Mtayarishaji

Morning Star Radio

Alhamisi, Desemba 04, 2014

Bawa la Kipepeo




● Rangi maridadi inayong’aa juu ya mabawa ya vipepeo fulani hubadilika ikitegemea upande ambao unatazama. Rangi ya bawa la vipepeo wa aina fulani ni laini na inang’aa sana hivi kwamba inaweza kuonekana umbali wa mita 805. Ni nini kinachofanya bawa la kipepeo liwe la kipekee hivyo?


Fikiria hili: Mistari midogo iliyobonyea kwenye sehemu ya juu ya mabawa ya kipepeo anayeitwa green swallowtail (Papilio blumei) hurudisha nuru kwa njia kadhaa. Kwa mfano, sehemu ya katikati ya eneo lililobonyea hurudisha nuru yenye rangi ya manjano na kijani, huku sehemu za nje zikirudisha nuru yenye rangi ya bluu. 

Pia, sehemu ya katikati ya eneo lililobonyea hurudisha nuru moja kwa moja, lakini nuru inapopiga sehemu za kando inalazimika kupitia kwenye matabaka kadhaa, ambayo huongeza na kuzungusha mawimbi ya nuru. Mchanganyiko wa mwisho unaotokea huwa tata sana.



Watafiti walitumia miaka kumi kutokeza kitu kinachofanana na sehemu ya juu ya bawa la kipepeo. Wanatumaini kwamba teknolojia hiyo itawasaidia kutokeza noti za benki na kadi za mkopo zisizoweza kuigwa kwa urahisi na mabamba yanayoweza kunasa nguvu za jua kwa njia nzuri zaidi. 

Hata hivyo, ni vigumu sana kuiga sehemu ya juu ya bawa la kipepeo. “Ingawa wanasayansi wanaelewa mambo mengi sana kuhusu elimu ya nuru,” anaandika Profesa Ullrich Steiner wa Chuo Kikuu cha Cambridge, “unamna-namna wa rangi wenye kushangaza unaopatikana katika bawa hilo unazidi mambo yanayoweza kutokezwa kwa kutumia teknolojia.”

Una maoni gani? 

Je, sehemu ya juu ya bawa la kipepeo ilijitokeza yenyewe? 

Au ilibuniwa?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni