Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Mei 25, 2016

MCHUCHUMIO (HIGH HEELS)


Wengi hawafahamu kuwa ni Viatu hatari kwa afya ya miguu ya wanawake japo pia wapo wanaofahamu hilo ila wanakaidi tu. ‘Mchuchumio’ ama viatu vyenye visigino virefu, ni mojawapo ya vitu vinavyopendwa na baadhi ya wanawake mbalimbali, si katika Tanzania bali dunia nzima.

Wataalamu wanaeleza kuwa viatu hivi huharibu pingili za uti wa mgongo na huvunjavunja mifupa ya visigino. Wanawake wenye maumbo ya kati, ambao si wanene wala wembamba wamekuwa wakipendelea viatu virefu. Kwa kiasi kikubwa wasichana wafupi, wamekuwa wakipendelea kuvaa viatu virefu ili angalau na wao waonekane warefu ingawa vinawatesa.

Kuna maelezo yanayosema kuwa viatu virefu vinaharibu visigino na misuli ya miguu na kutengeneza vigimbi ambavyo baadaye husababisha maumivu makali. Wasichana wengi wanafahamu ‘mchuchumio’ husababisha maumivu makali lakini je, ndiyo kutimiza usemi wa ukitaka uzuri shurti udhurike? Kwa kawaida, urembo hauwezi kusababisha maumivu, lakini kuvaa viatu virefu kuna athari kubwa.

Utafiti mbalimbali unaonesha kuwa viatu virefu havifai hata kidogo. Kimsingi, uvaaji wa viatu virefu husababisha maumivu makali ya misuli ya miguu pamoja na nyama za nyuma kwenye maungio ya magoti na enka. Uharibifu ni mkubwa pia huweza kutokea ndani ya magoti kwa kuhamisha maungio (dislocate). Kwa jinsi mhusika anapovaa viatu virefu kwa muda mrefu, ndipo inaposababisha madhara ya muda mrefu.



Mbali na hayo, vilevile, husababisha mwili kukosa usawa wakati wa kutembea, misuli ya miguu kubana, kupoteza mwelekeo wa mwendo halisi na wakati mwingine husababisha mhusika kuanguka na kumsababishia maumivu makali. Katika uchunguzi uliochapishwa kwenye jarida la Journal of Applied Physiology, Dk Cronin anasema wanawake wengi waliofanyiwa utafiti wamebainika kutokuwa imara katika miguu yao, kupatwa na maumivu makali na kuharibiwa misuli na enka ya mguu.

Naye Dk Orly Avitzur, Mganga Mshauri kwenye kitongoji cha Tarrytown, New York, Marekani anasema kuwa alifanya utafiti kwa wanawake wa zaidi ya miaka 40 kuwa hawawezi kuvaa viatu virefu kwa kuwa miguu yao tayari imeharibiwa. Katika uchunguzi uliochapishwa kwenye jarida la Journal of Applied Physiology, Dk Cronin anasema wanawake wengi waliofanyiwa utafiti wamebainika kutokuwa imara katika miguu yao, kupatwa na maumivu makali na kuharibiwa misuli na enka ya mguu.

Mtaalamu wa Mifupa katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam, Dk Edemeza Machange alieleza kuwa matatizo ni makubwa kwa mtumiaji wa viatu virefu na athari zaidi huwakumba wanawake wanene. “Ni mbaya sana…kwa wanawake wanene haishauriwi watumie viatu virefu kwa kuwa vitawaletea matatizo mengi katika miili yao,” anasema.

“Kwa kawaida mtu anapoteza mwendo halisi, sasa kutotembea kwa mpangilio, huharibu mfumo wa pingili za mgongo, hata kiuno na kusababisha maumivu makali”. Anawashauri kinamama hasa wasichana, wafahamu kuwa pamoja na kutaka urembo, lazima wajali afya zao kwa kuvaa viatu virefu katika kipindi kifupi na zaidi ni kuangalia madhara kwa baadaye kuliko kukimbilia kuvaa viatu virefu kwa ajili ya urembo.

Chanzo: Mwananchi

Jumanne, Mei 24, 2016

Kichwa cha Kigogota Kinachohimili Mshtuko

Photo Credit By: www.popsci.com
 

Msukumo unaozidi nguvu za uvutano kwa mara 80 hadi 100 unaweza kukufanya upoteze fahamu. Hata hivyo, kigogota anaweza kuhimili msukumo unaozidi nguvu za uvutano kwa mara 1,200 hivi anapopigapiga mti kwa mdomo wake. Ndege huyo anafanyaje kazi hiyo, bila kupoteza fahamu au hata kupata maumivu ya kichwa? 

Fikiria hili:  

Watafiti wamegundua sehemu nne za kichwa cha kigogota zinazofanya kichwa chake kiweze kuhimili mshtuko huo:

1. Ana mdomo wenye nguvu lakini unaonyumbulika
2. Ana kitu kinachoitwa hyoid kilichofanyizwa kwa mfupa na tishu inayoweza kutanuka kinachofunika fuvu la kichwa
3. Ana eneo fulani la mfupa ulio kama sifongo ndani ya fuvu
4. Ana nafasi ndogo kati ya fuvu na ubongo iliyo na umajimaji unaofanana na ule unaopatikana kwenye uti wa mgongo

Kila moja ya sehemu hizo huhimili mshtuko, na kumwezesha kigogota kuugonga mti mara 22 hivi kwa sekunde bila kuumiza ubongo wake.

Wakichochewa na muundo wa kichwa cha kigogota, watafiti wametokeza kifaa fulani kinachoweza kuhimili msukumo unaozidi nguvu za uvutano kwa mara 60,000. Huenda hilo likawawezesha kutokeza vifaa bora zaidi kutia ndani, vile vinavyolinda vifaa vya kurekodia jinsi ndege inavyoruka, ambavyo kwa sasa vinaweza kuhimili msukumo unaozidi nguvu za uvutano kwa mara 1,000 tu. 

Kim Blackburn, injinia katika Chuo Kikuu cha Cranfield huko Uingereza, anasema kwamba mambo ambayo yamegunduliwa kuhusu kichwa cha kigogota yanatoa “mfano mzuri wa jinsi vitu vya asili vinavyoweza kutusaidia kutokeza miundo tata na pia kutatua mambo ambayo hapo awali yalionekana kuwa hayawezi kutatuliwa.”

Una maoni gani?  

Kichwa cha kigogota kinachoweza kuhimili mshtuko kilijitokeza chenyewe? 

Au kilibuniwa?

Gundi ya Mnyoo Anayeitwa Sandcastle



Photo Credit By: https://en.wikipedia.org/




Je, Ni Kazi ya Ubunifu?


● Madaktari wapasuaji huunganisha mifupa ilivyovunjika kwa kutumia pini, mabati ya aina fulani, na skrubu, lakini ni vigumu sana kutumia vifaa hivyo kuunganisha mifupa midogo. Watafiti wametatizwa kwa muda mrefu jinsi wanavyoweza kutokeza gundi inayoweza kunata ndani ya mwili wa mwanadamu ulio na umajimaji. Walipata suluhisho kwa kuchunguza mnyoo anayeitwa sandcastle!


Fikiria hili:  

Mnyoo huyo hujenga makao yake chini ya maji kutokana na mchanga na makombe. Kila chembe huunganishwa kwa kutumia gundi ambayo mnyoo huyo hutokeza ndani ya tezi fulani iliyo kifuani mwake. Gundi hiyo inanata kuliko gundi za kisasa zinazotengenezwa na wanadamu. Ina mchanganyiko fulani wa protini ambazo zinapounganishwa zinafanya gundi hiyo ishikamane upesi sana chini ya maji! Mnyoo huyo amesemekana kuwa mwashi stadi, na inafaa sana kwamba anaitwa hivyo. Russell Stewart, wa Chuo Kikuu cha Utah, anasema kwamba mnyama huyo mdogo amesuluhisha “tatizo tata sana kuhusu gundi.”

Watafiti wametokeza gundi kama ya mnyoo huyo ambayo inanata kwa nguvu zaidi kuliko hata ya mnyoo huyo. Gundi ambayo mwishowe itatumiwa katika upasuaji inapaswa kuwa na uwezo wa kuoza ili inapotumiwa kuunganisha mifupa iliyovunjika, iweze pia kuyeyuka mfupa unapopona. Iwapo gundi hiyo itawasaidia wanadamu, bila shaka itakuwa ugunduzi muhimu wa kitiba.

Una maoni gani?  

Je, gundi ya pekee ya mnyoo anayeitwa sandcastle ilijitokeza yenyewe? 

Au ilibuniwa?

Watafiti wanatumaini wataweza kurekebisha mifupa iliyovunjika bila kutumia vifaa vya chuma

Sandcastle worm: © Peter J. Bryant, University of California, Irvine