Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Julai 24, 2012

Habari njema kwa wakazi wa MBEYA, MWANZA, KIGOMA na ARUSHA.



(Labda milima ambayo sijaona ikibuniwa ingawa nayo inatajwa kugunduliwa) 

Unayoyaona leo kesho unaweza usiyaone na kila linapoondoka moja jingine huja.
Hayo ndiyo maisha ya kila siku ya mwanadamu. Sasa ili uishi kwa raha kila ulipatalo sema ahsante kwa Mungu. 

Morning Star Radio imepanua wigo wa huduma ya utangazaji wa kazi za waimbaji wa nyimbo za injili hapa Tanzania, hii ni habari njema  kwa wakazi wa MWANZA sikiliza  matangazo yetu kupitia 102.1 fm, KIGOMA 103.3 fm, MBEYA 106.9 fm. ARUSHA 102.5
Na kwa wakazi walio jirani na hiyo mikoa niliyoitaja endeleeni kubarikiwa na ujio mpya wa kituo cha Radio kinacholeta.

Maisha yana kanuni moja kubwa nayo ni kubuniwa kwa vitu. 

Ukurasa ndani ya facebook BONYEZA HAPA

Jumatatu, Julai 23, 2012

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO

Photo By: www.rhodayouths.wordpress.com


Ukijua unachokithamini itakusaidia kuwa mkweli kwako binafsi, hata wakati mtu mwingine
anapokulazimisha kufanya kitendo unachodhani ni makosa. Maadili yako yatakusaidia kuchagua
lililojema kwako; ambalo wakati mwingine, baada ya kuchagua, itabidi uishi nalo daima.

StaDi Za MaiSha
Unahitaji stadi za maisha pia ili uwe salama. Kusema kweli “Stadi za maisha” zinaweza kuwa stadi za kuokoa maisha, kama vile;

Kuelezea hisia zako. 
Hisia zako ni muhimu, lakini watu wengine hawawezi kujua unavyojisikia mpaka uwaeleze. Jifunze jinsi ya kuwafanya watu wengine wajue kile unachofikiri na unachokitaka kwa kusema moja kwa moja na kutumia sentensi zinazoanzia na “mimi” – “mimi ninataka” “mimi ningelipenda” “mimi ninahitaji”“mimi Sipendi” ………… .” Fanya mazoezi ya kutumia sentensi zinazoanza na “mimi” mpaka utakapozoea na kujisikia huru kuzitumia.

Tetea hoja yako. 
Una uhuru wa kufikiri na kujihisi unavyopenda. Ni vema kujifunza jinsi ya kuwasilisha
mawazo yako kwa wengine bila ya kuwaudhi au kuwafanya wajisikie vibaya, usionyeshe uadui, ugomvi wala kukosoa sana.

Tetea unachoamini bila kujali wanayosema watu wengine.
Kila mtu ana imani na yaliyo sahihi na yasiyo sahihi, mazuri na mabaya. Imani hizi zinaitwa kanuni. Wakati mwingine unaweza ukawa unajua kanuni zako lakini mambo yanaweza yasiwe wazi sana kiasi cha kukufanya utumie muda kufikiria lipi ni sahihi kwako na ni kwa nini. Iwapo unao uhakika wa usahihi wa kile unachofikiria na kwa nini unakifanya, na kwa nini hupendelei kukifanya utaweza kusimama imara na lile unaloamini. Hivyo basi msimamo wa namna hii utakupa heshima mbele za watu.

Jihadhari na yanayotokana na shinikizo.
Jinsi unavyoelekea kwenye utu uzima unatakiwa kufanya maamuzi mengi peke yako. Wakati mwingine watu wengine wanaweza kukuhimiza na kukusukuma kufanya maamuzi fulani na ukushawishika kufanya hivyo.

Lakini ufahamu kuwa kufanya maamuzi mazuri maana yake ni kupima chaguo zote zilizopo na kufikiria matokeo kwa kila chaguo.Inaweza ikawa kazi ngumu iwapo kuna mtu anakuharakisha au anakushinikiza uamue haraka. Kitu muhimu katika kufanya maamuzi bora ni kuwa na uhakika wa kanuni zako na malengo yako ya maisha kwa ujumla.
Kuwa na msimamo wa pekee ndiyo stadi za Maisha.

Jumapili, Julai 22, 2012

BADILIKO KUBWA, CHANGAMOTO KUBWA

Image By: www.imkeepingup.com

 Mahali pengi ujana umekuwa mgumu kueleweka, na hasa siku hizi vijana wanapata matatizo ambayo wazazi wao, mabibi hata babu zao hawakuwahi kuyapitia.
 
VIJANA TOKA KENYA NA GHANA WANAELEZA HIVI:
 
Patric, kutoka Kenya (Umri,miaka 16)
“Nilichokifurahia katika ujana balehe wangu ni kuwajibika katika majukumu ya nyumbani hasa wazazi wanapokuwa hawapo. Majukumau haya nayapenda kwasababu ninadhani nimeshakua na ninaweza kujidhibiti mimi mwenyewe na wadogo zangu”.

Naana, kutoka Ghana. (Umri; miaka 17)
“Yapo mambo mengi yanayomhusu kijana balehe ambayo siyapendi. Ninakumbuka nilipokiwa na umri mdogo nilikuwa na uhuru zaidi kuliko sasa.Lakini kwa sasa zipo sheria na miongozo mingi.”

TUKIANGALIA;

Mwonekano wako mpya na kujitambua kwako kunawafanya wazazi, shangazi zako na wajomba kuwa na wasiwasi kwa sababu wasingependa upate matatizo na wala wasingependa ufanye makosa makubwa kama vile kupata mimba (au kwa kumpa mimba rafiki wa kike) wakati ungali unasoma. Zaidi ya yote wanakuwa na wasiwasi kwa sababu wanafahamu kwamba umri kati ya 10-19 unaweza kuwa na athari kubwa katika ukuaji wako na aina ya maisha utakayokuwa nayo.

JE UNAFAHAMU VIJANA HUFIKIRIA KWAMBA HAKUNA JANGA LINALOWEZA KUWAPATA?

Ni tabia ya vijana duniani kote, katika nchi tajiri na maskini – kufikiria kwamba mambo mabaya
hayawezi kuwatokea. Hujiambia,

“ Haitatokea kwangu”. Wakati mwingine hujiamini sana na kuhisi wako salama mno.

Je wewe uko hivi? 
Unadhani unaweza kujaribu kitu cha hatari na lisikupate jambo? 
Kwa mfano, wewe na rafiki yako wa kike (msichana) mnafahamu kuhusu dawa za kuzuia mimba. Lakini
mnadhani kwamba ili mradi hamjamiiani mara kwa mara, msichana hawezi akapata mimba.

Au unaweza ukawa na ufahamu mkubwa kuhusu VVU, virusi vinavyo sababisha UKIMWI. Unaweza
ukafahamu kwamba maambukizi yanaweza kutokea kwa njia ya kujamiiana bila kinga, lakini unafikiri kwamba rafiki yako wa kiume hawezi kuwa na maambukizo. Unakataa kufikiri kuwa unaweza kupata maambukizo ya VVU na haiwezekani pia kwa wale watu unaowafahamu kupata ugonjwa huo.

Je haya yanakuhusu? 
Kama ndivyo, hapa kuna mambo ambayo unahitaji kuyazingatia:

Nitarejea kukwambia kuhusu: 
WEWE, MAISHA YAKO NA NDOTO ZAKO.

Jumamosi, Julai 21, 2012

Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Magumu




Tanzania ni moja kati ya nchi nyingi barani Africa zinzokabiliwa na wimbi kubwa la watoto wanoishi katika mazingira magumu .
Utafiti ulliofanyika ulitambua makundi mbalimbali ya watoto hao ikiwa ni pamoja na:-

01. Watoto yatima ( Orphan children)
02. Watoto wenye ulemavu ( Children with disabilities)
03. Watoto wanaojilea ( Children parents)
04. Watoto wanaoishi na virusi vya ukimwi (Children with HIV/AIDS)
05. Watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albino)
06. Watoto wa mtaani (Children in/of street)
07. Watoto walioathirika kwa ubakaji (Children victim of rape)
08. Watoto wanaolelewa na wazee kupindukia (Children in eldery families)
09. Watoto walio kwenye ajira hatarishi (Children in exploitative labour)
10. Watoto walio kwenye biashara ya ngono ( Children sex workers)
11. Watoto wenye magonjwa sugu k.m. kifafa ( Chronicaly ill children)
12. Watoto waliopata mimba za mapema (Early pregnancy)
13. Watoto waliotelekezwa (Children in foster families)
14. Watoto walioathirika kwa madawa ya kulevya (Drug abuse children)
15. Watoto waliolazimishwa kuingia kwenye ndoa (Forced marriage)

HOJA.
1. Jamii inajua nini kuhusu makundi haya ya watoto?
2. Mikakati gani ifanyike ili kuhudumia makundi haya ya watoto hasa vijijini?
3. Serikali ichukue hatua zipi ili kunusuru maisha na ongezeko la watoto hawa?
4. Njia gani zitumike ili kupata takwimu zinazoonyesha tatizo hili kila wakati kitaifa?

Ijumaa, Julai 20, 2012

SABABU GANI ‘NIMHESHIMU BABA YANGU NA MAMA YANGU’?





“WAHESHIMU baba yako na mama yako.”

Kwa vijana wengi maneno hayo yanasikika kama ni jambo la zile enzi za giza.


Kijana-msichana Veda alijulisha uasi wa waziwazi dhidi ya babae kwa kufanya matembezi na mvulana aliyetumia vibaya madawa ya kulevya na alkoholi. Kwa kukaidi, angelienda pia kucheza dansi mpaka chee.


“Nilihisi kwamba yeye alikuwa mzuivu mno,” aeleza Veda.

“Nilikuwa na umri wa miaka 18, name nilifikiri mimi ni mjuzi wa yote. Nilihisi baba yangu alikuwa bahili na hakutaka kamwe nione raha, kwa hiyo mimi nikaenda nje na kufanya nililotaka kufanya.”


Yawezekana kijana; walio wengi hawatakubaliana na vitendo vya Veda. Lakini, kama wazazi wao wa masomo ya nyumbani, au wawe wamefika nyumbani saa Fulani, wengi wangechacha kwa uchungu wa moyo au, jambo baya hata zaidi, wangekaidi wazazi wake inaweza hatimaye kumaanisha si kama tu itakuwa ni vita au amani nyumbani bali pia uhai wake mwenyewe.


Kwa maana amri ya ‘kuheshimu wazazi’ inatoka kwa Mungu, na anaambatanisha motisha ifuatao na kutii amri hiyo”. (Waefeso 6:2, 3) Inaweza kumaanisha faida kubwa au hasara kubwa.


Kwa hiyo, tuangalie upya linalomaanishwa hasa na kumheshimu babako na mamako.




Alhamisi, Julai 19, 2012

Picha za Tukio la Tigo Ilivyokabidhi Fedha za TUCHANGE Kwa Hassan Majaar Trust




























HUU NI MPANGO WA MUDA MREFU ULIOUNDWA ILI KUBORESHA MAZINGIRA YA KUSOMA MASHULENI KWA KUGAWA MADAWATI KATIKA SHULE MBALIMBALI ZA WAHITAJI.

SHEREHE ZA MAKABIDHIANO ZILIHUDHURIWA NA MHESHIMIWA DK SHUKURU KAWAMBWA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI, WANACHAMA WA HMT, MWANDAMIZI MTENDAJI WA TIGO NA WAFANYAKAZI.

Picha zote kwa hisani ya: Prince Ema. Hebu tembelee H A P A

UPANDE WA NYUMBANI




Hapa Tutashughulika na Washiriki wa Familia Kwa Namna hii:

“Nyumbani kuzuri.” Usemi huu unaojulikana sana unaeleza hisia ambayo siku hizi yaonekana ya kizamani na isiyofaa. Migongano yenye kuendelea ya familia inageuza nyumba nyingi kuwa kwa halisi Nyanja za mapigano. Na pengo kubwa la ukosefu wa uwasiliano mara nyingi huzuia majaribio yoyote ya kufanya suluhu.

Je! Wataka nyumba yenu iwe pumziko la amani badala ya kuwa kao lenye ugomvi unaochacha? Ni kweli, washiriki wengine wa familia lazima wafanye sehemu yao. Lakini kwa kushika kanuni chache za Biblia, kuuna mengi unayoweza kufanya ili kuchangia amani nyumbani mwenu.

Jumatano, Julai 18, 2012

YALIYO YA KUKUMBUKA


Rudolf II 
 Alizaliwa 18 Julai, 1552 na kufariki 20 Januari, 1612 alikuwa Kaizari wa Dola la Ujerumani kuanzia 12 Oktoba, 1576 hadi kifo chake. Alimfuata baba yake, Maximilian II, na kufuatiwa na mdogo wake, Matthias.


Hendrik Antoon Lorentz 
 Alizaliwa 18 Julai, 1853 na kufariki 4 Februari, 1928 alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uholanzi. Alitafiti nadharia ya elektroni. Pia alichunguza nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory) na ya kwanta. Mwaka wa 1902, pamoja na Pieter Zeeman alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.


Nelson Rolihlahla Mandela 
alizaliwa tarehe 18 Julai, mwaka 1918. Ni rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Afrika Kusini. Alikuwa mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa ya Apartheid katika Afrika Kusini. Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka 27 kutokana na harakati zake za kuupinga ubaguzi wa rangi. Alifungwa katika kisiwa cha Robben. Baada ya kuachiliwa huru mwaka 1990 alianzisha sera ya maridhiano. Mwaka wa 1993, pamoja na Frederik Willem de Klerk alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.


Roald Hoffmann 
Alizaliwa 18 Julai, 1937 alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Marekani akiwa amezaliwa nchini Poland. Hasa alichunguza utaratibu wa athari za kikemia. Mwaka wa 1981, pamoja na Kenichi Fukui alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.


Hartmut Michel 
Alizaliwa 18 Julai, 1948. Ni mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza ugandishaji wa protini. Mwaka wa 1988, pamoja na Johann Deisenhofer na Robert Huber alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.


Joseph Nestroy Kizito 
Amezaliwa 27 Julai, 1982 Uganda ni mchezaji wa mpira wa miguu wa kulipwa kutoka nichini Uganda, ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya FK Vojvodona nchini Serbia tangu Januari mwaka 2005. Yeye pia ndio kapteni wa Timu ya Taifa ya Uganda. Kizito alifunga goli dhidi ya wa pinzani wao wa kuu FK Crevena Zvezda katika Ligi kuu ya Serbia katika msimu wa mwaka 2005/2006 mechi hiyo ilichezeka nyumbani kwao. Goli hilo lilivunja rekodi ya kukaa muda mrefu bila kuwafunga wapinzani wao wa jadi FK Crvena Zvezda zaidi ya miaka kumi.

Jumapili, Julai 15, 2012

Je Unafahamu Kwamba Muziki ni TIBA?




Leo ktk kipindi Morning Star Radio nimeona nikuletee jambo muhimu sana ambalo weeengi walikuwa hawafahamu. Ni suala ambalo hata wewe ukitumia muda wako kuchunguza utabaini ukweli ulio ukweli halisi.


Usikilizaji wa muziki huweza kuwasaidia wagonjwa walio na matatizo sugu ya mkandamizo wa mawazo (stress) na tiba ya kiwango fulani kwa maradhi ya moyo pale mishipa ya moyo inapoelekea kuziba. Utafiti wa kitiba uliofanyika nchini Marekani umebaini kuwa kusikiliza muziki uliotulia unaweza kupunguza ongezeko la msukumo mkubwa wa damu na kuchanganyikiwa kwa wagonjwa wa moyo.

Wataalamu hao wanasema kuwa kuishi huku ukiwa na matatizo ya moyo ni jambo linalosumbua sana kwahiyo hali hiyo inahitaji tiba mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushauri wa matumzi ya vyakula, vinywaji , lakini pia kuufanya ubongo usipate mkandamizo bila sababu.



Lakini hata hivyo Dr. Joke Bradt wa kituo cha sanaa na ubora wa maisha katika kituo cha utafiti wa kitiba katika Chuo Kikuu huko Philadelphia nchini Marekani anasema ‘majaribio yaliyokwisha fanyika ni machache na hasa aina ya muziki unaofaa ni kwamba usikilizwe kwa muda gani na kwamba bado wanalifanyia kazi suala hilo. Tafiti zilizokwisha fanyika ni 23 kwa wagonjwa 1,461 kwa kuwapatia muziki maalum uliorekodiwa na kuungwa katika mishipa , na kazi hiyo hufanywa na wataalamu mabingwa wa masuala ya maradhi ya moyo na sanaa.

Tayari wanamuziki duniani kila mtu anakuna kichwa kufikiria kitu gani atunge na kukiweka katika muziki mororo ili uteuliwe kuwa ‘dawa’ na bila shaka atakuwa billionea ghafla. Penda kusikiliza muziki laini unapojikuta umetindikiwa na mawazo kibao…

Jumatano, Julai 11, 2012

ISHARA YA KUTAMBUA

Picha kwa hisani ya: www.telecomcircle.com

MASWALI yanaibuka. Je, kikosi kilichomteka daktari huyo na kumpeleka kwenye msitu wa Mabwepande, Dar es Salaam kimefadhiliwa na serikali au magaidi?
Dokta Steven Ulimboka, mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari alikumbana na kikosi cha watekaji, watesajii na wauaji. Kama ni magaidi walikusudia nini? Magaidi walikuwa na nongwa ipi na Dk. Ulimboka? Watekaji wametoa ujumbe wowote? Je, kuna historia ya ugaidi wa namna hii nchini?

Je, watekaji hawawezi kuwa mawakala wa serikali? Je, hakiwezi kuwa kikosi maalum cha kutesa watu kwa siri chini ya udhamini wa serikali? Jibu la maswali mawili hayo ni ndiyo, maana hiyo, ndiyo hasa ina nongwa na Dk. Ulimboka aliyeongoza mgomo wa madaktari nchi nzima kudai hali nzuri ya utumishi.

Sikia. Mtu wanayemfahamu kutoka ikulu anampigia simu Dk. Ulimboka ili wakutane kujadili ufumbuzi wa mgomo. Dk. Ulimboka na mwenzake Dk. Deogratius Michael wanakwenda eneo la kikao; wanamkuta mtu anayejiita Abeid; lakini ghafla wanatokea watu na kumchukua yeye tu.

Watekaji wanakwenda naye Mabwepande, msitu uleule ambao mwaka 2006, polisi wa serikali walitumia kuua watu wanne – wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva teksi mmoja.

Vijana wale wafanyabiashara walitekwa na polisi, wakateswa, wakaporwa mali waliyokuwa nayo kisha wakatwangwa risasi za kisogoni – wakafa. Unyama mkubwa. Mambo yalipojulikana, polisi wakadai kuwa walikuwa majambazi.

Rais Jakaya Kikwete akaunda tume; ikahoji watu, ikapata ushahidi kwamba polisi walihusika kuteka, kuwapeleka msituni na kuua. Kesi ikafunguliwa, lakini “mahakama” ikasema polisi walioteka na kuwapeleka Mabwepande na kuua hawana hatia; ikawaachia!

Wiki iliyopita, ‘mawakala’ waliokuwa na nongwa kubwa na mgomo, wakafanya juhudi usiku wa kuamkia siku ambayo serikali ilisema itatoa msimamo juu ya mgomo huo, wakatekeleza lile Waziri Mkuu, Mizengo Peter Pinda alilosema “…liwalo na liwe” wakamteka, wakampiga, wakamng’oa meno na kucha kushinikiza ametumwa na nani kuongoza mgomo. Serikali inatoka vipi hapa?

Mwaka 2008 Pinda alisema wanaoua albino wauawe, kauli inayotafsiriwa sasa kuwa hata wanaoua watu kwa njia ya mgomo wauawe. Ndiyo, waliotenda unyama huo wakawapigia simu madaktari wakachukue “mzoga” wao.

Serikali imekana kuhusika. Lakini hakuna serikali yoyote duniani iliyowahi kukiri kuhusika katika mauaji ya wanasiasa au wanaharakati au waandishi wa habari au wapinzani.

Vikosi maalum vya kuteka watu, kuwapoteza, kutesa na hata kuua, hutekeleza unyama huo kutetea au kulinda maslahi fulani, kama vile biashara haramu au ufisadi au maslahi ya kisiasa.

Mathalani magenge ya wahuni na wauzaji wa dawa za kulevya Mexico na Colombia huteka viongozi wa juu serikalini au jamaa zao na hushinikiza walipwe mamilioni ya dola kama kikombozi.

Magaidi wa Colombia waliounda jeshi linalofahamika kama Revolutionary Armed Forces of Colombia (FARC) huteka, hutesa na kuua viongozi wa serikali wanaopinga biashara ya dawa za kulevya.

Miaka ya 1970 vilikuwepo vikundi vingi vya kigaidi na kimojawapo kiliongozwa na Ilich Ramírez Sánchez “Carlos the Jackal,” raia wa Venezuela.

Matukio ya kuteka na kuua wanasiasa yakifanywa na vikundi vya watu, serikali hutumia rasilimali zake zote kuwasaka wahusika.

Hii ndiyo sababu, Carlos ambaye aliitesa sana Ufaransa na kuvamia ofisi za makao makuu ya Umoja wa Nchi za OPEC mjini Vienna, Austria mwaka 1975 na kuua mawaziri watatu na wengine 63 kutekwa wakiwemo mawaziri 11, alinaswa na sasa anatumikia kifungo cha maisha jela nchini Ufaransa.

Hata Osama bin Laden aliyetikisa dunia kuanzia miaka ya 2000, aliuawa huku kikundi cha Al-Shaabab cha Somalia kikisakwa. Ikumbukwe kila kikosi cha watu maalum kikiteka watu maarufu, hulenga ama kulipwa fedha au kushinikiza wenzao waliofungwa waachiwe kabla hawajauawa au masuala ya siasa.

Lakini huwa vigumu kuikamata serikali. Ukweli hata kama serikali itakanusha, kama ilivyofanya sasa kwa Dk. Ulimboka au kwa mkurugenzi mstaafu wa Usalama wa Taifa, Imran Kombe na kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Zanzibar, Abdullah Kassim Hanga na wengineo, ushahidi wa mazingira unathibitisha serikali inahusika.

Katikati ya mapambano dhidi ya ufisadi, Mkurugenzi wa MwanaHALISI, Saed Kubenea alipigwa ofisini na akamwagiwa tindikali machoni. Polisi wakafungua kesi; mahakama ikatupa eti ni ugomvi wa mapenzi.

Twende Kenya. Jaramogi Oginga Odinga (baba wa Raila Odinga), licha ya kuwa kiongozi katika serikali ya Kenya, alishtuka serikali kuhusika kisiri kuua watu.

Sababu za kuamini hivyo ziko wazi. Odinga ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kabla ya mwaka 1964 kuwa Makamu wa Rais alishangaa kuona uhusiano ukibadilika haraka na marafiki zake wakiuawa.

Mwaka 1965 Odinga alishtuka mshirika wake mkuu, mwanasiasa Mkenya mwenye asili ya Asia, Pio Gama Pinto akiuawa. Serikali ilipohojiwa ilikanusha kuhusika.

Baada ya kutafakari mauaji hayo na siasa zisizo na mwelekeo, mwaka 1966 alijiuzulu na kuunda chama cha Kenya People's Union (KPU). Mwaka 1967 alitunga kitabu kiitwacho Not Yet Uhuru yaani Uhuru Bado Kidogo kilichoeleza kwa kina siasa za Kenya.

Humo alieleza kwa kina kwamba mambo yaliyokuwa yanafanywa na wakoloni dhidi ya Waafrika, wanasiasa kutekwa, kupigwa na kuuawa kwa madai ya uhaini, ndiyo yalikuwa yanafanywa chini ya serikali yao dhidi ya raia.

Mwaka 1969 aliuawa Tom Mboya (Waziri wa Uchumi na Mipango), halafu Josiah Mwangi Kariuki (1975), na mwaka 1990 akauawa Robert Ouko (Waziri wa Mambo ya Kigeni), na wanaharakati wa haki za binadamu, Oscar Kamau Kingara (2009) na John Paul Oulo (2009).

Nani alimuua Ouko? John Troon, mchunguzi kutoka Scotland Yard alitaja wanasiasa kadhaa wakiwemo Nicholaus Biwott na Hezekiah Oyugi lakini serikali iliwakingia kifua. Alipoona mazingira ya kutoa ripoti kamili yanahatarisha usalama wake, Troon alirudi Uingereza.

Baadaye Kamati ya Bunge iliyoundwa kubaini muuaji wa Ouko, ilikwenda Uingereza kuonana na Troon ambaye alisema “Ouko aliuawa kwa amri ya serikali.”

Amri hiyo ya serikali “haikutolewa na mtu mwingine yeyote isipokuwa Rais Daniel arap Moi”.

Tena ilielezwa kuwa Ouko, alitekwa shambani kwake Koru, akasafirishwa hadi Nairobi, ambako aliuawa ikulu kisha wakaurudisha mwili wake shambani na kuuchoma moto. Ukatili ulioje?

Hapa Tanzania kuna hukumu zinazotia shaka. Mwaka 1995 walimfukuza Kombe wakamtwanga risasi kwa madai eti walimfananisha na jambazi aliyeiba gari la tajiri mmoja.

Kabla ya kumiminiwa risasi, Kombe alinyanyua mikono juu akiomba wasimdhuru, lakini wapi. Ikafunguliwa kesi eti ya kuua bila kukusudia, wakafungwa na sasa wako huru.

Unatakiwa kuwa na moyo mgumu kuhoji kilichowakuta Hanga, Othman Sharrif na wengineo. Nani aliondoa uhai wao, maradhi au mkono katili wa serikali?

Ili kila mmoja aridhike kwamba serikali haihusiki, Rais Kikwete aunde TUME HURU ya kuchunguza kadhia hiyo basi.
HII KITU NIMEIPATA KTK LINK HII  H A P A

William Shakespeare



Waingereza mara nyingi humtazama kuwa ni mwandishi mkuu wa lugha yao. Aliandika hasa maigizo na tamthiliya. Alifanya pia kazi ya uigizaji.
Maigizo yake hupangwa katika vikundi vya
  • michezo tanzia
  • tamthiliya kuchekesha
  • tamthiliya ya kihistoria
Wataalamu wengine hawakubali ya kwamba maandiko yote yanayojulikana kama "Shakespear" yameandikwa na mtu yeye yule. Walio wengi wameridhika ya kwamba huyu Shekespear wa kihistoria mwenyewe alikuwa mwandishi..

William Shakespeare amezaliwa Aprili 1564 - 23 Aprili, 1616 alikuwa mwandishi mashuhuri nchini Uingereza.

Jumatatu, Julai 09, 2012

Kuku wa nyama


Ni aina ya kuku anayefugwa kwa ajili ya nyama. Kuku wa nyama wa kisasa wa biashara, wanaojulikana kwa kawaida kama Cornish crosses au Cornish-bred Rocks huzalishwa kwa wingi, huwa na nyama fanisi na hukua kasi zaidi kuliko kuku wa mayai au kuku wanaotumika kwa zote mbili. Wao wanabainishwa kutokana na ukuaji haraka , uwiano kula ulio juu na viwango vya chini ya shughuli. Kuku wa nyama mara nyingi huwa tayari wafikia uzito wa paundi 4-5 katika wiki nane tu.

Wao wana manyoya meupe na ngozi ya manjano . Kuku hawa wa faida katika nyama kwa sababu inakosa "nywele" za kawaida ambazo wengi wa aina tofauti wanabidi kuchomwa baada ya kutoa manyoya. Kuku wote wa kike na kume huchinjwa kwa ajiliya nyama zao. Katika mwaka wa 2003, kuku wa nyama takriban bilioni 42 walizalishwa,asilimia 80% ambao walitayarishwa na makampuni nne: Aviagen, Cobb-Vantress, Hubbard mashamba, Hybro.

Ilivyoanza

Kabla ya kuanzisha vizao vya nyama (ng'ombe, kuku, nk) kuku wa nyama walikuwa kuku wa kiume (jogoo) ambao hupunguzwa katika shamba la mifugo. Kuku wa walichinjwa kwa ajili ya nyama na wa kike (mwera) waliadhimishwa kwa uzalishaji wa mayai. Ikilinganishwa na leo, nyama ilikuwa chache na ghali ikilinganishwa na mayai, na ilikuwa nyama ya kifahari. Maendeleo ya uzalishaji wa kukumaalum wa nyama ulitenganisha usambazaji wa mahitaji kuku wa mayai kutoka kwa mayai. Hii, pamoja na mafanikio katika lishe na uzalishaji ambako kuliruhusu kuku wa nyama kuzalishwa kila wakati, kulisababisha gharama ya nyama ya kuku kuwa nafuu.

Broilers mara nyingi huitwa "Rock-Cornish," akimaanisha antagandet ya aina ya kuku hybrid zinazozalishwa kutoka msalaba wa kiume wa kawaida breasted Cornish mbili Strain na mwanamke wa tall, boned kubwa Strain wa kizungu Plymouth Rocks.  jaribio hili la kwanza la zao la kuchanganywa la kunyama kuletwa katika 1930s na akawa dominerande katika miaka ya 1960. Kuchanganya huku kwa awali uzazi, ukuaji polepole, na ugonjwa susceptibility, na kuwa na taratibu za kisasa broilers kuwa tofauti sana kutoka Cornish x Rock hybrid.


Mazao na UKisasa Wake

Kuku wa nyama wa sasa ni kizazi tatu (zao la F2 ). Mababu wa kuku hizi za nyama wametoka katika asili nnne tofauti,Wawili ambao wako katika laini ya kiume na wawili ambao wako katika laini ya kike , ambao wanapatana ili kuzaa kuku wa nyama . Uhusiano huu huzuia tabia za kipekee kwa kuwa Matatizo haiwezi tena kusambazwa katika jamii ya kuku wa mayai.  Kwa kuongeza, laini kiume na kike hazizalishwi kwa ajili ya tabia moja;laini ya kike inafaa kuytaga mayai mengi iwezekanavyo , kwani idadi ya mayai yaliyotagwa na kila mwera huchangia katika gharama ya mayai ya kuku wa nyama na hivyo broiler vifaranga vyake. Uwezo wa kutaga mayani chini muhimu katika male Mpya, wakati jogoo uzazi ni muhimu sana.

Kuku wa mayai hulelewa katika mazingira yaliyodhibitiwa pamoja na maelfu ya w vifaranga wenzake. Kuku huyu anapatiwa chakula bila kipimo kupata ambacho ni mlo maalum wenye kiwango cha juu cha protini na hulishwa kutumia mfumo wa kulisha wenye kujiendesha. Hii ni pamoja na hali ya taa bandia inayochochea ukuaji na kwa hivyo uzito wa mwili unaotakikana unafika kwa muda wa wiki 4-8 , kutegemea uzito wa mwili unaotakikana na kiwanda cha kutayarisha nyama. Baada ya kutayarisha, kuku hawa husambazwa kwenye maduka wakiwa freshi au waliohifadhiwa .

Kwa sababu ya ufanisi katika kupata nyama, kuku wa nyama pia ni maarufu katika mashamba ndogo ya familia katika jamii za vijijini, ambapo familia zitalisha kundi ndiogo za kuku hawa.

Kuku hawa wa nyama wakati mwingine hufugwa katika makao ya nyasi kwa kutmbinu mbalimbali inayoitwa pastured kuku, kama ulioendelezwa na Joel Salatin na kukuzwa kwa wazalishaji wa kuku Pastured American Association.

Neno "broiler" ni linajulikana sana katika Amerika ya Kaskazini na Australia lakini siyo mahali pengine katika kuzungumza Kiingereza duniani. Neno "kuku wa mayai" linakutumika sana nchini Pakistan na India, kama ilivyokuwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kijerumani zamani na bado sikuhizi katika baadhi ya sehemu ya mashariki ya Ujerumani. Neno hili pia hutumiwa nchini Indonesia, Sweden, Finland, Poland na katika Balkan.

Hoja Yenye Suala la Msingi

Mara nyingi kuku hawa wanaweza kupata matatizo ya miguu kwa sababu miguu yao haiwezi kubeba miili yao mizito. Uchunguzi uliofanywa na Slu Skara (Chuo Kikuu cha Kilimo cha Swedis) ulibaini kuwa tu 1 / 3 ya kuku wa nyama ambao wako karibu kuchinjwa wana afya. Pia, si jambo la kupendeza na hatari kutokan na wanyama wanaokula kuku, na haifai kwa ujumla kufugwa katika mashamba madogo mbalimbali.

Kama taka haifagiliwi katika vyumba hivi na kuzuia kuku hawa kusimama juu ya kinyesi cha Vidonda miguu na Malengelenge yanaweza kutokea. Ndege wanaobadilishwa mara nyingi hawana masuala haya.





Jumapili, Julai 08, 2012

RAISE & SHINE QUARTET


Ni kundi la vijana wadogo linalojihusisha na muziki wa Acappella na linapatikana katika kanisa la Waadventista wasabato Tegeta.

Hapo walikuwa ktk Kipindi Morning Star Radio.

Alhamisi, Julai 05, 2012

MELI



ni chombo kikubwa cha usafiri kwenye maji. Siku hizi meli huwa na bodi ya chumaikisogezwa kwa nguvu ya injini inayochoma diseli. Hadi karneya 19 meli zilijengwa kwa kutumia ubao zikasongezwa hasa kwa nguvu ya upepo kwakutumia tanga. Jahazi ziko hadi leo. Meli hutumiwa hasa kwa kubeba mizigo na abiria. Kuna pia meli za kijeshizinazoitwa manowari. Kuna njia mbalimbali kutofautisha ukubwa wa meli na njia ya kawaida imekuwa tani GTinayotaja mjao wa chombo. Mkuu na kiongozi kwenye meli anaitwa nahodha. Watu wanaofanya kazi kwenyemeli kwa jumla ni mabaharia.

Muundowa meli
  1. Omo ni sehemu ya mbele ya bodi ya meli
  2. Pua la omo linapunguza ukinzani wa maji wakati wa mwendo na kupunguza matumizi ya mafuta ya injini
  3. Nanga hutiwa hadi chini ya maji na kushika meli ikisimama
  4. Bodi ya meli imetengenezwa kwa mabamba ya feleji
  5. Rafadha (au: jembe) ya meli inasogeza chombo mbele ndani ya maji
  6. Tezi (au: shetri) ni sehemu ya nyuma ya meli
  7. Dohani ni faneli au eksosti kwa hewa chafu ya injini
  8. Majengo juu ya sitaha ni kama nyumba kwa ajili ya mabaharia na abiria, huwa pia na chumba cha kutawala meli
  9. Sitaha ni uso wa juu wa meli; ni dari juu ya bodi ya meli; meli kubwa huwa na sitaha mbalimbali chini ya sitaha ya juu

Historia


Vyombo vya usafiri vya kwanza kwenye maji yalikuwa mashua na maboti madogo kama mtumbwi.
Kuanzia mwaka 4000 KK watu wa Misriya Kale wameanza kutengeneza jahazi ndogo. Manmo 1200 KK watu wa Finisia na Ugirikiya Kale walijenga jahazi kubwa zaidi yenye urefu wa mita 30. Wachinawanajulikana walijenga jahazi kuanzia 2000 KK. Waromawa Kale walitengeneza meli iliyobeba watu 1,000.

Katika mazingira ya Mediteranea meli hizi za kwanza zilisogezwa kwa kasia pamoja na tanga. Meli kubwa zakiroma zilikuwa na kasia kubwa zilizopigwa na watumwa wawili au watatu kwa kilakasia.
Jahazi ziliboreshwa hadi kuvuka bahari kuanzia karne ya 15 BK. Wachina naWareno ni watu wa kwanza waliovuka bahari za mbali. Ila tu Wachina baada yakutembelea mara kadhaa pwani za Afrika chini ya Zheng Hemnamo mwaka 1400 waliamua kuacha upelelezi huu lakini Wareno waliendelea kuvukaAfrika na dunia yote na kuanzisha kipindi cha ukoloni cha Ulaya.
Katika karne ya 19 injini ya mvuke ilipatikana hata kwa meli. Melizikawa kubwa zikaendelea kukua wakati injini ya diseli imepatikanakatika karne ya 20.

Aina na idadi ya meli

Bila kuangalia maboti madogo dunianikuna
  • meli za kibiashara 34,882 zenye ukubwa wa tani GT zaidi ya 1,000; jumla ya meli hizi ni tani bilioni 1.04. (mwaka 2007)
    • meli hizi zilibeba jumla ya shehena (mzigo) tani bilioni 7.4 (mwaka 2006) na kiasi hiki kimekuwa asilimia 8 kila mwaka.
    • 37.5% za meli hizi zilibeba shehena ya mafuta
    • 35.8% za meli hizi zilibeba shehena zilizofunguka kama vile madini, makaa mawe, nafaka au simiti
    • 10% zilikuwa meli za kontena
    • 10% ni meli zinazochanganya kila aina ya mizigo
  • manowari 1,240 bila kuhesabu maboti madogo ya kijeshi (mwaka 2002)
    • Marekani ilikuwa na tani milioni 3 za manowari, Urusi na tani milioni 1.35, Uingereza na tani milioni 0.5 na China na tani milioni 0.4.
  • meli za kuvua samaki ni nyingi lakini ziko za kila ukubwa si rahisi kuzipanga. Kuna vyombo 38,400 zenye tani zaidi ya 100. Nyingi zaidi ni ndogo sana; meli kubwa ya kuvua samaki zafikia tani 3,000 halfu kuna meli za viwanda ambako kundi la meli zinapeleka windo la samaki na samaki hizi zinakatwa mara moja na kufungwa tayari kwa kuuzwa madukani zikitunzwa katika barafu.