Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Novemba 28, 2011

LARVENIE MASS...MWALIMU WA UIMBAJI NA EDITOR KTK MEDIA

Harusi ni sherehe kwa ajili ya kufunga ndoa. Ndoa ni muungano wa maisha yote kati ya watu wawili unaokubaliwa na kuheshimiwa na jamii yaani mwanamke na mwanamme.

*******************************************

Mwanaume ni binadamu wa kiume. Kwa kawaida ni mtu mzima anayeitwa hivi kwani wanaume wadogo huitwa watoto wa kiume tu au wavulana.

Wanaume ni takriban nusu ya binadamu, wengine huwa wanawake. Wanaume na wanawake ni jinsia mbili ambazo zinahesabiwa kwa kawaida kati ya binadamu.


*******************************************

Mwanamke ni mwanadamu wa jinsia ya kike. Kwa kawaida anaitwa hivyo aliyefikia utu uzima au walau amebalehe. Kabla ya hapo huwa anaitwa mtoto wa kike.

*******************************************

Mitara (au Upoli au Upali) ni hali ya watu zaidi ya wawili kuishi katika uhusiano wa kindoa.

Hali hiyo ilikuwa ya kawaida barani Afrika, ambapo mwanamume mmoja aliweza kuwa na wanawake zaidi ya mmoja, lakini kwa sasa inazidi kupungua.

Ya nadra zaidi ni hali ya wanaume kadhaa kuchanga mwanamke mmoja. Baadhi ya nchi zinakubali hali hiyo, lakini nyingi zinaikataza.

Vilevile baadhi ya dini zinakubali mitara, hususan Uislamu, lakini nyingine zinaikataza, hususan Ukristo. Katika Biblia tunakuta maendeleo ya ufunuo kuhusu hali hiyo kati ya Agano la Kale na Agano Jipya.

*******************************************

Katika utamaduni wa nchi nyingi uhusiano huo yaa ni wa NDOA ni kati ya mwanamume mmoja na mwanamke mmoja tu na unalenga ustawi wao na uzazi wa watoto katika familia.

Katika nchi nyingine inakubalika ndoa kati ya watu wawili ambao mmojawao ana au anaweza kuwa na mwenzi au wenzi wengine pia (mitara), hususan ndoa ya mwanamume mmoja na wanawake zaidi ya mmoja. Kumbe kwingine hilo ni kosa la jinai.

Mara nyingi harusi inafanyika kwa ibada maalumu kadiri ya dini ya wahusika.

PAMOJA NA MAELEZO YOOTE HAPO JUU, LENGO LIILIKUWA NI HILI.

MTANGAZAJI NA MTAYARISHAJI WA VIPINDI VYA RADIO LARVEN DAVID MASIKA WA MORNING STAR RADIO 105.3 FM AMBAYE PIA NI EDITOR KATIKA TANZANIA ADVENTIST MEDIA CENTRE NA NI FOUNDER WA ACACIA SING’ERS TAREHE 27, NOVEMBER, 2011 ALIAGA UKAPERA NA KUJITWALIA MKE AITWAYE PENDO.

BLOG YA MTAYARISHAJI INAMTAKIA MAISHA MAREFU NA YA FURAHA SIKU ZOTE HADI MUNGU ATAKAPOKUJA KUTUCHUKUA, HII NI CHANGAMOTO LAKINI NINAAMINI ATAWEZA KUKABILIANA NA KILA HALI ATAKAYOKUTANA NAYO. MUNGU NI MWEMA.



Jumamosi, Novemba 26, 2011

MAJIBU YAFANYAYO KAZI

Ukweli ni lengo la akili katika kujua mambo yote kwa dhati iwezekanayo.


Unaweza kujulikana kuanzia hisi kwa kufikiria, lakini pia kwa kushika imani ya dini fulani inayosadikiwa imefunuliwa na Mungu.


Wazo hilo ni la msingi hasa katika Ukristo, na kwa namna ya pekee katika Injili ya Yohane.


Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...

(Namaanisha JumaMosi)

Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo tutatizama:

2011 General Conference Spring Council at Oakwood University (Full Sabbath Service)





MAJIBU YAFANYAYO KAZI NI KIPENGELE KINACHOONGELEA MASUALA YA KIROHO.

Jumatano, Novemba 23, 2011

TUJIKUMBUSHE UJASIRI WA DEMOKRASIA TARIME

UJASIRI WA KIDEMOKRASIA TARIME -Part 1




UJASIRI WA KIDEMOKRASIA TARIME -Part 2




UJASIRI WA KIDEMOKRASIA TARIME -Part 3





SOURCE:
http://phillipmogendi.com/documentary

Jumatatu, Novemba 21, 2011

…Bongoland YA Tanzania

Tanzania ni nchi iliyoko Afrika ya Mashariki. Imepakana na Uganda na Kenya upande wa Kaskazini, Bahari Hindi upande wa mashariki, Msumbiji, Malawi na Zambia upande wa kusini, Kongo, Burundi, Rwanda na Uganda upande wa magharibi.

Nchini Tanzania kuna lugha za kikabila zaidi ya mia moja. Hakuna lugha rasmi ya sheria. Lakini Kiswahili ni lugha ya kitaifa ya Tanzania. Kiswahili kinatumika kama lugha baina ya watu wa makabila mbalimbali na kwa mambo ya rasmi; kwa hiyo Kiswahili ni lugha rasmi ya dhati. Baada ya uhuru, Kiingereza (iliyokuwa lugha ya kikoloni kabla ya uhuru) iliendelea kutumika kwa mambo kadhaa rasmi, na kwa hiyo ilichukuliwa lugha rasmi ya dhati pamoja na Kiswahili. Lakini utumizi wa rasmi wa Kiingereza imepungua katika milongo iliyopita, na sasa utumizi huu karibu umekwisha. Kwa hiyo siku hizi ni kawaida zaidi kuchugulia Kiswahili kama lugha rasmi ya dhati ya pekee.

Tanzania ni nchi mwanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki.

Mji mkuu: Dodoma, Makao makuu ya serikali: Dar es Salaam, miji mikubwa mingine: Mbeya, Arusha

Historia

Zanzibar na Afrika ya Mashariki ya Kijerumani)

Jina "Tanzania" limeundwa kutokana na majina ya TANganyika na ZANzibar (pamoja na athira ya jina la kale la "Azania").

Nchi hizo mbili zilikuwa zote chini ya utawala wa Uingereza hadi kupata uhuru lakini hazikuwa makoloni ya kawaida. Zanzibar ilikuwa na hali ya nchi lindwa kutokana na mikataba kati ya masultani wa Zanzibar na Ufalme wa Uingereza. Tanganyika iliwahi kuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kijerumani hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia halafu ikawa chini ya Uingereza kama eneo la kudhaminiwa kutokana na azimio la Shirikisho la Mataifa iliyoweka Tanganyika katika ngazi "B" ya maeneo ya kudhaminiwa.

Tanganyika na Zanzibar zilikuwa nchi mbili tofauti hadi 1964, zilipoungana na kuwa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Kiongozi wa Tanganyika Mwalimu Julius Nyerere alikuwa Rais wa kwanza na kiongozi wa mapinduzi ya Zanzibar Abedi Amani Karume akawa Makamu wa Kwanza.

Tanzania, chini ya Rais wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi iliruhusu mfumo wa vyama vingi vya siasa Tanzania na kuanza mpango wa kurekebisha uchumi kuendana na masharti ya Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani.

Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa aliendeleza mfumo wa uchumi wa soko huria ambapo mashirika ya umma yanabinafsishwa.

Tarehe 21 Desemba 2005 Kikwete, Jakaya Kikwete ameapishwa kuwa Rais wa nne wa taifa.

Tanzania ni moja kati ya nchi maskini duniani ambazo zimefanikiwa kufutiwa madeni katika mpango wa kusamehe madeni wa Kundi la Nchi Nane.


Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar:

Tangu muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 Tanzania imefuata miundo ifuatayo:

  • Nchi inatawaliwa na serikali ya muungano ikitekeleza sheria zinazotolewa na bunge la Tanzania.
  • Tanganyika au Tanzania bara haina serikali au bunge la pekee
  • Zanzibar (Unguja na Pemba) ina serikali na bunge lake zinazoratibu mambo yasiyo ya muungano.

Mambo yafuatayo yalikubalika kuwa shughuli za muungano:

  • Mambo ya nje
  • Jeshi
  • Polisi
  • Mamlaka ya dharura
  • Uraia
  • Uhamiaji
  • Biashara ya nje
  • Utumishi wa umma
  • Kodi ya mapato, orodha
  • Bandari, Usafiri wa anga, Posta na Simu

Demografia

Watu wa Tanzania hawaenei sawasawa. Katika maeneo makavu sana, kunaishi mtu mmoja tu kwenye kilomita moja ya mraba (1/km²) lakini sehemu zenye rutuba za bara, kuna watu 51 kwa kila kilomita ya mraba. Hatimaye huku Unguja kuna watu 134 kwa kilomita ya mraba. Zaidi ya asilimia themanini huishi vijijini. Dar es Salaam ni mji mkubwa kabisa wenye watu karibu milioni tatu.

Kuna makabila zaidi ya 120. Makabila yenye watu zaidi ya milioni moja ni Wasukuma, Wanyamwezi, Wachaga, Waha, Wagogo, Wahaya na Wamakonde.

Idadi kubwa sana ya Watanzania ni Wabantu. Nje ya hao, kuna Waniloti, kwa mfano Wamasai na Wajaluo ambao wengi wao zaidi wanaishi Kenya. Kundi lingine ni makabila ya Wakushi wanaoishi kaskazini mwa Tanzania; hao ni makabila ya Wairaqw, Wafiome na Wasi. Kuna vikundi viwili vya Wakhoisan wanaofanana na makabila ya Botswana na Namibia; majina yao ni Wasandawe na Waburunge. Hatimaye kuna Wahadzabe wachache ambao utafiti wa DNA umeonyesha hivi karibuni wana uhusiano wa asili na Watwa wa nchi za Afrika ya Kati.

Ingawa kila kabila lina lugha yake, lugha ya taifa ya Tanzania ni Kiswahili ambacho ni mojawapo kati ya lugha za Kibantu. Hali hii imesaidia sana kukubaliwa kwa Kiswahili nchini kwa sababu idadi kubwa ya Watanzania ni wasemaji wa lugha za Kibantu.


Dini

Nchi haina dini rasmi na katiba ya Tanzania inatangaza uhuru wa dini kwa wote. Mara nyingi idadi ya wafuasi wa dini hutajwa kuwa theluthi moja Waislamu, theluthi moja Wakristo na theluthi moja wafuasi wa dini za jadi. Lakini tangu uhuru swali la dini ya wananchi halijaulizwa tena katika sensa, kwa hiyo kadirio la theluthi-theluthi halina msingi halisi bali ni zaidi azimio la kisiasa.

Waislamu hudai mara nyingi ya kwamba wenyewe ni sehemu kubwa ya Watanzania, angalau zaidi ya nusu. Kamusi ya "World Christian Encyclopedia" (2002) yataja Wakristo kuwa 52%, Waislamu kuwa 32% na wafuasi wa dini za jadi kuwa 14%.

Kwenye visiwa vya Zanzibar idadi ya Waislamu huaminiwa kuwa takriban 95%.

Usafiri

Usafiri nchini Tanzania ni hasa kwa njia ya barabara. Mengine ni reli na ndege. Kwenye maziwa makubwa na pwani la Bahari Hindi kuna pia usafiri kwa meli.

Hadi sasa idadi ya barabara za lami si kubwa. Kuna hasa njia nzuri kati ya Dar es Salaam, Mbeya katika kusini-madharibi, Dodoma katika kitovu cha nchi, Arusha / Tanga katika kaskazini-mashariki. Kusini-Mashariki na Magharibi ya nchi kwa jumla haina barabara nzuri na mawasiliano ni magumu.

Shirika mbili za reli zahudumia Tanzania ni TRC (Shirika ya Reli Tanzania - Tanzania Railways Corporation) na TAZARA (Tanzania-Zambia Railways Corporation). TRC imetawala reli ya kati kuanzia Dar es Salaam hadi Kigoma halafu reli ya Tanga kati ya Tanga na Arusha. Tazara imeunganisha Dar es Salaam na kusini ya nchi hadi Zambia. Zote hazikutunzwa vizuri na usafiri unakumbwa na huduma mbaya pamoja na ajali.

Huduma kwa ndege zatumia hasa nyanja za ndege 11 penye barabara ya lami kwa ajili ya ndege hasa Julius Nyerere/Dar es Salaam, Kilimanjaro /Arusha-Moshi na Zanzibar-Kisauni.

Utamaduni

Sanaa

Kati ya wasanii wa Tanzania ni hasa wajume wa ubao na wachoraji waliojulikana kimataifa.

Mabombwe ya Kimakonde yamesifiwa tangu mwanzo wa karne ya 20. Wamakonde wengi wamehamia Daressalaam au Arusha wanapohudumia soko la watalii pia soko la nje.

Tangu miaka ya 1970 uchoraji wa "tingatinga" umejulikana uliopata jina kutoka kwa Edward Tingatinga naye mtu wa Umakonde.

Urithi wa Dunia

Mahali pafuatapo katika Tanzania pamepokelewa katika orodha ya UNESCO ya "Urithi wa Dunia".

(mwaka wa kukubaliwa - jina la mahali)

NIWIE RADHI, SABABU YA MAJUKUMU NDIO MAANA NIMEKUWA SIWEKI PACHIKO LA MARA KWA MARA. TATIZO HILO NIMELIMALIZA NA SASA KILA SIKU NITAKUWA NAKUWEKEA KITU KIPYA.

Jumatatu, Novemba 14, 2011

Kuimba...NA kwa tafakari!.

Kuimaba ni kitu cha muhimu sana katika kumtolea Mungu sifa. Kuimba nyimbo huzifanya za tafakari. Kwa kutumia maneno machache nyimbo hizi huonyesha msingi wa kweli wa imani, ambao haraka haraka huingia na kukaa akilini. Jinsi ambavyo maneno yanaimbwa kwa mara nyingi, ukweli huu hupenya taratibu ndani ya ubinadamu wetu mzima. Kwa hiyo kuimba kwa kutafakari kunakuwa njia yetu ya kumsikiliza Mungu. Kunamruhusu kila mmoja wetu kushiriki kwa pamoja wakati wa sala na kubaki pamoja katika utulivu tukimsubiri Mungu, bila kuhitaji kujiwekea muda maalumu kwa uhakika sana.

Kufungua njia za kumuamini Mungu, hakuna kinachoweza kukaa badala ya sauti nzuri za binadamu zilizounganishwa pamoja katika nyimbo. Uzuri huu unaweza kutuonjesha chembe za “furaha za mbinguni tukiwa duniani”, kama Wakristo wa Mashariki wanavyoiweka. Na maisha ya ndani yanaanza kuchanua na kung’ara ndani mwetu.

Pia nyimbo hizi husaidia muendelezo wa sala za binafsi. Kwa kupitia nyimbo hizi, kidogokidogo, ubinadabu wetu hupata umoja ndani yetu na Mungu. Zinaweza kuendelea katika ukimya wa mioyo yetu wakati tukiwa kazini, tunapoongea na wengine, au tukiwa tumepumzika. Kwa namna hii sala na maisha ya kila siku ni kitu kimoja. Zinatuwezesha kuendelea kusali katika ukimya wa mioyo yetu, hata tukiwa hatutambui.


“Nyimbo” zinachapishwa katika lugha tofauti tofauti na rahisi, hata hivyo maandalizi yanahitajika ili kuzitumia. Maandalizi haya ni vizuri yakifanyika kabla ya sala yenyewe, ili sala yenyewe ikianza hali ibaki kuwa tulivu na ya kuruhusu tafakari.

Wakati wa sala ni vizuri kwa namna hii kila mtu anaweza kulazimu mtu mmoja kuongoza, Pia, kwa umakini mkubwa sana, kikundi kidogo cha vifaa vya muziki au waimbaji wanao saidia kutia nguvu wengine, wanaweza kuimba, isipokua daima wakumbuke kuwa hawafanyi maonyesho kwa wengine).

Kwani nyimbo zikianzishwa tu hivihivi, sauti itakua ya chini sana. ‘A turning fork or pitch pipe’ vinaweza kusaidia, au vyombo vya muziki kutoa nota ya kwanza au kusindikiza sauti. Na kuhakikisha kasi ya wimbo haiwi ndogo sana, kama inavyotokea wimbo ukiimbwa kwa muda mrefu. Kadiri idadi ya washiriki wa sala inavyoongezeka, kunakua na umuhimu wa kutumia kipaza sauti, na ingefaa zaidi kilongalonga cha kushika kwa mkono, kwa ajili ya kuanzishia na kumalizia wimbo (Wimbo unaweza kumalizwa kwa kuimba “amina” katika nota ya mwisho). Mtu anaye anzisha wimbo anaweza kuwasaidia wengine kwa kuimba kwenye kipaza sauti, lakini kwa uangalifu ili asimeze sauti za wengine. Mfumo mzuri wa sauti ni muhimu kama mkusanyiko ni mkubwa; kama ni muhimu kuukagua, ukaguliwe kabla na fanya majaribio na wale watakao tumia


Nyimbo zilizoko katika lugha mbalimbali ni mwafaka kwa mkusanyiko unaohusisha mataifa mbalimbali toka dunia nzima. Kwa sala zinazo husisha watu wa rika zote kutoka maeneo ya jirani, ni vizuri nyimbo nyingi ziwe katika lugha inayoeleweka na baadhi ya washiriki. Kama inawezekana kila mtu apewe karatasi au kitabu cha nyimbo. Inawezekana pia kuweka nyimbo moja au mbili zinazojulikana vizuri kwa eneo hilo.

Vyombo vya muziki: Gita au kinanda chaweza kusaidia mpangilio mzuri wa nyimbo. Ni vya msaada mkubwa sana katika kuhakikisha sauti si ya juu/chini sana na kasi ya wimbo ni ya kawaida. Gita lipigwe katika mtindo wa ‘classical’ na siyo katika mtindo wa ‘folk style’. Kipaza sauti kinaweza kuwa cha muhimu ili vyombo visikike. Kama nyongeza ya hivi ambayo ni vya msingi, kuna vifaa vingine vya kusaidia katika vyombo vya muziki

Jumamosi, Novemba 12, 2011

Tatizo la KUFIKIRIA kabla ya KUFANYA kitu!






Tuanze kwanza kwa kusikiliza na kutazama nyimbo hizi, kikubwa hapa ni kutafakari ujumbe uliomo ndani ya nyimbo hizi maana tukisema tuanze kuzichambua bado tutakuta ndani kuna vionjo vya Rock and Roll.



 ....na kama hakutakuwa na haja zaidi basi hii itasaidia jambo.



 Ndio kweli yenyewe kwamba:







...naam sasa tuendele.

Ukifikiria hata DHAMBI ,...
....halafu  ukafanya DHAMBI,...
.... labda  LADHA ya dhambi  huongezeka CHACHU!:-(

Swali:
  • Huwa unafikiria kabla ya KUFANYA kitu?
  • Na hufikiri  UKIFANYA bila KUFIKIRIA na UKIFIKIRIA na KUFANYA  kitu kilekile UGALI labda   chaweza kuwa na LADHA mbili tofauti?

Jifunze KUFIKIRIA kwanza ,....
..... na UKISHA kuwa MASTA wa KUFIKIRIA  kabla ya KUFANYA,...
...FIKIRIA halafu FANYA sasa ,...
.... kuna wadaio ndio  WAFANYAO kwa BUSARA wafanyavyo.

Swali:
  • Lakini kwa KUFIKIRIA si yasemekana ndio maana mengi  ya busara kama yangefanyika bila KUFIKIRIA ndio maana WENYE BUSARA hawayafanyi  na kusababisha tatizo liko palepale  kwa kuwa hakuna AFANYAYE TATUZI kwa kuwa wenye TATUZI kitakiwacho kufanyika KIKIFIKIRIWA kwanza HAKIFANYIKIKI?

Ndio,...
.... labda moja ya tatizo la KUFIKIRIA kabla ya KUFANYA kitu,...
..... sio tu kuwa MUDA wa KUFANYA   hautatosha  kwa kuwa muda utatumika pia na KUFIKIRIA kabla ya KUFANYA.:-(

Habari hii ila sio nyimbo za pale juu nimeipata ktk link hapo chini.

http://simon-kitururu.blogspot.com/2011/11/tatizo-la-kufikiria-kabla-ya-kufanya.html

Jumatatu, Novemba 07, 2011

Tabibu na mtaalamu wa saikolojia kutoka nchini Austria aliyeanzisha mtindo wa uchunguzi nafsia...(psychoanalysis).



Sigmund Freud umaarufu wake unatokana na nadharia yake ya uchunguzi nafsia alimochunguza hasa sehemu ya nafsi iliyofichika yaani sehemu zisiziofahamika au zisizofikiwa na akili. Ilikuwa imani yake ya kwamba matatizo ya kiroho na ya kiakili yana msingi katika mvurugo wa kumbukumbu kwenye sehemu hizi ya nafsi zisizoeleweka na mtu mwenyewe. Alibuni njia za kufunua kumbukumbu hizi rohoni kwa majadiliano marefu na kuchungulia ndoto za mtu.

Alizaliwa katika jimbo la Moravia (leo: Ucheki) la Milki ya Austria-Hungaria katika familia ya Wajerumani wa Kiyahudi akapewa jina Sigismund Schlomo Freud na alibadilisha jina hili kuwa Sigmund Freud alipofikia umri wa miaka 21. Familia ilihamia baadaye mjini Vienna alipomaliza shule na kusoma tiba kwenye chuo kikuu na mwaka 1881 alipata digrii ya daktari wa tiba.

Kazi yake ya kwanza ilikuwa katika hospitali kuu ya Vienna alipoendelea kufanya utafiti wa bongo za wagonjwa. Akachungulia pia athira ya dawa ya kulevya kokain kwa roho ya binadamu.
1885 alifanya safari ya masomo kwenda Paris (Ufaransa) alipokaa kwenye hospitali ya magonjwa ya akili alipoangalia hasa matibabu ya hali ya umanyetu (mpagao). Mwaka uleule alimalita tasnifu yake ya profesa akapewa nafasi ya kundisha kozi za magonjwa ya neva na akkili kwenye chuo kikuu cha Vienna.
1886 alifungua kliniki yake ya binafsi akawa pia daktari kiongozi wa idara ya magonjwa wa neva na akili kwenye hospitali ya watoto ya Vienna. 

Mwaka uleule alimwoa Martha Bernays (1861-1951) aliyekuwa binti wa familia ya wataalamu Wayahudi Wajerumani kutoka Hamburg. Aliendelea kuzaa naye watoto sita.
Tangu 1889 alianza kutambua kuwepo kwa nafsi iliyofichika ndani ya roho ya mwanadamu kuwa sababu na chanzo ya mahonjwa mengi ya akili. Aliendelea kutibu na kuandika mjini Vienna hadi mwaka 1938.
Baada ya Ujerumani ya Hitler kuvamia Austria siasa ya Chama cha Nazi ilitisha Wayahudi wote na Freud aliweza kuhamia Uingereza pamoja na familia yake. Lakini dada zake walibaki Austria waliuawa katika makambi ya mauti.

Freud mwenyewe alizaliwa 6 Mei 1856 alikuwa mgonjwa tayari akiwa na kansa iliyoendelea tayari. Mwaka 1939 alimwomba rafiki na daktari yake apewe kiasi kikubwa cha morfini akaaga dunia 21 Septemba 1939.

Hebu jionee mwenyewe The Question of God: 

C.S. Lewis and Sigmund Freud hapa chini.


Jumapili, Novemba 06, 2011

Je unafahamu kuwa Scientology ni dini mpya iliyoanzishwa na L. Ron Hubbard ili kueneza mitazamo na mbinu za Dianetics aliyoibuni mwaka 1950.






Lakini inakubaliwa hadhi ya "dini" katika nchi ya Marekani, Australia na nyingine chache, kwa sababu toka mwanzo imehusishwa na makosa mbalimbali ya jinai, hususan ujasusi, utapeli na kuathiri hali ya nafsi ya wafuasi wake.
Kadiri ya hesabu yake, hao mwaka 2005 walikuwa milioni 8, lakini watu wa nje wanakadiria kuwa ni nusu milioni tu.

Makao makuu ya Scientology yako Marekani, katika kijiji cha Clearwater.
Baada ya Hubbard kufariki mwaka 1986, kiongozi mpya ni David Miscavige.
Jina linatokana na neno la Kilatini "scio" (yaani "najua" kwa maana pana), na neno la Kigiriki "logos" (yaani "somo").Historia ya Scientology inaendana kabisa na maisha ya mwanzilishi wake ambaye tangu miaka ya 1930 aliandika vitabu vya ubunifu mkubwa, mpaka alipojingiza katika masuala ya saikolojia akipinga kabisa misingi na maelekeo ya sayansi hiyo.

Kisha kupata umaarufu wa muda mfupi, akaelekea upande wa roho, aliyoiona haitegemei mwili wala akili, ila inavitumia ili kutenda ulimwenguni.
Kuanzia miaka ya 1960 alifukuzwa na nchi mbalimbali na kuhukumiwa na mahakama tofautitofauti.
Scientology imeitwa "dini ghali" kuliko zote duniani. Kila huduma inatolewa kwa bei iliyopangwa na uongozi wa juu.
Ili kufikia hali ya "Clear", mtu anahitaji kugharimu euro 25.000, na ili kufikia hali bora ya "OT VIII", zinahitajika euro 250,000 hivi.

Kuna kitu unafahamu zaidi?

Jumanne, Novemba 01, 2011

Mkoa na Mlima Kilimanjaro...kwa pamoja.



Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 26 za Tanzania. Makao makuu ya mkoa huu ni Moshi. Mlima wa Kilimanjaro, mlima mkubwa kupita yote barani Afrika umo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Jina la mlima huu ndio limeupatia mkoa huu jina lake.

Mkoa wa Kilimanjaro umepakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa Kusini na mikoa ya Manyara na Arusha upande wa magharibi.

Kilimajaro kuna wakazi wapatao 1,381,149 (sensa ya mwaka 2002). Kabila kubwa ndio Wachagga. Makabila mengine mkoani humo ni Wapare na Wamasai

Wilaya

Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 7 ambazo ni: Rombo, Hai, Siha, Moshi Vijijini, Moshi Mjini, Mwanga na Same.


Kilimanjaro ni mlima mrefu kuliko yote Afrika, pia ni wa pili kwa urefu Duniani. Mlima huu uko nchini Tanzania katika Mkoa wa Kilimanjaro. Una urefu wa futi 19,340 (mita 5,895). Hali halisi Kilimanjaro ni zaidi kuliko mlima tu ni kama safu ndogo ya milima mitatu: Kibo, Mawenzi na Shira. Hii mitatu inaonekana kama vilele vitatu vya mlima mmoja hivyo si vibaya kusema Kilimanjaro ni mlima.

Kilimanjaro ni volkeno iliyolala kwa sasa. Kwenye kilele cha Kibo gesi bado inatoka. Kumbukumbu ya wenyeji ina habari ya mlipuko takriban mnamo mwaka 1730.

Kilele cha juu cha Kibo kinaitwa Uhuru Peak. Mtu wa kwanza wa kufika kileleni hapo alikuwa Johannes Kinyala Lauwo kutoka Marangu aliyewaongoza Wajerumani Hans Meyer na Ludwig Purtscheller tarehe 6 Oktoba, 1889 wakati wa ukoloni wa Ujerumani. Wakati ule waliita ncha ya juu  kwa heshima ya Kaisari wa Ujerumani.

Kibo ina theluji na barafuto kadhaa ndogo.