Nyota za Neutron ni viini vizito zinavyobakia baada ya nyota kubwa kufa na kulipuka huko
 angani. Matabaka ya nje ya nyota hurushwa mbali katika milipuko hiyo, 
lakini maada katika viini vya nyota hizo husambaratika vyenyewe na 
hutengeneza burungutu kubwa la maada. Kinachobakia baada ya hapo ni kitu
 kilichokandamizwa chenye mkandamizo mkubwa katika ulimwengu wote nje 
shimo jeusi: nyota ya neutron!
Picha
 hii mpya iliyopigwa huko angani inaonyesha kundi la nyota lijulikanalo 
kama ‘globular cluster’. Ambayo ni baadhi tu ya vitu ambavyo ni vya kale
 sana huko angani— umri wake unakaribiana kabisa na umri wa ulimwengu 
wenyewe! Hii inamaanisha kuwa nyota nyingi zilizopo ndani yake 
zimeshakufa. Na zile kubwa zaidi zimekwishalipuka na kuacha nyota za 
neuton.
Kwa kutumia nyota ya neutron katika kundi
 hili pamoja na nyingine nyingi, wanaastronomia wameweza kutambua 
uhusiano kati ya uzito wa nyota (kiasi cha maada inayobeba) na ukubwa 
wake.
Taarifa mpya zinaonyesha kuwa nyota ya 
neutron ya kawaida, yenye uzito wa mara moja na nusu ya Jua letu inaweza
 kuwa na kipenyo cha kilometa 12. Urefu ambao ni karibu sawa na eneo la 
mji mdogo! Likiwa na maada zote hizi zimekandamizwa katika sehemu hiyo 
ndogo. Hivyo basi nyota za neutron ni nzito mno. Nguvu ya mkandamizo 
(Presha) katika kiini chake ni zaidi ya trilioni kumi kuliko nguvu ya 
mkandamizo inayohitajika kutengenezea almasi ndani ya Dunia.
Dokezo: Nyota za neutron
 zimepakiwa na kukandamizwa sana hivyo kuzifanya ziwe na duara pete. 
Mlima unaoweza kutokea katika uso wake unaweza kuwa na urefu wa milimita
 5 tu!
Kwa Taarifa Zaidi 
Swahili Space Scoop hii imetokana na Taarifa kwa vyombo vya habari ya Chandra

 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni