Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Desemba 31, 2010

MATUNDA MENGINE NAYO!!! MH.

HIVI NI KWA NINI
MATUNDA MENGINE YANAIKIMBIA NDIZI??

UNAJUA CHANZO CHA HARUFU MBAYA KTK NYETI

Kuna vijana wengi wamekuwa wanakumbwa na tatizo la kutoa harufu katika maeneo nyeti.. hili tatizo lipo na mimi binafsi linanikera ndio maana naamua kulieleza leo ili watu wajirekebishe hasa wanaume sisi.. Yaani hii inaboa na najua hata mademu zetu wanakereka ila wanashindwa la kufanya kwa kuwa wanatupenda! ila kwanini tuwape wademu zetu nawengine wachumba zetu karaha wakati tunaweza kuepukana na hii aibu?

Sababu kubwa ya tatizo hili ni:

1.Kuvaa nguo ya ndani kwa muda mrefu...

2.Kuvaa nguo ya ndani bila ya kujikausha vizuri hivyo kubakiwa na unyevu..

3. Kuvaa nguo za ndani zisizoendana na khali ya hewa ya eneo uloishi...

4. kushindwa kuoga au kujisafisha nyeti baada ya kumaliza kuzini au kufanya tendo la ndoa kwa walio oa!

Hizo ni baadhi ya sababu kubwa na njia rahisi na kuepukana na tatizo hili ni:

Jitahidi kuoga mara tatu kwa siku au mbili kama ni mtu uliye bize na kazi...na mara baada ya kuoga jikaushe vizuri kwa kutumia taulo lililotengenezwa kwa pamba.

Boxers au chupi za material ya mpira si nzuri kwa mikoa ya joto kama Dar es salaam, Morogoro na dodoma kwa kuwa zinasababisha joto amablo hupelekea kutoa harufu....

Vaa boxer za matelia ya pamba ni bora zaidi na kufanya maeneo nyeti kuwa makavu wakati wote.


Pia hakikisha huvai nguo ya ndani kwa zaidi ya siku moja!!

Nakuhakikishia ukifanya hivyo uatakuwa msafi na kuvutia muda wote hata mahusiano yako na mpenzi wako yatadumu na kuwa yafuraha zaidi...

Jumatano, Desemba 29, 2010

Historia ya Krismasi

Wakati wa zama za kale, siku ya mwisho ya majira ya baridi huko sehemu za Kusini kulisherehekewa mfano wa usiku ambao mungu wa Mama Watakatifu alijifungua mtoto akijulikana kuwa ni mungu wa Jua. Pia (siku hii) inaitwa Yule, siku ambayo inasherehekewa mno kwa kurushwa pashpashi. Ambapo kila mtu atacheza na kuimba ili kuliamsha jua kutokana na usingizi wake mnono wa majira ya baridi.

Wakati wa Warumi, iliadhimishwa kwa kumsifu Satunusi (mungu wa mavuno) na Mithrasi (mungu wa kale wa nuru), huo ni mtindo wa kuabudia jua ambao umekuja ukitokea Syria hadi Urumi. Karne kabla ya madhehebu ya Sol Invictus, ilitangaza ya kwamba, majira hayo ya baridi sio ya milele, na kwamba maisha yanasonga mbele, na ni mualiko wa kubaki kwenye nguvu nzuri.

Siku ya mwisho ya majira ya baridi huko sehemu za mviringo za Kusini ni baina ya siku ya 20 au 22 Disemba. Warumi waliadhimisha Saturnalia baina ya tarehe 17 na 24 Disemba.

Wakristo wa kale

Ili kuepuka kuchunguzwa wakati wa sherehe ambazo ni za wapagani, Wakristo wa kale walikaa majumbani mwao pamoja na mtakatifu Saturnalia. Kwa vile idadi ya Wakristo iliongezeka na mila zao zikaenea, sherehe zikachukua shuruti za Kikristo. Lakini, Makanisa ya kale hakika hayakusherehekea mwezi wa Disemba kwa kuzaliwa Kristo hadi alipokuja Telesforusi Telesphorus, ambaye alikuwa askofu wa pili wa Roma kutoka mwaka 125 hadi 136 AD, askofu huyo ndiye aliyetangaza kwamba huduma za Kanisa zifanywe wakati huu ili kuadhimisha “Kuzaliwa kwa Bwana wetu na Mwokozi”. Hata hivyo, kwa vile hakuna mtu hata mmoja aliye na uhakika wa mwezi ambao amezaliwa Kristo, kawaida ya Uzawa ulikumbukwa Septemba, ambao ulikuwa ni wakati wa Sherehe za Kiyahudi za Trumpetsi (kwa sasa ni Rosh Hashanah). Ukweli ni kuwa, kwa zaidi ya miaka 300, watu walielewa kuzaliwa kwa Yesu katika tarehe tofauti.

Katika mwaka 274 AD, kikomo cha jua kiliangukia tarehe 25 Disemba. Mfalme wa Roma aitwaye Aurelian alitangaza tarehe hiyo kama ni “Natalis Solis Invicti”, ‘Sherehe Ya Kuzaliwa Jua Lisiloshindikana’. Katika mwaka 320 AD, Papa Julius I aliitangaza tarehe 25 Disemba kama ni tarehe rasmi ya kuzaliwa Yesu Kristo.

Mnamo mwaka 325 AD, Krismasi ilitangazwa rasmi, lakini kiujumla haikutiliwa maanani. Mtakatifu Constantine, ambaye ni Mfalme wa mwanzo wa dhehebu la Ukristo la Kirumi, aliitanguliza Krismasi kama ni sherehe isiohamishika kwa tarehe 25 Disemba. Pia aliitanguliza Jumapili kama ni siku kuu ndani ya siku saba za wiki, na aliitanguliza (Pasaka) kama ni sherehe yenye kuhamishika. Mnamo mwaka 354 AD, Askofu Liberius wa Rumi, alitoa amri rasmi kwa wafuasi wake kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu ndani ya tarehe 25 Disemba.

Hata hivyo, ingawa Constantine aliifanya rasmi tarehe 25 Disemba kama ni sherehe ya kuzaliwa Kristo, Wakristo wakiitambua kama ni tarehe ya sherehe iliyofanana na mapagani, hawakushiriki katika mambo mazuri (kwa siku hii) iliyopangwa na Askofu. Krismasi ilishindwa kupata utambulisho wa kilimwengu miongoni mwa Wakristo hadi kipindi cha hivi karibuni. Huko Uingereza England, Oliver Cromwell alizipiga marufuku sherehe za Krismasi baina ya miaka 1649 na 1660 kupitia kwa inayoitwa Sheria za Rangi Samawati Blue Laws, akiamini kwamba iwe ni siku ya kumuabudu mungu tu.

Hamu ya kuifurahia sherehe ya Krismasi ilikirimiwa pale Waprotestanto (Wakristo wasiokubali baadhi ya mafundisho ya Kanisa la Kirumi) walipokimbia uchunguzi kwa kutorokea sehemu za makoloni yote duniani. Hata hivyo, Krismasi bado haikuwa ni sikukuu halali hadi miaka ya 1800. Na, weka akilini, hakukuwa na picha ya Baba Krismasi (Santa Claus) kwa wakati huo.

Krismasi inaanza kuwa maarufu

Umaarufu wa Krismasi ulianza ghafla mnamo mwaka 1820 kutokana na kitabu cha Washington Irving The Keeping of Christmas at Bracebridge Hall ‘Kuiadhimisha Krismasi Kwenye Jukwaa La Bracebridge’. Mnamo mwaka 1834, Malkia wa Uingereza aitwaye Victoria, alimkaribisha mumewe wa Kijerumani Prince Albert ndani ya Ngome ya Windso Windsor Castle, akimuonesha tamaduni za mti wa Krismasi Christmas tree na Nyimbo Za Kumsifu Yesu Kristo carols ambazo ziliadhimishwa Uingereza kwa Mfalme wa Uingereza. Mwaka 1834, wiki moja kabla ya Krismasi, Charles Dickens alichapisha Nyimbo za Kumsifu Yesu za Krismasi Christmas Carols (ambapo aliandika kwamba Scrooge alimuamrisha Cratchit kufanya kazi, na kwamba Baraza Kuu la Marekani US Congress lilikutana Siku ya Krismasi). Ilikuja kuwa ni maarufu mno hadi kufikia kwamba sio makanisa wala serikali kukana umuhimu wa sherehe za Krismasi. Mnamo mwaka 1836, Alabama ilikuja kuwa ni taifa la mwanzo ndani ya Marekani kutangaza Krismasi kama sikukuu halali. Mnamo mwaka 1860, mfananishi illustrator wa Marekani aitwaye Thomas Nast alichukua kutoka hadithi za Kiingereza kuhusu Mtakatifu Nicholas, muangalizi mtakatifu wa watoto, kumtengeneza Baba Krismasi Father Christmas. Mwaka 1907, Oklahoma ilikuwa ni ya mwisho miongoni mwa mataifa ya Marekani kutangaza Krismasi kama ni sikukuu halali. Mwaka baada ya mwaka, nchi za dunia nzima zilianza kuitambua Krismasi kama ni siku ya kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu.

Nakuombea Krismasi Njema Have a merry Christmas

Leo, mambo mengi yasiyokuwa ya Kikristo yananasibishwa ndani ya Krismasi. Yesu alizaliwa mwezi wa Machi, bado siku yake ya kuzaliwa inasherehekewa Disemba ya 25, wakati wa solstice. Sherehe za Krismasi zinamalizikia siku kumi na mbili za Krismasi (Disemba 25 hadi Januari 6), ni idadi hiyo hiyo ya siku ambazo zilisherehekewa na wapagani wa ki-Rumi wakale kwa kuadhimisha kurudi kwa jua. Hivyo, hakuna mshangano wowote kwamba Wakristo waliosafi puritans – au Wakristo wasiotaka mabadiliko conservative – watahamaki kwa Krismasi kuwa “sio ya kidini kama ilivyotakikana kuwa,” wakisahau kwamba Krismasi haikusherehekewa hata kidogo hadi siku za hivi karibuni.

Yesu Alisemaje Kuhusu Krismasi?

Mazoea ya Krismasi

Mti ulio bora wa Krismasi unanunuliwa. Ukipambwa kwa madoido yenye kung’ara pamoja na kumetameta, unasimamishwa karibu na dirisha. Maduka yanajazana wanunuzi wakisaka zawadi na vile viduchu vinasubiri kwa hamu kubwa ya Baba Krismasi Santa.

Ni mshughuliko na ni homa ya Krismasi Christmas fever, umewahi kufikiri kabla? Je, Biblia au Yesu aliwahipo kusababisha homa ya Krismasi?

Tafakari juu ya mchanganuo ufuatao kuhusu Krismasi, na ukweli utakuja kuwa wazi zaidi na zaidi.

Je, Krismasi Ina Ushahidi wa Biblia?

Neno ‘Krismasi’ halipo ndani ya Biblia. Biblia ilifunga midomo ya sherehe yote inayohusiana na Krismasi, isipokuwa kwa kitu kimoja; upambaji wa mti. Biblia wenyewe inashutumu upambaji wa miti (ya Krismasi):

“Mila za watu si chochote, wanakata mti kutokana na msitu, na mchongaji anauchonga kwa patasi yake, wanaupamba kwa fedha na dhahabu, wanaugandanisha kwa nyundo na misumari ili usipate kutikisika” (Jeremia 10-3,4).

Wazungu wa ki-Pagani kabla ya Ukristo, waliamini miujiza kwamba miti ya kijani ina nguvu maalum za ulinzi. Hakika, matumizi ya Miti ya Krismasi imeanza hivi karibuni tu mwa karne ya 17 huko Strasbourg, Ufaransa na kutoka huko ukaenea hadi Ujerumani, Uingereza na baadaye Marekani. “Ibada ya miti ilikuwa ni jambo la kawaida kwa dini miongoni mwa watu wa Tyutoniki Teutonic na Skandinavia Scandinavia wa Ulaya ya kaskazini kabla ya kuingia kwenye Ukristo…Walowezi wa ki-Jerumani walileta mila za Mti wa Krismasi kwenye makoloni ya Kimarekani mnamo karne ya 17. Kufikia karne ya 19, matumizi yake yalienea sehemu tofauti”. (Angalia Encyclopedia ya Compton, Toleo la 1998)

Je, Yesu Alizaliwa Disemba ya 25?

Si tarehe ya Disemba 25 wala tarehe nyengine yoyote iliyotajwa ndani ya Biblia kuhusu kuzaliwa kwa Yesu. Ilikuwa ni hivyo hadi kufikia mwaka 530 C.E kwamba mtawa monk aitwaye Dionysus Exigus, aliweka tarehe isiyobadilika ya kuzaliwa kwa Yesu kuwa ni Disemba 25. “Kulingana na taratibu za ki-Roma, alikosea kuipanga tarehe ya kuzaliwa kwa Kristo (yaani, miaka 754 baada ya kupatikana nchi ya Rumi) kama ni Disemba 25, mwaka 753”. (Angalia: Encyclopedia Britannica, toleo la mwaka 1998) Tarehe hii ilichaguliwa ili iendane pamoja na sikukuu ambazo zimeshagandana na imani za kipagani.

Mapagani wa Kirumi walisherehekea Disemba 25 kama ni ya kuzaliwa kwa ‘mungu’ wao wa nuru, aitwaye Mithra.

“Mnamo karne ya pili A.D, hiyo sherehe ya Mithra ilikuwa ni ya kawaida zaidi ndani ya Ufalme wa Rumi kuliko Ukristo, ambayo ilizaa mifanano iliyo mingi” (The Concise Columbia Encyclopedia, toleo la mwaka 1995).

‘Waungu’ wengine wakipagani waliozaliwa Disemba ya 25 ni: Hercules mtoto wa Zeuz (Wagiriki); Bacchus, ‘mungu’ wa mvinyo (Warumi); Adonis, ‘mungu’ wa Kigiriki, na ‘mungu’ Freyr wa Ugiriki-mapagani wa Roma.

Je, Vipi Kuhusu Baba Krismasi Santa Claus?

Kama viumbe visivyokuwa binaadamu aliens watafika duniani katika wakati wa Krismasi, bila ya shaka wataamini Krismasi kuwa ni sherehe ya kufurahikia kuzaliwa kwa Baba Krismasi Santa. Majina ya ‘Santa Claus’, hayamo popote ndani ya Biblia.

Hata hivyo, Mtakatifu Nikolas Saint Nicholas (Baba Krismasi Santa Claus) alikuwa ni mtu halisi, askofu, ambaye alizaliwa miaka 300 baada ya Yesu. Kwa mujibu wa hekaya za kale, alikuwa ni mtu mwenye huruma mno na alitenga nyakati za usiku kwenda kutoa zawadi kwa mafukara. Baada ya kifo chake mnamo Disemba ya 6, watoto wa shule huko Ulaya walianza kusherehekea siku hiyo kwa karamu kila mwaka.

Baadaye Malkia Victoria aliibadilisha sherehe hiyo kutoka Disemba ya 6 kuwa ni Disemba ya 24 kuamkia Krismasi.

Je, Yesu au Wafuasi Wake Waliwahi Kusherehekea Krismasi?

Kama Yesu alimaanisha kwa wafuasi wake kusherehekea Krismasi, angeliifanyia kazi yeye mwenyewe na kujikusanya pamoja na wafuasi wake. Hakuna sehemu iliyotajwa ndani ya Biblia kwamba kuna mfuasi yeyote aliyewahi kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu kama Wakristo wanavyofanya leo.

“Kanisa halikupatapo kuweka sikukuu kwa ajili ya sherehe za tukio la Krismasi hadi ilipofika karne ya 4” (Angalia: Encyclopedia ya Grolier)

Hivyo, tunaona kwamba sio Biblia wala Yesu na wafuasi wake waliosema kitu kuhusu sherehe za Krismasi ambazo sasa zinahusisha viingilio vya sherehe, biashara, na matumizi yaliyochupa mpaka, ni utovu wa akili kwa mfananisho wowote wa imani.

Hukumu Ya Krismasi Na Mwaka Mpya

Shukrani Ziende kwa Allaah

Shaykh al-Islaam bin Taymiyah (Allaah Amrehemu) alisema kwenye fafanuzi yake katika Aayah (tafsiri ya maana):

{{Na wale ambao hawashuhudii shahada za uongo (az-zuur)…}} [al-Furqaan 25:72]

Ama kuhusu sherehe za mushrikiyn: wanakusanya pamoja mambo yenye kutia wasiwasi, mahitaji ya mwili na uongo, hakuna chochote ndani yake ambacho kina faida ya kidini, na mwisho wa kutosheleza hizo shahawa, ni maumivu. Hivyo, vitendo vyao ni vya uongo, na kuvishuhudia kunamaanisha kuvifanya. Hii Aayah peke yake inawapandisha daraja na kuwapa moyo (wale ambao hawashuhudii uongo), ambayo ina maana ya kuwahimiza watu kuachana na kushiriki kwenye sherehe zao (mushrikuun) na aina nyenginezo za uongo. Tunafahamu kwamba ni vibaya kushiriki kwenye sherehe zao kwa sababu wanaitwa az-zuur (waongo). Inamaanisha kwamba ni haraam kufanya hivi kwa sababu zilizo nyingi, kwa sababu Allaah Ameiita ni az-zuur.

Allaah Anamlaumu yule anayezungumza uongo (az-zuur) hata ikiwa hamna yeyote atakaeathirika nao, kama ilivyo ndani ya Aayah ikikataza Dhwihaar (aina ya talaka ambapo mume anamwambia mkewe “Wewe kwangu ni kama mgongo wa mama yangu”), ambapo Yeye Anasema (tafsiri ya maana):

{{…Wanasema neno baya na la uongo (zuuran)…}} [al-Mujaadilah 58:2].

Na Allaah Anasema (tafsiri ya maana):

{{…basi jiepusheni na uchafu wa masanamu na jiepusheni na usemi wa uongo.}} [al-Hajj 22:30].

Hivyo yule ambaye anafanya az-zuur analaumiwa kwa mtindo huu. Ndani ya Sunnah:

Anas bin Maalik (Allaah Amrehemu) amesema: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja (Madiynah) na walikuta siku mbili ambazo kipindi cha Jaahiliyyah watacheza (na kujipumzisha).” Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Allaah Amekupeni kilicho bora zaidi kuliko mambo hayo: Yawm adh-Dhuhaa (‘Iyd al-adh haa) na Yawm al-Fitr (‘Iyd al-Fitr).” (Imesimuliwa na Abuu Daawuud).

Hii inaonesha wazi kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya shaka alizuia Ummah wake kusherehekea sherehe za kikafiri, na alihakikisha kuziondosha kwa njia zozote zinazowezekana.

Ukweli wa kwamba dini ya Watu wa Kitabu inakubaliwa, haina maana kwamba sherehe zao zinakubalika au ziendelezwe na Ummah, kama yalivyo matendo yao mengine ya kikafiri yasivyokubalika, na dhambi zao pia hazikubaliki. Hakika, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifikia hadi kuamrisha Ummah wake kujitofautisha nao kwenye mambo mengi ambayo ni mubaah (yanaruhusiwa) na kwa taratibu nyingi za ibada, kwa sababu tu; kwamba vinapelekea kuwa sawa nao kwenye mambo mengine pia. Hii kuweka tofauti; ni kuonesha kizuizi katika nyanja zote, kwa sababu namna utakavyokuwa tofauti na watu wa Motoni, ndivyo utakavyokuwa mchache wa kutenda matendo ya watu wa Motoni.

Ushahidi wa mwanzo ni Hadiyth ya: “Kila watu wana sherehe zao, na hii ndio sherehe yetu” ambayo ina kusudio maalum kwamba; watu wote wana sherehe zao wenyewe, kama Allaah Anavyosema (tafsiri ya maana):

{{Na kila ummah ulikuwa na Qiblah walichokielekea…}} [al-Baqarah 2:148] na

{{Na kila (ummah) katika nyinyi (binaadamu) Tumeujaalia sharia yake na njia yake.}} [al-Maaidah 5:48].

Hii inamaanisha kwamba kila taifa lina njia zake wenyewe. Hiyo laam ndani ya li-kulli (“kwa kila”, “katika nyinyi”) ina maana kwa watu maalum. Hivyo, kama Mayahudi wana sherehe na Wakristo wana sherehe, ni za kwao wenyewe, na sisi hatuna sehemu yetu ndani ya hizo sherehe, kama vile tusivyotumia Qiblah kimoja au sheria zao.

Ushahidi wa pili ni: masharti aliyoweka ‘Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ‘anhu) na kukubaliana pamoja na Swahaabah na Fuqaaha wote baada yao ni: kwa wale Watu wa Kitabu ambao wamekubali kuishi chini ya hukumu za Kiislamu (ahl adh-dhimmah) wasisherehekee sherehe zao wazi wazi ndani ya Daar al-Islaam (ardhi zilizo chini ya hukumu za Kiislamu). Kama Waislamu wamekubaliana kuwazuia ahl adh-dhimmah kusherehekea wazi wazi, ni namna gani itakuwa sahihi kwa Waislamu kushereheka nao wazi wazi? Kama Muislamu atawasherehekea, jee sio zaidi ya kafiri anavyofanya wazi wazi?

Sababu iliyokuwepo ya sisi kuwazuia wasisherehekee sherehe zao wazi wazi ni kwa sababu ya machafu yaliyokuwemo humo. Kwa sababu ya dhambi au alama ya dhambi. Katika kesi yoyote, Muislamu anazuiwa kutenda dhambi au kujaribu kutenda dhambi. Hata kama hakuna uadui wowote kwa Muislamu kuwa nao pamoja katika kusherehekea wazi wazi isipokuwa kafiri kupata nguvu ya kuendelea na matendo yake. Inakuwaje Muislamu anatenda hivyo? Uadui uliokuwemo (ndani ya sherehe zao) utaelezwa chini, insha Allaah.

Al-Bayhaqiy amesimulia ikiwa na isnaad swahiyh kwenye Baab karaahiyat ad-dukhuul ‘ala ahl adh-dhimmah fi kanaa’isihim wat-tashabbuh bihim yawmi nawruuzihim wa maharjaanihim (Sura kuhusu karaha ya kuingia kwenye makanisa ya ahl adh-Dhimmah (Makafiri walio katika nchi ya Kiislam) katika kuadhimisha Mwaka wao Mpya na sherehe nyengine): Kutokana na Sufyaan ath-Thawri na kutokana na Thawr bin Yaziyd na kutokana na ‘Atwa’ bin Diynaar ambao wamesema: ‘Umar amesema: “Musijifunze lugha ya wasiokuwa Waarabu, musiingie pamoja na mushrikiyn kwenye makanisa yao katika siku za karamu zao, kwani laana (za Allaah) zinawashukia juu yao.”

‘Umar bin al-Khattwaab amesema:

“Jiepusheni na maadui wa Allaah kwenye sherehe zao.” Imesimuliwa kutokana na Abuu Usaamah ikiwa na isnaad iliyo sahihi kwamba: ‘Awn alituambia kutokana na Mughiyrah kutokana na ‘Abdullaah bin ‘Amr: “Yeyote anayeishi ndani ya ardhi ya wasiokuwa Waarabu na kusherehekea Mwaka wao Mpya na sherehe zao, na kujifananisha nao hadi anafariki akiwa na hali hiyo, atakusanywa pamoja nao kwenye Siku ya Malipo.” ‘Umar alikataza kujifunza lugha zao, na hata kuingia kwenye makanisa yao katika siku ya sherehe yao, jee ni vipi kwa kufanya baadhi ya mambo wanayoyafanya kwenye siku hizo, au kufanya vitu ambavyo ni sehemu ya dini yao? Je, sio kufanya baadhi ya vitu wanavyofanya kwenye sherehe zao ni (uovu) zaidi ya kuingia tu kwenye sherehe zao? Kama laana za Muumba zitaanguka juu yao kwenye siku ya sherehe yao kwa sababu ya yale wanayofanya, je, adhabu hiyo haitokuwa sawa kwa yule anayefanya yale wanayotenda wao, au sehemu ya hayo? Je, sio maneno ya: “Jiepusheni na maadui wa Allaah, kwenye sherehe zao” yana maana kwamba tusikutane nao au kushirikiana nao kwenye siku hizi? Je, ni vipi kwa mtu ambaye hakika anasherehekea sherehe zao?

‘Abdullaah bin ‘Amr amesema kwa uwazi:

“Yeyote anayeishi ndani ya ardhi ya wasiokuwa Waarabu na kusherehekea Mwaka wao Mpya na sherehe zao, na kujifananisha nao hadi anafariki akiwa na hali hiyo, atakusanywa pamoja nao kwenye Siku ya Malipo.”

Hii inamaanisha kwamba yule anayejikusanya nao kwenye mambo yote haya ni kafiri, au kwamba kufanya hivi ni miongoni mwa dhambi kubwa (kabaa’ir) kwamba itampelekea mmoja wao Motoni; maana ya iliyopita ni ile iliyo wazi kutokana na mpangilio wa maneno. Alitaja – Na Allaah Ndie Ajuaye Zaidi – yule anayeishi kwenye ardhi yao, kwa sababu wakati wa ‘Abdullaah bin ‘Amr na Swahaabah wengineo, walikuwa wakizuia sherehe zilizo wazi za kikafiri ndani ya ardhi za Waislamu. Na hakuna Muislamu aliyewaiga kwenye sherehe zao; hilo (la kusherehekea) pale ambapo wanapoishi kwenye ardhi za kikafiri. ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikataa hata kulitambua jina la sherehe zao ambazo zilikuwa mahsusi kwa ajili yao, je, itakuwaje kwa kushereheka nao kisawasawa? Ahmad ametaja maana ya simulizi zilizopokelewa kutokana na ‘Umar na ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kwenye mada hii, na wafuasi wake walijadili masuala ya sherehe.

Imaam Abul-Hassan al-‘Aamidiy alisema: mwandishi anayejulikana kwa jina la Ibn al-Baghdaadi alisema ndani ya kitabu chake Umdat al-Haadhwir wa Kifaayat al-Musaafir: “Hairuhusiwi kuingia kwenye sherehe za Wakristo na Mayahudi.” Ahmad alitamka hili kwenye simulizi ya Muhannaa, na ushahidi wake wa hilo ni Aayah (tafsiri ya maana):

{{Na wale ambao hawashuhudii shahada za uongo (az-zuur)…}} [al-Furqaan 25:72]

Alisema: (Hizi sherehe ni) ash-Sha’aaniyn pamoja na sherehe zao. Alisema: Waislamu wazuiliwe kuingia kwenye masinagogi (makanisa ya Kiyahudi) na makanisa (ya Wakristo).”

Kutokana na Iqtidhwa’ as-Swiraat al-Mustaqiym Mukhaalifat Aswhaab al-Jahiym iliyoandikwa na Shaykh al-Islaam bin Taymiyah, uk. 183.

Kuwatakia kheri ya Krismasi Makafiri na hata sikukuu nyengine za dini tofauti ni haraam kwa mujibu wa makubaliano ya wengi, kama Ibn al-Qayyim (Allaah Amrehemu) alisema kwenye Ahkaam Ahl adh-Dhimmah.

Kuwatakia kheri Makafiri katika mwenendo ambao ni kwa ajili yao ni haraam kwa makubaliano ya wengi, kama ilivyo haraam kuwatakia kheri katika sherehe zao na funga zao kwa kusema ‘Kila la kheri katika sherehe’ au ‘Nakutakia sherehe njema’, na mengineyo. Hata kama yule anayesema haya ameepushwa na ukafiri, lakini bado imekatazwa. Ni kama vile kumpa hongera mtu kwa kuuhami msalaba, au zaidi ya hivyo. Ni kama mfano wa dhambi iliyo kubwa sawa na kumpa hongera mnywaji ulevi, au kumuua mtu, au kuwa na mahusiano ya kinyama, na mengineyo. Wengi miongoni mwa wasio na heshima ya dini yao wanaangukia kwenye kosa hili; hawakai kufikiria ubaya wa vitendo vyao. Yeyote anayempa hongera mtu kwa kutovukwa na adabu au bid’ah au ukafiri amejiweka wazi na laana pamoja na ghadhabu za Allaah.”

Kuwapatia hongera makafiri kwenye sherehe za kidini ni haraam kama alivyokwenda mbali Ibn al-Qayyim kwa kufananisha na kwamba yule anayetoa salamu hizo amekubali au ameidhinisha matendo yao ya kikafiri, hata kama mtu hatovifanya mwenyewe vitu hivyo. Lakini Muislamu asikubali mienendo ya kikafiri wala kumpa hongera yeyote kwa ajili yao, kwa sababu Allaah hakubali matendo yoyote kati ya hayo, kama Alivyosema (tafsiri ya maana):

{{Mkikufuru, basi Mwenyezi Mungu hana haja nanyi; lakini Haridhii kufuru kwa waja Wake; na kama mkishukuru; hayo Yanamridhisha kwenu.}} [Az-Zumar 39:7]

{{…Leo nimekukamilishieni Dini yenu, na kukutimizieni neema Yangu, na Nimekupendeleeni Uislamu uwe Dini yenu…}} [Al-Maaidah 5:3]

Hivyo kuwapa hongera kunazuiwa, hata ikiwa ni mwenzio kazini au vyenginevyo. Kama wao watatutakia kheri kwa kuadhimisha sherehe zao, hatutakiwi kujibu, kwasababu hizi sio sherehe zetu, na kwasababu sio sherehe ambazo zinakubalika na Allaah. Sherehe hizi ni uzushi ndani ya dini zao, na hata zile ambazo zimetajwa huko kabla zimetenguliwa na dini ya Kiislamu, ambayo Ameileta Allaah kwa wanaadamu wetu kupitia kwa bwana Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Allaah Anasema (tafsiri ya maana):

{{Na anayetaka dini isiyokuwa ya Kiislamu basi haitakubaliwa kwake. Naye Akhera atakuwa katika wenye khasara (kubwa kabisa)}} [Aaali-‘Imraan 3:85]

Ni haraam kwa Muislamu kukubali mialiko katika sherehe kama hizo, kwa sababu ni zaidi ya kuwatakia kheri kama inavyoonesha kushiriki katika sherehe zao. Vile vile, Waislamu wanazuiwa kuwaiga makafiri katika kuadhimisha huko kwa kushiriki kwenye tafrija parties, au kwa kubadilishana zawadi, au kutoa peremende au chakula, au kuacha kufanya kazi, n.k. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema “Yeyote anayewaiga watu ni mmoja wao.”

Shaykh al-Islaam bin Taymiyah amesema ndani ya kitabu chake Iqtidhwaa’ as-Swiraat al-Mustaqiym Mukhaalifat Aswhaab Al-Jahiym:

“Kuwaiga katika baadhi ya sherehe zao inamaanisha kwamba mtu amefurahia imani zao za uongo na vitendo vyao, na anawapa matumaini kwamba wanaweza kuwa na nafasi ya kuwanyanyasa na kuwapeleka ovyo wanyonge.” Yeyote anayefanya mambo kama haya ni mtenda dhambi, ikiwa anafanya kwa ukarimu au urafiki, au kwa sababu anaona hayaa kukataa, au kwa sababu nyengine yoyote. Kwa sababu ni unafiki ndani ya Uislamu, na kwa sababu inawafanya makafiri kujisikia fakhari kwa dini yao.

Allaah Pekee ndiye tunayemuomba kuwafanya Waislamu kuwa fakhari na dini yao, kuwasaidia kuwa thaabiti katika kushikamana na dini yao, na kuwafanya kuwa washindi dhidi ya maadui zao, kwani Yeye Mwenye Nguvu ndiye Mwenye Kuweza.

MTAYARISHAJI



Ni mtu anayechukua hatua ya kufanya myenendo ya rekodi za muziki, ambaye anataka kufanana kabisa na mwongozaji wa filamu pale anachokua hatua ya kuongoza filamu. Mtayarishaji wa muziki husaidia
|mwanamuzik
i|wanamuziki
na wa
sanii wanaofanya rekodi zao za nyimbo moja-moja au albamu iliyokamili.



Mtayarishaji:

Ni mtu anayetengeneza kitu au kukiandaa, kuangalia mazingira gani yatafaa kutayarishia k.m. filamu n.k. Pia mtayarishaji huwa anapata msaada mkubwa kutoka kwa muongozaji ambaye yeye huwaweka wasanii sawa vipi filamu itatakiwa iwe n.k.
Ila kwa mtazamo ambao watu wengi wamezoea kuuona na kusikia ni kwamba mtayarishaji huwa mtu anayetengeneza filamu au nyimbo.

Mwongozaji ni mtu anayetoa msaada wa kuongoza pindi mtu anapoigiza filamu. Wanaangalia vitu vya kisanii visiende kombo. Wanatoa maelekezo kwa waigizaji na kuongoza watu katika uigizaji wa filamu.

Mwongozaji:

wa filamu yeye ndiyo anayochukua jukumu zima la wanachama wanaofnya kazi ya uigizaji (waigizaji, watayrishaji, na kadharika). Kwa mfano, mtu yule ambaye anashughulika na taa anamwambia mtindo gani unaotakiwa taa imulikwe pindi yeye anapotoa maelekezo kwa waigizaji.

Ni kawaida sana kwa waongozaji wa filamu kufanya kazi pamoja na mtayarishaji. Mtayarishaji wa filamu ni mtu asiyehusika na upande wa kisanii wakati wa utengenezaji wa filamu. Kwa mfano, wao ndiyo wanaoshikiria fedha zote ambazo zinatumika kwa ajili ya utengenezaji wa filamu.



Jumanne, Desemba 28, 2010

Wanauchumi wa China watajirika kutokana na uvumbuzi

Hivi sasa uchumi wa China unakuzwa kwa haraka, watu wanasikia habari kuhusu watu wengi wanaotajirika au kuwa mashuhuri kwa usiku mmoja. Katika kipindi hiki cha leo nitawafahamisha vijana wawili waliojiajiri katika miaka ya 80 ya karne iliyopita. Vijana hao ni wenye umri wa miaka 24 au 25 hivi, lakini walipewa mikopo ya kuwekeza vitega-uchumi kutokana na uvumbuzi wao. Hivi sasa wamekuwa matajiri wenye Yuan milioni kumi kadhaa hata mia kadhaa, hivi sasa wakati vijana chipukizi wenye umri wa miaka kama wao, wanapoanza kuingia katika jamii, hao wamekuwa mahiri katika masoko ya biashara.

Mao Kankan ana umri wa miaka 22, ni kama vijana wengi wa mijini, moja ya burudani anayopenda sana ni kwenda kuimba katika jumba la Karaoke. Lakini baada ya kufika ofisini anaonekana kama ni mtu mwingine kabisa, yeye ni ofisa mtendaji wa kwanza wa kampuni ya kazi za viwanda ya Aihang. Jambo linalostaajabisha ni kuwa hivi sasa anaongoza kampuni ya Aihang kuwekeza Yuan za Renminbi milioni 300 kujenga kituo pekee cha michezo ya tarakimu mjini Beijing.

"Mnamo alasiri ya tarehe 28 mwezi Mei, mwaka 2010 saa 9 na dakika 58, ndege moja ya kijeshi ya nchi ya A ilitunguliwa ikiwa njiani kupeleka habari muhimu za siri, na habari hizo zikapotea. Hivyo nchi mbili za A na B zikawa na mchuano mkali wa kugombea kupata habari hizo muhimu."

Bw. Mao Kankan alikuwa akieleza mchezo alioubuni yeye pamoja na kundi lake, ambao utachezwa kwenye bustani moja ya Beijing. Wazo la kubuni mchezo huo utakaochezwa na watu ni la Bw. Mao Kankan, kwa kufuata wazo lake kila mtu anayeingia kwenye bustani anatakiwa kuvaa mavazi yanayolingana na mhusika wa mchezo. Kwa kutumia teknolojia ya mwigo (dummy) ya kisasa, hatimaye kutakuwa na watu zaidi ya 100, ambao wanashindana katika kutafuta hazina ndani ya bustani.

Mchezo wa elektroniki kubadilishwa kuwa maonesho ya watu halisi, kwa Mao Kankan ni mradi mkubwa unaoweza kutimiza tumaini lake.

"Ikiwa mambo hayo yanaweza kutendeka, baada ya miaka 5 yataweza kuleta faida ya zaidi ya Yuan bilioni 1, nimekadiria faida itakuwa Yuan bilioni 1.5."

Mao Kankan mwenye umri wa miaka 22, hajawekeza hata senti moja, lakini kutokana na wazo lake hilo, atapata karibu 20% ya hisa za mradi huo, ambao utaweza kuleta faida ya Yuan bilioni 1.5 kwa mwaka. Endapo mradi huo utatekelezwa, mali ya Mao Kankan itakuwa kubwa ajabu.

Wakati watu wengi wanashangaa kuhusu mali nyingi atakayopata Mao Kankan, tunamfahamu kijana mwingine, ambaye ana umri wa miaka karibu sawa na Mao Kankan, tofauti iliyopo ni kuwa kijana huyu alishapata mali nyingi.

Kijana huyu ni Li Xiang, ofisa mtendaji wa kwanza wa tovuti ya Mapovu. Hivi sasa anaongoza tovuti ya chombo kimoja cha habari inayotoa huduma kwa aina mbalimbali za bidhaa za teknolojia ya tarakimu. Bw. Li Xiang alipozungumzia tovuti aliyoanzisha, alisema,

"Tunatoa huduma kamili, ambayo ni ya kipekee kwa hivi sasa miongoni mwa tovuti kwenye mtandao wa Internet. Pengine tovuti yetu ni tovuti inayoweza kuunganisha vizuri web 1.0 na web 2.0, na kuweza kuleta faida pia."

Mwaka 2005, pato la tovuti ya Mapovu lilikuwa Yuan zaidi ya milioni 20, na faida ilikuwa Yuan zaidi ya milioni 10, na hisa anazomiliki kijana Li Xiang ni zaidi ya 50%.

Mafanikio waliyoyapata vijana hao wawili yanawashangaza sana watu. Lakini jambo lingine linalowashangaza watu zaidi ni kuwa vijana hao wawili wote hawana elimu ya chuo kikuu. Basi, vijana Mao Kankan na Li Xiang walifanyaje hadi kupata mafanikio makubwa ya namna hii?

Mao Kankan alikosa nafasi ya kushiriki kwenye mtihani wa kuingia vyuo vikuu kutokana na mafanikio duni katika somo la jiografia alipokuwa shule ya sekondari, halafu aliacha kabisa masomo ya shuleni. Lakini alisema kutosoma katika chuo kikuu hakukuwa na maana ndiyo mwisho wa elimu yake. MaoKankan alisema, "Wakati ule watu walithamini uthibitisho wa kampuni kubwa za kimataifa ikiwemo kampuni ya Microsoft, lakini sasa kuna thibitisho za aina nyingi, hata mtu anaweza kuziokota barabarani, lakini zilipokuwa na thamani, nilizipata nikiwa na umri wa miaka 17. Bado ninakumbuka kuwa wakati ule katika bara la Asia kulikuwa na vijana wawili wenye umri wa chini ya miaka 18, nilipata thibitisho 7 au 8 hivi, karibu nilipata uthibitisho wote."

Mafanikio ya Li Xiang kwenye tovuti ya Mapovu yanatokana na shauku yake kubwa juu ya kompyuta. Alipenda sana kompyuta tangu alipokuwa anasoma katika shule ya sekondari, na alianzisha tovuti yake katika Internet ya kutoa habari kuhusu vipuri za kompyuta.

Li Xiang hakutazamia kuwa shauku yake inaweza kuleta nafasi ya biashara, wafanyabiashara wa matangazo waliwekeza kwenye tovuti ya Li Xiang, ilikuwa kiasi cha Yuan zaidi ya 6,000 kwa mwezi. Hali hiyo iliendelea kwa miaka 3, kabla ya mtihani mkuu wa kuingia chuo kikuu, Li Xiang alifanya uamuzi muhimu wa kuacha masomo ya chuo kikuu ili apate nafasi ya kushughulikia tovuti yake.

Mao Kankan hakujali sana kuhusu kukosa nafasi ya kusoma katika chuo kikuu, isipokuwa anaona masikitiko kidogo kwa kukosa uzoefu wa kipindi hicho. Lakini Mao Kankan na Li Xiang wote wanaona kuwa vijana wakitaka kupata mafanikio, kitu muhimu siyo kama kuwa shahada au la, bali ni kuona kama ameweka lengo lake au la, na kama amefanya juhudi za kutosha kutimiza lengo lake.

Ingawa Mao Kankan na Xi Xiang wamepata mafanikio ambayo vijana wengine wa rika hilo huenda hawawezi kuyapata, lakini bado kuna watu wengi ambao wana mashaka kuhusu Mao Kankan na Li Xiang kama wanaweza kusimamia vizuri kampuni zao. Vijana wenye umri wa miaka 20 na kidogo, ambao wanamiliki mali nyingi, lakini hawakupata elimu ya juu, wana uwezo wa kuepusha kampuni zao na mambo ya hatari katika masoko yaliyojaa "mawimbi na upepo mkubwa"? Li Xiang alisema, katika muda wa miaka 8 iliyopita tangu aanze kushughulikia mambo ya biashara, amepambana na shida nyingi, na amepata uzoefu muhimu wa usimamizi. Alisema, "Nilifanya makosa mengi, na nilipatwa na shida za aina mbalimbali. Lakini niliweza kuzitatua vizuri, tena nimekuwa na uwezo wa kutatua matatizo hayo, hivyo nimepanda ngazi, ninaona hilo ni jambo zuri, na sioni mambo kama hayo ni mabaya."

Kwa Mao Kankan na Li Xiang, njia yao ya mbele ni ndefu sana. Sasa hatuwezi kutabiri mustakabali wao na wa kampuni zao. Lakini matokeo ya baadaye, kwa kundi la vijana wanaotafuta mali, linalowakilishwa na Mao Kankan na Li Xiang, yatabadilisha kanuni za shughuli za masoko ya jadi ya China, na kuongeza uvumbuzi mpya wa mali.

Laptop OR Desktop

Kansa ya vidole jamani .
Imeonekana ipo kama mtu atatumia sana laptop/desktop/baada ya muda flani atapata kansa ya vidole usiku nimeota ndoto hii.

Kuna mdau mmoja kwenye Facebook alieleza kuhusu jambo hili.
See or Visit hapa:
http://www.facebook.com/amani.ngussa


SI MNAJIDAI MNAWEZA MAZOEZI? HAYA SASA


SI LELE MAMA ATI! UP JUU! UP JUU! SHUSHA TENA

Jumanne, Desemba 21, 2010

SARAKASI


Dawaz ni usanii wa jadi wa mchezo wa sarakasi wa kabila la Wauyghur. Maana ya "Dawaz" katika lugha ya Kiuyghur ni "kutembea kwenye kamba iliyofungwa juu". Mchezo wa Dawaz una historia zaidi ya miaka 2,000, na unapendwa sana na watu wa makabila mbalimbali wanaoishi katika mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Wauyghur. Kikundi cha sarakati ya Dawaz cha shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang ni kikundi maalumu kwa ajili ya kufanya maonesho ya mchezo wa Dawaz, na wamefanya juhudi kubwa katika kurithisha na kuendeleza usanii wa mchezo wa Dawaz, na kufanya usanii huo uwe na mvuto mkubwa duniani siku hadi siku.

Kiongozi wa kikundi hicho Bw. Adil Hoxur ni mrithi wa kizazi cha sita wa usanii wa mchezo wa Dawaz. Bw. Hoxur alizaliwa mwaka 1971 katika familia moja ya wachezaji wa Dawaz iliyoishi katika wilaya ya Yingjisha ya sehemu ya Kashi mkoani Xinjiang. Baba yake ni mchezaji maarufu wa Dawaz wa sehemu hiyo. Alipokuwa mdogo, mara kwa mara aliwasikia mama na kaka yake wakisema baba yake anaweza kufanya kitendo cha ajabu anapotembea kwenye kamba. Alisema, "Mimi na ndugu zangu tulishindwa kujifunza kitendo hicho. Baba yetu aliweza kupanda kamba iliyofungwa juu kwa pembe ya digrii 45 kwa miguu tu huku akiwa amebeba mtu, na miguu yake inashikilia kamba vizuri kama koleo. Baba yangu aliweza kufanya kitendo hicho mpaka alipokuwa na umri wa miaka 72, na mwaka huo alifanya maonesho yake ya mwisho ya Dawaz kwa wakazi wa wilaya ya Yingjisha."

Baba wa Bw. Hoxur alikataa kumfundisha Hoxur ufundi wa Dawaz, kwani alifahamu sana kuwa ni mchezo wenye hatari kubwa. Bw. Hoxur alipokuwa mdogo, hakujua sana Dawaz. Alisema, "Baba yangu alifariki dunia nilipokuwa na umri wa miaka mitano. Nilipokuwa mdogo sikujua sana Dawaz. Mama yangu aliniambia kuwa familia yangu imekuwa familia ya wachezaji wa Dawaz kizazi baada ya kizazi. Alinielezea maana ya Dawaz akichora picha kwenye ardhi, na kusema wachezaji wa Dawaz wanaweza kutembea kwenye kamba iliyofungwa juu kwa urefu wa mita 21 ardhini. Nilishagaa sana kuwa baba yangu aliweza kupanda sehemu iliyo juu namna hii, nikaamua kuiga mfano wa baba yangu na kujifunza Dawaz. Baadaye nilifahamu vizuri mchezo wa Dawaz hatua kwa hatua na kuupenda mchezo huo siku hadi siku."

Wakati wa kusherehekea sikukuu, watu wa kabila la Wauyghur hawawezi kukosa maonesho ya Dawaz. Kwa kawaida maonesho hayo yanafanyika kwenye uwanja ulio wazi, wachezaji wa Dawaz wanatembea tembea juu ya kamba inayofungwa juu kwa urefu wa mita kumi kadhaa kutoka ardhi, na kufanya vitendo mbambali. Maonesho hayo huwasisimua sana watazamaji.



Mwaka 1986, Bw. Hoxur alikwenda mjini Urumuqi kwa mara ya kwanza, na kufanya maonesho ya Dawaz kwa ajili ya wanamichezo wa Michezo ya tatu ya watu wa makabila madogo madogo nchini China. Maonesho hayo yalimfanya afahamike sana na watu wengi. Bw. Hoxur alisema, "Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufanya maonesho hadharani mbele ya watu wengi. Watazamaji hao walishangilia na kupenda sana maonesho yangu, na wengi wao walituomba kupiga picha nao. Nilitambua kuwa chaguo langu la kujifunza Dawaz ni zuri, na niliona kuwa mimi ni shujaa, naweza kufanya jambo ambalo watu wengine hawathubutu kufanya."

Ili kuendeleza na kustawisha usanii ywa mchezo wa Dawaz, mwaka 1990 serikali ya mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Wauyghur iliwakusanya wachezaji wa Dawaz wa kabila la Wauyghur na kuunda kikundi cha maonesho. Hali hii ilitoa fursa nzuri kwa ajili ya maendeleo ya Dawaz. Mkuu wa shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang Bw. Anwar Mammat alisema, "Baada ya wachezaji hao 20 wa Dawaz kujiunga na shirika letu, tulifanya kazi nyingi za kuhakikisha usalama. Dawaz ni mchezo wa jadi, ili kuufanya mchezo huo uwe na thamani kubwa zaidi ya kisanaa, tulifanya marekebisho katika mambo mbalimbali."

Zamani maonesho ya mchezo wa Dawaz yalifanyika kwenye uwanja ulio wazi, hivi sasa maonesho hayo pia yanafanyika kwenye jukwaa la opera. Katika miaka ya hivi karibuni, Bw. Hoxur pamoja na wenzake walivumbua vitendo vingi vipya vyenye hatari kubwa, vikiwemo kupanda baiskeli yenye gurudumu moja, kuvingirisha bakuli na kuruka kamba juu ya kamba.

Mwaka 1997, Bw. Hoxur alifanikiwa kupita kamba ya chuma cha pua yenye urefu wa mita 600 iliyofungwa kati ya kando mbili za Mto Changjiang katika Magenge Matatu kwa dakika 13 na sekunde 48, bila kuwekwa zana za kuhakikisha usalama, na kuvunja rekodi ya Guinness kwa mara ya kwanza. Tarehe 6 Oktoba mwaka 2000, alipita kamba ya chuma cha pua yenye urefu wa mita 1399.6 iliyofungwa juu ya Mlima Heng, bila kuwekwa zana za kuhakikisha usalama, na kuvunja rekodi ya Guinness tena. Mwaka 2002, Bw. Hoxur alikaa juu ya kamba iliyofungwa juu ya ziwa Jinhai huko Pinggu kitongoji cha Beijing kwa siku 25. Jambo hilo lilifuatiliwa na dunia nzima, na alisifiwa kuwa "Mfalme wa Anga ya Juu" wa China.

Mafanikio hayo ya Bw. Hoxur yamewafanya watu wengi zaidi wafahamu usanii wa mchezo wa Dawaz. Hivi sasa sanaa hiyo ya kabila la Wauyghur imewekwa kwenye orodha ya mali za urithi wa utamaduni usioonekana ya China. Wakati huo huo shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang pia linajitahidi kufundisha wachezaji wengi zaidi wa mchezo wa Dawaz. Bw. Hoxur na wanafunzi wake wanaimani kuwa mchezo huo utarithishwa kizazi baada ya kizazi.







YALIYOMO KWENYE KUNG FU YA CHINA










HISTORIA

mwanzo wa martial arts China ulitokana na haja ya ulinzi binafsi, ilikuwa ni mbinu ya uwindaji na mafunzo ya kijeshi katika China ya kale . mkono-kwa-mkono kupambana na silaha mazoezi yalikuwa muhimu katika kutoa mafunzo ya kale kwa askari wa china.

Ancient depiction of fighting monks practicing the art of self-defense .
Kale depiction ya kupambana na watawa kufanya mazoezi ya sanaa ya -kujilinda .


According to legend, Chinese martial arts originated during the semi-mythical Xia Dynasty more than 4,000 years ago. It is said the Yellow Emperor Huangdi (legendary date of ascension 2698 BCE ) introduced the earliest fighting systems to China.
The Yellow Emperor is described as a famous general who, before becoming China's leader, wrote lengthy treatises on medicine, astrology and the martial arts.

Kulingana na hadithi, China martial arts asili wakati wa nusu-mythical Xia Nasaba zaidi ya 4,000 iliyopita. [ Ni alisema Yellow Emperor Huangdi (hadithi tarehe ya kupaa 2698 KK ) ilianzisha mwanzo na mifumo ya kupambana na China .


The Emperor Yellow ni kama ilivyoelezwa maarufu ujumla ambao, kabla ya kuwa kiongozi wa China, aliandika treatises urefu juu ya dawa, Astrology na martial sanaa.

One of his main opponents was Chi You (èš©å°¤) who was credited as the creator of jiao di , a forerunner to the modern art of Chinese Wrestling .

Mmoja wa wapinzani wake kuu Chi You (èš©å°¤) ambaye alikuwa na sifa kama muumba wa Jiao di , a forerunner ya kisasa ya sanaa ya china Wrestling.


Tembelea hapa:
http://en.wikipedia.org/wiki/Chinese_martial_arts