Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumapili, Novemba 21, 2010

MPANGO WA MUZIKI WA ACAPPELLA TANZANIA

NI BAADHI YA VIKUNDI NA CHOIR ZINAZOJIHUSISHA NA MUZIKI WA ACAPELLA, MSIKILIZAJI ENDELEA KUNIJULISHA IKIWA UNAFAHAMU KUNDI AMA CHOIR POPOTE DUNIANI HASA WANAOJIHUSISHA NA AINA HII YA MUZIKI, ACAPPELLA.
  1. WATEULE - KIBAMBA SDA DSM TANZANIA
  2. VOICE OF SANCTIFICATION - BUGURUNI SDA DSM TANZANIA
  3. GRACIOS VOICE - KANANI SDA TANZANIA
  4. AGAPE CHOIR. AKERI LUTHERAN PARISH TANZANIA
  5. THE HOPE SCORES - MACHIMBO S.D.A DSM TANZANIA
  6. MABALOZIWA YESU - BOKO SDA DSM TANZANIA
  7. GLORYSHINE - MONGOLANDEGE SDA DSM TANZANIA
  8. SOUL INFLUENCE - SOUTH AFRICA
  9. PASUWA - MOSHI TANZANIA
  10. NO LIMITS - SOUTH AFRICA
  11. KINGS HERALD - USA
  12. SDA SOUTH AFRICA CORAL
  13. LADY SMITH BLACK MAMBAZO - SOUTH AFRICA
  14. ACAPPELLA COMPANY - USA
  15. FINAL TRUMPET - DSM TANZANIA
MCHAKATO UKO HIVI:
KATIKA SIMU YAKO YA KIGANJANI SEHEMU YA UJUMBE MFUPI ANDIKA NENO MATUMAINI ACHA NAFASI ANDIKA NENO AC ACHA NAFASI ANDIKA JINA LA KIKUNDI AMA CHOIR NA MAHALI WANAPOPATIKANA ANDIKA PIA MAWASILIANO YAO KAMA UNAYO KISHA TUMA KUWENDA NAMBA 15551. ZOEZI HILI NI KWA WALE WAOOOTE WALIOPO TANZANIA.

Nitaendelea Kukupatia Majina ya Vikundi na Mahali Yanapopatikana.

Jumamosi, Novemba 13, 2010



Dj Cartoon/CartoonHome:
Dj, Producer, Entrepreneur,Radio Presenter.

SIKIAA!!!!
DJ Cartoon started Djing 10 years ago, but his love for music could be seen by the time he was 12 years old. He remembers his first equipment as two tape decks and a old mixer he got from a friend and within weeks of self training became the neighborhood house party DJ.

His quest to be a seasoned DJ was only bogged by the lack of equipment. However, through a link of friends he was introduced to a mobile DJ owner and from there on things started picking up.

He clearly remembers his first turntable feel just like it was yesterday and marveled at himself being on the opposite side of the turntables, many Djs knowing what to play to keep the crowd on their feet, transitions to getting to know what a hit is which gradually made Cartoon start producing "Isikie Beats".

He set up his own production company, Ritungu Inc,Friends Entertainment and Digital Media Creation four years ago and hasn't looked back since. In less than 3 years Cartoon has emerged from a DJ into one of the most versatile producers in the game."I see a lot of people making a big deal out of what producer uses what.

What matters is the end result. If the beats is banging, it doesn't matter what equipment was used". You might have recorded you're vocals in the bathroom, but if it's a hit and the quality compares to everybody else, why knock the recording.

His ability to produce gospel music and work with artists from all over the world of music makes Cartoon versatile in producing for some of the hottest up and coming acts who seek out his talent.

Cartoon also continues to raise the par in the Mixtape game, by creating mixtapes featuring artists from all over the world, thus making his mixtapes internationally sought.


THANK YOU *GOD*.

THANK YOU "TANZANIA".

Alhamisi, Novemba 11, 2010

MEZA YA MAOMBI KILA J5 NA J'PILI

HAYA NI MAHITAJI YA KUOMBEA YALIYOTUFIKIA KATIKA KIPINDI CHA
ANZA NA BWANA AMBACHO KILIRUSHWA 105.3 FM
SIKU YA Jumatano 10th, November, 2010
KATIKA WASAA WA MEZA YA MAOMBI.
JAMBO HILI HUFANYIKA KILA JUMAPILI NA JUMATANO
KUANZIA SAA
11:00 ALFAJIRI - 12:00 ASUBUHI.

1. Bwana Apewe Sifa Ndugu Yusufu.Nasema Ahsante kwa Maombi yenu.Naomba Mniombee maana leo naenda kufanya Interview saa mbili ili niweze kufaulu na kupata kazi.Ahsante na Mbarikiwe sana!.

2. Bwana apewe sifa!,Naomba mniombee Mungu aniponye kwani huu ni mwezi wa pili naumwa- nipo Banana!.

3. BWANA APEWE SIFA. NAOMBA MUNGU KWA KUTUAMSHA SALAMA SIKU YA LEO PIA ATUBARIKI SIKU ZOTE ZA MAISHA YETU NA WENYE SHIDA WENYE HUZUNI MUNGU AWAPE NGUVU

4. Bwana asifiwe ,naomba mniombe kazi za mikono yangu ziwe za mafanikio.

5. Bwana asifiwe naomba mniombee mapenzi yatimie katika ndoa yetu itakayofungwa mwenzi wa kumi na mbili naomba tuliweke miguuni pa yesu

6. Bwana asifiwe sana,naamini Bwana akipenda kaka yangu Abeid mifupa yake itaimarishwa na hatahitaji kufanyiwa operation, yuko MOI.Mbarikiwe hapo studio kwa somo zuri, nipo Ilala.

7. Bwana asifiwe, naenda kufanya enterview naomba mniombee Yesu aniongoze na niipate hii kazi kama ni mpango wa Bwana.

8. BWANA ASIFIWE. NAOMBA MUNGU ANIBARI KTK KAZI YANGU ANIEPUSHE NA MAPITO MAGUMU NIWEZESHE KTK MAISHA YANGU. NIKO CHAMAZI KWA MKONGO .

9. Bwana asifiwe.mm ni mama mjane naomba mniombe na familia yangu watoto wangu waxe vichwa na si mikia katka masomo yao. NIPO TABATA.¬

10. Bwana Yesu apewe sifa..!naomba mniombee macho yananisumbua sana,asante mbarkiwe, nipo ubungo.


11. Bwana Yesu asifiwe,naomba mumuombee dada yangu aache madawa ya kulevya na kaka yangt aache pombe.pia namshukuru Mungu kwa kuwa amenitendea miujiza na naomba mniombee kampuni ninayofungua ikamilike na pia biashara ninayoanza leo iwe ni mbaraka katika maisha yangu.Mungu awabariki hapo studio.

12. BWANA YESU ASIFIWE. NAOMBA MAOMBI KWAAJILI YA MUMEWANGU ANASUMBULIWA NA MOYO UMETANUKA. NIPO BANANA.

13. Elieza Asraji: kulinga na lmaniyangu ya usabato napitia changamoto nyingi.mniombee MUNGU anipe imani imara. Muombeeni babangu arudisheupendo,kwangu mimi mwanawe,ingawaje nimezaliwanjeyandoa,pia yeye mwisram,mimi msabato na usabato wangu wanidharau kweli. Tuombee koo hizi,ukoowa Asraji,sala,joji,mpole,mama Asha Sef,j.Bada.koohizi zimepungukiwa ROHO MTAKATIFU.mungu aingiliekati kiroho na kimwili.

14. Habar y asubuhi hapo studio mungu awa bariki cn na mahur mazur naomba mumuombe bi b naumwa kichwa na mm pia uniombe niwe na afya nzur il niweze kufanya vizur shulen.

15. Habari za asubuhi studio.nahitaji mniombee nipate school fees kwa ajili ya chuo.pia muiombee familia yangu.

16. Halo Mr. Yusufu hapo Morning star mna nyimbo nzuri ambazo hazipatikani kwenye maduka ya nyimbo. Je hapo morning star mnauza CD/kanda za nyimbo? Nipo magomen

17. M/STAR MBARIKIWE.BABA YANGU ANAOMBA AOMBEWE MAOMBIYA TOBA REUBEN NEHEMIA NA MJUKUU WAKE WA JINA LAKE AACHE POMBE .

18. mbariki we naomba mniombe mimi fundi ujenzi nipateka kazi

19. Mbarikiwe hapo studio,ninawaomba mniombee kwa ajili ya kampuni zangu ambazo zipo kwenye interview,natanguliza shukrani zangu kwa Bwana.


20. MBARIKIWE WATUMISHI NAOMBA MAOMBI KWA AJILI YA BIASHARA NIPATE KUUZA NI WAWA MNDEWA

21. Mbarikiwe watumishi wa Mungu mniombee haya yafuatayo mama yangu apone apate kumbukumbu ya ufahamu na mwanangu aendelee kutulia arudie tabia yake ya utulivu

22. Mimi ni mshiriki mwadventista nina umri wa miaka 10 kanisani nina miaka 33 sina mume na nimemuomba mungu miaka 10 yote na mungu amenyamaza na ninamwomba sana mungu aniepushe na jarabu la uzinzi lakini imefika sehemu nimeanguka ktk jaribu la uzinzi na moyo wangu umekosa amani kwa mungu wangu nisaidieni ijapo niko ije ya maada nielewesheni na muniombee niishinde hiyo dhambi amen

23. mimi.ninamkewangu.wandoa.lakini.tunaishi.kama.mtunadadayake.tumezawatoto.wawili.mkubwayuko.kidatochasita.tunaishizaidi.yamiaka.mitatu.hatushirikitendo.landoa.anadai.yeye.ajisikimnisaidie.nikiowa.nitafanya.makosa.

24. Mungu aguse roho za washiriki wa kinondoni wahudhurie effort inayoanza leo biafra na ampatie afya na ujumbe mzito mch tuvako anaeendesha hii.

25. Mungu awabariki.mniombee shetani analeta roho ya hasira kwenye ndoa yetu

26. Mungu naomba unisaidie nipate kazi Crdb..naomba unisaidie kama mchumba huyu ndiye mapenz yako yatimizwe nikifanye maamuz haraka na yasiyo na maumiv kwa yeyote..pia mniombee baba yangu aache pombe kwan amepitiliza na kama familia tunaumizwa sana..AMEN.

27. naitwa Leah, naomba mniombee niishi kwa amani na watu wote,pia naomba Mungu nipate kazi ambayo nimeshafanya interview. Amina

28. NAITWA UPENDO NINANDOA YA MIAKA KUMI NA TATU. NAOMBA MNIOMBEE NIPATE WATOTO NDILO HITAJI LANGU KUBWA KWA SASA.

29. NAMSHUKURU MUNGU KWAMAOMBI YENU YAJUMAPILI NIMEANZA KUPATA AMANI.NIOMBEENI SINA KAZI.MUNGU ANIBARIKI NIPATE KAZI.NIMEMALIZA CHUO MWAKAJANA.PIA NIWE NA AMANI.


30. NAOMBA MAOMBI KWA AJILI YA WATOTO WANGU CHED NA PAULO WAMETUMA MAOMBI YA KAZI HAWAJAPATA

31. Naomba maombi yenu ninasumbuliwa kifua.

32. Naomba mmuombee Ben anafanya mitihani ya taifa leo. Mungu afungue fahamu zake.amina


33. Naomba mniombee mdogo wangu amepata chuo lakin ada haijatosha. Mbarikiwe sana.

34. NAOMBA MNIOMBEE MTOTO WANGU MNDEWA AACHE POMBE ARUD4 KWA MUNGU AENDE KANISANI NI MAMA MNDEWA

35. Naomba mniombee nimechukuliwa nguo ya ndani ikiwa imechafuka na hedhi –

36. Naomba muniombee mungu anijengee nyumba ya kuishi'

37. Naomba mwombee rafiki yangu Lugwisha Ngofilo ili aache pombe,na Mungu amsaidie kuijua kweli na aifuate hiyo kweli.

38. Naomba nione ndoa yangu.ni moses mzakwe wa kimara.

39. Naomba tumwombee yatima huyu aache pombe amekuwa mlevi kupindukia. na mungu amwepushe na marafiki wabaya

40. NAOMBAUMUOMBEE BABA DOMINIKI AMEPARALAIZI AMELAZWA MUHIMBILI AMINA

41. Nataka kuja hapo ofisin kwa maombi na ushauri nijlishe utaratibu tafadhali.

42. Nilimsubili kwa mda wamiaka minne amalize masomo na bado hajamaliza mwaka kesho anamaliza. Leo ananiambia haki kuniowa. Mchungaji naomba uniombe. Kilasiku wazi Wananisema kwa nini hauolewi ? Mimi nawajibu ninamchu yuko chuo .ANAITWA CHALESS. LEO HANITAKI. MIMI NAITWA AGRIPINA NAOMBA UNIOMBEE ILI TUOANE.

43. Nimefungua ofisi ya fenicha .Naomba muiombee . Bwana ailinde. Na aibaliki.

44. Niombeeni jaman, nilikuwa na mchumba. Matokeo yake akanipa mimba na kuniacha sasa nimejifungua namlea mtoto peke yangu! Kwakweli napata maumivu makali kiasi ambacho

45. naweza yanaweza kuniua ghafla na kumuacha mtoto wangu! Niombeeni maumivu haya yaishe pia mungu anibariki ili niweze kumlea mtoto wangu.

46. Niombeeni naumwa ninatumia dawa bila mafanikio


47. NIOMBEENI NIPATE KUOLEWA, NIOMBEENI NIPONE MBA.

48. Tuendelee kuombea nchi yetu iwe na amani. Rais apate safu ya viongozi wazuri. Phillip

49. watu wamungu mniombee kifua kinauma na kuna kunakitu kimekwama kooni

Ikiwa una maoni, ushauri ama hitaji la kiroho usisite kutujulisha.
Sema nasi kwa namba ifuatayo: +255 22 278 0 680.

CHANGAMOTO


Jumanne, Novemba 09, 2010

KINONDONI SDA CHURCH

MKUTANO MKUTANO MKUTANO.
NI MKUTANO MKUBWA WA INJILI KARIBIA KUANZA, NI KATIKA VIWANJA VYA BIAFRA VILIVYOPO KINONDONI DAR ES SALAAM KARIBU NA CHUO KIKUU HURIA (OPEN UNIVERSITY)KILA SIKU KUANZIA SAA 10 JIONI HADI SAA 12 JIONI, USIPANGE KUKOSA JAMBO MUHIMU KWA MAISHA YAKO YA KIROHO. ILIKUWA UANZE TAREHE 7 NOVEMBER 2010 KUTOKANA NA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO UTAANZA RASMI JUMATANO YA TAREHE 10, NOVEMBER, 2010.
DO NOT MISS BANA.

Jumapili, Novemba 07, 2010

Information about Turnround Music Academy

Hi, below is a write up on our music school to help you prepare for the radio programme tomorrow,please check the brochure and see if there is anything you can add .

We have about 20 students from all backgrounds, church , secular, religious, working class, students etc. We teach all kinds of instruments guitar, keyboard, trumpet, music theory, sight playing voice training etc we have most of these instruments but we also teach those we don't have and ask our students to bring them along and we teach them.

The turnup of students is very encouraging with about 70 students who have expressed an interest to learn and join and of these about 20 have enrolled. The staff of Turn round have formed a music group and we have gone to several institutions to perform live and explain what we do and demonstrate at our music school, some of the schools we have gone to are: 1/Laureate Internatinal School. 2/ Dar-es -salaam International School.

Many schools are going to form partnerships with us with a view of us teaching at their schools or them bringing students to our school. We intend to expand and move to other campuses as demand grows, also we intend to form live bands to perform both gospel amd secular music which will be performing in many diverse occasions.

We also intend to build recording studios and record all upcoming musicians and performing artists. We train musicians to do international exams like those of the Associated Board of Royal Schools of Music.of London.We are training musicians to prepare for the famous Tusker project Fame and Bongo Flavour Star search.

Turn Round Music Academy ni chuo kipya kinachowaletea mafunzo mbali mbali ya kozi za upigaji wa kinanda, (keyboard piano) gitaa, zeze, tarumbeta, upulizaji wa saksafoni (midomo ya bata), upulizaji wa filimbi (recorder au flute) pia inatoa elimu ya muziki kwa nadharia, mazoezi ya sauti (uimbaji) Vocals upigaji ngoma tumba na drumset chuo kipo mikocheni B barabara ya old bagamoyo mtaa wa huruma kabla ya kituo cha njia panda coka.

kwa mawasiliano zaidi piga namba:
+255-758-000-881 au +255-762-865-343.
Noah E.O.W.Omolo
Director and teacher of Music.
(noaheowomolo@yahoo.com)

Wote mnakaribishwa.

Please feel free to call me about the school on any issue of music.
Thank you.

PAMOJA TWAWEZA

JOSEPH/YUSUPH

Jinsia: Mwanamme

Linakotumika: Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, kwa watumiaji wa Biblia.

Linavyotamkwa:
1. JO-SEF (Uingereza).
2. ZHO-ZEF (Kifaransa).
3. YO-ZEF (Kijerumani).

Linatokana na jina la kilatini lililotokana na jina la kiyunani (LOSEPHOS), lililotokana na jina la Kiebrania (YOSEF) likiwa na maana ya:

“ATAZIDISHA au ATAONGEZA” (He Will Add).

Katika agano la kale Biblia takatifu inaeleza Yusufu na Joseph ni mwana wa kumi na moja wa Yakobo (Israel).

Kwa sababu ya kupendwa sana na baba yake Yusufu alionewa wivu na ndugu zake, wakamchukia, wakamuuza akapelekwa Misri kisha wakaenda kumweleza baba yao uongo kwamba alikuwa amekufa.

Lakini huko Misri Yusufu aliongezewa neema ya Mungu akapandishwa cheo na kuwa Mshauri mkuu wa Farao.

Jina hili pia limetumiwa na watu wengine wawili ndani ya biblia takatifu waliocheza nafasi muhimu sana ya kiroho na kimaandiko ambao ni Yusufu mume wa Bikira Mariam na Yusufu tajiri wa Arimathaya aliyenunua kaburi la kifahari akalitumia kuhifadhi mwili wa Bwana Yesu Kristo baada ya kufa msalabani.

Jumanne, Oktoba 19, 2010

KUPATA MORNING STAR RADIO FM

KUTUPATA KWA HOPE CHANNEL INTERTAIONAL
Big Satelite Dishes freq,04070 symbol rate 03003 vertical polrity 2/3.
Small Satelite Dishes freq,26657 vertical polrity 7-10,all frm intelsat Satelite located 68.5 degree east

Jumamosi, Oktoba 16, 2010

MAPANGO YA AMONI

MAPANGO YA AMBONI

Mapango ya Amboni yako katika eneo la Kiamoni, kata ya kiamoni, tarafa ya chumbageni, wilaya ya tanga, mkoa wa tanga. Ni eneo zuri la kupumzikia, kwa tafi za kihistoria, kijiografia, kijiolojia, n.k


Mapango haya yako umbali wa kilomita 8 toka tanga mjini kupitia barabara kuu inayoelekea Mombasa. Unaweza kufika katika hifadhi ya mapango kwa kupitia mojawapo ya njia zinazoelekea huko. Ya kwanza ni barabara ya changarawe iliyo upande wa kushoto meta 200 baada ya kuvuka daraja la hofu, ya pili iko kilometa 1.5 kutoka daraja la utofu katika kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu. Njia zote zinapitia katikati ya kijiji cha kiamoni.


Mapango haya yametokana na mabadiliko ya nguvu za asili zilizobadilisha maumbile ya miamba ya chokaa kipindi cha jurasiki (Jurassic period) kama miaka inayosadikiwa kuwa zaidi ya milioni 150 iliyopita. Kulingana na tafiti zilizokwishafanywa, eneo hili la mapango lilikuwwa tena chini ya maji miaka milioni 20 iliyopita na linakadiriwa kuwa na ukubwa wa kilometa za mraba 234 lenye mazingira ya miamba ya chokaa. Ni eneo ambalo linapitiwa na mito na limejaa uoto wa asili.


Miamba ya chokaaa kwa asili huundwa na madini ya kashiamu kabonate [ Calcium carbonate=CaCo3]. Miamba hii ni migumu kumomonyolewa na maji ya kawaida, lakini ni rahisi kuyeyushwa na maji yenye kiasi kidogo cha tindikali ya kaboni (Carbonic Acid). Tindikali ya kaboni iliyobadilisha maumbile ya miamba hii kwa kumomonyoa na kusababisha mapango yaweza kutokana na maji ya mvua yanapochanganyika na dioksidi ya kaboni (carbodioxide) hewani kabla ya kufika ardhini au na dioksidi ya kaboni inayopatikana ardhini. Maji yanapojipenyeza ardhini huendelea kupokea dioksidi ya kaboni kutoka muozo wa viumbe hai kama mimea na wanyama na kutengeneza tindikali. Tindikali ya kaboni inapopambana na madini ya kashiamu kaboneti (calcium carbonate) katika miamba ya chokaa husababisha kumomonyoka kwa miamba hii katika maeneo mbalimbali na kusababisha mapango. Mabadiliko haya huitwa kabonesheni (carbonation). Angalia mchanganuo wa kemikali ufuatao.


Wataalam wanaelezea njia mbalimbali zilizosababisha mapango katika eneo hili.


Kulingana na utafiti uliofanywa na mturi (1979), njia ya kwanza ni ile ya maji ya mvua yanapochanganyika na hewa ya “Carbondioxide” katika anga na kutengeneza tindikali (carbonic acid) ambayo inauwezo wa kuyeyusha madini ya calcium carbonate yanaunda sehemu kubwa ya miamba ya chokaa. Maji haya yenye tindikali husababisha mabadiliko kidogo yanapotelemka kuelekea ardhini. Yakifikia meza ya maji (water table) huku yakiendelea kuongezeka huzidi kuchanganyika na carbondioxide) iliyoko kwenye maji ardhini.


Kina cha maji kikiongezeka maji haya yenye tindikali huwa na uwezo wa kuyeyusha maungio ya miamba katika sehemu laini zaidi za miamba na kusababisha nyufa. Nyufa hizi huzidi kupanuliwa na maji yanayotembea na kusababisha baadhi ya mawe kuporomoka na kufanya mapango. Kasi ya maji inapozidi njia ndogondogo hupanuliwa na kuwa kubwa zaidi na upo uwezekano mapango madogo madogo hupanuliwa na kuwa kubwa zaidi na upo uwezekano mapango madogo madogo kuunganishwa na hatimaye kuwa na mfululizo wa mapango kama yanavyoonekana katika eneo hili.


Kina cha maji kinapopungua eneo huachwa likiwa kavu, lakini mabadiliko hayo huweza kuendelea kutokea chini zaidi na kusababisha njia na mapango mengine katika kina kingine ambapo hutokea muunganiko wa mapango kwa baadhi ya maeneo.


Njia nyingine ni pale ambapo inasemekana eneo hili lilikuwa chini ya usawa wa bahari yaani pembeni ya ufuko wa bahari. Mawimbi ya bahari yakamomonyoa miamba ya chokaa na kusababisha mapango. Baada ya bahari kurudi nyuma kutokana na kupungua kwa kina chake katika eneo hili, eneo la mapango likaachwa likiwa kavu.


Njia zote zilizoelezwa zimehusika katika kutokea kwa mapango haya, Mapango ya kwanza yatakuwa yalitokana na mmomonyoko wa miamba ya chokaa kutoka na maji ya ardhini yenye tindikali yaliyoyeyusha maungio ya miamba ya chokaa na kusababisha mapango. Kina cha bahari kilipopanda, maji ya bahari yalifikia eneo la mapango na mawimbi yake kusababisha kupanuliwa kwa mapango au mabadiliko katika kuta za nje na ndani ya mapango. Kina cha bahari kiliposhuka, eneo la mapango kilikuwa chini sana, maji ya mvua yenye tindikali yamekuwa na uwezo wa kuendelea kupanua na kubadilisha mfumo wa mapango.


Haijulikani mapango haya yaligunduliwa lini, bali taarifa zilizopo zinaonesha kwamba watu wa makabila yaliyoishi jirani na eneo la mapango: Wabondei, Wasambaa, Wadigo, na Wasegeju wamekuwa wakiya tumia kwa ajili ya matambiko ya mizimu tangu karne ya 16. Eneo hili la mapango kwa wakati huo lilijulikana kama eneo la mzimu wa mabavu.


Watu wanaamini habari za nguvu za mizimu katika kutatua matatizo ya uzazi, kuongeza kipato, magonjwa n.k. Kwa hivi sasa hutoka sehemu mbali mbali za Afrika Mashariki na kuja kuomba au kutambikia mizimu katika vijipango mbali mbali. Mbali na matumizi hayo, kampuni ya kigeni iliyojulikana kama “Amboni Limited” ilimiliki mashamba ya mkonge katika eneo la ta nga na kuweka eneo hili chini ya himaya yake mwaka 1892 ili kulitumia kama sehemu ya kupumzikia. Hii inatokana na mazingira mazuri na yenye utulivu ya mapango ya Amboni. Baadaye kampuni hii ilijulisha serikali kuhusu kuwepo kwa mapango haya. Serikali ilichukua hatua kutangaza eneo la mapango kuwa eneo la hifadhi mwaka 1922.


Mwaka 1937 ilipitishwa sheria ya mambo ya kale (Monuments Preservation Ordinace of 1937) iliyofuatiwa na ile ya 1953 (Monuments Preservation Ordinace of 1953) ambayo ingesaidia kulinda mambo ya kale ikiwa ni pamoja na mapango ya amboni. Mwaka 1963 serikali ya Tanganyika ikayaweka mapango chini ya usimamizi wa idara ya mambo ya kale. Mwaka 1964 serikali ilisimamisha sheria ya kikoloni ya 1937 na 1953 na kupitisha sheria ya mambo ya kale ya mwaka huo (The Antiquities Act of 1964) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 1979 (Amendments Acts of 1979) kwa ajili ya kulinda mambo ya kale nchini. Kwa upande wa mapango ya Amboni, mbali na mambo mengine sheria inakataza kuandika au kuchora kwenye kuta za mapango.

VIVUTIO:



  1. Kuna maeneo maalum yaliyotengwa kwa ajili ya kuomba au kutambikia mizimu ambapo utaona vitu vingi vinavyohusiana na imani za kijadi.

  2. Kuna miamba yenye maumbo ya kuvutia yanayofanana na Sofa/Kochi, Meli, Mamba, Tembo, Sanamu ya bikira maria n.k. Kuna vitu vinavyoonekana kama michoro inayofanana na unyayo wa mguu wa binadamu, na mnyama inayotokana na uchafu, hasa vumbi na udongo ambao hunywea pamoja na maji ya mvua na hatimaye kuganda katika paa la pango. Alama nyingine ni zile zilizosababishwa na popo wanaoishi mapangoni.

  3. Kuna miamba inayokua au kuongezeka (Speleothems/Dripstones) kutokana na mabadiliko ya kikemikali katika miamba ya chokaa. Mabadiliko haya hutokana na maji yenye tindikali kuyeyusha madini ya “Calicium Carbonate”, kuyahamisha na kuya rundika katika eneo jingine. Mtokeo ni kupata miamba inayokuwa kutoka juu kuelekea chini (stalactite) au inayoelekea juu (stalagmite). Kulingana na utafiti uliofanywa na Mapunda na Msemwa (2005:101). Miamba ya aina hii huongezeka/kukua kwa kasi zaidi kipindi cha mvua kuliko kipindi cha kiangazi. Katika miaka kumi iliyopita, ukuaji wa miamba ya aina hii ni milimeta 0.5 kila baada ya miaka 100. Na kwamba iliwahi kuongezeka kwa kasi ya milimeta 7 katika kila miaka 100 kipindi cha kati ya miaka 38,000 na 34,000 (38 & 34 Ka)


Yapo masimulizi mengine yanayohusu mapango haya, mfano:


Kuna simulizi zinazoelezea njia za mapango zinazoelekea Mombasa, Maweni, Mkoa wa Kilimanjaro n.k. Vile vile zipo simulizi za Osale Otango (Samuel Otango) na (Paulo Hamis). Watu hawa waliwahi kutumia kituo namba tatu ndani ya pango kubwa kama sehemu yao ya kujificha kati ya mwaka 1952 na 1956 huku wakiendesha harakati za kupambana na walowezi waliokuwa wamewekeza katika maeneo ya Tanga. Walipora mali na kutishia maisha ya walowezi katika maeneo mbalimbali. Serikali ya kikoloni iliwatambua kama wahalifu na kujaribu kuwakamata bila mafanikio kwa kipindi kirefu. Mwaka 1957 Paulo Hamis alipigwa risasi maeneo ya Lushoto na kufariki. Wananchi wa kawaida wanawakumbuka kama mashujaa walioendesha harakati za ukombozi wa watu wanyonge kutoka katika mikono ya walowezi na watawala wa kikoloni.


NUKUU:


Habari hizi zimeandikwa kutokana na masimulizi pia maelezo kutoka katika vitabu mbalimbali:-


1. Institute of Curriculum Development: Geography Coourse Book for Secondary Schools Book 3.


2. Lutgens, F.K and Edward J.Tartbuck (2000). Essentials of GEOLOGY. SEVENTH EDITION. Upper Saddle River, New Jersey: Printice-Hall, Inc.


3. Mapunda, B.B.B and Paulo Msemwa (2005). Slavaging Tanzania’s culture Heritage, Dar es Salaam. Dar es Salaam University Press.


4. Mturi, A.A (1998). Archeology of Tanzania, Dar es Salaam: The Open University of Tanzania.


5. Mturi, A.A (1975). A guide to Tongoni Ruins, Dar es Salaam.


Ama, unaweza kupata maelezo zaidi kwa kuwasiliana kupitia mawasiliano haya:


Mapango ya Amboni.
S.L.P 5028,
TANGA.

Simu: +255 784 788 990 na +255 784 546 302.

Ijumaa, Oktoba 15, 2010

HAMU HAIISHI LEO

NI MWANZO MGUMU LAKINI WENYE NEEMA, SIKU YA KULA MAZIWA NA ASALI. UNAWEZA DHANI NI SUALA LA KUFIKIRIKA LAKINI NI ZAIDI YA KIKOMO CHA MAWAZO NA FIKRA ZETU ZINAPOISHIA. SASA, TARAJIA ZAIDI MAANA MWENENDO WETU UNATULETEA MAMBO MAGUMU NA KUYAFANYA MAISHA KUWA KITU KISICHO MUHIMU NDIO MAANA LEO MWANAMKE AMA MWANAMME YUPO RADHI ASIKUPE RUHUSA YA KUCHEZEA AMA KUTUMIA GARI LAKE LINALOTUMIA MAFUTA IWE NI DIESEL AMA PETROL LAKINI MWILI UNAWEZA KUUFANYIA CHOCHOTE ILIMRADI ETI UNAITULIZA TAMAA!!! HAMU HAIISHI JAMANI.

Jumamosi, Mei 22, 2010

UTARATIBU NA CODE NAMBA YA HUKU NA KULE 105.3 fm

CHANZO CHA KUFELI

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KUHUSU MATOKEO YANGU YA KIDATO CHA NNE 2008

(Nimeiandika 8th, February 2009)
Kumbukumbu ya matokeo yalivyotoka na kunihusu mimi mdogo wako.

Hayo yote yalitokana na msichana mmoja ambaye niliwahi mpenda na kujikuta na zama katika kufeli mtihani na maisha yangu kupinda. Kisa hiki kina husu yale yote yaliyonikuta shuleni na hatimaye kushindwa kutimiza ahadi yangu, ilikuwa hivi:

Nilikuwa nasoma shule moja iliyopo Arusha, kwa ujumla afya yangu haikuwa njema kwa kipindi chote cha masomo yangu. Niliugua sana muda wote wa maisha ya pale shuleni. Ndipo siku moja nikaaamua kwenda nyumbani kutibiwa.

Nilitumia mda mrefu kutibiwa baada ya hosipitali kushindwa kunitibu ndipo nikaacha shule ili niwe nyumbani kwa ajili ya matibabu, nilitibiwa kwa muda wa miezi sita hatimaye nikapata nafuu ya kuweza kuendelea na masomo ya sekondari kidato cha pili na nilifaulu mtihani wangu wa kidato hicho.

Baada ya hapo, ndipo nilipokutana na msichana mmoja aliyenipenda yeye mwenyewe nami nikajikuta nampenda kulingana na jinsi tulivyokuwa tumezoeana kwa muda mrefu, ni kweli tulipendana sana tena sana, tuliheshumiana na kila mmoja alimjali mwenzake.
Hapo ilikuwa mwezi wa kumi na mbili baada ya kumaliza mtihani wa kidato cha pili.

Matokeo yalipotoka, wote tulifaulu kuendelea na kidato cha tatu. Sasa huo ndio mda matatizo yalipoanzia hasa kwa upande wangu mimi. Ugonjwa ulianza tena kwa kasi ya ajabu ambayo muda wote ulinifanya mimi kuwa mgonjwa sana

Wakati huo huyo msichana kumbe yeye alikuwa na msela mwingine ambaye ni rafiki yangu sana, kadri nilipokuwa nikimuuliza na kumwambia kwamba yeye ana mtu mwingine alikuwa anakataaa kata kata kwamba hana. Tuliendelea na uhusiano wetu kwa muda, siku moja mimi mwenyewe nikamkuta akitoka kwao na huyo jamaa.

Kumbe alikuwa akienda mara kwa mara kwao, nikaamua kuachana nae kabisa. Kuna wakati aliniomba msamaha, alinisihi sana nami niliaamua kumsamehe kutokana na jinsi nilivyokuwa nikimpenda. Lakini kadri nilivyozidi kuwa nae ndivyo nilivyokuwa na ugua sana.

Mara kifua kuuma sana, mara malaria kali ambayo haikuwa inaisha katika mwili wangu nilivumilia sana mpaka tukamaliza kidato hicho cha tatu lakini kwangu ilikuwa shida sana. Baadae alianza dharau, chuki na kuniona mimi simfai, niliachana nae hapo sasa niliugua nusura kufa!!

Nakumbuka baada ya kuachana naye siku hiyo niliugua usiku huku akinitokea mimi akiniambia kwamba kwa nini nimemwacha huku akiniambia nitakiona. Kesho yake nilienda hospitali kupimwa nikakutwa nina malaria kali sana. Daktari aliamua kunichoma sindano za malaria nikaanguka chini nakupoteza fahamu.

Hiyo ilikuwa mara yangu ya kwanza mimi kuzimia, baada ya hapo nilipozinduka na kupata nguvu niliamua kumfuata, nilienda nikamueleza yote, yeye alijibu kwamba aliomba kwa Mungu wake anifunulie mimi na kunionesha kwamba yeye alikuwa hana huyo ninaye hisi kwamba alikuwa naye.

Kwanza alicheka sana baada ya mimi kumwambia hayo yote yaliyonisibu, nikaamua kumuomba msamaha. Cha ajabu ni kwamba ugonjwa uliisha baada ya maongezi kwa muda na kesho yake nilikuwa mzima sana nikarudi shule.

Baada ya kurudi shule, niliendelea vyema na masomo yangu huku nikiendelea kumpenda na kumjali sana yeye kama mpenzi wangu, haukupita mda mrefu tukiwa kidato cha nne ndipo alipoamua kubadilika kabisa alinitenda alivyotaka. Baada ya kuona hayo mimi nikaamua kuachana nae tena kabisa mpaka mda wa wa kipindi cha mitihani kufika nilipatwa na tatizo la kufukuzwa shule na mwalimu wangu.

Kosa ni kufokeana na kiranja pale shuleni, huyo mwalimu hakujali hili wala lile akanifukuza shule. Kumbe huyo mwalimu alikuwa akitembea nae kwa maana ya mahusiano, ndipo alipopata nafasi ya kunifukuza shule huku akisema kwamba;…nilikuwa nakutafuta kwa mda mrefu.

Nilihangaika sana kuweza kumshauri huyo mwalimu anisamehe lakini alikataa kabisa nami niliamua kurudi nyumbani huku yeye akisema kwa marafiki zake kwamba amenikomoa sana mimi na kwamba alikuwa akinichukia sana mimi.

Baadae nilifanikiwa kurudi shule alipoona nimerudi akataka tena turudiane! mimi nikakataa, akawa ananitusi lakini sikuwahi hata kidogo kuongea nae jambo lolote lile hata kumjibu mpaka ikafikia hatua yeye alianza kujenga urafiki lakini nilikataa

Kwamba simtaki kabisa na kujiwekea msimamo wa aina hiyo mpaka sasa, lakini huyo mwalimu aliekuwa nae alisema jambo moja; tataona kama utafaulu mtihani wako wa mwisho!! Sikumjibu jambo lolote lile hata moja na kweli matokeo yalipotoka ndipo nikaamini kwamba nimefeli mtihani wangu lakini sikukata tama hata moja shule nitakwenda.

HII NDIO STORY YA MAISHA YALIYONIKUTA SHULENI, NIMESHINDWA LAKINI MUNGU HATANIACHA KAMWE.

Kaka, naomba kama kuna uwezekano wa mtu yeyote kutumia stori hii ili aweze kutoa mkanda ama kitabu sio jambo la uongo ni TRUE STORY. Sitasahau kamwe, jina la filamu iwe SELINA kuashiria matatizo yaliyonipata.

Mpaka sasa Yule msichana anataka turudiane lakini mimi nimeshaamua kuwa mwenyewe kabisa sitaki kupenda tena hata kidogo. Faida ya kupenda ndio hiyo iliyonikuta mimi na hasara ndio hiyo. Je, kama ni wewe ungefanyeje kuhusu yote hayo? Toa maoni yako kaka kwa kadri utavyoweza.

Hakika imeniuma sana na bado yeye anatuma salaam kwangu lakini mimi nilimjibu kwamba salaam zake ampe mpenzi wake ambaye alimuona anafaa kwake ndipo aliponitusi mimi mpaka na matusi ya mama yangu!! nilimuuliza mama yangu anamahusiano gani kati ya jambo hilo na yeye angepaswa anitusi mimi.

Kweli iliniuma sana mimi, lakini sitasahau kamwe mkasa huu ulionikuta mimi, ingawa mpaka sasa anatamani nimsamehe lakini mimi simtaki hata kidogo na wala jambo lolote kutoka kwake sihitaji kabisa.

Ahsante kunielewa.
Ni mimi mdogo wako,
E.D.M

Najaribu kufanya kile kitakachosaidia wazo lililoanza.
Wakati mwingine unaweza dhani kuwa hii siyo kawaida lakini ukweli unaonesha MAISHA ni sawa na mashindano ya aina yoyote yanayofanyika.
Kwa nini nasema hivi;
KILA SIKU INAHITAJI WAZO JIPYA, NAMNA JINSI UTAKAVYOJIKWAMUA KATIKA HALI UNAYOKABILIANA NAYO KATIKA MAZINGIRA ULIPO.
Kwa maana hiyo basi, naanza kuashiria mwanzo uliokwisha anza.
NINA MENGI YA KUONESHA

Fikiria Jambo Hili kwa KINA:

VIPI KAMA HALI HII INGEKUWA HIVYO SIKU ZOTE BILA KUBADILIKA
(No Jioni Wala Mchana na Hata Asubuhi)
**************
SIKU YA KWANZA

Ni simulizi ya kweli, iliyotokea halisi.
Tangu mwanzo hata sasa tunapoendelea.
SIKU YA KWANZA mara baada ya kuanza jambo.
Kumbuka siku ya kwanza wewe kupanda ndege.Au hivi, ile siku ya kwanza uliyokutana na ambaye kwa sasa!!, naamaanisha sasa hivi (kwa aliyeoa) ndie mama mkwe wako wakati ule ulipoenda kutoa posa.

**********

Mimi siku ya kwanza kula wali hata siikumbuki! Lakini nakumbuka siku ya kwanza kupanda gari!!... ni kisa cha kuchekesha sana kwa namna flani hivi ingawa ndani yake kuna fundisho. Hivyo ndivyo binadamu anavyokabiliana na mazingira.

************

Maisha yanaendelea kuwa na maana kutokana na mapitio, changamoto tunazokutana nazo na jinsi tunavyokabiliana nazo. Nitakupatia mfano mmoja, jinsi kipimo cha upendo kilivyo baina ya mwanamke na mwanamme. Angalia mapitio na changamoto walizokutana nazo vijana hawa wawili, kila mmoja kwa muda wake na mazingira aliyokuwemo.

****************

SIKU YA KWANZA NI SIMULIZI INAYOGUSA MAISHA HALISI YA BINADAMU.

Yusuph D. Mcharia.

Radio Presenter,

Story & Song wrighters, Producer and much more...!

Watoto Wanapenda Kucheza Kwenye Maji.


Jumamosi, Aprili 10, 2010

HII NI ISHARA TU, MOJA YA MAJUKUMU TUNAYOKABILIANA NAYO KILA MAWIO YANAPOFIKA NA HATA MACHWEO YANAPOJITOKEZA.

KAMA UNAWEZA JIULIZE JUU YA JUKUMU LINALOKUKABILI KILA SIKU INAYOPITA. DHAMIRA YANGU TANGU MDOGO NDIO HII NILIYOIFIKIA UKUBWANI, MTAYARISHAJI.

SASA, NAKULETEA MUHIMU YANAYOTUHUSU SOTE MAANA NATAMBUA WENGI TUNAPENDA BURUDANI.

NAYASEMA HAYA KWA SABABU NIMEMUDU KUFIKIA, ENDELEA BLOGINI...

Jumatatu, Machi 29, 2010

Hellow wote mtandanoni!!
Ni yangu imani kuwa haujambo msomaji wa blog hii.
Ni kwa siku nyingi nimekuwa kimya bila kuendeleza nia ya fikra zangu.
Namshukuru Mungu kwa jinsi anavyoendelea kuniweka katika namna ambayo kwa hakika sikuitaraji.
Kwa ufupi napenda kusema nimerejea tena.
MUZIKI WA ACAPPELLA NDIO JAMBO AMBALO LIMENICHUKULIA MDA WANGU MWINGI LENGO NIKUUFANIKISHA KWA KUUFIKISHA KATIKA NGAZI INAYOTAKIWA, WENGI WANAIITA YA KIMATAIFA.
Hellow wote mtandanoni!!

Ni yangu imani kuwa haujambo msomaji wa blog hii. Ni kwa siku nyingi nimekuwa kimya bila kuendeleza nia