Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Februari 11, 2013

MAANA YA KOMPYUTA


Kompyuta au Kinakilishi katika tafsiri ya Kiswahili ni kifaa au mashine ambayo inafafanua
na kunyumbulisha/kuchakata (process) habari isiyo rasmi (data) kwenda katika habari
rasmi (information) ambayo mtumiaji au mtu anaweza kuielewa na kuifanyia kazi
kutokana na maelekezo kiliyopewa na mtu. Hivyo kompyuta kama kompyuta kwa hakika haifanyi
kazi bila kupewa maelekezo. Bila kupewa maelekezo ifanye jambo gani kompyuta ni kama kopo!
Hii inabadilisha kabisa imani kuwa kompyuta inafanya kazi kuliko binadamu na kwamba ina
uwezo wa juu kuliko hata ubongo wa binadamu! Bila binadamu kompyuta haiwezi kuwapo.
Hiki ni kifaa ambacho hakika kimebadilisha maisha ya binadamu katika karne ya ishirini na
kuweza kuyafanya kuwa rahisi zaidi kwa maana ya kutenda kazi kwa ufanisi wa hali ya juu. Neno
Kompyuta, kwa kimombo ‘Computer’; linataokana na neno ‘computing’ likiwa na maana ya
kukokotoa au kuchanganua hesabu kama kujumlisha, kugawanya, kutoa na kuzidisha. Kompyuta
ina historia ndefu kutoka katika kipindi cha kabla ya kuzaliwa Kristo ambako watu mbalimbali
kama Charles Babbage,

Lakini kifaa cha kwanza kabisa ambacho kinafanana kiutendaji na kompyuta ya leo hii
kiligunduliwa mnamo karne ya 20 (kati ya mwaka 1940 – 1945) ingawa nadharia ya kompyuta na
mashine mbalimbali zinazofanana nayo vilikuwapo kabla kama nilivyosema hapo mwanzo.
Mfululizo wa ugunduzi wa kompyuta ambazo zilikuwa na nguvu ya kutosha kufanya hisabati na
hata kutunza kiasi kidogo cha kumbukumbu ulifanyika kati ya miaka ya 1930 na 1940. Utumiaji
wa vifaa vya ki-eletroniki katika mfumo wa digital ambao uligunduliwa na kuendelezwa kwa kiasi
kikubwa na mtu aliyeitwa Claude Shannon mnamo mwaka 1937 ulifanikisha kwa kiasi kikubwa
kuimarisha ubora wa kompyuta hizo.

Kompyuta inaweza kuelezewa kuwa imepitia hatua kadhaa katika kufikia ubora ilionao sasa. Kati
ya miaka ya 1940 mpaka miaka ya 1950 kompyuta ilikuwa ikitengenezwa kwa teknolojia
iliyojulikana kama vacuum tube. Hii ilikuwa ni teknolojia ambayo ilikuwa ikitumia tubes ndogo
mfano wa vichupa vidogo ambavyo viliondolewa hewa ndani na kuvitengeneza katika mfumo
ambao viliweza kupitisha umeme ambao ndiyo uliunganishwa katika chombo kizima kwa ajili ya
kufanya kazi(kumbuka hata kompyuta ya sasa hufanya kazi kwa kutumia mtiririko wa elektron
ambao umefanywa katika mfumo maalum). Mfano wa kompyuta hizi ni Konrad Zuse's
electromechanical au "Z machines" au Z3 (1941), Atanasoff–Berry Computer (1941), Colossus
computer (1944) ambayo ilitumika kwa ajili ya shughuli za siri katika jeshi la uingereza na
ilitumika katika kupata taarifa za siri za jeshi la ujerumani katika vita ya pili ya dunia, Harvard
Mark I (1944) na kompyuta iliyotumika na jeshi la Wamarekani iliyojulikana kama ENIAC.

Hata hivyo teknolojia hii ya vacuum tubes ilitumika mpaka mwishoni mwa miaka ya 1950 na
mwanzoni mwa miaka ya 1960 kulizinduliwa teknolojia mpya inayofahamika kama transistor
technology. Kompyuta zilizotumia teknolojia hii ziliweza kufanya kazi kwa urahisi zaidi, hazikuwa
aghali sana, zilikuwa ndogo, zilitumia umeme mdogo zaidi na ziliweza kufanya kazi kwa uhakika
zaidi kuliko zile za mwanzo. Kumbuka kuwa kompyuta za mwanzo zilikuwa na ukubwa sawa na
chumba kikubwa cha nyumba! Teknolojia ambayo mpaka sasa inatumika katika utengenezaji wa
kompyuta inaitwa integrated circuit technology. Teknolojia hii ilizinduliwa mnamo miaka ya 1970.
Ni teknolojia hii ambayo imesababisha kuzaliwa kwa kompyuta ambazo ni ndogo zaidi kuweza hata kubebwa katika kiganja cha mkono! Hii ni kea sababu ya kuundwa kwa kifaa kijulikanacho
kama microprocessor ambacho ndicho kama ubongo wa kompyuta. Kifaa hiki kina ukubwa wa
kama saizi ya milimita tano kwa nne. Ingawa kina umbo ndogo sana lakini kina jumla ya zaidi ya
transistor (sakiti ndogondogo zinazofanya kazi kwa ushirikiano) milioni moja!


Alhamisi, Februari 07, 2013

TEKNOHAMA - UTANGULIZI



Kompyuta ama Tarakilishi katika lugha ya Kiswahili ni kifaa ambacho kimebadilisha
kabisa mfumo wa maisha ya binadamu katika miongo takribani sita iliyopita. Kutokana na kuwapo kifaa hiki dunia imejikuta katika maendeleo makubwa kabisa kuliko kipindi chochote kile katika historia ya kuwapo kwake. Kifaa hiki kimeleta mabadiliko makubwa Sana katika maisha ya kawaida ya binadamu. Kifaa hiki kimesababisha mambo mengi kufanyika katika hali ambayo hakika isingewezekana au ambayo awali ingeonekana kama ya kufikirika!.

Kompyuta imeyafanya maisha kuwa rahisi zaidi. Kompyuta imeifanya dunia kuwa Kama
kijiji kidogo ambacho unaweza kukizunguka katika muda mfupi Sana wa sekunde chache! Lakini je unaifahamu kompyuta? Je wajua kuwa ni kifaa kidogo sana lakini chenye uwezo wa kufanya mambo mengi? Je wajua kuwa ndicho kifaa kinachoiendesha dunia katika Nyanja za kijamii, kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni?

Bila shaka umekwisha sikia na kukiona kifaa kinachoitwa kompyuta. Umekwisha sikia habari nyingi tu juu ya kifaa hiki ambacho hakika kimeifanya dunia nzima kukitegemea katika shughuli zote za kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na hata kisiasa. Bila shaka umekwisha sikia kuwa unaweza kununua bidhaa kwa kutumia kompyuta ukiwa nyumbani kwako bila ya hata kwenda huko sokoni au dukani. Bila shaka umekwisha sikia kuwa mabenki, hospitali, taa za kuongozea magari barabarani, kamera za usalama, ndege za abiria na kivita na hata lift unazopanda kila siku unapoingia na kutoka ofisini katika jengo refu huendeshwa kwa msaada wa kompyuta. Bila shaka umekwisha jionea mwenyewe au kusikia habari kama hizi. Umekwisha sikia kuwa mtu anaweza kumchagua mgombea wa urais au ubunge kwa kutumia kompyuta! Haya na mambo chungu nzima hufanyika kwa msaada wa kompyuta.

Katika nchi zilizoendelea matumizi ya kifaa hiki yanaendelea kushika hatamu kiasi kwamba kila
kitu sasa kinafanywa Kwa kutumia mashine zinazoongozwa Na kifaa hiki.

Lakini pia wengi hubaki wakijiuliza maswali mengi juu ya kifaa hiki. Je, ni vipi kifaa hiki kinakuwa na uwezo mkubwa kiasi hiki? Kinaweza vipi kufanya kazi automatically? Je kinaweza kufanya jambo lolote? Je ni nani ambaye alitengeneza kifaa hiki? Je kompyuta ikitengenezwa hujiendesha yenyewe bila msaada wa binadamu? Je kompyuta imetengenezwa Kwa kutumia vifaa gani na viko vingapi? Haya ni maswali ambayo kila mtu ambaye haifahamu vizuri teknolojia hii atapenda kupata majibu yake. Katika mfululizo wa makala haya nitakuletea ufafanuzi wa kina juu ya kifaa hiki ambacho hakika kinasisimua katika ufanyaji kazi na katika uundwaji wake.

Jumatano, Februari 06, 2013

WAJIBIKA KUTAFUTA FURAHA KATIKA UHUSIANO ULIONAO


Kila Mmoja Bila Kutegeana.


Inawezekana kuwa na furaha na amani katika ndoa au uhusiano ulionao kama wote wawili mtawajibika bila kutegeana,kwani ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha uhusiano alionao unakuwa na furaha wakati wote,haiwezekani katika muungano wa watu wawili kama mke na mume mmoja akaonekana kufaidi zaidi ya mwingine tupeane haki sawa kila mmoja amfurahishe mwenzie.




Inapendeza kuwa na amani na furaha kwa wote wawili kwani kila mmoja anajua jukumu lake kwa mwenzi wake ikiwa ni baba au mama alimradi kuwepo na maelewano baina yao,na kama utafahamu nini mwenzio anakipenda naye pia akawa anatambua kipi unapenda ni rahisi kudumu katika ndoa hata mahusiano kutokana na maelewano mazuri






Kama itatokea mahusiano yana mapungufu ya mmoja kukosa kujituma ili  kutimiza mahitaji ya ndoa kwasababu zilizo ndani ya uwezo,,basi uwezekano wa kuwepo na migogoro ni mkubwa,na katika hali kama hii haitashangaza suala la uaminifu kukosekana kutokana na kwamba mmoja anaona hapati mahitaji ya msingi kutoka kwa mwenzake mume au mke.maisha ya ndoa yanaitaji mawasiliano ya mara kwa mara,kwani kwa kufanya hivyo inaleta ushirikiano ,na uwazi ukiwa ni silaha ya kujenga zaidi..usinyamaze kimya kwa matatizo yanayojitokeza kwani kwa kufanya hivyo ni kuhatarisha mahusiano yenu.

Ijumaa, Februari 01, 2013

UTAFITI ULIOGUNDUA SAUTI ZA WATU, INASADIKIKA WANATESEKA KUZIMU.

Kikundi cha wanajiolojia watafiti

 

Katika makala haya, tutaangalia jinsi wanasayansi wa kawaida, tena ambao walikuwa hawaamini  kabisa kwamba kuna Mungu au shetani, katika utafiti wao ambao haukuwa na uhusiano wowote na masuala ya rohoni, walijikuta wanagundua mambo ambayo yaliwatia hofu hadi wengine kukimbia kazi. Waliweza kusikia waziwazi sauti za vilio vya mateso kutokea katikati ya dunia! Sauti hizo walizirekodi; na mwisho wa makala haya utaona anwani inayoweza kukupeleka kuzisikia sauti hizo za kutisha na kusikitisha mno, mno!!

Ni nani ambaye hajasikia habari za kwamba wanga huenda baharini, wakatupa mayai viza kisha malango yanafunguka nao wanashuka hadi kuzimu? Bila shaka habari hizi si ngeni masikioni mwa wengi wetu? Ni mambo ambayo ni rahisi kuaminika katika ulimwengu wa kawaida lakini unapoyaongelea kwa mtazamo wa Biblia, hapo watu wanaanza kukosa imani na kudhani kuwa si za kweli.

Makala haya yanatokana na habari ambayo iliandikwa katika gazeti la Ammennusatia la kule Finland katika toleo lake la Julai 1989.

 

       

Sehemu ya gazeti

Kikundi kimoja cha wanajiologia (wana elimu ya miamba) wa Kirusi walikuwa katika mradi wa kutoboa tundu katika eneo la Kola, karibu na Murmansk; maili takriban 150 kaskazini mwa Duara la Aktiki, nchini Siberia. Watafiti hao waliweza kutoboa tundu ardhini lenye urefu wa kilometa 14.4 kwenda chini.

Dr Azzacov, ambaye alikuwa ndiye meneja wa mradi alisema kuwa wakati wa kutoboa, ghafla drili ilianza kuzunguka bila utaratibu, hali iliyoonyesha kwamba drili imefika kwenye sehemu iliyo na uwazi.

 

 

“Taarifa tunazokusanya ni za kushangaa sana, kiasi kwamba kwa kweli tumeingiwa na hofu maana hatujui kile tunachoweza kukikuta huko chini,” alisema Dr Azzacov. 

“Jambo la pili lililotushangaza lilikuwa ni kiwango cha joto tulichokigundua katikati ya dunia. Mahesabu yanaonyesha kuwa joto hilo lilikuwa takribani nyuzi 1,000 za Selsiasi,” aliongeza kusema Dr Azzacov. “Hii ni zaidi ya kile tulichotegemea. Inaonekana ni kama moto wa jehanamu unawaka kwa nguvu sana humo ndani, katikati ya dunia!”

“Ugunduzi wa mwisho ndio uliokuwa wa kushitua sana masikioni mwetu kiasi kwamba wanasayansi wana hofu kubwa ya kuendelea na mradi huu. Tulikuwa tukijaribu kusikiliza mjongeo wa dunia kila baada ya muda fulani kwa kutumia vinasasauti vya hali ya juu sana (supersensitive microphones), ambavyo tulikuwa tukivishusha hadi chini kupitia kwenye tundu tulilotoboa.”                                                                                 

Dr Azaccov anaendelea kueleza kwamba, “Kile tulichosikia, wanasayansi hawa ambao wamezoea tu kuamini mambo yanayoleta mantiki akilini, kiliwafanya kutetemeka kwa hofu kubwa mno!  Wakati mwingine hicho tulichokisikia kilisikika kwa sauti ya chini lakini kali ambayo mwanzoni tulidhani inatokana na vifaa vyetu.”                                                                                                                 

“Lakini baada ya kuvirekebisha, tulibaini kwamba zilikuwa ni sauti zilizotoka katikati ya dunia kabisa. Hatukuamini masikio yetu. Tulisikia sauti ya mwanadamu akipiga kelele kwa maumivu. Japokuwa sauti moja ilikuwa inasikika kwa uwazi zaidi, tuliweza kusikia kwa nyuma sauti za maelfu, na huenda mamilioni ya watu wakilia kwa mateso na maumivu.

“Baada ya ugunduzi huu wa kutisha, nusu ya wanasayansi waliachana na mradi huo kutokana na hofu. Ni matumaini yangu kuwa hicho kilichoko huko chini kitabia hukohuko,” aliongezea Dr Azzacov.

“Na kilichowamaliza kabisa nguvu hawa wanasayansi wa Kisovieti, mbali na hizo sauti walizozisikia, ilikuwa ni kutokea usiku uleule kwa gesi inayong’aa kutoka kwenye tundu lile walilokuwa wamelitoboa; na katikati yake alijitokeza kiumbe mwenye mabawa kama ya popo pamoja na maneno yaliyokuwa yameandikwa kwa Kirusi ‘Nimeshinda’.”

 

 

Baada ya mkasa huo, Dr Azzacove alisema, “Mimi kama mkomunisti, siamini juu ya mbingu au Biblia, lakini kama mwanasayansi, hivi sasa naamini juu ya kuwapo kwa kuzimu. Ni kweli tuliogopa sana kutokana na ugunduzi huo. Lakini tunajua fika kile tulichokiona na kukisikia. Tunaamini kabisa kuwa tulitoboa tundu kwenye lango la kuzimu yenyewe!”

 

MAELEZO

Hili lilikuwa ni tukio ambalo liliwatokea watu ambao hawaamini kabisa habari ya Mungu. Wengi tunakumbuka kwamba kabla ya kusambaratika kwa Urusi ya zamani, ambayo ilikuwa ni dola kubwa ya umoja wa nchi za kisovieti, itikadi ya kisiasa ya dola hiyo ilikuwa ni ya kikomunisti ikiongozwa na falsafa za akina Marx, Lennin, Angels na Stalin.

Wao waliamini katika uyakinifu (materialism), yaani kwamba mwanadamu pamoja na ulimwengu wote ni kile tu kinachoonekana kwa macho au kuthibitika kisayansi. Suala la Mungu, shetani na chochote cha kiroho kwao kilikuwa ni uzushi. Na yeyote aliyejaribu kueneza itikadi za kidini, alishughulikiwa na dola ipasavya.

Karl Marx, kwa mfano , alisema, “Religion is an opium dose of the people.” – kwamba, “Dini ni dozi ya afyuni (dawa za kulevya) kwa watu.” Hii ikimaanisha kwamba dini ni kama ulevi wa kupumbaza akili za watu na kuwafanya wasiendelee.

Kwa hiyo, isingewezekana kabisa wakomunisti hawa waanze kueleza mambo ya rohoni ambayo katika maishani yao yote tangu wakiwa watoto waliaminishwa kwamba hakuna Mungu wala shetani kama anavyokiri Dr Azzacov mwenyewe kwenye maneno yake ya mwisho.

Sasa je, ugunduzi wao huo uliowajia bila kutegemea uhusiano wowote na Biblia?

Biblia inasema kwamba Yesu amepewa heshima kubwa na Mungu: “… ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi.” (Wafilipi 2:10).

Habari za Dr Azzaccov na timu yake unaweza kuzisoma mwenyewe mtandaoni kwenye www.diggsjourney.com. Hata hizo sauti za watu wanaoteseka kuzimu ambazo walizirekodi zimo humohumo; ni vizuri uzisikilize!!