Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Septemba 07, 2016

SHUKRANI MUNGU KWA ZAWADI HII YA MAISHA KTK SIKU YANGU YA KUZALIWA





LEO TAREHE 7 SEPTEMBA NI MAPENZI YA MUNGU KUNIFIKISHA KATIKA TAREHE NA MWEZI NILIOZALIWA NA SASA NIMETIMIZIA MIAKA ZAIDI. NICHUKUE FURSA HII KUWAKUMBUKA KWA KUWASHUKURU WALIOTENDA YALIYOTENDEKA.

Si mnakumbuka mapitio ya udogoni, kucheza pamoja, kukaa pamoja katika shida na raha wakati mwingine kupigana pale tulipoudhiana, ila tulisameheana kwa vile tulifundishwa upendo. Mara zote tuliamini kwamba japo tulizaliwa katika hali ya umasikini ila hatutakufa masikini, kwa vile si lengo la Mungu watu wake wataabike katika dhiki.


Kwa watoto yatima wote na wale waishio katika mazingira magumu;


..Nawapenda sana na daima nakuwa na amani sana kuwaona mkitabasamu na kufurahi, bila kujali matatizo mliyonayo maishani. Sio lengo la Mungu mteseke kwa kuwakosa wazazi ama ndugu mliowapenda na kuwategemea kwa namna moja ama nyingine. Mungu si mwanadamu hata tuseme anakosea kufanya maamuzi..ishini mkimtegemea Mwenyezi Mungu, baba wa mbinguni ajuaye idadi ya nywele kichwani nina hakika ipo siku majonzi yenu yatageuka kuwa Furaha..hamtanung'unika tena..nawapenda sana!


Nichukue fursa ya awali kumshukuru Mungu baba wa mbinguni kwa kunifanya moja kati ya viumbe alivyoviumba chini ya jua ..ni kwa neema yake tu kuwepo kwangu hadi leo hii kwani sina haki kuliko wale wote waliotangulia umautini. Namshukuru zaidi kwa kunipa ufahamu wa kuelewa mambo..asante Mungu kwa kunijaalia karama nyingi mbalimbali..naomba uniwezeshe kuzitumia vizuri kwa wengine!




Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitawashukuru wazazi wangu kwa kunileta duniani..nawapenda sana na daima napenda kuona mnaishi maisha ya ujana, yenye kila aina ya furaha..narudia kusema nawapenda sana na kuna kitu nitafanya kwa ajili yenu! 


Shukrani za kipekee ziwafikie walimu wangu tangu shule ya msingi hadi wakufunzi wa chuo kwa juhudi kubwa walizofanya za kunifuta ujinga..hakika nisingakuwa nilipo kama si jitihada zenu! Mungu akujaalieni kheri popote mlipo!


Nitakuwa mchoyo wa fadhila nisiposhukuru majirani na waumini wenzangu kwa kuwa mentor, influencer na watu mlioni-jengea hekima ya hali ya juu! Niwaombe radhi wale tuliocharuana kwa sababu moja ama nyingine pale tulipopishana!


Wapo pia ambao siwezi kuwaacha japo majina ni mengi ila kazi yao ilinifanya niwaone kuwa role model wangu katika vipindi vya radio walivyokuwa wanarusha kupitia SAUTI YA UJERUMA, BBC SWAHILI, SAUTI YA AMERIKA, RADIO TANZANIA DSM, KBC SWAHILI NA ENGLISH SERVICE na nyingine nyiiingi popote zilipo. 


Mungu awajaalie miaka 900 kama enzi za Adamu na Hawa bila kujali mapungufu mliyonayo! Nyote mmechangia kupata zawadi nzuri sana ya maisha tangu kuzaliwa, kukua kwangu hadi kufikia leo ninapotimiza umri huu nilionao.

MUNGU WEWE NI MUWEZA WA VYOTE HAKIKA UNATUPENDA SANA. 

p>

Jumanne, Septemba 06, 2016

JE UMESHASIKIA KUHUSU SMARTPHONE MPYA?



Kutana na TURING ya CADENZA, hakuna smartphone duniani kama hii. Smartphone Hii ni mama na baba yao wote na 12GB ya RAM na 2 Snapdragan 830 SoCs.


Fikiria smartphone iliyo na Snapdragon mbili 830 SoCs , 12GB ya RAM , kamera ya mbele ni 12MP, na 60MP kwa kamera ya nyuma

Ndiyo! Hizi ni specs ya smartphone ijayo kutoka nyumba ya Turing ambayo ni maarufu kwa ushahidi wa kudukua smartphones.


Wakati wazalishaji wengine wanajaribu kushinikiza ivuke mipaka ya RAM 6GB , Turing Cadenza itakuwa ni mara mbili hasa kwamba itakuwa na RAM ya 12GB.


Turing mpya super smartphone itatolewa mwaka 2017 na kuitwa Turing Simu Cadenza.

UTOFAUTI KATI YA MWANAMKE NA MWANAUME:



01. Kwenye mshituko; mwanaume hushituka halafu huangalia nini kimemshitua, mwanamke hushituka halafu huzimia hivyo ataambiwa na mwanaume kilichomshitua.

02. Kwenye kupenda; mwanaume huanza kutamani alafu hupenda, mwanamke huanza kupenda moja kwa moja bila kumjua vizuri huyo ampendae.

03. Kwenye kusaidia; mwanaume hutoa msaada alafu uhuzunika, mwanamke huuzunika badae ndo anakumbuka km msaada unahitajika.

04. Kwenye maamuzi; mwanaume hufikiri ndipo hutenda, mwanamke hutenda halafu hufikiri.

05. Kwenye kudanganya; Mwanaume hudanganya ili kumlinda mwanamke, mwanamke hudanganya ili kumkomoa mwanaume.

06. Kwenye ugomvi; wanaume hupigana halafu hueshimiana, wanawake hupiga mikelele alafu kila mmoja hurud kwake, kesho tena.

07. Kwenye ndoa; mwanaume hutafuta maisha ndipo huoa, mwanamke huolewa ndipo atafute maisha.

08. Kwenye kukata tamaa; mwanaume hukata tamaa mapema ili jambo lisimsumbue, mwanamke hajui kukata tamaa hadi aumizwe.

09. Kwenye kula;Mwanaume hushiba alafu huanza madoido, mwanamke huanza na madoido alafu badae hujilaumu hakushiba.

10. Kwenye siri; Mwanaume hutunza siri hasa za aibu, mwanamke humueleza shoga yake.. baadae hugombana nae yakishamrudia mwenyewe kwa siku 2 tu.

Hizi ni baadhi tu ya sifa tofauti kati ya mwanaume na mwanamke kama kuna nyingine ziongezee katika comments hapo chini ili kupeana elimu na maarifa kuhusu saikolojia.

Alhamisi, Septemba 01, 2016

NAMNA YA KUTAMBUA TABIA YA MTU



Hakuna anayependa kusahihishwa, kugombana au kukemewa mbele za watu, hii ndiyo tabia ya watu wajeuri na walio na tabia za kitukutu. Mara nyingine hudhani wanapata sifa. Wako watu wa jinsi hii ambao hawawezi kukugombeza au (kukupa vidonge vyako) mkiwa wawili peke yenu, watangoja watu wengine wawepo ndiyo waanze kubwabwaja, cha kufanya jiepushe nao.

Kwa kule kukimbiwa na marafiki, na kuwa mpweke, huongeza tabia za kitukutu na kijeuri na hii huwafanya watu hawa kutambulika haraka na kiurahisi zaidi.


Zifuatazo ni alama zitakazokutambulisha mtu jeuri na mtukutu:


a) Alama za kimaneno

Mara kwa mara hupendelea kusema maneno haya vinywani mwao.
Nakwambia bora unge…"
Wewe sichochote, silolote…"
Nakwambia, lazima u..."
Fanya vile ninavyokuambia mimi…"
Nataka u..."
Wewe endelea tu tutaona..."


b) Alama za kimwili

Hupendelea kusimama wima
Huwa wenye pozi kavu, ngumu (still and rigid pause)
Hupenda kukunja mikono
Hupenda kupayuka au kupigia wengine kelele
Hupenda kuwanyooshea wengine vidole.
Hupenda kuwazodoa wengine na vidole (hawezi kukuelekeza hadi kidole chake kikusukume)
Hupenda kupiga au kugonga meza na viti akizungumza


2. Watu wapole, waliotayari kukubali kushuka (Submissive)

Hawa ni watu wanaopenda kujitoa sadaka kwa ajili ya manufaa ya wengine. Kwa hali hii ni rahisi watu hawa kujikuta wanatumiwa vibaya na watu wengine hasa wale wajeuri na watukutu tulio waangalia awali.


Mara nyingi watu walio wapole na wanaokubali kushuka hupenda kuwatia moyo wengine wawe kama wao. Katika vizazi vilivyopita, wanawake walitegemewa zaidi kuwa watu wa kundi hili. Ni mabadiliko ya maisha na ya jamii ya leo ambayo yamemfanya hata mwanamke kuwa mjeuri na mshindani tofauti na jamii za awali.

Kwa upande mwingine mfumo wa maisha wa vizazi vya nyuma ulimweka chini mwanamke na kuzuia maendeleo yake hasa katika kujiendelezea vipawa alivyonavyo kwa vigezo tu kwamba yeye ni wakukubali chochote na wakati wowote sasa tunayaona mabadiliko kwa kiasi fulani.


Mara kwa mara watu wapole, na waliotayari kushuka wamekuwa wenye hisia za kinyonge na kutengwa, wakijihisi kutokuwa salama wakati mwingi. Kujijali, kujipenda na kujithamini kwa watu hawa siyo kwa kudumu, bali kunakuwa na nyakati za kuyumbayumba kutokana na mazingira. Hawa siyo watu wenye ujasiri ndani yao wenyewe na hata katika vile wavifanyavyo.


Mara mtu wa kundi hili anapokutana na mtu mjeuri na mtukutu, hofu na ujasiri wake hupungua sana, na anaweza kukubali kupingwa hata kama alikuwa ana haki. Kwa sababu mara nyingi watu wa jinsi hii wanajua kuwa kwa upole wao watu wengi wamekuwa wakiwatumia na kuwachezea, hii imewafanya wawe ni watu wenye vihasira vya mara kwa mara.


Kwa sababu wameunganishwa na hisia zao zaidi, ni rahisi wao kuzielezea hisia zao kwa mtu mwingine, hata kama hisia zao ni za kujutia kile walicho kifanya wenyewe. Mara nyingi husikia amani kwa yale wanayofanya au kuyaamua.


Ingawa mara nyingine mambo huwaendela tofauti na walivyopanga, watu hawa hufahamu kuwa hawanabudi kukubali kosa au na kuwa tayari kujifunza kutokana na yale makosa.


Mambo yanapowaendea vema hupenda kujisifia na kujiona walio juu. Mara nyingine misimamo yao huwashawishi na kuwavutia wengine watazame kama wao, sio watu wanaopenda kuwatumia wengine vibaya (being manipulative) kama vile kuwasema au kuwasengenya wengine, hii huwafanya kuwa na wafuasi au washabiki wengi zaidi.


Kule kujiamini kwao na kuwa na ujasiri hupunguza sana msongo wa mawazo maishani mwao na hii huwasaidia kuelekeza nishati na nguvu zao zote katika kufikia malengo waliojiwekea.


Mara kwa mara sio watu wenye mabadiliko ya hisia (change of attitude) na hii hufanya mahusiano yao na wengine kuwa yasiyoyumba na mawasiliano baina yao na wengine huwa wazi, sio watu wakuficha wanachokiona, uwazi walionao kuwaweka huru.

Hujisikia vema hujipenda na kujithamini muda mwingi. Hujijengea hisia za usalama na imani kwa sababu ya mawasiliano bora walionayo na wale wanaowazunguka, hii pia husababishwa na wao kuelewa fika wajibu wao na wajibu wa wengine pia.


Ingawa wanaweza kuwa wabishi, lakini huheshimu misimamo ya wengine na kupenda ya kwao iheshimiwe pia na hii huwafanya kuwa na ushirika na wale wanaowazunguka. Mara nyingi ni wazuri katika kuwatia wengine moyo kujitahidi zaidi.


Alam za kuwatambua:

Alama za maneno

Nahisi……. Najisikia kuu……………"
Ningependa kuu…………"
Wewe unaonaje hapa/mawazo yako nini………….."
Unadhani njia gani bora kulishuhulikia hili ……….."
Nafikiri……….."
Hembu tu…………….."


Alama za kimwili

Hupenda kuwa wima ila wenye pozi laini (relaxed stance)
Huangalia kijasiri na kuangalia usoni (kukodoa macho).
Huwa na hisia za upole, kujitawala na kujimiliki wenyewe

Kwa vyovyote vile, mara zote unapokutana na mtu mwenye tabia yeyote kati ya hizi tatu kumbuka una haki ya kufanya yafuatayo;

Jifunze kuelezea hisia zako njema (usiogopoe au kuona aibu kwakuwa hutokuwa umejitendea haki)
Jifunze kuzielezea hisia zako mbaya au za hasira, kamwe usifunike. Mfano; "Sipendi kabisa unavyokula"
Jifunze kusema hapana, Mfano; "Hapana sitaweza kufika leo"

Toa wazo la kweli, usipake watu mafuta kwa mgongo wa chupa. Mfano; "Mimi siliafiki hilo jambo hata kidogo"
Kiri kuwa umekasirika, hasa pale ambapo haunabudi kukasirika.

Mfano: "Kweli umeniudhi sana baada ya kusema hayo maneno". Usitoe tabasamu la mamba tu, kutabasamu wakati ndani yako unahisi kuungua moto.


Credit: MziziMkavu