa maisha yote. Kulikuwa na utaratibu ambako watoto wa mtumwa walikuwa watumwa tena hivyo kuzaliwa watumwa; kulikuwa pia na utaratibu ya kwamba watoto wa watumwa walitazamiwa kama watu huru.

Kulikuwa na jamii ambako watumwa hawakuwa na haki kabisa yaani mabwana waliweza kuwatendea jinsi walivyotaka (vyovyote vile utavyojisikia kutenda) hata kuwaua lakini kulikuwa pia na jamii zilizojua haki fulani za watumwa; watumwa waliweza kuwa na mali ya binafsi na kwa njia hii hata kununua uhuru wao kutoka kwa mabwana. Watumwa katika utumishi wa watawala waliweza kupata nafasi muhimu katika jamii; mfano ni wamameluki wa Misri waliokuwa watumwa wanajeshi wakatawala nchi hii kwa karne kadhaa…hizi habari ukuzifuatilia zinauma!!!

Chanzo cha utumwa

Ni hivi; kilikuwa yaani kutokana mara nyingi ama vita ama madeni. Vitani wafungwa wakauzwa kama watumwa wakihesabiwa kama sehemu ya uwindo wa washindi. Sababu kuu nyingine ilikuwa madeni ya watu waliokamatwa na kuuzwa ili madeni yalipiwe kwa njia hii. Mahitaji wa kiuchumi kwa watumwa wengi yalisababisha biashara ya watumwa.


Biashara ya watumwa ni nini sasa:


Msomaji wangu!!, biashara ya watumwa ni biashara inayohusu watumwa yaani watu wasio huru wakitazamiwa kuwa mali ya wengine. Katika historia ilitokea mara nyingi. Uchumi wa Roma ya Kale ilitegemea watumwa waliokamatwa na kusafirishwa kati ya pande zote za mazingira ya Bahari Mediteranea. Milki za makhalifa wa Uislamu ziliendelea kutegemea watumwa. Waosmani walichukua watoto wa kikristo kutoka nchi za Balkani na kuwapeleka kama watumwa katika sehemu za kusini za milki yao kama Misri walipofanya kazi za wanajeshi.

Mahitaji ya uchumi wa kimataifa tangu karne ya 15 yalisababisha kuongezeka kwa biashara ya watumwa hasa kutoka Afrika; mamilioni walikamatwa na watawala wa milki kwenye pwani za Afrika na kuuzwa kwa wafanyabiashara wazungu waliowapeleka Amerika walipohitajika kwa kazi kwenye mashamba makubwa ya miwa na pamba,,, hebu piga picha.

Biashara hii ilianza kupingwa tangu mwisho wa karne ya 18; Mkutano wa Vienna (1814-15) ilikuwa na nia na ndio chanzo cha mapatano ya kwanza ya kimataifa yaliyolenga kukataa biashara ya watumwa kutoka Afrika. Hata hivyo yaliendelea kwa miaka kadhaa hasa upande wa bahari Hindi ambako wafanyabiashara kama Tippu Tip waislamu waliendelea kukamata watumwa na kuwapeleka pwani.

Ukoloni ulimaliza biashara hii pia kwa njia gani.


Tangu karne ya 20 utumwa na pia biashara ya watumwa zimepigwa marufuku katika mapatano ya kimataifa chini ya usimamizi wa Umoja wa Mataifa (japo haijaisha). Lakini miaka za nyuma imeona biashara mpya inayotumia nafasi za usairi wa kisasa; hata kama hakuna utumwa kisheria tena duniani ni hasa wanawake na mabinti wanaouzwa kwa kazi haramu ya ukahaba kati ya nchi na nchi.


Utumwa Kiroho.


Nabii Isaya anaagua neno hili la Mungu wakati Waisraeli wako utumwani. Wana mashaka na wanamlalamikia Mungu maana muda unapita na Mungu hatekelezi ahadi yake. Hatimaye Mungu anaibua kati yao, nabii Isaya awatie moyo akiwakumbusha kuwa ahadi za Mungu ni za milele, hazibadiliki. Anawafundisha kwa kutumia mfano wa mvua inyeshayo kuwa mara inyeshapo hairudi angani bali hurutubisha ardhi ili iweze kuzaa matunda. Kumbe ahadi ya Mungu ya kuwatoa katika utumwa wa kiroho na kimwili haitasimama kamwe na wala haibadiliki. Ndiyo kusema, neno la Mungu tulilolipokea halitarudi bure bali litazaa matunda.