Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Machi 12, 2008

UNAONAJE UKIWA HAPAAAAAAA?


MADE IN TANZANIA TU


Januari 23, 2008

JOHN Nolan, yule raia wa Ireland aliyejaribu kuighilibu Serikali ya Tanzania imruhusu aanzishe mashamba ya kamba (prawns) ambayo yangeiharibu kabisa Delta ya Rufiji, alipata kuliambia gazeti moja la Uingereza kwamba kati ya nchi za "ajabu" alizopata kuishi ni Tanzania .

Nolan aliliambia gazeti hilo ya kwamba Tanzania ndiyo nchi pekee duniani ambayo Mzungu anaweza kuingia akiwa na dola tano tu mfukoni na akaondoka miaka mitano baadaye akiwa milionea!

Alitoa mfano wa yeye mwenyewe kwamba aliingia Tanzania akiwa hana kitu, lakini 'akatengeneza pesa' akiwa katika chumba chake cha hoteli kutokana na dili walizochonga na viongozi ambao walimwamini kwa kuwa tu ni Mzungu!

Lakini Nolan si mgeni pekee aliyepata kuikejeli Tanzania . Mwaka jana gazeti la Mtanzania lilipata kumnukuu mwekezaji mmoja kutoka China , anayefanya biashara ya kuuza kamba na kambakochi Mashariki ya Mbali, akiikejeli Tanzania kwamba rushwa yake ni "poa".

Kwa mujibu wa Mchina huyo, ni katika Tanzania tu ambapo unaweza kumwita hakimu nyumbani kwako na kumpa rushwa ya Sh. 100,000 tu, na kisha kumpa maelekezo ya namna ya kutoa hukumu ya kesi ya mamilioni ya pesa inayokuhusu!

Lakini kama utashangaa na kutoziamini kauli hizo za Nolan na za Mchina huyo, utasemaje kuhusu hii ya Rais mstaafu, Benjamin Mkapa kuanzisha kampuni yake ya biashara (ANBEM) yeye na mkewe, mwaka 1999, akiwa bado Ikulu?. Kwa kufanya hivyo, Mkapa akawa Rais wa kwanza katika historia ya Tanzania kufanya biashara akiwa Ikulu. Historia bwana, nani hapendi kuweka historia ya ujasiriamali?

Lakini hakuishia hapo. Mwaka mmoja kabla ya kuondoka madarakani; yaani Desemba 29, 2004, Mkapa huyo huyo akashirikiana na aliyekuwa Waziri wake wa Fedha na baadaye Nishati na Madini, Daniel Yona, kusajili kampuni nyingine binafsi iitwayo Tanpower Resources Company, na akaisimamia kununua asilimia 85 ya uliokuwa mradi wa umma wa makaa ya mawe wa Kiwira mkoani Mbeya.

Lakini pia hakuishia hapo. Akautumia wadhifa wake wa urais kuhakikisha kampuni yake hiyo mpya – wakurugenzi wakiwa ni pamoja na mkewe na mtoto wake, kuingia mkataba wa kuiuzia Tanesco megawati 200 za umeme katika gridi ya taifa.

Raia wema waliohoji iwapo hakuna mgongano wa maslahi kwa Rais kufanya biashara akiwa bado Ikulu; huku akinunua kampuni ya umma (Kiwira) na kuingia mkataba wa kibiashara na kampuni nyingine ya umma (Tanesco), walinyamazishwa haraka kwa kuambiwa Mkapa ni "mjasiriamali", na kwamba anaonyesha "ujasiriamali" kwa vitendo akiwa Ikulu! Upo hapo?

Kama hiyo haitoshi kukuthibitishia vioja vya Tanzania , utaielezeaje hii ya Jeetu Patel kufanikiwa kughushi na kuchota Sh. bilioni 90 kutoka Benki Kuu kwa kutumia makampuni manane tofauti aliyoyasajili?

Ilikuja ya kwanza ikachota, ikaja ya pili ikachota, ikaja ya tatu ikachota, na vivyo hivyo mpaka kampuni ya nane! Na bado Watanzania tunatakiwa tuamini kwamba hakuna aliyejua kuwa hati zilizotumiwa na makampuni hayo ni za kughushi, hadi majuzi ripoti ya ukaguzi ya Ernest & Young ilipotua mezani kwa Rais Kikwete!

Lakini kama hilo halikushangazi au kukushtua, hebu tafakari na hili jingine: Watanzania masikini wanapandishiwa umeme kwa asilimia 21 kwa sababu Tanesco iko hoi kifedha. Kwa nini iko hoi? Kwa sababu vigogo serikalini wameiingiza katika mikataba mibovu ya Richmond , IPTL na Songas.

Kwa sababu ya mikataba hiyo mibovu, Tanesco inailipa IPTL Sh. bilioni 3.3 kila mwezi, Songas Sh. bilioni 5.8 na Richmond Sh. bilioni 4.7. Kwa viwango hivvyo vya malipo, unahitaji kuwa na kampuni yenye utajiri wa Microsoft ya Bill Gates, kutotetereka kifedha. Na hivyo Tanesco ilitetereka. Ili isife, ikaamua kuongeza umeme kwa asilimia 21!

Hiyo maana yake ni nini? Hiyo maana yake ni kwamba Watanzania masikini na walalahoi wa nchi hii ndiyo "wanaobebeshwa" zigo hilo la Tanesco la kufidia gharama zilizosababishwa na vigogo serikalini za mikataba ya IPTL, Richmond na Songas. Cha kushangaza zaidi, vigogo hao waliotubebesha zigo hilo kwa kuingia mikataba hiyo mibovu, bado wanadunda mpaka leo serikalini!

Na bado wameona hiyo haitoshi. Sasa Serikali inajiandaa kuwasilisha bungeni muswada wa sheria kuziruhusu kampuni binafsi kufanya biashara ya kuuza umeme nchini. Yaani; Serikali inakuwa mstari wa mbele kulitafutia shirika lake (Tanesco) wapinzani wa kuliua kibiashara, tena inafanya hivyo ikiwa yenyewe tayari imeshalikamua hadi kuwa hoi bin taaban!

Na Tanesco ikifa na biashara hiyo ikashikwa na makampuni binafsi ya nje, (ambayo bila shaka baadhi ya vigogo nchini watakuwa na hisa), nani atayazuia yasipange bei ya pamoja ya kuuzia umeme (cartel) ili yanufaike zaidi kwa kuwakamua zaidi Watanzania? Na bado tunaambiwa kuna vita inayoendelea nchini ya kuwakomboa masikini.

Biashara ya chakula ipo mikononi mwa watu binafsi, nishati nayo sasa inawekwa mikononi mwa watu binafsi, maji nayo yataelekea huko huko …mwishowe sekta zote nyeti zinazohusu usalama wa taifa zitakuwa mikononi mwa watu binafsi hususan wageni. Tusisahau Nyerere alitabiri: "Mtabinafsisha hata Magereza."

Lakini yawezekanaje mambo yote haya yatokee nchini na umma wa Watanzania ukae kimya tu? Jibu ni kwamba ni kwa sababu Tanzania ni nchi 'poa', nchi ya amani. Watanzania ni watu wasiotaka makuu, na ndiyo maana kina Nolan wanaamini kwamba duniani hakuna nchi kama Tanzania . Hayo aliyoyaona Nolan akiwa Tanzania ni Made in Tanzania tu. Huwezi kuyakuta kwingineko duniani!

Jumatatu, Machi 10, 2008

SIKUKUU YA KUVUTA MARIJUANA MAREKANI

Ilikuwa saa kumi na dakika ishirini tarehe ishirini mwezi wa nne. wanafunzi wa chuo kikuu cha Brown walifurika uwanjani kwa madai eti wanasherehekea majilio ya msimu wa joto. Uwanja mzima ulifurika vimwana na maghulamu weupe wengi na weusi wachache. Kama kawaida kwota sketi zilikuwa nyingi huku baadhi ya mibabe wakiwa kifua wazi kuonyesha malaika zao. Busu zilikuwa si haba. za waume kwa waume, wake kwa wake na zingine za waume kwa wake. Kila mtu alionekana mwenye furaha iliyovuka mipaka. Vicheko havikuwa vya kawaida. Ungefika pale ndugu ungedhani wanafunzi jamani wameanza kupagawa. Wachuuzi wa vyakula walikuwa chonjo kuokota dola. Walijua hii ni siku ambayo wanafunzi hula pasipo kuweka breki.

Hali hii isiyo ya kawaida ilinipelekea kuuliza maswali mbona leo wanafunzi wa chuo kikuu wana furaha isokuwa na kifani? Wanafunzi wangu hawakuachwa nyuma pia bali waliniomba rukhsa ya kujumuika na wenzao. Waliita sikukuu ile 4:20 at 4:20 maanake tarehe ishirini Aprili, saa kumi na dakika ishirini. Kwa kawaida niliwajua Wamarekani kama watu wasokuwa na furaha; watu wanaovalia tabasamu kwa muda unapokutana nao; watu waliojawa na upweke kiasi cha kulala vitandani na mbwa wao; watu wasiojumuika na wenzao kwa urahisi labda kuwe ile waiitayo 'appointment'.

Kulikuwepo harufu aina yake katika uwanja mzima. Kila mmoja alionekana kuvuta kitu fulani chenye muundo wa sigara. Moshi wa kile walichovuta ulipeperushwa na upepo mwororo hadi nilipokuwa. Hapo nikajua kuna jambo linaendelea uwanjani. Harufu hii haikuwa ya kawaida. Nilianza basi kuchanganua matukio na kuyaoanisha. Kicheko na vitendo visivyo vya kawaida uwanjani nilivioanishwa na walichokuwa wakivuta wana wa watu. Nilipokuwa mchanga niliambiwa kwamba mtu anapovuta Marijuana huwa na tabia zisizo za kawaida. Mojawepo ya ngano nilizopashwa ni za mvutaji fulani, aliyepika ugali mkubwa kisha akapika 'kijiugali' kingine kidogo eti kiwe kitoweo cha ugali ule mkubwa.

Lakini iwapo hawa wanavuta marijuana mbona basi polisi wamejaa uwanjani? Sikuamini hadi nilpopata habari kutoka kwa Wamarekani zaidi ya watano. Kwamba siku hii inasherekewa takribani katika shule zote nchini Marekani zikiwepo shule za upili pia. Siku hii haiitwi sikukuu hadi wanaoisherehekea wavute Marijuana kupindukia. Eti kusherehekea mwanzo wa joto ni kisingizio tu; swala kuu ni kusokota Marijuana.

Iwapo utajiuliza maswali ndugu basi hivi ndivyo Marekani inawasaidia wafanyibiashara wa Marijuana. Kumekuwepo fununu pia baadhi ya madaktari Marekani wanawashauri wateja wao kutumia Marijuana. Piga hesabu huku ukitilia maanani mamilioni ya wanafunzi wanaovuta marijuana siku hii 'tukufu'. Siku hii pekee imewazalishia walanguzi wa marijuana mabilioni ya dola. Baada ya kufanya hesabu, jiulize sheria za U.N. zasemaje kuhusu madawa ya kulevya? Juzi Marekani wamevunja sheria ya U.N. na kushambulia Iraq. Hivi jana wamevunja ya madawa za kulevya kwa kuwaruhusu walanguzi kuuza na wanafunzi kununua.

MAREKANI INAOZA KWA KASI NDUGU.

BEAUTIFUL MESSAGE


Little girl and her father were crossing a bridge.
The father was kind of scared so he asked his little daughter, 'sweetheart, please hold my hand so that you don't fall into the river. The little girl said, 'No, Dad. You hold my hand, 'What's the difference?' Asked the puzzled father. 'There's a big difference, 'replied the little girl.

'If you hold your hand and something happens to me, chances are that I may let your hand go. But if you hold my hand, I know for sure that no matter what happens you will never let my hand go.'

In any relationship, the essence of trust is not in its bind, but in its bond.

So hold the hand of the person who loves you rather than expecting them to hold yours...
This message is too short......but carries a lot of Feelings.

Alhamisi, Machi 06, 2008

VOCAL UNION


Vocal Union is an all-vocal, contemporary Gospel group from Nashville,Tennessee। They began as a group of studio interns in 1995 experimentingwith recording vocal arrangements of traditional gospel music। The soundthey produced found a niche in many churches around the country, and thedecision was made in 1998 to make Vocal Union a touring group. Since thattime, Vocal Union has traveled extensively, performing for special churchevents, community concerts, and fundraisers. The group primarily travelsthroughout the United States, but has also ventured to select venues inCanada and Jamaica. Vocal Union has performed at a wide variety of venuesincluding a performance of sacred Christmas music at Carnegie Hall inDecember of 2005 in Manhattan, New York, and two performances at the WhiteHouse Christmas celebration in Washington, D.C. in December of 2006. Thegroup's fan base has spread worldwide through distribution by Word Records.Fans from Iceland, Nigeria, Brazil, and many other countries all over theworld have signed the group's online guest book and illustrate Vocal Union'sstrong international appeal.Two Vocal Union recording projects: "Once Upon A Tree" and "All Around Me"have earned awards from the Contemporary Acappella Society of America."Once Upon A Tree" was awarded the Best Religious Album of the Year in 2001against stiff competition from the very highly acclaimed groups Take 6 andAcappella."All Around Me" was awarded runner up for Best Religious Album of the Yearin 2005 from The Contemporary Acappella Society of America. This album alsoproduced the song "Livin Love" which was awarded runner up for the BestReligious Song of the Year. The group's most recent project: "Just Like theOld Days" was released in 2007 and is a return to the high-energytraditional sound that the group began with in 1995. Thus far, the albumhas received a warm reception from audiences throughout the United States,and the group has already started putting together material for their nextproject. "Once Upon A Tree", "All Around Me", and "Just Like the Old Days"are available online at the group's website www.vocalunion.com, in manyChristian bookstores, and in seven major international markets.Vocal Union's style ranges from high-energy traditional, to tight-harmonyjazz and soulful spirituals, to contemporary street corner acappella. Thegroup tailors the set list to match the demographics of the audience soeveryone from the very young to the very old will find something to enjoyduring their concerts. Many of their songs feature vocal percussion and"vocal bass guitar" to firmly establish the rhythmic element, and the innervoicings are meticulously arranged and seriously performed to perfection.The group is blessed with some of the finest soloists in Christian music andall of them love to sing with their hearts!"Our goal is to sing the Gospel to as many as possible - whenever andwherever - to teach, uplift, and encourage!"


Jumanne, Machi 04, 2008

Jokate Mwegelo


KAMA umfuatiliaji najua hii ushaishtukia; Jokate Mwegelo Balozi wa Redds 2006, aliyekuwa pia balozi wa gazeti bora kabisa la kiingereza nchini linalochapishwa na kampuni ya Mwananchi Communications, The Citizen ambaye pia alitwaa taji la Miss Tanzania namba 2 ni miongoni mwa vijana wa kitanzania wenye vipaji lukuki na mashaallah anavitumia ipasavyo.

Utakumbuka kuwa kabla ya Jokate kutwaa mataji hayo, cheche zake zilianza kuonekana mara tu alipojitosa katika kinyang?anyiro cha kumsaka Miss Kurasini na hatimaye alitwaa taji la Miss Temeke.

Dj Cartoon



Dj Cartoon/CartoonHome: Dj, Producer, Entrepreneur,Radio Presenter.
SIKIAA!!!! DJ Cartoon started Djing 8 years ago, but his love for music could be seen by the time he was 12 years old. He remembers his first equipment as two tape decks and a old mixer he got from a friend and within weeks of self training became the neighborhood house party DJ. His quest to be a seasoned DJ was only bogged by the lack of equipment. However, through a link of friends he was introduced to a mobile DJ owner and from there on things started picking up. He clearly remembers his first turntable feel just like it was yesterday and marveled at himself being on the opposite side of the turntables, many Djs knowing what to play to keep the crowd on their feet, transitions to getting to know what a hit is which gradually made Cartoon start producing "Isikie Beats". He set up his own production company, Ritungu Inc,Friends Entertainment and Digital Media Creation four years ago and hasn't looked back since. In less than 3 years Cartoon has emerged from a DJ into one of the most versatile producers in the game."I see a lot of people making a big deal out of what producer uses what. What matters is the end result. If the beats is banging, it doesn't matter what equipment was used". You might have recorded you're vocals in the bathroom, but if it's a hit and the quality compares to everybody else, why knock the recording.His ability to produce gospel music and work with artists from all over the world of music makes Cartoon versatile in producing for some of the hottest up and coming acts who seek out his talent. Cartoon also continues to raise the par in the Mixtape game, by creating mixtapes featuring artists from all over the world, thus making his mixtapes internationally sought.

Dj Dona - Be Heard

Dj Dona - Be Heard

Karibu Sana!


Safari in Swahili simply means "journey".
While the typical Safari in Tanzania will usually includes Elephants, Giraffes, Lions and a hike up Kilmanjaro, these are just a few examples of a thousand fantastic experiences possible in Tanzania. You may wish to forgo the game parks and plan your safari around the Usambara mountains, Zanzibar or Tanzania's lively coastal towns, where you can meet the people, jam along to the music, and discover the delicious foods on offer.

Visit;

DONDOO ZAIDI

Mugabe apitisha sheria mpya


Vyombo vya habari vya serikali nchini Zimbabwe vimesema kuwa Rais Robert Mugabe amekubali kupitisha sheria mpya ya kuwarudushia wazimbabwe weusi uwezo wa kuwa na dau kubwa zaidi katika makampuni ya umma na yale yanoyomilikiwa na mataifa ya nje.

Sheria hiyo mpya imekuja wiki 3 kabla ya uchaguzi wa rais nchini humo kufanyika ambapo Bw. Mugabe anachuana na mpinzani mkongwe Bw. Morgan Tsvangirai na aliyekuwa waziri wa fedha Bw. Simba Makoni.

Bw. Mugabe amesema kuwa sheria hiyo itasaidia kuwapa uwezo mkubwa zaidi wa kiuchumi wazawa wa kizimbabwe japokuwa wanompinga wanasema kuwa hatua hiyo itaongeza matatizo ya kiuchumi nchini humo.

Taarifa zinasema kuwa makampuni yatakayoathirika na sheria hiyo mpya ni pamoja na kampuni kubwa sana ya madini Rio Tinto na benki ya Barclays.