Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Januari 10, 2011

MIWANI YENYE CAMERA

Wakati Dr. Dre na wenzake kama 50cents wamekaza nia kwenye upande wa Wireless Headphones!!!

Mwanadada ambaye ni mwanamuziki usio wa injili anayeitwa Lady Gaga a.k.a Queen of Twitter amekuja na kitu tofauti na kipya kinachoitwa Camera Glasses.
Ni miwani yenye swaga ambayo yanaweza kupiga picha, kurekodi video na kufanya sharing kwenda kwenye mitandano maarufu kama facebook n.k
Mambo hayo

UZINDUZI WA WIRELESS HEADPHONES

Juzi Teentz iliwapa ishu ya headphones mpya za 50cent zinazoitwa Sleek by 50cent…, Sasa headphones hizo zimezinduliwa rasmi hivi karibuni kwenye mkutano 50cent aliofanya na waandishi wa habari akiwa na Team nzima ya kampuni yake mpya pamoja na kuzielezea kiundani zaidi akizilinganisha na zile za Beats by Dre.. kwa kusema kuwa zake ni Platinum na zimekuja na teknologia mpya ya signal inayoitwa KLEAR.. ambayo badae itatumika kwenye simu kama vile ilivyo Bluetooth.

Tembelea mwenyewe hapa:
http://www.teentz.com

MUKESH AMBANI HOUSE



Mmoja wa matajiri wakubwa duniani, Mukesh Ambani, raia wa nchini India, aliemaliza ziara yake katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kutoa ahadi ya kuitangaza hifadhi hiyo ili iweze kupata watalii wengi zaidi kutoka mataifa mbalimbali. Ambani anayedaiwa kuwa ni tajiri namba nne duniani, aliingia nchini tangu Septemba 30, mwaka jana kupitia katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) akiwa na ndege nne binafsi pamoja na ujumbe wa watu 48.

Tajiri huyo mwenye kumiliki majengo makubwa ya kifari nchini India yenye huduma zote (mojawapo hili kushoto) alisema amefurahishwa na kuvutiwa na vivutio vilivyomo katika hifadhi hiyo. Aidha, tajiri huyo alisema ataisaidia Serikali ya Tanzania kutafuta wawekezaji wa kuwekeza katika hifadhi hiyo ikiwa ni pamoja na kujenga mahoteli makubwa ambayo yatavutia watalii wengi zaidi.

DIOKSIDI KABONIA

Dioksidi kabonia (pia: Dioxidi ya kaboni) ni kampaundi ya kikemia inayounganisha atomi mbili za oksijeni na atomi moja ya kaboni katika molekuli. Fomula yake ni CO2.

Katika mazingira ya kawaida hutokea kama gesi inayoganda kwenye halijoto chini ya -78.5°C. Katika hali ya gesi haina ladha wala harufu.


Dioksidi kabonia inatokea wakati viumbehai wanapumua na kutoa pumzi; inatokea zaidi wakati wa kuchoma mada ogania yaani mada yenye kaboni ndani yake. Mimea inahitaji gesi hii kwa mchakato wa usanisinuru ilimojenga chakula chao. Inabadilisha CO2 kuwa sukari aina za glukosi.

Kiasi cha kaboni dioksidi hewani imeongezeka katika miaka 150 iliyopita kutokana na kuchoma kwa fueli kisukuku kama makaa mawe na mafuta ya petroli. Uchumi wa viwanda, uzalishaji umeme na usafiri kwa magari yenye Injini mwako ndani kumeleta kuchomwa kwa kiasi kikubwa cha fueli hizi ambazo yote zina kaboni ndani inayomwagwa sasa kwenye angahewa kwa umbo la dioksidi kabonia.




Kuongezeka kwa gesi hii hewani kunasababisha kupanda kwa halijoto duniani2infraredi yaani joto. Maana yake nishati ya mwanga unaoonekana unaingia katika angahewa ya dunia lakini joto peke yake halitoki kirahisi. Tabia hii ni muhimu kwa uhai duniani kwa sababu kaboni dioksidi hewani inazuia kupoa kwa dunia wakati wa usiku; ila tu kuongezeka kwa gesi kutokana na shughuli za kibinadamu kunasababisha pia kupanda kwa halijoto duniani na matokeo yake yasiyotakiwa. kunakuonekana kama tatizo kubwa kwa wakati ujao. Muhimu ni tabia ya CO kupitisha nuru inayoonekana kama nuru ya jua lakini kuzuia mnururisho wa

Dioksidi kabonia ina matumizi mbalimbali kwa mfano kama gesi katika vinywaji aina za soda na bia, katika kizima moto za kupambana na moto penye umeme na mengi mengine.

Alhamisi, Januari 06, 2011

KUPANDA KWA HALI JOTO DUNIANI

Kupanda kwa halijoto duniani kunaonekana kwa kulinganisha vipimo vya halijoto vinavyopatikana. Kupanda huku kunaleta mabadiliko ya hali ya hewa yaliyoanza tayari kuathiri maisha ya watu na uhai duniani kwa ujumla.

Kuna hofu ya kwamba mabadiliko haya yataleta hatari kubwa kwa jamii za watu.

Kati ya wanasayansi kuna tofauti ya maoni kama sababu za mabadiliko ni shughuli za kibinadamu au kama kuna sabau asilia. Siku hizi wataalamu wengi wanafikiri ya kwamba sababu kuu ni kuchoma kwa makaa na mafuta katika viwanda, magari na vituo vya umeme kunachopuliza gesi hewani kama dioksidi kabonia.


Vipimo na data

Duniani kuna upimaji wa kisayansi wa halijoto tangu mwaka 1860. Kabla ya hayo kuna kumbukumbu ya hali ya hewa katika karne zilizopita kutoka mahali mbalimbali ambazo hazikusanifishwa wakati ule. Leo hii wanasayansi wanatumia vipimo na taarifa za kale wakipiga makadirio juu ya hali ya hewa katika historia.

Hapo wanatumia pia mbinu kama kulinganisha miviringo kwenye mashina ya miti inayonyesha miaka yenye mvua mwingi au kidogo au wanapima kiwango cha dioksidi kabonia kwenye barafu ya chini nchani yenye umri wa miaka 10,000 na zaidi.

Kwa jumla makadirio ya hali ya hewa hutofautiana lakini kwa jumla kuna picha juu ya miaka 1,000 iliyopita. Watalaamu wanakubaliana ya kwamba mnamo mwaka 1000 kulikuwa na kipindi cha joto kiasi na tena kipindi cha baridi kiasi kuanzia manmo mwaka 1600.

Lakini hakuna uhakika bado juu ya athira duniani kwa sababu sehemu kubwa ya data ni kutoka upande wa kaskazini ya dunia.

Vipimo vya kisayansi vinavyopatikana vinaonyesha ya kwamba halijoto ya wastani duniani imepanda sentigredi 0.7 kati ya 1906 na 2005. Hii si kiwango kidogo; wakati wa zama za barafu kubwa miaka 100,000 iliyopita halijoto ilikuwa tu 6 °C chini ya wastani ya leo na hii ilitosha kufunika seehmu kubwa za Ulaya, Asia na Amerika ya Kaskazini na mabapa manene ya barafu.

Dalili zote zinadokeza ya kwamba kupanda kwa halijoto kuliharakishwa tangu 1970 na kunaelekea kupanda zaidi.


Sababu za kuongezeka kwa halijoto

Kwa miaka kadhaa wataalamu hawakukubaliana juu ya sababu za kongezeka kwa halijoto. Kwa jumla kuna maelezo mawili tofauti:

  • Kupanda kwa halijoto ni jambo la kawaida lenye sababu asilia; historia inaonyesha vipindi vya joto na vipindi vya baridi na sababu kuu ni mabadiliko ya kiwango cha mnururisho wa jua uanofika duniani. Mabadiliko haya hayakueleweka bado lakini labda kuna kitu kama majira ya jua yenyewe yanaobadilia kila baada ya miaka mia kadhaa.
  • Kupanda wa halijoto kwa sasa si jambo la kawaida kwa sababu kunaenda sambamba na kuongezeka kwa gesi kama dioksidi kabonia hewani kutokana na shughuli za kibinadamu hasa kuchoma kwa makaa na mafuta ya petroli.

Siku hizi wataalamu wengi wanelekea upande wa pili maana wanaona mbali na sababu asilia kuna athira za kibinadamu zinazobadilisha hali ya hewa.


Matokeo yanayotarajiwa

Wataalamu wanaonya ya kwamba kupanda kwa halijoto inaweza kuleta mabadiliko kama yafuatayo:

  • kuongezeka kwa halijoto ya angahewa itaongeza pia halijoto ya bahari na kusababisha uvukizaji mkubwa utakaoleta mawingu na mvua wa nyongeza duniani
  • mikondo ya bahari itabadilika na kubadilisha hali ya hewa katika nchi nyingi
  • sehemu kadhaa penye jangwa zitapokea mvua lakini maeneo mengine yatakosa mvua hivyo kuleta matatizo kwa kilimo na njaa kwa watu
  • barafu kwenye ncha za dunia itaendelea kuyeyuka. Hii itasababisha kupanda kwa uwiano wa bahari, kuleta mafuriko kwenye pwani za dunia na kuhatarisha makazi ya watu karibu na bahari hasa miji ya bandari na nchi za visiwani. Nchi kadhaa kama Maldivi zitazama baharini na kupotea kabisa.
  • Kwa jumla upepo na tufani zitaongezeka na kuwa kali zaidi
  • Magonjwa kama malaria yataongezeka kwa sababu mbu wanaopitisha ugonjwa watapata nafasi mpya katika sehemu zilizokuwa baridi mno hadi sasa.

Jumatatu, Januari 03, 2011

FIKIRI TENA FIKIRI

1.
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.


2.
Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.



3.
Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

4.
Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,


5.
Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Jumapili, Januari 02, 2011

MUZIKI WA INJILI VIPENGELE VYA KIHISTORIA




kwa kuanza nitaanza na uchambuzi wa mtindo wa muziki wa Injili 'Gospel' na hii ni hatua nyingine ya mfululizo wa uchambuzi wa kina wa mitindo mbalimbali ya muziki hapa duniani leo tutiririke katika mtindo huu wa kiimani zaidi kama nilivyowagusia wiki iliyopita, hasa juu ya fungamano zake na imani ya Kikristu.

Mitindo ya kiimani ipo mingi, siku za usoni kadri tutakavyopata nafasi tutaweza kuichambua na hiyo mingine pia, hii ni mitindo kama ya Bingi ambayo ni ngoma ya kuabudia ya kirastafari, Quasida, inayohusika sana na Uislamu.

Mbali na hilo pia ipo mathalan, mitindo ya kuimba ya imani lukuki duniani kama vile Bhudha, Hare Krishna na hata imani za Kihindu, ambayo muziki wake pia una mchanganyiko na muziki wao wa kienyeji kama ule uliokuwa ukipigwa na gwiji wa mtindo huo aliyefariki hivi huko India akiwa na umri wa miaka tisini na moja, Ustaa Bismilkhan.

Ustaa Bismilkhan aliyekuwa akipiga Classicalâ za Ki-hindu kwa takriban miaka sabini na tano, tangu alipokuwa na miaka kumi na sita na tutayaona siku za mbeleni panapo majaliwa, kwa sasa tujikite katika mtindo wetu huu wa Gospel 'miondoko ya kumsifu Mungu'.



Sina shaka nikikutajia jina unajenga picha ya haraka ya wasanii waliojizolea umaarufu mkubwa sana kwa sasa katika muziki huu.

Kwa hapa nyumbani hawa ndio mastaa wetu wa muziki huu kwa nyakati hizi japo kihistoria kabla ya hapo kulikuwa na watu waliotamba katika anga hizi, baadhi ya wanamuziki waliotamba katika muziki wa kidunia na baadaye kuingia kwenye Gospel.

Hivi ni nini hasa maana ya jina la muziki huu, kwa lugha ya Kiingereza linalotamkwa Gospel? Wengi huuita mtindo huu kwa Kiswahili kama Muziki wa kumtukuza Mungu au Muziki wa Injili

Yote haya yako sawa, lakini katika namna tofauti na uelewa wa wengi wetu, tafsiri ya neno la Kiingereza Gospel kwa Kiswahili ni mafundisho matakatifu ya neno la Mungu katika maandiko yake yanayopatikana katika kitabu kitakatifu cha Biblia.

Mengi zaidi yakihusisha Agano jipya na mafundisho ya Bwana Yesu Kristo, kama yanavyosimuliwa katika injili nne zilizoandikwa na Mathayo, Marko, Luka na Yohana.

Neno Injili linalomaanisha Habari Njema linatokana na neno la Kigiriki Eungelion.

Katika hilo hilo agano jipya zaidi ya injili hiyo iliyoandikwa mara nne huku tatu zikifanana sana kwa ukaribu, kuna mafundisho pia ya Mtume Paulo hasa kupitia nyaraka zake mbalimbali.

Kama nilivyoeleza hapo awali, ni sahihi kwa muziki huu kuitwa wa Injili na wa kumtukuza Mungu pia kwa maana ya kupitia Injili hiyo ya Yesu.

Lakini kwa maana halisi ya mwanzo wa neno la Mungu ambalo lilianza katika Agano la Kale linaloanza na kitabu cha Mwanzo, kabla hata hawajazaliwa manabii waliokuja kubashiri kuzaliwa kwa Masihi.

Hiyo ina maana gani? Kwamba Mungu alianza kuimbiwa na kutukuzwa mara baada ya kumaliza kazi ya kuumba dunia kabla ya kumuumba binadamu.

Maana viumbe vingi alivyoviumba wakiwamo wanyama, miti, ndege, pepo vyote vilitoa sauti na kuimba katika namna yake na kutimiliza utukufu wake.

Msikilizaji, kimsingi muziki unaundwa na sauti kwanza na usipate dhana kwamba ni vyombo, vyombo havitaweza kujenga msingi wa kuundwa kwa muziki kama hakuna sauti na ndio maana vyenyewe vimetengenezwa kutoa sauti.

Lakini kama tunafuata msingi wa maandiko, sauti za kwanza kuwepo duniani ni hizo za viumbe nilivyovitaja kabla ya kuumbwa Adam.

Ukisoma katika Agano la Kale, unaona pia kutukuzwa kwa Mungu katika kitabu cha Kutokaâ 15:1-18 na 19:20:21 hizi zikiwa ni nyimbo za kumsifu Mungu baada ya kuwakomboa wana wa Israel kutoka utumwani huko Misri.

Zipo pia nyingine alizoimbiwa kutokana na mema yake, kama katika kitabu cha Samuel (2):6:5 na 22:2-51 alizoimbiwa na Mfalme Daudi na pia katika kitabu cha Isaya 26:2-19.

Mbali na hizo zipo nyingi sana katika maandiko kwa nyakati na nafasi mbalimbali, kwanini inatupasa kuyajua yote hayo? Ni kwa sababu muziki huu wa kumtukuza Mungu unatokea mbali sana kulikoni unavyoweza kuufikiria.

Katika kukutayarisha kabla hatujaanza uchambuzi rasmi, naomba nikugusie kuwa tutasafiri kiuchambuzi tangu kuanza kuumbwa kwa ulimwengu na tutapitia nyakati hizo za Agano la Kale, tutakuja katika zama za masinagogi na wakati wa Yesu na tutapitia pia katika Ukristo na kuanza kwa kanisa.

Tutachambua kuanza kwa madhehebu na mgawanyiko wake kulikosababisha kuzaliwa kwa mirindimo tofauti ya kikanisa kutokana na hilo.

Tukitoka hapo tutaelekea katika mitindo mbalimbali ya kimuziki katika hiyo ya Gospel usishangae maana kuna hadi Hip Hop za ki-Gospel eti!!!.

Tutajikita pia katika Modern Gospel na nguvu ya muziki huu katika soko la kibiashara, kama ilivyo kwa Biblia kuwa ni kitabu kinachouza sana na hatimaye tutaperuzi madai ya baadhi ya wadau wa muziki.

Kwamba huu ndio mtindo uliokuja kuupoka ufalme wa Bongo Fleva katika anga za muziki hapa nyumbani, ACAPPELLA. Sina shaka basi utajiandaa vyema kupokea mtiririko huu maridhawa, na natazamia kupata changamoto, maoni na mengi kutoka kwako msikilizaji wa kipindi cha muziki wa acappella na msomaji wa blog hii.


Jambo hili linawalenga hasa wadau wenyewe wa muziki huu wa acappella ambao wengi wao ni wasikilizaji wa Morning Star Radio 105.3 fmDar es salaam.