Mtayarishaji

Morning Star Radio

Alhamisi, Februari 19, 2015

UMASIKINI NI NINI?


Watu tofauti hufasiri maana ya umasikini kwa njia mbalimbali. Viongozi kwa kawaida hufikiria juu ya umasikini kwa kuangalia uwezo wa watu katika kununua mahitaji yao na kuuza bidhaa zao. Lakini fasiri ya umasikini ni kubwa zaidi. Kuna fasiri ya kuzingatia matatizo ya kuwa na mgawanyo sawa katika kupata elimu na afya bora, kuwa na heshima na hadhi katika jamii, kujisikia kuwa una uwezo wa kutatua tatizo lolote linalotokea katika maisha yako, na hivyo kuwa na matumaini ya maisha. Kwa hiyo kuna mengi ya kufikiria wakati unapotaka kuondoa umasikini. Kwa hakika fikra nyingi haziko wazi mpaka unapofikiria kwa makini yanayotendeka katika jamii.


Watu wa kawaida, wafanyabiashara, wafanyakazi serikalini, Mawaziri na viongozi wa nje wana mawazo tofauti kuhusu swali la umasikini ni nini. Wana mawazo tofauti kuhusu sababu za umasikini na jinsi ya kuuondoa. Hata hivyo, kuna mawazo ya jumla yafuatayo yanayokubalika:

Kama jamii huru haiwezi kuwasaidia watu wengi ambao ni masikini, haiwezi kuwaokoa wachache ambao ni matajiri.

[John Fitzgerald Kennedy 1917 – 63, Raisi wa 6 wa Marekani].

Wataalamu wanavyoliona suala la Umasikini

Katika dunia ya sasa watu hununua mahitaji yao kwa kutumia pesa. Kama hawana njia za kupata pesa watakuwa maskini. Umasikini mbaya zaidi ni ule ambao unawafanya watu wasiweze kupata chakula. Kwa hali hiyo, wanakuwa dhaifu na wanaweza kufa kwa njaa. Hali nyingine ya umasikini ni ile ambayo watu wanaweza kuwa na chakula kiasi au kidogo lakini hawana maji salama, huduma za matibabu, nyumba au mavazi bora.
panya-3.jpg (20167 bytes)
Takwimu za mwaka 1992 zinaonyesha kuwa karibu robo ya Watanzania wanaangukia katika kundi la kwanza la umasikini na nusu ya Watanzania wanaangukia katika kundi la pili. Katika mwaka 1995 karibu theluthi (1/3) ya idadi ya Watanzania walikuwa masikini. Hali hiyo huenda ni mbaya zaidi hivi sasa. Lakini umasikini una vipengele vingine zaidi licha ya kutokuwa na fedha za kutosha kununulia chakula, nguo, kujenga nyumba na kumudu gharama za matibabu. Utafiti kuhusu umasikini unaonyesha kuwa watu maskini zaidi:

bulletWamedumaa kwa sababu ya lishe duni
bulletWanapata vifo zaidi vya watoto wachanga, vijana na kuwa na maisha mafupi
bulletWanapata maji yasiyo salama ·
bulletWanapata elimu duni
bulletUmasikini unajitokeza katika maeneo tofauti: Sehemu fulani za nchi zina unafuu zaidi kuliko sehemu nyingine.
bulletKuna umasikini zaidi vijijini kuliko mijini, japokuwa dalili zinaonesha ongezeko la umasikini kwa kasi mijini.
bulletVijana na wazee na wale ambao wanatoka katika familia kubwa zisizo na uwezo wanakuwa masikini zaidi kuliko wengine
Utafiti unaonyesha pia kuwa watu masikini: · Hawalindwi kikamilifu na sheria · Hawashirikishwi katika maamuzi katika nyanja za kisiasa · Hawasaidiwi wakipata majanga kama vile ukame, mafuriko, n.k.

Watu wa kawaida wanavyoliona suala la umasikini

Watu wa kawaida walipoulizwa wajiepushe na nini ili wasiingie katika hali ya umasikini walitoa mawazo yafuatayo: · Wamiliki ardhi · Wapate zana za kilimo na teknolojia inayofaa · Wapate misaada na mikopo · Wawe na usafiri mzuri (barabara na magari) · Waweze kupata masoko kwa urahisi · Wawe na mipango bora ya matumizi ya maji · Kujenga uwezo wa kuweka akiba · Usalama kazini · Wapate huduma bora za jamii na miundo msingi (hasa afya ya elimu) · Kupunguza rushwa, kuwe na uwazi zaidi, kuimarisha uwajibikaji na ushirikishwaji katika kuchangia kutoa maamuzi katika kiwango cha Serikali za mitaa na Serikali kuu · Kujijengea fikra za kimaendeleo · Kujenga uwezo wa mipango mizuri katika ngazi ya kijiji · Kuunda upya na kuimarisha vyama vya Ushirika · Kuwawezesha Wanawake wawe na madaraka zaidi katika kudhibiti mali ya familia · Kujenga umoja, mshikamano, kuaminiana na hali ya kushirikiana

Tofauti Kimkoa

Mwaka 1999 Serikali ilitathmini mikoa ambayo ina umasikini zaidi. Tendo hili halikuwa rahisi kwa sababu kulikuwa na njia nyingi za kupima umasikini. Mambo ambayo yalijumuishwa katika zoezi hili ni pamoja na afya, lishe, chakula, elimu na ukuaji wa uchumi. Haikukusudiwa kuonyesha nani kashinda au kashindwa, lakini matokeo yalionyesha kuwa mikoa ambayo ni masikini zaidi ni Dodoma, Kagera, Lindi, Kigoma na Pwani. Mikoa ambayo ni masikini kidogo ni Dar es Salaam, Ruvuma, Kilimanjaro, Singida na Tabora.

Picha Kubwa zaidi

Wakati wa mkutano wa kitaifa uliojadili mkakati wa kwanza kuhusu mbinu (njia) za kuondoa umasikini (PRSP), mawazo yote yaliyotajwa hapo juu yalikubaliwa. Hata hivyo watu waliona kuwa palikuwa na haja ya: · Kushughulikia tatizo la ajira kwa vijana na hasa mijini · Kuzuia uharibifu wa mazingira · Kuzuia ajira ya watoto ·

Kuongeza fedha zilizopo kwa ajili ya kuondoa umasikini (hii ni pamoja na kufutiwa madeni ya nje na kutafuta njia nyingine ya misaada ya nje) · Kuendeleza mfuko wa fedha ili kusaidia wakulima wadogo wadogo · Kuwasaidia watu kuendeleza biashara ya kati · Kuifanya nchi ivutie biashara kubwa · Kufanya utafiti zaidi ili kutambua jambo gani linapaswa kufanywa na tuna uwezo gani wa kulifanya jambo hilo.

“Watu wa asili duniani wana mali chache, lakini si masikini. Umasikini si kuwa na mali chache, wala si uhusiano kati ya uwezo na ukomo wa mali; kwa hakika ni mahusiano kati ya watu. Umasikini ni hadhi katika jamii. Kwa hakika ni matokeo ya hali bora ya kuishi.”

[Marshall Sahlins, Mwana athropolojia wa Kimarekani]

Umasikini wa Mapato na Usio wa Mapato

Kwa kuwa kuna njia nyingi za kuzingatia suala la umasikini ni vyema kuwa na makubaliano ya fasili za umasikini. Fasili hizi zitasaidia katika majadiliano na katika kufanya mipango. Kutokana na tulivyosema hapo juu, ni vyema kufikiria juu ya umasikini kwa namna mbili:

Umasikini ulio na kipato kidogo:

Kinafikiriwa kuwa wakati mapato ya watu ni chini ya dola moja kwa siku (kama shilingi 800/= za Tanzania). Hii ina maana kwamba hawatakuwa na chakula cha kutosha, uwezo wa kupata tiba, watakuwa na mavazi na nyumba duni.
panya-4.jpg (23069 bytes)

Umasikini Usio wa Kipato:

Kuna wakati watu wanakuwa na fedha kidogo na hivyo hawawezi kumudu shule nzuri au kuwa na maji salama. Watu wanaoishi katika umasikini usio na kipato wanategemewa kudumaa na kufa mapema. Aidha, watu wa aina hiyo hawategemewi kushirikishwa katika kutoa maamuzi yanayohusu maisha yao.
panya-5.jpg (25701 bytes)

Kipato cha kimasikini kinapima watu wananunua na kutumia pesa kwa kiasi gani. Umasikini usio na kipatounahusu ubora wa maisha na maisha ya kijamii. Unapima vitu vingi ambavyo vinawaondoa watu katika hali duni ya umasikini na kuwaingiza katika hali bora.
Kutoka hali duni ya umasikini Kuingia hali bora
Rushwa Uaminifu na haki
Vurugu Amani na usawa
Kutokuwa na uwezo Demokrasia ya watu
unyonge Uwezo wa kutenda
Riziki ndogo Mali na amani
Mali na amani

Mtaji wa Jamii

Watu wote wana utaratibu ulio rasmi na usio rasmi wa makundi ambayo hujihusisha nayo katika kuendeleza maisha yao. Hali hii ndiyo inayoitwa “mtaji wa jamii”(social capital) na tunaweza tukaikuza. Njia za kuondoa umasikini ni pamoja na kuzingatia wakati ujao ambapo mtaji huu wa jamii hukua na kuingiza ushirikishwaji na ushirika katika ngazi zote hadi taifa na hata kimataifa. Ikiwa tutafikiri na kufanya kazi pamoja basi Watanzania wote wataishi katika hali njema.

Chanzo: http://www.hakikazi.org/