Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Desemba 12, 2014

Mapinduzi ya Tasnia ya Filamu Nchini Tanzania



 ZAMARADI MKETEMA ameandika sehemu....

“…Natamani sana siku moja atokee mtu kwenye hii sekta atutambulishe hata kama sio kimataifa basi africa tu.  KANUMBA alianza kuonesha mwangaza na juhudi binafsi zilionekana na kila mtu aliona huenda angefika mbali.. lakini baada ya hapo sioni tena!!!!

Mbona hapa nyumbani ni wakubwa tu..? Nini kinawakwamisha..? Kwanini wasanii wetu wa filamu ukubwa wao unaishia nyumbani tu....!!? Tatizo ni nini!!!????? kiukweli ni kama inakatisha tamaa na inaonekana kabisa watu wamerelax na ustar wa bongo wakati wana nafasi ya kufanya vizuri zaidi... wana bongo movie tukifika kwa wenzetu unaona kabisa tunapwaya kiasi gani.. 


Ujanja wetu ni nyumbani tu!!?? why!!!?? tukianza utanzania wa kufichaficha tutasifiana uongo lakini tukiwa wakweli na nafsi zetu tutaliona hilo na kuchukulia kama challenge..!!! ukweli ni kwamba hii tasnia inasikitisha!!! tena sana nahisi sasahivi tunafanya filamu kwa ajili ya nyumbani tu na tukiingia kwenye mabendi tukisharushwa tumeridhika!! kweli!! hapa ndio mnapotaka mfike!!? ukifika sehemu ukiwa juu nchini kwako tunachotegemea ni wewe kupasua mawimbi uende mbali zaidi nje ya mipaka!! lakini ukiamua kurelax hapo ulipo inamana unasubiri kushuka sababu kiukweli huwezi kukaa juu milele!!! kwanini mmeridhika hivi!!! kaka JB tatizo ni nini!!!??

Mi nakuangalia wewe kama mfano wa msanii mkubwa sana kwenye tasnia kwa sasa... mbona umerelax!!!??? umeridhika na ustar wa tanzania!!!? una kila kitu cha kukufikisha mbali... kinachohitajika ni juhudi binafsi tu ili kesho na sisi tufike mahala pazuri!! hebu tuongee wapenzi.. mnahisi huku kwenye bongo movie TATIZO LIKO WAPIII…!!???

JB Akajibu;

“Kwako Zamaradi na wengine wote..

Kwanza napenda niwashukuru wote kwa jinsi mnavyotuwazia mema. Naomba nichukue nafasi hii kuwapongeza waigizaji wote wa Tz na waandaaji wa filamuU kwa kuthubutu kutengeneza filamu hizi katiks mazingira magumu. Najua watanzania wengi wangependa kuona tukipeperusha bendera nje,lakini naomba muwape wasanii muda.

Tasnia hii ni changa na ina changamoto ambazo zinakatisha tamaa. Hebu tujiulize kwa nini wasomi wengi waliosomea filamuu UDSM na BAGAMOYO hawafanyi filamu hizi? Wasambazaji wengi wakubwa mamu,wananchi na hata hans pop walijaribu wakakimbia, kuna producer mkubwa hapa nchini JOHN RIBER ambaye ametengeneza filamuu kama NERIA na YELLOW CARD lakini naye ukimwambia njoo kwenye hizi filamu atakupa jibu.

Nakubali tuna makosa mengi kama ubora wa filamu zetu na stori lakini nataka niwaambie mazingira ya kufanya filamu bongo yanakatisha tamaa wizi wa kazi zetu umezidi na wasambazaji wengi wamekimbia. Binafsi najipanga kuwa mtayarishaji zaidi kuliko mwigizaji kwa sasa kupitia JERUSALEM FILMS na ndio maana filamu nyingi natoa nafasi kwa vijana ambao kama mabadiliko ya sera ya filamu yatafanywa watatuwakilisha nje.

Kiswahili kisichukuliwe poa kwani kina nafasi kibwa sana. Tukumbuke SHARUK KHAN ni ‘actor’ tajiri2 dunian lakini filamu zake ni za kihindi. Hebu sote tusaidiane kupambana na changamoto hizi na tuanze na EAST AFRICA kwanza huku tukiboresha, wasomi wa filamu msikimbie njooni tuanze wote na tuwape moyo wasanii wetu waliojaribu kusimamisha tasnia hii kwa vimtaji toka mifukoni mwao na vipaji walivyopewa na mungu bila msaada kutoka popote. Asanteni kwa kutuunga mkono kwemye filamu zetu.”
===================================




===================================


Tulitazame sasa hili suala kwa Pamoja;

Tasnia yetu pendwa nchini, Tasnia ya sanaa ya maigizio, hasa kwenye upande wa Filamu, Sina shaka hata kidogo kwamba baada ya Muziki, Sanaa ya Filamu na Maigizo ndiye inafuatia kupendwa zaidi hapa nchini, Idadi ya watazamaji na wafuatiliaji inathibitisha hilo!

Bahati mbaya Tasnia hii inaelekea kufa kibudu. Narudia, Tasnia ya Filamu nchini inaelekea kufa KIBUDU. Hali ni mbaya sana kwenye upande huu wa sanaa nchini licha ya kuwa ndiyo FANI inayoongoza kwa kutoa Ajira kwa vijana wengi zaidi nchini. Tukubaliane hapo kwanza!

Makosa yapo Mengi. Mbaya zaidi yote si makosa yanayohitaji kuonwa mpaka na Mtaalamu pekee. Hata Asiye na utaalamu wa Sound engineering atajua kwamba sauti kwenye Bongo movies ni tatizo, asiyefahamu mambo ya script akitazama tu atajua, Asiyejua umuhimu wa continuity naye hali kadhalika, achilia mbali yule asiyejua kiingereza kwa ufasaha, inamuhitaji elimu ya kujua tafsiri ya toilet tu kung'amua kwamba kiingereza cha kwenye subtitlles ni majanga. Mtiririko wa hadithi na uhalisia ni tatizo sugu. Inasikitisha sana.

Sitagusia hata moja katika hayo!

Leo Nagusa upande wa Mapinduzi ya Ujumla. Kwanini tasnia hii inaporomoka badala ya kukua zaidi? Kwanini hakuna mabadiliko chanya? Kwanini filamu nchini zimebaki kuwa na mabaka mabaka ya ulalahoi? Kwanini hatuvuki mipaka? Kwanini hatufanyi kweli? Kwanini muziki unatoboa zaidi kuliko filamu? Nini tatizo?

MAONI YANGU:

KWANZA, Wasanii waanze kutengeneza 'Image' nzuri;

Maana kwa sasa imeshachafuka. Nasema ukweli, Tasnia hii ina taswira ya uhuni kupitiliza. Na hii ni kutokana na wasanii wakubwa (vioo) kukumbwa na kashfa chafu. Kucha kutwa magazetini kuandikwa upuuzi, pengine wapo wanaolipwa kwa kuuza gazeti, lakini sidhani kama wanacholipwa kina thamani kubwa kupita kazi ya sanaa wanayoifanya.

PILI, Ianzishwe Mikakati Madhubuti;

Ni wakati sasa kwa wasanii kutengeneza Mipango Madhubuti na mikakati (Action plans) itakayowaongoza kufanya kazi kwa usiriaz. Inawezekana, najua mlishajaribu huko nyuma, lakini bado inawezekana.

TATU, Upekee na Usasa;

Hapa namaanisha kufanya movie kisasa na kwa upekee kabisa. Itazamwe mifano ya filamu kama ya CHUMO (Starred by Sharo Milionea & Jokate), Soap ya Siri ya Mtungi na kadhalika (wataalamu sio kikwazo panapo fedha).

NNE, Kushirikisha Wadau;

Watanzania na wapenzi wa filamu za kibongo ni wengi sana. Hakuna tu utaratibu wa kufanya research ili kuwa na data kamili, lakini kwa observation tu ni dhahiri kwamba Bongo Movie haijatupwa kivile. Ni basi tu wana-tasnia wenyewe mnachosha. Sijui lengo lenu ni nini haswa! Ni ajabu mtu kuua ajira yako kwa mikono yako mwenyewe!

Supporters wapo wengi sana. Wapo watazamaji wa hizi movies ni watu wenye uwezo mkubwa pengine hata wa kuwekeza. Achana na Mapedjee wanaohonga kwa lengo la kufurahisha nafsi zao, kuonekana, au malengo yao binafsi yasiyo na tija (japo wakitumiwa vizuri inaweza kusaidia sehemu). Hapa nazungumzia Matajiri, wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa, hata mawakala wa biashara, wakitumika vizuri, watafanya kitu.

Kinachohitajika ni ushawishi tu! Yaani wasanii wenyewe wahakikishe wawe na mipango na uwezo wa kumshawishi mtu/shirika/kampuni kuwekeza (kama si kufadhili) kazi zao. Serikali Pengine Imeshindwa hili!

Na ushawishi huja pale penye tija. Mtu aone umuhimu wa kufanya hivyo. sio kuchoma pesa zake bure. Mbona Michezo Mingi inadhaminiwa? Mpira wa miguu, Ndondi, Riadha n.k., Kwanini isiwe Bongo Movie? - Jikagueni upya kabla hamjachelewa.

TANO, Kuomba Fedha na Access Kubwa zaidi;

Kilio cha wasanii wengi kushindwa kufanya movie zenye ubora ni Mitaji. Wanalalamika hawana fedha za kutosha kuweza kucheza baadhi ya story. Ni kweli kabisa. Na hii pengine ndiyo sababu kubwa hata thamani ya kazi zao kwa wasambazaji inashuka siku hadi siku. Hii ni kutokana na bidhaa kuwa ni low quality.

Sasa basi, katika mikakati yao, Ni vyema wakazingatia ni vipi watapata mitaji ya kucheza story zinazohusika. Kisha watafute Soko zuri la kuuza bidhaa yao kwa bei itakayowanufaisha, sio watakayopangiwa na 'muhindi'.

Hatua za kupata mitaji zaweza kuwa;

* Kuomba udhamini kutoka kwa makampuni rafiki - Hapa namaanisha yale makampuni yanayohusiana na kazi zao. Kwa mfano Makampuni ya bidhaa za Camera, Deki, Simu, na kadhalika. Kwa ufupi, yale makampuni yanayoshabihiana na kazi za filamu yatakuwa rahisi zaidi kuitika!

* Kuomba mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha - Kwa kuwa filamu ni biashara kama zilivyo biashara nyingine kubwa, kampuni za utengenezaji wa hizi filamu (RJ, Jerusalem, 5effects, Timamu African Media n.k) zikiandaliwa mazingira mazuri zinaweza kukopesheka.

* Kutoa fursa kwa wahisani na wawekezaji - Kampuni za utayarishaji wa filamu zinaweza kutoa nafasi kwa wawekezaji kuwekeza kwenye kiwanda cha filamu nchini. Hapa kutawawezesha wawekezaji kuweza kuikuza zaidi tasnia hii kwa kuweka mitaji yao mikubwa na kuisimamia ili ipatikane faida. Inawezekana!

Pia, wasanii waombe access kubwa kutoka serikalini ili waweze kutambulika Rasmi na kuaminiwa. Haya yote yatawezekana endapo shirikisho la filamu nchini (TAFF) litakuwa na makali na sauti ya nguvu.

SITA, Wasanii watumie wataalamu kwenye kazi zao;

Hapa namaanisha ni wakati sasa waandaaji wa filamu pamoja na wasanii kwa ujumla waanze kushirikisha wataalamu kwenye kazi zao. Kwa maana wafanye tafiti ndogo ndogo kuhusiana filamu husika (mfano kwenda maktaba kutafuta vitabu vinavyoelezea let's say masuala ya historia, kama hadithi ya movie inagusia huko) na kupata majibu ya kitaalamu kutoka kwa wataalamu hao. Hii ni faida kwani 'uhalisia' wa movie utakuwa maradufu!

Ushirikishwaji uanzie kwenye masuala ya story, production mpaka kwenye masuala mazima ya masoko. Uwanja huu ni mpana sana, nadhani mwanga umeanza kuonekana hapo!

===================================


===================================

 
Kwa kipekee kabisa, Niwapongeze Timamu Effects / Timamu African Media, kwa kuonyesha njia. Nathubutu kusema hawa ndio role models kwenye filamu za Kitanzania. Ni wenzetu, walianzia chini, lakini wamejitahidi kukua kifani, kimaudhui na kimapinduzi hususan kwenye ubora wa story na quality ya uandaaji wa filamu zao zote.

Nashauri waigwe na kuwa dira ya tasnia ya filamu nchini, waendelee kufanya mambo makubwa zaidi ili hatimaye na Tanzania tufikie levo angalau za Nigeria na Ghana. Nimefurahi kuona Wamepata tuzo kadhaa za kimataifa, na kubwa zaidi ni za hivi karibuni huko Marekani katika Future Africa Awards. Hongera Timoth Conrady na Timu yako!


Naomba niishie hapa, ili kutoa nafasi kwa wengine kuchangia mawazo yao, na kwa pamoja tuweke mitazamo chanya na yenye taswira ya kimapinduzi kweli ili hatimaye tuwe tumeshiriki kwenye kuboresha tasnia ya filamu nchini.

Nawasilisha....


Chanzo By:  MR. CONFIDENT, on JamiiForums

MSITU MSITUNI



Ukiwa mbali na msitu, yaani kabla hujaingia msituni utauona msitu ni mkubwa sana. Utaona eneo lote la msitu limejaa miti na huwezi kuona hata ardhi. Kwa umbali uliopo unaweza kuamini kwamba hakuna hata sehemu ya kupita kwenye msitu huo.

Ila unapoingia kwenye msitu huo, huoni tena msitu. Yaani unapokuwa msituni huoni tena msitu, bali unaona mti mmoja mmoja na kuna sehemu kubwa ya kupita. Unaweza kuupita mti mmoja baada ya mwingine na kuendelea kufanya yako…

Kabla hujaingia kufanya jambo lolote utaona vikwazo vingi sana, utaona hatari na ilivyo rahisi kushindwa. Ila unapoingia kwenye jambo hilo, vikwazo vilivyokuwa vinakutisha mwanzo unakuta sio vikubwa kama ulivyokuwa unafikiri. Unakuta ni changamoto ndogo ndogo ambazo unaweza kuzimudu.

Usiogope tena kufanya kile unachotaka kufanya, huwezi kuona msitu ukiwa msituni…

Nakutakia kila la kheri.


Chanzo: Makirita Amani

HATMA YA WASANII TANZANIA NI MBAYA WASIPOBADILIKA

BI CHEKAAA


LAZIMA nimshukuru Mungu sana kuwa mimi ni msanii wa hapa Tanzania na bado sijapotea sana kwenye masikio na macho ya watu. Lakini kuna wenzangu wengi waliokuwa maarufu kuliko mimi waliokuwa na mafanikio ya kisanii na kiuchumi kuliko mimi kwa sasa hali zao za maisha ni mbaya sana. Kuna sababu kadhaa za matokeo haya, lakini kuna moja kubwa nalo ni kukosa ufahamu wa haki zao. 
 
Wakati msanii anapoanza kutafuta umaarufu huwa mtu wa kutaka kupata ushauri, lakini pindi anapojulikana hataki tena ushauri hasa kuhusu haki anazostahili kuzipata kutokana na kazi yake. Hali hii hutokana na sababu mbili kubwa, moja ni kiburi kinachojengeka kutokana na umaarufu hivyo kumfanya muhusika kuona kuwa haiwezekani kamwe akashuka na kuwa mtu wa kawaida. Pili ni mtego ambao wasanii wengi huingia na kujikuta chini ya wafanya biashara wahuni ambao ili waendelee kuwamiliki wasanii huwa wanawakataza kujihusisha na harakati zozote ambazo zitaweza kuwaamsha akili zao kudai haki yao. 

Na wafanyabiashara wengine huweza hata kuwafundisha mambo yasiyo ya ukweli katika biashara na kuwafanya wasanii waamini kuwa hawataweza kufanya kazi bila ya kuwa na wafanya biashara hawa. Lakini ubora wa wanamuziki hawa unaposhuka wafanyabiashara hawa hawa huwatema kama kaa la moto na wasanii kujikuta wakihangaika maisha ya tabu bila msaada wowote.

HAKIMILIKI 

Ni haki zaidi ya kumi anazopata msanii katika kila kazi yake, wasanii wengi hawajui haya na wengi wala hawataki kujua, mmoja aliwahi kunijibu, ‘Hakimiliki ni Ulaya tu”, japo alikuwa hajui hata hiyo hakimiliki ina beba nini. Namjua mfanya biashara mmoja ambaye moja ya kampeni zake kuu ni kuhakikisha wasanii walio chini yake hawajui Hakimiliki, wala hawahudhurii semina au warsha yoyote ya Hakimiliki. Lakini Hakimiliki ni mali ya mtunzi maisha yake yote na miaka 50 baada ya kifo chake kadri ya Sheria ya Hakimiliki ya Tanzania. Kwa kipindi hicho  Hakimiliki inakulindia haki za kiuchumi, ‘Economic Rights’ ambazo ndizo zinazokupa uwezo wa kupata halali yako kiuchumi kutokana na kazi zako. Katika kila kazi, kwa mfano wimbo, kuna haki zifuatazo; 

i. Kurudufu,
ii.Kusambaza,
iii. Kukodisha,
iv. Kuonyesha hadharani (exhibition),
v. Kutafsiri,
vi.Kutangaza hadharani (Public Performance),
vii. Kurusha katika vyombo vya utangazaji (Broadcasting),
viii Kubadili matumizi,
ix. Njia zozote zile nyingine za utangazaji hadharani (ikiwemo Cable network),
x. kuingiza nakala nchini 

Hali ilivyo mbaya hapa Tanzania, wanamuziki wetu siku hizi hawasambazi, wengi hawana album rasmi, japo wanaweza kuwa na nyimbo zinazotosha album, baada ya kurekodi hutumia kipengele cha vi, na kuweka nyimbo zao kwenye mtandao kama youtube  ili kila anaeutaka anaweza kuutumia bure, hiyo ikidhaniwa kuwa ndio njia bora ya promosheni ya wimbo mpya, wajanja hutumia kipengele cha i. na ii, wanarudufu na kusambaza na kutengeneza pesa bila kuwashirikisha wasanii, kisha wasanii huruhusu kazi zao zitumiwe kwa haki na vii, redio na tv huingiza mabilioni ya fedha kutokana na matangazo, kwa kupiga nyimbo hizo bila kulipa hata senti tano.

 Zikiwemo radio za wale wanaotambulika kuwa ni watu wasafi na wakombozi wa vijana na wanyonge, na hata radio ya Taifa nayo imo katika ufisadi huu. Hatimae tunaona nakala za DVD na CD za wasanii wa Kitanzania zikiingizwa nchini kutoka Uchina na kuuzwa mitaani zikiwa zinavunja kipengele x.

Wasanii wengi wakiona kazi zao zimesambaa hujisifu kuwa ‘Kazi yangu inafanya vizuri’.  Umbumbumbu huu wa hakimiliki unawafanya wasione umuhimu wa mikataba itakayoelekeza matumizi yatakayoleta tija kwenye maisha yao, hivyo baada ya muda msanii anajikuta hata fedha ya nauli kwenda kudai chake hana. Na wengine huona njia ni kuendelea kurekodi, bila kujali kilichokwisha rekodiwa kiliingiza na nini na kusababisha hasara gani.

Masikitiko zaidi ni pale unapokuta msanii yuko katika hali mbaya kimaisha wakati kazi zake bado zinaendelea kuingiza mamilioni kutokana na matangazo katika vyombo vya utangazaji na muhusika wala hajui kuwa anastahili mgao wa pesa inayotokana na jasho lake.

Umoja ni nguvu na kila mtu anajua hivyo, hata wale wanyonyaji wa wasanii wanalijua hilo hivyo kati ya vitu vinavyopigwa vita na wanyonyaji ni umoja wowote wa wasanii. Ukionekana unafanikiwa patapenyezwa rupia ili kuchafua jitihada zozote za kuunda umoja wenye nguvu. Japo wanyonyaji hao wao wamejitengenezea umoja wenye nguvu sana kulinda maslahi yao ya kuwanyonya wasanii.

Katika wizi wa kazi za sanaa kadri unavyokuwa maarufu zaidi ndivyo unavyoibiwa zaidi, ungetegemea kuwa wasanii maarufu ndio wangekuwa wakihakikisha kunakuweko na umoja na pia kuhamasisha ulinzi wa haki zao, hilo ndilo kinyume, nadra sana watu maarufu kuhuduhuria mikutano ya wasanii, labda kama huo mkutano umehamasishwa na wafanyabiashara wanaonyonya wasanii hapo utakuta mkutano una wasanii wote muhimu na mara nyingi mada hapa huwa hazina umakini wa kutoa elimu kwa wahusika.


NI jambo la kusikitisha kusikia mama huyu Bi Cheka ambaye miaka miwili tu iliyopita alikuwa kwenye masikio ya kila mtu anaishi kwenye nyumba ya udongo. Tuombee iwe ni hadithi tu na si kweli kuwa hali ni hiyo, japo haitashangaza kamwe kwa nchi hii iliyojaa ufisadi kila kona.


Stori zaidi: Gladness Mallya na Mayasa Mariwata

DAH MASIKINI! Hivi ndivyo unavyoweza kusema wakati unapomuona msanii wa muziki wa kizazi kipya, Cheka Hija, maarufu kama Bi. Cheka kutoka Kundi la Mkubwa na Wanawe, linaloongozwa na Said Fella ‘Mkubwa’ lenye maskani yake, Temeke jijini Dar es Salaam.

Bi Cheka akiwa nje ya nyumba anayoishi.

Mtoa habari wetu aliwasiliana na gazeti hili na kulieleza kuwa msanii huyo mwenye umri wa miaka 55, hivi karibuni alianguka ghafla nyumbani kwake na kukata kauli, wakati alipokuwa akienda chooni kujisaidia.

Wikiendi iliyopita, Amani lilifika nyumbani kwa msanii huyo mzee, anayeishi Bunju B, nje kidogo ya jiji la Dar na kumkuta akiwa na wajukuu zake huku hali yake ikiwa tete tokea alipoanguka Oktoba mwaka huu.

Akiwa anaishi katika kijumba chake kilichojengwa kwa miti na kukandikwa udongo, mtu anayemuona katika luninga akifanya vitu vyake, asingeweza kuamini kama hapo ndipo anapoishi.



Upande wa nyumba yake.

“Ukweli nilikuwa na hali mbaya, afadhali sasa, naongea na kusimama kwani nilikuwa siwezi kutembea, wiki iliyopita alikuja meneja wetu, Yusuf Chambuso na akina Dogo Aslay.

“Jamani maisha yangu kwa sasa ni magumu kwani siwezi kufanya kazi yoyote na sina msaada na kwenye muziki sijaona faida yoyote labda ya nguo tu, kwamba nilizoea kuvaa madela na kanzu sasa nina suruali,” alisema Bi Cheka kwa machungu.


Bi Cheka akiwa na wajukuu zake.

Alisema anasikitishwa na maisha yake kwani kutokana na umaarufu wake, mtaani kwao anaonekana kama mtu mwenye uwezo, wakati siyo kweli kwani anaishi kwenye nyumba ya tembe katikati ya nyumba nzuri.

“Kuhusu malipo makubwa kuwahi kupata ni shilingi laki tatu nilizolipwa kwenye shoo ya Fiesta mwaka juzi, hizo ndizo hela kubwa niliyowahi kupata katika muziki.”Gazeti hili lilimtafuta Fella ambaye alikiri Bi. Cheka kuumwa, akisema anasumbuliwa na magonjwa ya uzee na kwamba ahadi yake ya kumsaidia kujenga nyumba imeishia kwenye mchango wake wa matofari.


...Bi Cheka akiimba na Chege.

“Mimi kama Fella nimesaidia ninapoweza, nimemchangia matofari kidogo, kwa hiyo watanzania wenzangu nao tuungane tumchangie ili aweze kurekebisha kibanda chake,” alisema.

Global Publishers inaanzisha kampeni maalum ya kumsaidia na hivyo inawaomba watanzania kumchangia msanii huyu ili apate nyumba nzuri na matibabu yake. Ili kumsaidia tuma fedha kwenye namba 0654-880707 ambayo itasimamiwa na kampuni.

 Chanzo: INGIA HAPA

Ijumaa, Desemba 05, 2014

Nyigu na Mrija Utoboao Miti






 Nyigu wa kike ambaye hutoboa miti na kutaga mayai ndani ya misonabari, amewashangaza sana wanasayansi kwa mbinu yake ya kutoboa miti na kuwachochea kubuni vifaa bora zaidi vya kufanya upasuaji kwa njia salama zaidi.

Fikiria hili: 

Nyigu huyo hutoboa msonobari kwa kutumia mrija ulio kama sindano na wenye mitaimbo miwili, au “valvu” zilizoingiana, ambapo kila moja imefunikwa kwa meno yanayoangalia nyuma. Meno ya valvu moja hushikilia mti na hivyo kumfanya asisonge, na valvu ile nyingine husonga hatua moja mbele. 

Kisha meno ya valvu hiyo ya pili hushikilia mti tena na hivyo ile valvu ya kwanza inasonga mbele. Katika mwendo huu wa kasi unaofanyika kwa kurudia-rudia—ambapo valvu hizo hubadilishana kushikilia mti na kusonga mbele—mrija huo huchimba milimita 20 hivi bila kutumia nguvu nyingi kwenye sehemu laini ya nje ya mti bila kujipinda wala kuvunjika.


Wanasayansi wamechochewa na mrija huo hivi kwamba wanabuni kifaa cha kufanya upasuaji katika ubongo ambacho kitachimba kwa kutumia mbinu hiyo. Sindano yake ya silikoni ina valvu mbili ambazo husonga mbele na nyuma, kila moja ikiwa na meno madogo ambayo yanaweza kuingia katika sehemu za ndani zaidi za ubongo bila kusababisha madhara makubwa. Hata hivyo, kifaa hicho kitaweza kufanya jambo lingine. 

Gazeti New Scientist linaeleza, “Tofauti na vifaa vingine vya upasuaji visivyoweza kujipinda, kifaa hiki kitaweza kujipinda kwa kiasi kikubwa hivi kwamba kitapitishwa katika sehemu salama zaidi za ubongo, bila kugusa sehemu nyeti wakati wa upasuaji.” Kifaa hicho pia kitafanya iwe rahisi kufikia sehemu ambazo huwa ni vigumu kufikia bila kukata viungo ambavyo havina tatizo.

Zaidi INGIA HAPA

Alhamisi, Desemba 04, 2014

Bawa la Kipepeo




● Rangi maridadi inayong’aa juu ya mabawa ya vipepeo fulani hubadilika ikitegemea upande ambao unatazama. Rangi ya bawa la vipepeo wa aina fulani ni laini na inang’aa sana hivi kwamba inaweza kuonekana umbali wa mita 805. Ni nini kinachofanya bawa la kipepeo liwe la kipekee hivyo?


Fikiria hili: Mistari midogo iliyobonyea kwenye sehemu ya juu ya mabawa ya kipepeo anayeitwa green swallowtail (Papilio blumei) hurudisha nuru kwa njia kadhaa. Kwa mfano, sehemu ya katikati ya eneo lililobonyea hurudisha nuru yenye rangi ya manjano na kijani, huku sehemu za nje zikirudisha nuru yenye rangi ya bluu. 

Pia, sehemu ya katikati ya eneo lililobonyea hurudisha nuru moja kwa moja, lakini nuru inapopiga sehemu za kando inalazimika kupitia kwenye matabaka kadhaa, ambayo huongeza na kuzungusha mawimbi ya nuru. Mchanganyiko wa mwisho unaotokea huwa tata sana.



Watafiti walitumia miaka kumi kutokeza kitu kinachofanana na sehemu ya juu ya bawa la kipepeo. Wanatumaini kwamba teknolojia hiyo itawasaidia kutokeza noti za benki na kadi za mkopo zisizoweza kuigwa kwa urahisi na mabamba yanayoweza kunasa nguvu za jua kwa njia nzuri zaidi. 

Hata hivyo, ni vigumu sana kuiga sehemu ya juu ya bawa la kipepeo. “Ingawa wanasayansi wanaelewa mambo mengi sana kuhusu elimu ya nuru,” anaandika Profesa Ullrich Steiner wa Chuo Kikuu cha Cambridge, “unamna-namna wa rangi wenye kushangaza unaopatikana katika bawa hilo unazidi mambo yanayoweza kutokezwa kwa kutumia teknolojia.”

Una maoni gani? 

Je, sehemu ya juu ya bawa la kipepeo ilijitokeza yenyewe? 

Au ilibuniwa?

Jumatano, Desemba 03, 2014

Maisha ya Nyota Baada ya Kufa Angani



Nyota za Neutron ni viini vizito zinavyobakia baada ya nyota kubwa kufa na kulipuka huko angani. Matabaka ya nje ya nyota hurushwa mbali katika milipuko hiyo, lakini maada katika viini vya nyota hizo husambaratika vyenyewe na hutengeneza burungutu kubwa la maada. Kinachobakia baada ya hapo ni kitu kilichokandamizwa chenye mkandamizo mkubwa katika ulimwengu wote nje shimo jeusi: nyota ya neutron!


Picha hii mpya iliyopigwa huko angani inaonyesha kundi la nyota lijulikanalo kama ‘globular cluster’. Ambayo ni baadhi tu ya vitu ambavyo ni vya kale sana huko angani— umri wake unakaribiana kabisa na umri wa ulimwengu wenyewe! Hii inamaanisha kuwa nyota nyingi zilizopo ndani yake zimeshakufa. Na zile kubwa zaidi zimekwishalipuka na kuacha nyota za neuton.

Kwa kutumia nyota ya neutron katika kundi hili pamoja na nyingine nyingi, wanaastronomia wameweza kutambua uhusiano kati ya uzito wa nyota (kiasi cha maada inayobeba) na ukubwa wake.




Taarifa mpya zinaonyesha kuwa nyota ya neutron ya kawaida, yenye uzito wa mara moja na nusu ya Jua letu inaweza kuwa na kipenyo cha kilometa 12. Urefu ambao ni karibu sawa na eneo la mji mdogo! Likiwa na maada zote hizi zimekandamizwa katika sehemu hiyo ndogo. Hivyo basi nyota za neutron ni nzito mno. Nguvu ya mkandamizo (Presha) katika kiini chake ni zaidi ya trilioni kumi kuliko nguvu ya mkandamizo inayohitajika kutengenezea almasi ndani ya Dunia.

Dokezo: Nyota za neutron zimepakiwa na kukandamizwa sana hivyo kuzifanya ziwe na duara pete. Mlima unaoweza kutokea katika uso wake unaweza kuwa na urefu wa milimita 5 tu!

Kwa Taarifa Zaidi 

Swahili Space Scoop hii imetokana na Taarifa kwa vyombo vya habari ya Chandra