Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Novemba 26, 2010

VIONGOZI ECD NA TZ UNION

VIONGOZI WAPYA WA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO KATIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI NA KATI: WAKURUGENZI WALIOCHAGULIWA KUSIMAMIA NA KUONGOZA IDARA MBALIMBALI KATIKA KANDA YA AFRIKA MASHARIKI NA KATI.
1. JP Mulumba - Elimu na Mafunzo ya Uongozi.
2. Elkana Kerosi - Uhusiano, Uhuru wa dini na UtumeUlimwenguni.
3. Uwakili - William Bagambe.
4. Vijana na mambo ya Kiroho - Magulilo Mwakalonge.
5. Huduma ya uchungaji na Familia - Rudatinya Mwangachuchu.
6. Afya na Mratibu wa VVU na UKIMWI - Dr. FesahaTsegaye.
7. Philip Gai - Uchapishaji ,Sauti ya Unabii na Roho ya Unabii.
8. Steven Bina - Mawasiliano na Uinjilisti kwa njia ya Satelite.
9. Elimu - Andrew Mutero.
10. Idara ya Wanawakike na watoto - Debbie Maloba.
11. Elam Musoni - Huduma za Washiriki na Shule ya Sabato.

WATAKAONGOZA IDARA MBALIMBALI KATIKA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO NCHINI TANZANIA TUKIANZA NA NGAZI YA JUU KABISA KAMA VILE RAIS MAKAMU NA WAZIRI:

1.Mwenyekiti - Godwin Ole Lekundayo
2.Katibu - Davis Fue
3.Mhazini - Dennis Wairaha

WAKURUGENZI WA MAIDARA:
1. AFYA, KIASI, VVU NA UKIMWI - GODFEY MABUBA.

2. VIJANA NA MAMBO YA KIROHO - JOSEPH D'ZOMBE.

3. HUDUMA ZA KICHUNGAJI NA FAMILIA - MUSA MITEKALO.

4. ELIMU, UHUSIANO NA UHURU WA DINI - ELIAS KASIKA.

5. MAWASILIANO, MORNING STAR RADIO, AWR NA SAUTI YA UNABII - MIKA MUSA.

6. WANAWAKIKE, WATOTO NA SHULE SABATO - WINFRIDA MITEKALO.

7. UCHAPISHAJI NA ROHO UNABII - ANNA MUHOHO.

8. UWAKILI - JEREMIAH IZUNGO.

Jumatano, Novemba 24, 2010

NI MUHIMU KUFANYA MAZOEZI

Ni muhimu kufanya mazoezi,
ni kwamba unauweka mwili wako safi na pia unaepukana magonjwa madogo madogo
Bibi anasema, usidhani wewe tu unaweza.
Hata mimi naweza usidhani umri ni kitu ha ha ha ha:-)!!!!
...Mmmmmhhh!!
Nawaza kwa sauti hivi huyu bibi ana mifupa kweli?

Riwaya

KIZUNGUMKUTI

HAFSA Hashimu alikuwa na kila kitu chenye kumfanya ayafurahie maisha. Elimu nzuri. Kazi nzuri. Mume aliyempenda kwa dhati ya moyo wake. Alikuwa mwenye furaha ya ndoa yake.
Aliamini hakuna kitu kitakachoharibu furaha ya ndoa yao zaidi ya maradhi na kifo.
Aliamini hivyo, hadi jinamizi la Benito, rafiki yake wa kiume wakiwa shule ya sekondari lilipojitokeza na kumweka katika wakati mgumu zaidi.



HAYA MAISHA

TEKLA Mbena, asingeweza kuisahau maishani mwake siku moja iliyoubadilisha mwelekeo wote wa maisha yake. Alitoka kwenye familia bora. Lakini haya yaliyeyuka mithili ya pande la barafu kwenye pipa la maji yachemkayo.
Mapenzi. Kijana Jimmy anayaharibu matarajio ya Tekla katika maisha yake.
Kila kitu kinamharibiakia Tekla.
Hata mambo yanapomnyookea tena, kivuli cha makosa yake ya nyuma hakimwachi akayafurahia maisha.
Kila kitu kilipopotea kutoka mikononi mwake, anaweza kufanya jambo moja tu.
Kulipa kisasi.


WAKATI FULANI

JANE Siame, anachaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza mwanamke Tanzania. Wanawake wote wananyanyua mikono yao kwa ushindi huo. Wanalazimika kuishusha huku vichwa vyao vikiwa chini kashfa kubwa inapoibuka kuhusiana na historia ya mwenendo wa maisha ya Jane.
Kamati Maalumu ya Maadili ikihusishwa wananchi na viongozi wa dini na siasa wanaoheshimika zaidi inaundwa kumhoji mheshimiwa Waziri Mkuu kabla hajaondolewa wadhifa wake. Kamati hiyo inakutana na mengi yanayoifanya ifikirie mara mbili. Nchi nzima inakuwa katika mkanganyiko mkubwa. Je, aondolewe wadhifa wake na kudharauliwa, ama apongezwe?


Kaa mkao wa kula ukisubiri ujio wa riwaya hizo zenye kukusisimua, na kukufanya usichoke kufungua kurasa kiasi kwamba ufikapo ukurasa wa mwisho, unatamani simulizi iendelee.
http://fadhymtanga.blogspot.com

Bonge la Zoezi

HAYA SASA!! KAZI KWAKO.

Milima ya Alps ,


Uswis 15/10/2010.
Uchimbaji wa barabara chini ya milima ya Alps ambayo itakuwa barabara ndefu duniani kupita ndani ya mlima imemalizika.

Uchimbaji huo amabo ulianza miaka 15 iliyopita ulimalizika leo kwa kuunganisha barabara hiyo na barabara ambayo iliyopo Gottard Base.
Barabara hiyo itaunganisha kusini na kaskazini mwa Ulaya kiusafiri hasa ule wa mizigo mikubwa.

Picha hapo juu anaonekana mmoja ya wafanyakazi akiwa kazini kuanza ujenzi wa reli itakayo tumika kubebea mizigo.

Mtayarishaji: UHABA WA SAFARI

Mtayarishaji: UHABA WA SAFARI

UHABA WA SAFARI


Mambo ya kutafakari kuhusu usalama wetu

Mambo ya Kiva

Saturday morning would mark the official end of Jonothan's KivaWalk. A group of nearly 40 supporters gathered at the Ferry Building to begin a full-day walk through and around beautiful San Francisco. The event would conclude at the Sports Basement in the Presidio, but not before a very important stop at the shoreline of the Pacific. With Jonathon and Kanoa leading the way, the group ran down to the waters edge to witness the end of an epic cross-country adventure. Jonathon eagerly jumped in the ocean, taking a brief moment to think about what he had accomplished: 3,030 miles on foot, from coast to coast , in support of Kiva. It was a wonderful moment to be shared.

Dubai, UAE - 30/10/2010.

Makachero wa UAE na makachero wa kimataifa wa nchi za Uingereza na Amerika wamefanikiwa kuukamata mizigo ambao inasadikiwa ilikuwa ndani ya ndege tayari kuelekea Amerika. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "mizigo hiyo ilikuwa imetokea nchini Yamen. Mizigo hiyo likutwa na aina fulani ya unga PETN ambao unasadikiwa ungetumika kuleta madhara." Picha hao juu inaonekana moja ya ndege ya kubebea mzigo ikiwa inafanyiwa ukaguzi mara ya habari kupatikana ya kuwa kuna moja ya ndege za kubebea mizigo imebeba mzigo wenye bomu.
http://launite.blogspot.com

Hawa Ndio Wabunge Wako

Huu ndiyo mtazamo wa bunge jipya!
http://innobanzi.blogspot.com

Jumapili, Novemba 21, 2010

MPANGO WA MUZIKI WA ACAPPELLA TANZANIA

NI BAADHI YA VIKUNDI NA CHOIR ZINAZOJIHUSISHA NA MUZIKI WA ACAPELLA, MSIKILIZAJI ENDELEA KUNIJULISHA IKIWA UNAFAHAMU KUNDI AMA CHOIR POPOTE DUNIANI HASA WANAOJIHUSISHA NA AINA HII YA MUZIKI, ACAPPELLA.
  1. WATEULE - KIBAMBA SDA DSM TANZANIA
  2. VOICE OF SANCTIFICATION - BUGURUNI SDA DSM TANZANIA
  3. GRACIOS VOICE - KANANI SDA TANZANIA
  4. AGAPE CHOIR. AKERI LUTHERAN PARISH TANZANIA
  5. THE HOPE SCORES - MACHIMBO S.D.A DSM TANZANIA
  6. MABALOZIWA YESU - BOKO SDA DSM TANZANIA
  7. GLORYSHINE - MONGOLANDEGE SDA DSM TANZANIA
  8. SOUL INFLUENCE - SOUTH AFRICA
  9. PASUWA - MOSHI TANZANIA
  10. NO LIMITS - SOUTH AFRICA
  11. KINGS HERALD - USA
  12. SDA SOUTH AFRICA CORAL
  13. LADY SMITH BLACK MAMBAZO - SOUTH AFRICA
  14. ACAPPELLA COMPANY - USA
  15. FINAL TRUMPET - DSM TANZANIA
MCHAKATO UKO HIVI:
KATIKA SIMU YAKO YA KIGANJANI SEHEMU YA UJUMBE MFUPI ANDIKA NENO MATUMAINI ACHA NAFASI ANDIKA NENO AC ACHA NAFASI ANDIKA JINA LA KIKUNDI AMA CHOIR NA MAHALI WANAPOPATIKANA ANDIKA PIA MAWASILIANO YAO KAMA UNAYO KISHA TUMA KUWENDA NAMBA 15551. ZOEZI HILI NI KWA WALE WAOOOTE WALIOPO TANZANIA.

Nitaendelea Kukupatia Majina ya Vikundi na Mahali Yanapopatikana.