Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Agosti 11, 2014

HISIA YA SITA


Naomba 'kushea' nawe kitu kinachojulikana kama TELEPATHY. Kwa kifupi, telepathy ni uwezo wa kuwasiliana na mtu mwingine bila kutumia hisia 5 za kawaida (kugusa, kuongea, kuona, kunusa au kusikia). Katika familia, walio na mapacha watakuwa wananielewa Kulwa  na Doto. 

 Kuna matukio mengi ya telepathy kuwahusu mapacha hao lakini nafasi hairuhusu kuyataja yote. Lakini si kwa mapacha tu.Mara nyingi kama upo mbali halafu msiba unatokea, kina uwezekano wa kuota ndoto inayohusiana na msiba usiku wa mkesha wa tukio hilo. Hiyo ni telepathy ya aina flani. 

Pia mara kadhaa unaweza kumfikiria mtu flani na muda huohuo akakupigia simu au kukutumia meseji. Hiyo pia ni telepathy. Au unaweza kutamani kuwasiliana na mtu flani, na ukicheki emails zako unakuta amekuandikia. Japo hakuna maelezo ya moja kwa moja kuhusu telepathy, inafahamika kuwa mtu anaweza kujifunza na kuboresha uwezo wake wa telepathy kwa kutumia meditation (sijui neno la Kiswahili ni nini). 

Mashushushu (spies) hufunzwa kuendeleza kitu kinachojulikana kama 'hisia ya sita' yaani zaidi ya hisia tano za kawaida nilizozitaja hapo juu. Hisia ya sita ambayo ni kama telepathy kwa namna flani huwawezesha kubashiri mambo karibu kabisa na usahihi. Lakini kama nilivyobainisha, hata mtu wa kawaida pia aweza kujifunza...lakini madhara yake ni pamoja na kufahamu matukio yatayojiri mbeleni bila kuwa na uwezo wa kuyazuwia. Anyway, I thought I should share with you about this interesting phenomenon.

Jumamosi, Agosti 02, 2014

MSAADA WA MAANA



Kwa sababu hiyo tunapaswa kutafuta majina tofauti kwa makala zinazohusu maana tofauti ya jina lilelile.

Mfano wa makala ya maana kuhusu "Mwezi"
Makala ya maana inakusanya maana hizi zote kwenye ukurasa wa pamoja. Haina maandishi marefu bali maelezo mafupi tu mfano: .

  1. mwezi (gimba la angani) - msindikizaji wa sayari
  2. mwezi (wakati) - mojawapo wa vipindi kumi na mbili vya mwaka
Vivyo hivyo:

  1. Ndege (mnyama) - aina wa wanyama ambao kwa kawaida wanaweza kuruka
  2. Ndege (uanahewa) - chombo cha usafiri kinachoweza kuruka wakati kikiwa na abiria au mizigo ndani yake
Isipokuwa kama maana mbalimbali yana historia ya pamoja au uhusiano wa pekee ni sawa kuongeza chini ya orodha ya viungo maelezo ya ziada. Zisihusu viungo moja-moja. Mfano:

Majengo inataja mahali pengi Afrika ya Mashariki kwa hiyo tunatofautisha Majengo (Kigoma), Majengo (Mbeya mjini) na kadhalika. Mitaa au kata hizi zote zina historia ya kufanana inayoelezwa chini ya orodha.