Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Desemba 12, 2014

Mapinduzi ya Tasnia ya Filamu Nchini Tanzania



 ZAMARADI MKETEMA ameandika sehemu....

“…Natamani sana siku moja atokee mtu kwenye hii sekta atutambulishe hata kama sio kimataifa basi africa tu.  KANUMBA alianza kuonesha mwangaza na juhudi binafsi zilionekana na kila mtu aliona huenda angefika mbali.. lakini baada ya hapo sioni tena!!!!

Mbona hapa nyumbani ni wakubwa tu..? Nini kinawakwamisha..? Kwanini wasanii wetu wa filamu ukubwa wao unaishia nyumbani tu....!!? Tatizo ni nini!!!????? kiukweli ni kama inakatisha tamaa na inaonekana kabisa watu wamerelax na ustar wa bongo wakati wana nafasi ya kufanya vizuri zaidi... wana bongo movie tukifika kwa wenzetu unaona kabisa tunapwaya kiasi gani.. 


Ujanja wetu ni nyumbani tu!!?? why!!!?? tukianza utanzania wa kufichaficha tutasifiana uongo lakini tukiwa wakweli na nafsi zetu tutaliona hilo na kuchukulia kama challenge..!!! ukweli ni kwamba hii tasnia inasikitisha!!! tena sana nahisi sasahivi tunafanya filamu kwa ajili ya nyumbani tu na tukiingia kwenye mabendi tukisharushwa tumeridhika!! kweli!! hapa ndio mnapotaka mfike!!? ukifika sehemu ukiwa juu nchini kwako tunachotegemea ni wewe kupasua mawimbi uende mbali zaidi nje ya mipaka!! lakini ukiamua kurelax hapo ulipo inamana unasubiri kushuka sababu kiukweli huwezi kukaa juu milele!!! kwanini mmeridhika hivi!!! kaka JB tatizo ni nini!!!??

Mi nakuangalia wewe kama mfano wa msanii mkubwa sana kwenye tasnia kwa sasa... mbona umerelax!!!??? umeridhika na ustar wa tanzania!!!? una kila kitu cha kukufikisha mbali... kinachohitajika ni juhudi binafsi tu ili kesho na sisi tufike mahala pazuri!! hebu tuongee wapenzi.. mnahisi huku kwenye bongo movie TATIZO LIKO WAPIII…!!???

JB Akajibu;

“Kwako Zamaradi na wengine wote..

Kwanza napenda niwashukuru wote kwa jinsi mnavyotuwazia mema. Naomba nichukue nafasi hii kuwapongeza waigizaji wote wa Tz na waandaaji wa filamuU kwa kuthubutu kutengeneza filamu hizi katiks mazingira magumu. Najua watanzania wengi wangependa kuona tukipeperusha bendera nje,lakini naomba muwape wasanii muda.

Tasnia hii ni changa na ina changamoto ambazo zinakatisha tamaa. Hebu tujiulize kwa nini wasomi wengi waliosomea filamuu UDSM na BAGAMOYO hawafanyi filamu hizi? Wasambazaji wengi wakubwa mamu,wananchi na hata hans pop walijaribu wakakimbia, kuna producer mkubwa hapa nchini JOHN RIBER ambaye ametengeneza filamuu kama NERIA na YELLOW CARD lakini naye ukimwambia njoo kwenye hizi filamu atakupa jibu.

Nakubali tuna makosa mengi kama ubora wa filamu zetu na stori lakini nataka niwaambie mazingira ya kufanya filamu bongo yanakatisha tamaa wizi wa kazi zetu umezidi na wasambazaji wengi wamekimbia. Binafsi najipanga kuwa mtayarishaji zaidi kuliko mwigizaji kwa sasa kupitia JERUSALEM FILMS na ndio maana filamu nyingi natoa nafasi kwa vijana ambao kama mabadiliko ya sera ya filamu yatafanywa watatuwakilisha nje.

Kiswahili kisichukuliwe poa kwani kina nafasi kibwa sana. Tukumbuke SHARUK KHAN ni ‘actor’ tajiri2 dunian lakini filamu zake ni za kihindi. Hebu sote tusaidiane kupambana na changamoto hizi na tuanze na EAST AFRICA kwanza huku tukiboresha, wasomi wa filamu msikimbie njooni tuanze wote na tuwape moyo wasanii wetu waliojaribu kusimamisha tasnia hii kwa vimtaji toka mifukoni mwao na vipaji walivyopewa na mungu bila msaada kutoka popote. Asanteni kwa kutuunga mkono kwemye filamu zetu.”
===================================




===================================


Tulitazame sasa hili suala kwa Pamoja;

Tasnia yetu pendwa nchini, Tasnia ya sanaa ya maigizio, hasa kwenye upande wa Filamu, Sina shaka hata kidogo kwamba baada ya Muziki, Sanaa ya Filamu na Maigizo ndiye inafuatia kupendwa zaidi hapa nchini, Idadi ya watazamaji na wafuatiliaji inathibitisha hilo!

Bahati mbaya Tasnia hii inaelekea kufa kibudu. Narudia, Tasnia ya Filamu nchini inaelekea kufa KIBUDU. Hali ni mbaya sana kwenye upande huu wa sanaa nchini licha ya kuwa ndiyo FANI inayoongoza kwa kutoa Ajira kwa vijana wengi zaidi nchini. Tukubaliane hapo kwanza!

Makosa yapo Mengi. Mbaya zaidi yote si makosa yanayohitaji kuonwa mpaka na Mtaalamu pekee. Hata Asiye na utaalamu wa Sound engineering atajua kwamba sauti kwenye Bongo movies ni tatizo, asiyefahamu mambo ya script akitazama tu atajua, Asiyejua umuhimu wa continuity naye hali kadhalika, achilia mbali yule asiyejua kiingereza kwa ufasaha, inamuhitaji elimu ya kujua tafsiri ya toilet tu kung'amua kwamba kiingereza cha kwenye subtitlles ni majanga. Mtiririko wa hadithi na uhalisia ni tatizo sugu. Inasikitisha sana.

Sitagusia hata moja katika hayo!

Leo Nagusa upande wa Mapinduzi ya Ujumla. Kwanini tasnia hii inaporomoka badala ya kukua zaidi? Kwanini hakuna mabadiliko chanya? Kwanini filamu nchini zimebaki kuwa na mabaka mabaka ya ulalahoi? Kwanini hatuvuki mipaka? Kwanini hatufanyi kweli? Kwanini muziki unatoboa zaidi kuliko filamu? Nini tatizo?

MAONI YANGU:

KWANZA, Wasanii waanze kutengeneza 'Image' nzuri;

Maana kwa sasa imeshachafuka. Nasema ukweli, Tasnia hii ina taswira ya uhuni kupitiliza. Na hii ni kutokana na wasanii wakubwa (vioo) kukumbwa na kashfa chafu. Kucha kutwa magazetini kuandikwa upuuzi, pengine wapo wanaolipwa kwa kuuza gazeti, lakini sidhani kama wanacholipwa kina thamani kubwa kupita kazi ya sanaa wanayoifanya.

PILI, Ianzishwe Mikakati Madhubuti;

Ni wakati sasa kwa wasanii kutengeneza Mipango Madhubuti na mikakati (Action plans) itakayowaongoza kufanya kazi kwa usiriaz. Inawezekana, najua mlishajaribu huko nyuma, lakini bado inawezekana.

TATU, Upekee na Usasa;

Hapa namaanisha kufanya movie kisasa na kwa upekee kabisa. Itazamwe mifano ya filamu kama ya CHUMO (Starred by Sharo Milionea & Jokate), Soap ya Siri ya Mtungi na kadhalika (wataalamu sio kikwazo panapo fedha).

NNE, Kushirikisha Wadau;

Watanzania na wapenzi wa filamu za kibongo ni wengi sana. Hakuna tu utaratibu wa kufanya research ili kuwa na data kamili, lakini kwa observation tu ni dhahiri kwamba Bongo Movie haijatupwa kivile. Ni basi tu wana-tasnia wenyewe mnachosha. Sijui lengo lenu ni nini haswa! Ni ajabu mtu kuua ajira yako kwa mikono yako mwenyewe!

Supporters wapo wengi sana. Wapo watazamaji wa hizi movies ni watu wenye uwezo mkubwa pengine hata wa kuwekeza. Achana na Mapedjee wanaohonga kwa lengo la kufurahisha nafsi zao, kuonekana, au malengo yao binafsi yasiyo na tija (japo wakitumiwa vizuri inaweza kusaidia sehemu). Hapa nazungumzia Matajiri, wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa, hata mawakala wa biashara, wakitumika vizuri, watafanya kitu.

Kinachohitajika ni ushawishi tu! Yaani wasanii wenyewe wahakikishe wawe na mipango na uwezo wa kumshawishi mtu/shirika/kampuni kuwekeza (kama si kufadhili) kazi zao. Serikali Pengine Imeshindwa hili!

Na ushawishi huja pale penye tija. Mtu aone umuhimu wa kufanya hivyo. sio kuchoma pesa zake bure. Mbona Michezo Mingi inadhaminiwa? Mpira wa miguu, Ndondi, Riadha n.k., Kwanini isiwe Bongo Movie? - Jikagueni upya kabla hamjachelewa.

TANO, Kuomba Fedha na Access Kubwa zaidi;

Kilio cha wasanii wengi kushindwa kufanya movie zenye ubora ni Mitaji. Wanalalamika hawana fedha za kutosha kuweza kucheza baadhi ya story. Ni kweli kabisa. Na hii pengine ndiyo sababu kubwa hata thamani ya kazi zao kwa wasambazaji inashuka siku hadi siku. Hii ni kutokana na bidhaa kuwa ni low quality.

Sasa basi, katika mikakati yao, Ni vyema wakazingatia ni vipi watapata mitaji ya kucheza story zinazohusika. Kisha watafute Soko zuri la kuuza bidhaa yao kwa bei itakayowanufaisha, sio watakayopangiwa na 'muhindi'.

Hatua za kupata mitaji zaweza kuwa;

* Kuomba udhamini kutoka kwa makampuni rafiki - Hapa namaanisha yale makampuni yanayohusiana na kazi zao. Kwa mfano Makampuni ya bidhaa za Camera, Deki, Simu, na kadhalika. Kwa ufupi, yale makampuni yanayoshabihiana na kazi za filamu yatakuwa rahisi zaidi kuitika!

* Kuomba mikopo kutoka kwenye taasisi za fedha - Kwa kuwa filamu ni biashara kama zilivyo biashara nyingine kubwa, kampuni za utengenezaji wa hizi filamu (RJ, Jerusalem, 5effects, Timamu African Media n.k) zikiandaliwa mazingira mazuri zinaweza kukopesheka.

* Kutoa fursa kwa wahisani na wawekezaji - Kampuni za utayarishaji wa filamu zinaweza kutoa nafasi kwa wawekezaji kuwekeza kwenye kiwanda cha filamu nchini. Hapa kutawawezesha wawekezaji kuweza kuikuza zaidi tasnia hii kwa kuweka mitaji yao mikubwa na kuisimamia ili ipatikane faida. Inawezekana!

Pia, wasanii waombe access kubwa kutoka serikalini ili waweze kutambulika Rasmi na kuaminiwa. Haya yote yatawezekana endapo shirikisho la filamu nchini (TAFF) litakuwa na makali na sauti ya nguvu.

SITA, Wasanii watumie wataalamu kwenye kazi zao;

Hapa namaanisha ni wakati sasa waandaaji wa filamu pamoja na wasanii kwa ujumla waanze kushirikisha wataalamu kwenye kazi zao. Kwa maana wafanye tafiti ndogo ndogo kuhusiana filamu husika (mfano kwenda maktaba kutafuta vitabu vinavyoelezea let's say masuala ya historia, kama hadithi ya movie inagusia huko) na kupata majibu ya kitaalamu kutoka kwa wataalamu hao. Hii ni faida kwani 'uhalisia' wa movie utakuwa maradufu!

Ushirikishwaji uanzie kwenye masuala ya story, production mpaka kwenye masuala mazima ya masoko. Uwanja huu ni mpana sana, nadhani mwanga umeanza kuonekana hapo!

===================================


===================================

 
Kwa kipekee kabisa, Niwapongeze Timamu Effects / Timamu African Media, kwa kuonyesha njia. Nathubutu kusema hawa ndio role models kwenye filamu za Kitanzania. Ni wenzetu, walianzia chini, lakini wamejitahidi kukua kifani, kimaudhui na kimapinduzi hususan kwenye ubora wa story na quality ya uandaaji wa filamu zao zote.

Nashauri waigwe na kuwa dira ya tasnia ya filamu nchini, waendelee kufanya mambo makubwa zaidi ili hatimaye na Tanzania tufikie levo angalau za Nigeria na Ghana. Nimefurahi kuona Wamepata tuzo kadhaa za kimataifa, na kubwa zaidi ni za hivi karibuni huko Marekani katika Future Africa Awards. Hongera Timoth Conrady na Timu yako!


Naomba niishie hapa, ili kutoa nafasi kwa wengine kuchangia mawazo yao, na kwa pamoja tuweke mitazamo chanya na yenye taswira ya kimapinduzi kweli ili hatimaye tuwe tumeshiriki kwenye kuboresha tasnia ya filamu nchini.

Nawasilisha....


Chanzo By:  MR. CONFIDENT, on JamiiForums

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni