Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Februari 19, 2008

UNAMKUMBUKA?

Sophia na Michael Kuyenga wakiandaa taarifa huko St Louis Marekani

Je wakumbuka kuwa mwaka 2005 AWR iliwapeleka Watangazaji wa AWR Sophia na Michael Kuyenga , huko St Louis, Missouri, nchini Marekani kwa ajili ya kuripoti matukio yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano Mkuu wa halmashauri kuu ya kanisa la Waadventista Wasabato duniani.

Michael Kuyenga ambaye kwa sasa ni Afisa Uhusiano wa Chuo Kikuu cha Arusha kinachomilikiwa na Kanisa la Waadvetista Wasabato Tanzania kilichoko Ngongongare,Usa River,Arusha alifanya kazi kubwa akishirikiana na AWR,Marekani kuhakikisha kuwa taarifa za mkutano huo zinawafikia wasikilizaji wetu kwa lugha ya kiswahili kila siku kwa muda usipungua siku 10.

Bofya hapa;

http://awr-swahili.blogspot.com/

Former Presdents


KAMPENI CCM

Dj wa Kike Clouds


Moja kati ya ma-Dj wachache sana hapa nchini ! Ni huyu Dj Fetty wa clouds Fm 88.4 akifanya mamboz Ma-Scrching ya kuajabisha ! Ki ukweli ni moja ya Dj anaeonekana kuja juu sana kwa kasi ya ajabu sana ktk fani hii ya U-Dj.

PICHA YA WIKI


Picha ya wiki hii ni ya huyo binti wa miaka kumi(10) anayeitwa Violet Sastoni kutoka kikundi cha burudani,sanaa na maonyesho kinachoitwa Splended cha jijini Dar-es-salaam.Violet alikuwa akifanya vitu hivi ndani ya kijiji cha Makumbusho jijini Dar juzi wakati wa wa tamasha lililoitwa Ya Kale Yanapokutana na ya Kisasa.Hii ndio picha ya wiki hii.Imepigwa na Ahmad Michuzi.

ORIGINAL FIRST LADY


Original First Lady,Mama Maria Nyerere,mke wa Rais wa kwanza wa Tanzania,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Kabla ya kuolewa na Mwalimu Nyerere alijulikana kwa jina la Maria Gabriel Magige.Alifunga ndoa na Mwalimu tarehe 24,Januari mwaka 1953.

Kp Leo


MAMBO YA IVOR COAST


Kina dada wa pwani ya pembe ambao kwa mujibu wa mchapo wa BBC shughuli huko ni pevu.Endeelea kwa wakati wako hapa;

http://news.bbc.co.uk/2/hi/africa/7233565.smt

Jumapili, Februari 17, 2008

10 THINGS GOD WON'T ASK


  1. God won't ask what kind of car you drove.He'll ask how many people you drove who did'nt have transpotation.
  2. God wont ask the square footage of your house.He'll ask how many people you wellcomed into your home.
  3. God wont to ask about the clothes you hard in your closet,H'll ask how many you helped to clothe.
  4. God wont ask what you highest salary was.He'll ask if you you compromised your character to obtain it.
  5. God wont ask what your job title was.He'll ask if you performed your job to the best of your ability.
  6. God wont ask how many friends you had.He'll ask how many people to whom you were a friend.
  7. God wont ask in what neighborhood you lived.He'll ask how you treated you neighbors.
  8. God wont ask about the color of you skin.He'll ask about the content of your character.
  9. God wont ask why it took you so long to seek Salvation.He'll lovingly take you to your mansion in heaven,and not to the gates of Hell.
  10. God wont have to ask how many people you forwarded this to.He already knows your decision.

EE BWANAEEEE!!!

THE VOICE


The Greatest Acapella Group in Tanzania.Ni kwa umoja na ushirikiano,japokuwa jitihada zaidi zimewapatia mafanikio ukweli ni kwamba asili ya kila kitu ni MUNGU pekee.Kwa ugumu ugumu tumetoka mbali,usidhani ni rahisi rahisi.Tuna shukuru sasa tupo hapa,bado tunasonga safari hatujafika.

SONDA YA DILU

Sonda ya Dilu ni jina kutoka katika kabila la wasukuma likiwa na maana ya "Nyota ya asubuhi"nao pia huimba nyimbo katika mtindo uitwao acapella style, ni uimbaji usiotumia ala ya aina yoyote.

THE FINAL TRUMPET


Haikuwa rahisi,
ingawa ilibidi iwe sawa na ilivyopangwa.

Hawa washkaji ndio wanaounda kundi hili,
dhamira yao ni kupeleka injili kwa njia ya uimbaji. Tangu mwanzo wao mpaka katika toleo hili la kwanza,maisha yamekuwa na sura mpya.
Jaribu kufanya kile moyo ulichotamani tangu ulipoanza.


Safari yao ya uimbaji wa muziki aina ya Acappella ilileta hamasa kwa vijana na wakaamka.
Ngoja nikudokezee majina yao kwa kila mmoja.


Nikianza na anaye onekana kuanzia kushoto kwako anaitwa ABIHUDI CHIKIRA. Anaemfuatia alieinua mkono wa kushoto ni Mtayarishaji na pia ni Mtangazaji wa Morning Star fm inayopatikana Dar es salaam Tanzania ktk Frequence 105.3 YUSUPH MCHARIA ("Dj Cartoon").

Mwenye shati lenye rangi nyeusi anaitwa MANASE RUSAKA nae ni miongoni mwa watangazaji wa Morning Star fm. Anaehitimisha safuu hii mwisho kulia kwako anaitwa MATHEWS SINGO.

Vijana hawa ukiwaona hakika wanadhihirisha kile MUNGU wanaemtumikia alichowapatia.
Jitahidi upate CD yao wanapatikana katika kanisa la Waadventista Wasabato Kinondoni jijini Dar es salaam Tanzania.

Alhamisi, Februari 14, 2008

NAAMINI NJIA HII


Matazamio na mafanikio, ubora na uhakika.
Siku pekee ya kufikia lengo, njia rahisi nikuwa na rafiki mwenye marafiki, kuishi kwa hakika.

Mambo yanakwenda sawa sawa kwa usawa upo???. Tizama jinsi maisha yanavyokuwa na furaha.

FRIENDS INTERTAINMENT/PRODUCTION
Rafiki wa marafiki! NAAMINI NJIA HII.
Siku yako kwangu imenipa zao.

Historia

Huyu ndiye hayati Oscar Kambona, mtangazaji aliyerusha matangazo ya kwanza ya Idhaa ya Kiswahili ya BBC tarehe 27 mwezi Juni mwaka 1957. Alifariki Uingereza akiwa na umri wa miaka 68.

GHASIA KENYA
































Kumekuwa na mafanikio kati ya mahasimu wa kisiasa - ikiwa na maana kwamba idadi ya vifo inaongezeka na watu wasiokuwa na makazi.

Ghasia hizo - ambazo kwa kiasi kikubwa zinawapambanisha watu wa jamii ya Kikuyu na Jaluo na

Mwezi mmoja baada ya matokeo ya uchaguzi kuzua mtafaruku, ghasia za kikabila zinaendelea kuizonga Kenya - hapa ni Naivasha kwenye bonde la ufa.Kalenjin ni mikasa ya kulipizana kisasi.

Baraza jipya la mawaziri

Shauku ya watanzania imetimia baada ya kusubiri kwa hamu kubwa kujua rais Jakaya Kikwete amewateua mawaziri gani katika baraza jipya na mawaziri gani wameachwa.

Baraza hilo jipya lilitajwa Jumanne adhuhuri katika Ikulu ndogo ya Chamwino mjini Dodoma.

Hatua hiyo imetokana na kuvunjwa baraza la mawaziri baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa huo kufuatia kuhusishwa kwenye kashfa ya Richmond Development, kampuni iliyoshinda zabuni ya kufua umeme wa dharura.

Kenya wajadili uwezekano wa serikali ya mseto

Aliyekuwa katibu wa umoja wa mataifa Kofi Annan amewaelezea wabunge wa Kenya kwa ufupi kuhusu maendeleo ya mazungumzo nchini humo yenye nia ya kutuliza mgogoro kufuatia uchaguzi wa rais.

Bw Annan aliwaeleza hayo kabla hawajahamia eneo la siri kuendeleza mazungumzo hayo.

Hakutoa taarifa zozote kwa waandishi wa habari lakini mwandishi kutoka BBC amesema kuwa huenda kukawa na mpango wa serikali ya mseto na uchaguzi mwengine kuitishwa mwakani.

Bw Annan amefutilia mbali wazo la kurudia kuhesabu kura na kuongeza kuwa nchi ya Kenya haiko tayari kwa uchaguzi mpya kwa sasa angalau baada ya muda wa mwaka mmoja kupita.

Watu wasiopungua 1000 wamefariki baada ya chama cha upinzani kutangaza kuwa kulifanyika hila katika uchaguzi huo.

Zaidi ya watu 600,000 wamelazimika kukimbia makazi yao kutokana na mapigano ya kikabila yanayoonekana kama wengine wanawaunga mkono upinzani na wengine serikali.

Nipo kando yangu,mahali pa tulivu,ng'ambo ya mto ububujishao ndege wanaimba,upepo tulivu unavuma,mwanga wapendeza kuona.Njiani sikati tamaa hakika safari nitafika.
Kimya moyo unasema,sawa na punda aimbaye.Panda itakapolia ni nani atakaye ningoja? Vazi safi harusini karamu karibu kuanza,safari hakika nitafika njiani sikati tamaaa.

Ndivyo mshkaji katika picha anavyojipa moyo,hebu fikiri kama ungekuwa ni wewe ng'ombe anakufukuza kwa namna ya aina yake ungefanyeje? kila unapokimbilia yeye yupo nyuma hapo jirani,mwisho wako unadhani ni nini? TAFAKARI.

Ijumaa, Februari 08, 2008

HAKUNA NJAAAAA


Keeeeeeeeeeeeeeeeeep GOING


There are people who always keep doing this to you . .
But be strong ... keep going anyway . . .

Sifa kwa Mungu


Mwimbieni Bwana wimbo mpya,na sifa zake tokea mwisha wa dunia;
Ninyi mshukao baharini,na vyote vilivyomo,Na visiwa,nao wakaao humo.
Jangwa na miji yake na ipaze sauti zao,Vijiji vinavyokaliwa na kedari;Na waimbe wenyeji wa sela,wapige kelele toka vilele vya milima.Na wamtukuze Bwana,
Na kutangaza sifa zake visiwani.
Bwana atatokea ka shujaaAtaamsha wivu kamamtu wavita;Atalia,naam,atapiga kelele;
Atawatenda adui zake mambo makuu.


Isaya 42:10-13

Dondoo za Uchumi

















Asilimia 60 ya biashara nchini zinafilisika kwa sababu watendaji wake wanaziendesha bila kuzingatia maadili.Wastani wa biashara mpya 65 kati ya 100 zinazofunguliwa,haziendelei licha ya kuwepo sababu za kiushindani,ukosefu wa mitaji,kufanyia sehemu zisizofaa na kutozingatia maadili.

Kampuni ya uwekezaji wa pamoja nchini NICOL itaelekeza nguvu zake za uwekezaji katika usindikaji wa bidhaa za kilimo viwandani kuanzia mwaka 2008.

Kampuni moja kubwa ya Malaysia ya Marrybrown inatarajia kufungua mgahawa wa kisasa Dodoma kuanzia april mwaka huu utakaogharimu dola za Marekani 500,000 (wastani wa Sh 596.5 million.

Jumatano, Februari 06, 2008

Hi Ndio Hakika



Ni sehemu tu,ninaamini kila kitu kilicho mbele yetu ni sehemu tu ya uhalisia uliotakiwa uonekane.Tuna upande usioonekana wa uhalisia.Kama vile hisia zetu na mihemko.tizama jinsi utakavyooanza safari kupitia njia hii kuanza.


Ni kweli kwamba tunajali sana vitu vilivyo nje yetu kwa kudhani kwamba hivyo pekee ndivyo vyenye kufanya uhalisia wa maisha.Vile vilivyo ndani tusivyoviona ndivyo ambavyo vinafanya maisha yawe na maana kubwa kuliko vile vilivyo nje yetu.