Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumapili, Desemba 23, 2012

ASILI NA HALI YA MAISHA YA KIBAIOLOJIA

Photo Credit By: http://www.smithsonianmag.com

Kufanya kazi kwa abayojenesisi hakueleweki kwa ufasaha: nadharia mashuhuri ni pamoja na nadharia ya dunia ya RNA (vitoaji aina sawa katika makao ya RNA) na nadhari ya dunia ya chuma-sulfuri (umetaboli bila Jenitiki). Nadharia ya mabadiliko ya viumbe haijaribu kuelezea asili ya maisha bali utaratibu ambao viumbe tofauti vimepitia katika kipindi chote cha historia kupitia mabadiliko ya ghafla ya kijenitiki na uteuzi wa kiasili.  

Wakati wa mwisho wa karne ya 20, kwa kuzingatia ufahamu kutoka mtazamo wa mbadiliko wa viumbe unaotegemea jeni haswa, wanabaiolojia George C. Williams, Richard Dawkins, David Haig, miongoni mwa wengine, wanahitimisha kwamba ikiwa kuna kazi msingi ya maisha, ni kujinakilisha kwa DNA na kuendelea kuwa hai kwa jeni za mtu. 


Hata hivyo, ingawa wanasayansi wameyachunguza maisha vilivyo Duniani, kuyafafanua maisha kibayana bado ni changamoto. Kimwili, mtu anaweza kusema kwamba maisha "hula entirofi hasi"  ambayo inahusu utaratibu ambao waliohai wanapunguza entirofi yao ya kindani kwa gharama ya aina fulani ya nishati inayochukuliwa ndani kutoka mazingira.


Wanabiolojia kiujumla wanakubaliana kwamba viumbe mbalimbali ni mifumo inayojipanga yenyewe inayosimamia mazingira ya ndani ili kudumisha hali hii ya mpango, shughuli za kimetaboliki hutumika kutoa nishati, na uzazi unaruhusu maisha kuendelea kwa vizazi vingi. Kawaida, maumbile huwa sikivu kwa uchochezi na habari za kijenitiki huelekea kubadilika kutoka kizazi hadi kizazi ili kuruhusu marekebisho kupitia mabadiliko ya kimwili, hizi sifa huongeza nafasi ya kuishi ya kiumbe binafsi na wazao wake kwa mtiririko huo. 

Viwakala visivyokuwa vya seli vinavyozaana, hasa virusi, kwa ujumla si havitazamwi kama viumbe kwa sababu haviwezi kuzaana kwa "kujitegemea" au kuendeza shughuli za kimetaboliki. Pambano hili ni tatizo, ingawa, baadhi ya vimelea na visimbayonti vya ndani ya mwili pia vinaweza kuishi maisha ya kujitegemea. Astrobaiolojia inajihusisha na masomo ya uwezekano wa kuwa na aina tofauti ya viumbe vyenye uhai katika ulimwengu mwingine, kama vile miundo ya kujinakilisha kutoka vifaa vingine visivyo DNA.