Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Desemba 29, 2010

MTAYARISHAJI



Ni mtu anayechukua hatua ya kufanya myenendo ya rekodi za muziki, ambaye anataka kufanana kabisa na mwongozaji wa filamu pale anachokua hatua ya kuongoza filamu. Mtayarishaji wa muziki husaidia
|mwanamuzik
i|wanamuziki
na wa
sanii wanaofanya rekodi zao za nyimbo moja-moja au albamu iliyokamili.



Mtayarishaji:

Ni mtu anayetengeneza kitu au kukiandaa, kuangalia mazingira gani yatafaa kutayarishia k.m. filamu n.k. Pia mtayarishaji huwa anapata msaada mkubwa kutoka kwa muongozaji ambaye yeye huwaweka wasanii sawa vipi filamu itatakiwa iwe n.k.
Ila kwa mtazamo ambao watu wengi wamezoea kuuona na kusikia ni kwamba mtayarishaji huwa mtu anayetengeneza filamu au nyimbo.

Mwongozaji ni mtu anayetoa msaada wa kuongoza pindi mtu anapoigiza filamu. Wanaangalia vitu vya kisanii visiende kombo. Wanatoa maelekezo kwa waigizaji na kuongoza watu katika uigizaji wa filamu.

Mwongozaji:

wa filamu yeye ndiyo anayochukua jukumu zima la wanachama wanaofnya kazi ya uigizaji (waigizaji, watayrishaji, na kadharika). Kwa mfano, mtu yule ambaye anashughulika na taa anamwambia mtindo gani unaotakiwa taa imulikwe pindi yeye anapotoa maelekezo kwa waigizaji.

Ni kawaida sana kwa waongozaji wa filamu kufanya kazi pamoja na mtayarishaji. Mtayarishaji wa filamu ni mtu asiyehusika na upande wa kisanii wakati wa utengenezaji wa filamu. Kwa mfano, wao ndiyo wanaoshikiria fedha zote ambazo zinatumika kwa ajili ya utengenezaji wa filamu.



Jumanne, Desemba 28, 2010

Wanauchumi wa China watajirika kutokana na uvumbuzi

Hivi sasa uchumi wa China unakuzwa kwa haraka, watu wanasikia habari kuhusu watu wengi wanaotajirika au kuwa mashuhuri kwa usiku mmoja. Katika kipindi hiki cha leo nitawafahamisha vijana wawili waliojiajiri katika miaka ya 80 ya karne iliyopita. Vijana hao ni wenye umri wa miaka 24 au 25 hivi, lakini walipewa mikopo ya kuwekeza vitega-uchumi kutokana na uvumbuzi wao. Hivi sasa wamekuwa matajiri wenye Yuan milioni kumi kadhaa hata mia kadhaa, hivi sasa wakati vijana chipukizi wenye umri wa miaka kama wao, wanapoanza kuingia katika jamii, hao wamekuwa mahiri katika masoko ya biashara.

Mao Kankan ana umri wa miaka 22, ni kama vijana wengi wa mijini, moja ya burudani anayopenda sana ni kwenda kuimba katika jumba la Karaoke. Lakini baada ya kufika ofisini anaonekana kama ni mtu mwingine kabisa, yeye ni ofisa mtendaji wa kwanza wa kampuni ya kazi za viwanda ya Aihang. Jambo linalostaajabisha ni kuwa hivi sasa anaongoza kampuni ya Aihang kuwekeza Yuan za Renminbi milioni 300 kujenga kituo pekee cha michezo ya tarakimu mjini Beijing.

"Mnamo alasiri ya tarehe 28 mwezi Mei, mwaka 2010 saa 9 na dakika 58, ndege moja ya kijeshi ya nchi ya A ilitunguliwa ikiwa njiani kupeleka habari muhimu za siri, na habari hizo zikapotea. Hivyo nchi mbili za A na B zikawa na mchuano mkali wa kugombea kupata habari hizo muhimu."

Bw. Mao Kankan alikuwa akieleza mchezo alioubuni yeye pamoja na kundi lake, ambao utachezwa kwenye bustani moja ya Beijing. Wazo la kubuni mchezo huo utakaochezwa na watu ni la Bw. Mao Kankan, kwa kufuata wazo lake kila mtu anayeingia kwenye bustani anatakiwa kuvaa mavazi yanayolingana na mhusika wa mchezo. Kwa kutumia teknolojia ya mwigo (dummy) ya kisasa, hatimaye kutakuwa na watu zaidi ya 100, ambao wanashindana katika kutafuta hazina ndani ya bustani.

Mchezo wa elektroniki kubadilishwa kuwa maonesho ya watu halisi, kwa Mao Kankan ni mradi mkubwa unaoweza kutimiza tumaini lake.

"Ikiwa mambo hayo yanaweza kutendeka, baada ya miaka 5 yataweza kuleta faida ya zaidi ya Yuan bilioni 1, nimekadiria faida itakuwa Yuan bilioni 1.5."

Mao Kankan mwenye umri wa miaka 22, hajawekeza hata senti moja, lakini kutokana na wazo lake hilo, atapata karibu 20% ya hisa za mradi huo, ambao utaweza kuleta faida ya Yuan bilioni 1.5 kwa mwaka. Endapo mradi huo utatekelezwa, mali ya Mao Kankan itakuwa kubwa ajabu.

Wakati watu wengi wanashangaa kuhusu mali nyingi atakayopata Mao Kankan, tunamfahamu kijana mwingine, ambaye ana umri wa miaka karibu sawa na Mao Kankan, tofauti iliyopo ni kuwa kijana huyu alishapata mali nyingi.

Kijana huyu ni Li Xiang, ofisa mtendaji wa kwanza wa tovuti ya Mapovu. Hivi sasa anaongoza tovuti ya chombo kimoja cha habari inayotoa huduma kwa aina mbalimbali za bidhaa za teknolojia ya tarakimu. Bw. Li Xiang alipozungumzia tovuti aliyoanzisha, alisema,

"Tunatoa huduma kamili, ambayo ni ya kipekee kwa hivi sasa miongoni mwa tovuti kwenye mtandao wa Internet. Pengine tovuti yetu ni tovuti inayoweza kuunganisha vizuri web 1.0 na web 2.0, na kuweza kuleta faida pia."

Mwaka 2005, pato la tovuti ya Mapovu lilikuwa Yuan zaidi ya milioni 20, na faida ilikuwa Yuan zaidi ya milioni 10, na hisa anazomiliki kijana Li Xiang ni zaidi ya 50%.

Mafanikio waliyoyapata vijana hao wawili yanawashangaza sana watu. Lakini jambo lingine linalowashangaza watu zaidi ni kuwa vijana hao wawili wote hawana elimu ya chuo kikuu. Basi, vijana Mao Kankan na Li Xiang walifanyaje hadi kupata mafanikio makubwa ya namna hii?

Mao Kankan alikosa nafasi ya kushiriki kwenye mtihani wa kuingia vyuo vikuu kutokana na mafanikio duni katika somo la jiografia alipokuwa shule ya sekondari, halafu aliacha kabisa masomo ya shuleni. Lakini alisema kutosoma katika chuo kikuu hakukuwa na maana ndiyo mwisho wa elimu yake. MaoKankan alisema, "Wakati ule watu walithamini uthibitisho wa kampuni kubwa za kimataifa ikiwemo kampuni ya Microsoft, lakini sasa kuna thibitisho za aina nyingi, hata mtu anaweza kuziokota barabarani, lakini zilipokuwa na thamani, nilizipata nikiwa na umri wa miaka 17. Bado ninakumbuka kuwa wakati ule katika bara la Asia kulikuwa na vijana wawili wenye umri wa chini ya miaka 18, nilipata thibitisho 7 au 8 hivi, karibu nilipata uthibitisho wote."

Mafanikio ya Li Xiang kwenye tovuti ya Mapovu yanatokana na shauku yake kubwa juu ya kompyuta. Alipenda sana kompyuta tangu alipokuwa anasoma katika shule ya sekondari, na alianzisha tovuti yake katika Internet ya kutoa habari kuhusu vipuri za kompyuta.

Li Xiang hakutazamia kuwa shauku yake inaweza kuleta nafasi ya biashara, wafanyabiashara wa matangazo waliwekeza kwenye tovuti ya Li Xiang, ilikuwa kiasi cha Yuan zaidi ya 6,000 kwa mwezi. Hali hiyo iliendelea kwa miaka 3, kabla ya mtihani mkuu wa kuingia chuo kikuu, Li Xiang alifanya uamuzi muhimu wa kuacha masomo ya chuo kikuu ili apate nafasi ya kushughulikia tovuti yake.

Mao Kankan hakujali sana kuhusu kukosa nafasi ya kusoma katika chuo kikuu, isipokuwa anaona masikitiko kidogo kwa kukosa uzoefu wa kipindi hicho. Lakini Mao Kankan na Li Xiang wote wanaona kuwa vijana wakitaka kupata mafanikio, kitu muhimu siyo kama kuwa shahada au la, bali ni kuona kama ameweka lengo lake au la, na kama amefanya juhudi za kutosha kutimiza lengo lake.

Ingawa Mao Kankan na Xi Xiang wamepata mafanikio ambayo vijana wengine wa rika hilo huenda hawawezi kuyapata, lakini bado kuna watu wengi ambao wana mashaka kuhusu Mao Kankan na Li Xiang kama wanaweza kusimamia vizuri kampuni zao. Vijana wenye umri wa miaka 20 na kidogo, ambao wanamiliki mali nyingi, lakini hawakupata elimu ya juu, wana uwezo wa kuepusha kampuni zao na mambo ya hatari katika masoko yaliyojaa "mawimbi na upepo mkubwa"? Li Xiang alisema, katika muda wa miaka 8 iliyopita tangu aanze kushughulikia mambo ya biashara, amepambana na shida nyingi, na amepata uzoefu muhimu wa usimamizi. Alisema, "Nilifanya makosa mengi, na nilipatwa na shida za aina mbalimbali. Lakini niliweza kuzitatua vizuri, tena nimekuwa na uwezo wa kutatua matatizo hayo, hivyo nimepanda ngazi, ninaona hilo ni jambo zuri, na sioni mambo kama hayo ni mabaya."

Kwa Mao Kankan na Li Xiang, njia yao ya mbele ni ndefu sana. Sasa hatuwezi kutabiri mustakabali wao na wa kampuni zao. Lakini matokeo ya baadaye, kwa kundi la vijana wanaotafuta mali, linalowakilishwa na Mao Kankan na Li Xiang, yatabadilisha kanuni za shughuli za masoko ya jadi ya China, na kuongeza uvumbuzi mpya wa mali.

Laptop OR Desktop

Kansa ya vidole jamani .
Imeonekana ipo kama mtu atatumia sana laptop/desktop/baada ya muda flani atapata kansa ya vidole usiku nimeota ndoto hii.

Kuna mdau mmoja kwenye Facebook alieleza kuhusu jambo hili.
See or Visit hapa:
http://www.facebook.com/amani.ngussa


SI MNAJIDAI MNAWEZA MAZOEZI? HAYA SASA


SI LELE MAMA ATI! UP JUU! UP JUU! SHUSHA TENA

Jumanne, Desemba 21, 2010

SARAKASI


Dawaz ni usanii wa jadi wa mchezo wa sarakasi wa kabila la Wauyghur. Maana ya "Dawaz" katika lugha ya Kiuyghur ni "kutembea kwenye kamba iliyofungwa juu". Mchezo wa Dawaz una historia zaidi ya miaka 2,000, na unapendwa sana na watu wa makabila mbalimbali wanaoishi katika mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Wauyghur. Kikundi cha sarakati ya Dawaz cha shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang ni kikundi maalumu kwa ajili ya kufanya maonesho ya mchezo wa Dawaz, na wamefanya juhudi kubwa katika kurithisha na kuendeleza usanii wa mchezo wa Dawaz, na kufanya usanii huo uwe na mvuto mkubwa duniani siku hadi siku.

Kiongozi wa kikundi hicho Bw. Adil Hoxur ni mrithi wa kizazi cha sita wa usanii wa mchezo wa Dawaz. Bw. Hoxur alizaliwa mwaka 1971 katika familia moja ya wachezaji wa Dawaz iliyoishi katika wilaya ya Yingjisha ya sehemu ya Kashi mkoani Xinjiang. Baba yake ni mchezaji maarufu wa Dawaz wa sehemu hiyo. Alipokuwa mdogo, mara kwa mara aliwasikia mama na kaka yake wakisema baba yake anaweza kufanya kitendo cha ajabu anapotembea kwenye kamba. Alisema, "Mimi na ndugu zangu tulishindwa kujifunza kitendo hicho. Baba yetu aliweza kupanda kamba iliyofungwa juu kwa pembe ya digrii 45 kwa miguu tu huku akiwa amebeba mtu, na miguu yake inashikilia kamba vizuri kama koleo. Baba yangu aliweza kufanya kitendo hicho mpaka alipokuwa na umri wa miaka 72, na mwaka huo alifanya maonesho yake ya mwisho ya Dawaz kwa wakazi wa wilaya ya Yingjisha."

Baba wa Bw. Hoxur alikataa kumfundisha Hoxur ufundi wa Dawaz, kwani alifahamu sana kuwa ni mchezo wenye hatari kubwa. Bw. Hoxur alipokuwa mdogo, hakujua sana Dawaz. Alisema, "Baba yangu alifariki dunia nilipokuwa na umri wa miaka mitano. Nilipokuwa mdogo sikujua sana Dawaz. Mama yangu aliniambia kuwa familia yangu imekuwa familia ya wachezaji wa Dawaz kizazi baada ya kizazi. Alinielezea maana ya Dawaz akichora picha kwenye ardhi, na kusema wachezaji wa Dawaz wanaweza kutembea kwenye kamba iliyofungwa juu kwa urefu wa mita 21 ardhini. Nilishagaa sana kuwa baba yangu aliweza kupanda sehemu iliyo juu namna hii, nikaamua kuiga mfano wa baba yangu na kujifunza Dawaz. Baadaye nilifahamu vizuri mchezo wa Dawaz hatua kwa hatua na kuupenda mchezo huo siku hadi siku."

Wakati wa kusherehekea sikukuu, watu wa kabila la Wauyghur hawawezi kukosa maonesho ya Dawaz. Kwa kawaida maonesho hayo yanafanyika kwenye uwanja ulio wazi, wachezaji wa Dawaz wanatembea tembea juu ya kamba inayofungwa juu kwa urefu wa mita kumi kadhaa kutoka ardhi, na kufanya vitendo mbambali. Maonesho hayo huwasisimua sana watazamaji.



Mwaka 1986, Bw. Hoxur alikwenda mjini Urumuqi kwa mara ya kwanza, na kufanya maonesho ya Dawaz kwa ajili ya wanamichezo wa Michezo ya tatu ya watu wa makabila madogo madogo nchini China. Maonesho hayo yalimfanya afahamike sana na watu wengi. Bw. Hoxur alisema, "Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufanya maonesho hadharani mbele ya watu wengi. Watazamaji hao walishangilia na kupenda sana maonesho yangu, na wengi wao walituomba kupiga picha nao. Nilitambua kuwa chaguo langu la kujifunza Dawaz ni zuri, na niliona kuwa mimi ni shujaa, naweza kufanya jambo ambalo watu wengine hawathubutu kufanya."

Ili kuendeleza na kustawisha usanii ywa mchezo wa Dawaz, mwaka 1990 serikali ya mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Wauyghur iliwakusanya wachezaji wa Dawaz wa kabila la Wauyghur na kuunda kikundi cha maonesho. Hali hii ilitoa fursa nzuri kwa ajili ya maendeleo ya Dawaz. Mkuu wa shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang Bw. Anwar Mammat alisema, "Baada ya wachezaji hao 20 wa Dawaz kujiunga na shirika letu, tulifanya kazi nyingi za kuhakikisha usalama. Dawaz ni mchezo wa jadi, ili kuufanya mchezo huo uwe na thamani kubwa zaidi ya kisanaa, tulifanya marekebisho katika mambo mbalimbali."

Zamani maonesho ya mchezo wa Dawaz yalifanyika kwenye uwanja ulio wazi, hivi sasa maonesho hayo pia yanafanyika kwenye jukwaa la opera. Katika miaka ya hivi karibuni, Bw. Hoxur pamoja na wenzake walivumbua vitendo vingi vipya vyenye hatari kubwa, vikiwemo kupanda baiskeli yenye gurudumu moja, kuvingirisha bakuli na kuruka kamba juu ya kamba.

Mwaka 1997, Bw. Hoxur alifanikiwa kupita kamba ya chuma cha pua yenye urefu wa mita 600 iliyofungwa kati ya kando mbili za Mto Changjiang katika Magenge Matatu kwa dakika 13 na sekunde 48, bila kuwekwa zana za kuhakikisha usalama, na kuvunja rekodi ya Guinness kwa mara ya kwanza. Tarehe 6 Oktoba mwaka 2000, alipita kamba ya chuma cha pua yenye urefu wa mita 1399.6 iliyofungwa juu ya Mlima Heng, bila kuwekwa zana za kuhakikisha usalama, na kuvunja rekodi ya Guinness tena. Mwaka 2002, Bw. Hoxur alikaa juu ya kamba iliyofungwa juu ya ziwa Jinhai huko Pinggu kitongoji cha Beijing kwa siku 25. Jambo hilo lilifuatiliwa na dunia nzima, na alisifiwa kuwa "Mfalme wa Anga ya Juu" wa China.

Mafanikio hayo ya Bw. Hoxur yamewafanya watu wengi zaidi wafahamu usanii wa mchezo wa Dawaz. Hivi sasa sanaa hiyo ya kabila la Wauyghur imewekwa kwenye orodha ya mali za urithi wa utamaduni usioonekana ya China. Wakati huo huo shirika la maonesho ya sarakasi la Xinjiang pia linajitahidi kufundisha wachezaji wengi zaidi wa mchezo wa Dawaz. Bw. Hoxur na wanafunzi wake wanaimani kuwa mchezo huo utarithishwa kizazi baada ya kizazi.







YALIYOMO KWENYE KUNG FU YA CHINA










HISTORIA

mwanzo wa martial arts China ulitokana na haja ya ulinzi binafsi, ilikuwa ni mbinu ya uwindaji na mafunzo ya kijeshi katika China ya kale . mkono-kwa-mkono kupambana na silaha mazoezi yalikuwa muhimu katika kutoa mafunzo ya kale kwa askari wa china.

Ancient depiction of fighting monks practicing the art of self-defense .
Kale depiction ya kupambana na watawa kufanya mazoezi ya sanaa ya -kujilinda .


According to legend, Chinese martial arts originated during the semi-mythical Xia Dynasty more than 4,000 years ago. It is said the Yellow Emperor Huangdi (legendary date of ascension 2698 BCE ) introduced the earliest fighting systems to China.
The Yellow Emperor is described as a famous general who, before becoming China's leader, wrote lengthy treatises on medicine, astrology and the martial arts.

Kulingana na hadithi, China martial arts asili wakati wa nusu-mythical Xia Nasaba zaidi ya 4,000 iliyopita. [ Ni alisema Yellow Emperor Huangdi (hadithi tarehe ya kupaa 2698 KK ) ilianzisha mwanzo na mifumo ya kupambana na China .


The Emperor Yellow ni kama ilivyoelezwa maarufu ujumla ambao, kabla ya kuwa kiongozi wa China, aliandika treatises urefu juu ya dawa, Astrology na martial sanaa.

One of his main opponents was Chi You (蚩尤) who was credited as the creator of jiao di , a forerunner to the modern art of Chinese Wrestling .

Mmoja wa wapinzani wake kuu Chi You (蚩尤) ambaye alikuwa na sifa kama muumba wa Jiao di , a forerunner ya kisasa ya sanaa ya china Wrestling.


Tembelea hapa:
http://en.wikipedia.org/wiki/Chinese_martial_arts

Jumatatu, Desemba 20, 2010

BARAZA LA SANAA TANZANIA


Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), liko mbioni kuachia mikakati mizito ya kukuza sekta ya sanaa hapa nchini Tanzania ikiwiwa ni pamoja na kujenga jumba la sanaa litakalokuwa na hosteli za wasanii kwa ajili ya kuishi wakati wakiandaa kazi zao za sanaa.

Akizungumza Katibu Mtendaji wa BASATA jijini Dar es Salaam Ghonche Materego alisema ya kwamba, lengo la nyumba hiyo ya sanaa ni kuwatengenezea sehemu ya eneo maalumu kwa ajili ya wasanii ili wawe na mahali pazuri pa kuandalia kazi zao na kufanya maonyesho.

Mbali na jumba hilo la sanaa, Materego aliongeza kwa kusema kwamba, BASATA iko kwenye hatua za mwisho za kukamilisha ukumbi mkubwa na wa kisasa wa sanaa na burudani wenye uwezo wa kuingiza watu zaidi ya 1,000 wakiwa wamekaa, ambao unatarajiwa kwamba utafufua rasmi sanaa za maonyesho ya jukwaani, ambazo zimekuwa katika hatari ya kutoweka kutokana na kukosekana kwa eneo maalum la kuzionesha na kuziuza.

“Ni matarajio ya Baraza la sanaa Tanzania kwamba, nyumba na ukumbi huo wa sanaa na burudani ulio katika hatua za mwisho utakapokamilika, kutakuwa na uhai mkubwa wa sekta hii hapa nchini, kiasi cha kuanza kuamsha ari na pia kumeesha mizizi kwa Watanzania wengi hususan wale ambao hawathamini sanaa za nyumbani kwao.”

Akizungumzia suala la haki na wizi wa kazi za wasanii, Materego alisema kwamba, pamoja na kuwepo mamlaka nyingine inayoliangaza jambo hilo, BASATA katika mipango na mikakati yake inakusudia kuunda kitengo maalumu cha kulifuatilia, hasa kwenye sanaa za asili ili kuhakikisha tatizo la wizi za wasanii zinapungua na kuimarisha kipato cha wasanii.

Aidha, Materego alieleza zaidi kwamba, muda umefika sasa wa kuwepo kwa sera ya sanaa inayojitegemea, badala ya ilivyo sasa, ambako sekta hiyo inayokua kwa kasi na kuwa tegemeo la vijana wengi.

“Baraza linakusudia kushawishi kupitia njia mbalilmbali, ili sera ya taifa ya sanaa iundwe na baadaye kuleta mageuzi makubwa katika tasnia hii.

Hakuna sababu ya sekta ya sanaa kufichwa ndani ya sera ya utamaduni, kwani kwa sasa imekua sana na kuhitaji muongozo huru wenye kuhitaji uratibu wa kitaifa wa moja kwa moja,” hapa alisisitiza kweli kweli.

Alizidi kusema kwamba, pamoja na sekta ya sanaa hapa nchini kuongozwa na sera ya utamaduni ya mwaka 1997, bado sheria za Bunge na zile ndogondogo zinazosimamia sekta hii ni za 1984, hali inayohitaji kufanyiwa marekebisho makubwa.

Baraza la Sanaa la Taifa ni shirika la umma lililoundwa kwa sheria ya Bunge namba 23 ya mwaka 1984 na kazi zake kubwa ni kuratibu matukio ya sanaa nchini, kusimamia na kukuza sekta ya sanaa nchini kupitia kuhimiza ubunifu wa sanaa bora asilia.

Sasa, kazi kwako mwana sanaa.

Jumapili, Desemba 19, 2010

ACAPPELLA KWANZA

Baadhi ya viongozi wa A CAPPELLA KWANZA TANZANIA, Kutoka kushoto ni Maduhu (Katibu), Amani (Mwenyekiti), Enosi(Mratibu/Mawasiliano) na Yusuph (Makamu Mwenyekiti)

A cappella Kwanza ni kikundi cha kijamii chenye makao makuu yake jijini Dar es salaam,kinachojihusisha na shughuli za sanaa ya muziki wa A cappella. Ni kikundi kilicho na lengo la kusimamia,kukuza na kuendeleza fani ya muziki wa A cappella ikiwa kama sehemu mojawapo ya kuhubiri neno la Mungu na kutoa elimu kwa jamii juu ya uwepo wa utajiri wa kihistoria wa sanaa ya muziki wa A cappella.

Ninapozungumzia A cappella ninamaanisha uimbaji usiotumia ala za muziki.

Msingi wa A cappella ni wa kihistoria ulianza karne nyingi zilizopita,Ulianza ambapo jamii za makabila mbalimbali zilikuwa zikiimba nyimbo za kidini,muziki huu pia ulianza zamani kabla ya hata ya ugunduzi wa vyombo vya muziki.

Mpaka sasa hakuna taasis ama kikundi chochote ambacho kimekuwa kikijihusisha na maendeleo ya muziki wa A cappella nchini Tanzania mbali na kikundi cha A CAPPELLA KWANZA kilichosajiliwa mwaka 2006 na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Morning Star radio na AWR-Morogoro.

Hapa Tanzania aina hii ya uimbaji imekuwa ikitumiwa sana na kwaya ama vikundi vya makanisa mbalimbali kama vile, Kanisa la waadventsita, kanisa la kiinjili la kirutheri, kanisa la baptist n.k

Vikundi ambavyo vimekuwa vikiimba muziki wa A cappela kwa haraka haraka baadhi wakati wa miaka yaaa 2006 kurudi nyuma ni The Voice, Tukumbukeghe Singers, Royal Advent Quartet, Ilala Male Chorus, Busy Bee Quartet, Magomeni Trio, Zanzibar Brothers, Magomeni Heralds, Sonda ya Dilu Singers n.k

Kwa mara ya kwanza hapa nchini A CAPPELLA KWANZA ilifanya kongamano la uimbaji wa A cappella katika ukumbi wa Msimbazi Center jijini Dar es salaam March 11,2007 ambapo Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Mhe.Hulda Kibacha alikuwa mgeni rasmi.

Hata hivyo tumeanzisha umoja wa A cappella TANZANIA na Januari 1, 2011 umoja huo utaanza kazi rasmi. Kuna Programme tumeanzisha inayoitwa ACAPPELLA MTAANI.

STAY TUNE

105.3 fm-Dar es salaam.

MENGI TUTAKUJULISHA HUMU HUMU NA KWENYE KIPINDI AMBACHO HURUKA KILA IJUMAA KUANZIA SAA 2:00-3:00 USIKU NA KILA JUMAPILI KUANZIA SAA 10:00-12:00 JIONI.

...kwa mawasiliano zaidi tumia namba ama email ktk Profile ktk Blog hii.


MTIZAMO KUHUSU BINADAMU

Binadamu wote ni sawa lakini tunatofautiana kimawazo, fikra, kiutendaji, kipawa nk. Haya nilikuja kuyadhitisha katika kufuatilia fikra za Mwanafalsafa aliyekuwa maarufu sana kwa uchambuzi wa fikra na mawazo ambaye alikuwa anaitwa Plato.
Katika kazi yake ya "Republic" Plato alisema kuwa kila binadamu ameubwa tofauti kutokana na wengine kuwa na akili nyingi ambaye yeye aliwaita "golden boy" ambao yeye hawa aliwaelezea kuwa ni wale wanaweza kuwa viongozi wa nchi yaani (Philosphers, Gvern Planners and Rulers)

Wengine wanaakili ya kawaida "Silver boy" kwa mujibu wa Plato hawa ni wale wanaotakiwa kuwa walinzi wa nchi yaani askali jeshi na polisi pia alisema kundi la mwisho wa wale ambao wanaakili finyu "Iron Boy "hawa Plato alisema kuwa kwa kuwa wanauwezo mdogo wa kupambanua mambo kazi yao ni kulima na kuwa wazalishaji wa bidhaa za nchi.

Hii ilikuja pale nilipojaribu kufanya uchunguzi wangu na kugundua kuwa kumbe hata katika suala la upendo binadamu tuko tofauti wengine wanapenda wanene wengine wembamba na wengine weupe wengine weusi.

Katika makabira wengine wanapenda kabira fulani, kama mimi ninapenda wachaga na wengine hawapendi wachaga wengine wasomi wengine hawapendi wasiomi kwahiyo kutokana na hili binadamu tuko tofauti.

Je, katika mtazamo wako wewe unaona je? tujadili.

YOUTH COUNCELING

Helping youth cope with personal difficulties through interviews and other procedures, with the aim of allowing them to reach solutions to those difficulties themselves. the Counselling covers a wide spectrum of therapeutic activity, from practical advice given during one or two meetings to sympathetic attention over months or years. Youth counseling may specialize in particular areas, such as bereavement, trauma after battle or disaster, or living with serious illness...

Visit:www.sdamagomeni.org

Alhamisi, Desemba 09, 2010

WAGENI MELODIES SDA SING'ES



From Wikipedia, the free encyclopedia
Gospel music is
music that is written to express either personal, spiritual or a communal belief regarding Christian life, as well as (in terms of the varying music styles) to give a Christian alternative to mainstream secular music. ________________________________

Like other forms of Christian music, the creation, performance, significance, and even the definition of gospel music varies according to culture and social context. Gospel music is composed and performed for many purposes, including aesthetic pleasure, religious or ceremonial purposes, and as an entertainment product for the marketplace. However, a common theme of most gospel music is praise, worship or thanks to God, Christ, or the Holy Spirit.


Style Gospel music in general is characterized by dominant vocals (often with strong use of harmony) referencing lyrics of a religious nature, particularly Christian. Subgenres include contemporary gospel,
urban contemporary gospel (sometimes referred to as "black gospel"), Southern gospel, and modern gospel music (now more commonly known as praise and worship music or contemporary Christian music). Several forms of gospel music utilize choirs, use piano and/or Hammond organ, drums, bass guitar and, increasingly, electric guitar. In comparison with hymns, which are generally of a statelier measure, the gospel song is expected to have a refrain and often a more syncopated rhythm.


Many attempts have been made to describe the style of late 19th and early 20th century gospel songs in general. Christ-Janer, et al. said "the music was tuneful and easy to grasp... rudimentary harmonies... use of the chorus... varied metric schemes... motor rhythms were characteristic.... The device of letting the lower parts echo rhythmically a motive announced by the sopranos became a mannerism..." Patrick and Sydnor emphasize the notion that gospel music is "sentimental", quoting
Sankey as saying, "Before I sing I must feel", and they call attention to the comparison of the original version of Rowley’s "I Will Sing the Wondrous Story" with Sankey's version. Gold said, "Essentially the gospel songs are songs of testimony, persuasion, religious exhortation, or warning. Usually the chorus or refrain technique is found."
Source --------------------------------------------------------

Description above from the Wikipedia article Gospel music, licensed under CC-BY-SA, full list of contributors here. Community Pages are not affiliated with, or endorsed by, anyone associated with the topic.

Ijumaa, Desemba 03, 2010

THE SHINE GROUP

HISTORIA YA KIKUNDI CHA THE SHINE

UTANGULIZI:
Kikundi cha THE SHINE kilianzishwa mnamo mwezi wa tano (5), mwaka 2006, kikiwa na wanakikundi watatu, ambao ni SAMWEL SAUL, DEOGRATIUS WASHINGTON na VENANCE H. NYAMBO. Ilipofika mwezi wa saba (7) mwaka huo huo, waliongezeka wanakikundi wengine wawili ambao ni TUMAINI DAUDI na EMANUEL JOSEPH. Hivyo kikundi cha THE SHINE kinaundwa na wanakikundi watano kwa jumla.



CHIMBUKO LA KIKUNDI
SWALI: Je, SAMWEL ukiwa kama mwenyekiti wa kikundi, unaweza kutueleza chimbuko la kikundi cha THE SHINE?
SAMWELI SAUL: Ahsante, manamo mwaka 2005 mwanzoni kabisa mwa mwaka , nilipata njozi ya kuanzisha kikundi cha uimbaji muziki wa ACCAPPELLA, baada ya kuvutiwa sana na uimbaji huu, kilichojulikana kwa jina la, THE HARPVOICE kikundi hiki kilikuwa na wanakikundi zaidi ya kumI (10) nikiwemo pamoja na mimi mwenyewe SAMWEL pamoja na DEOGRATUIAUS WASHNGTON na wengine wengi, ingawaje sikuwahi kusoma elimu ya muziki ila tu ilikuwa ni kipaji kutoka kwa mungu mimi kupenda muziki.

SWALI: Sasa SAMWEL Je waweza kutueleza, vipi kuhusiana na matumizi au kuanzishwa kwa jina la “THE SHINE”?

SAMWELI SAUL: Oh! Mnamo mwaka 2006 mwezi wa 4 kundi hili la “THE HARP VOICE” ulivunjika, kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kama wingi wa wanakikundi uliopelekea migongano ya mawazo na hivyo kutoelewana.
Mara tu baada ya “THE HARP VOICE” kuvunjika kwa kweli bado nilikuwa na njozi ya kuendelea kumtumikia mungu zaidi kwa njia ya uimbaji katika kikundi ambacho kitasimama na kuongozwa na Mungu mwenyewe. Kwa neema ya Mungu ndipo nilipopata njozi na kuanzisha kikundi cha “THE SHINE” bado nilikuwa mwenyewe. Ndipo nilipoungana na mwenangu aitwaye DEOGRATIUS WASHINGTON ambaye baada ya kuvunjika kwa “THE HARP VOICE” hakuwa na pakusimama wala kuimba.

SWALI: Je, mkiwa wawili mmeshawahi kufanya huduma ya uimbaji sehemu yoyote?

DEOGRATIUS WASHINGTON: kwa kweli, hatukuwahi, kufangy huduma ya uimbaji yoyote tukiwa wawili. Tulianza kufanya hudumaya uimbaji tulipokuwa watatu, mara baada ya kumpata mwenzetu aitwaye VENANCE HONEST NYAMBO. Ndipo tulianza kufanya huduma ya uimbaji kanisani yaani MANZESE S.D.A CHURCH pamoja na makanisa mengine ya jirani.

SWALI: Je, vipi kuhusu TUMAINI DAVID MGUTU na EMMANUEL JOSEPH kwenye kikundi?

SAMWEL SAUL: mnamo mwaka huohuo mwezi wa 7 tulifanikiwa kumpata mwenzetu aitwae TUMAINI DAVID MGUTU, na kushirikiana naye kwenye kazi hii ya uimbaji na pia akiwa kama katibu wa hii kikundi.

Mnamo mwaka 2007 mwezi wa 3 tena tulifanikiwa kumpata mwenzetu mwingine aitwaye EMANUEL JOSEPH MBWAMBO AKIWA KAMA mtunza ya kikundi. Na hivyo kutimia mana kikundi watano (5) kuunda neon “SHINE”


SWALI: Waweza kutueleza maan ya neno “SHINE”

TUMAINI DAVIDI MGUTU: Neno “SHINE ” llina asili ya kiingereza limaanishalo MNG’AO, NURU AU MWANGAZA. Yaani, “kungarisha neno la Mungu ulimwenguni kote”. Lakini kila herufi kwenye neno “SHINE” linamaa yake kwa lugha ya kiingereza kama ifuatavyo.
S – Smart
H – Honest
I – Intelligent
E – Experience

LENGO/DHAMIRA KUU
Tangu awali tulipokuwa tumekwisha timia watano basi tukawa na lengu kuu ambalo lilituongoza kwenye suala zima la uinjilisti yaani “kuangaza neno la mungu ulimwenguni kote (To shine the word of the lord all over the world)”. Lengo hili kuu lilituongoza katika malengo mengine madogo madogo yakiwa kama:

- huduma kwa jamii
- kukuza ushirikiano na mahusiano baina yetu na vikundi vingine vya ACCAPELLA pamoja na waimbaji wengine wengi.
- Kurekodi na kuzindua album yetu ya kwanza ilikyokua na AUDIO na VIDEO.
- Kuimba katka makanisa mbalimbali ya ndani na nje, ikiwa ni pamoja na mikutano mbalimbali.
- Ukuaji wa kiroho.
- Kuongoa roho.

MAFANIKIO
Kwa neema ya mungu kutokana na lengo letu kuu pamoja na malengo mengine madogo madogo, Mungu alituwezesha katika mambo yafuatayo kati ya hayo yaliyotajwa hapo juu, nayo ni kamka ifuatavyo:-
Tulifanikiwa kwa njia ya uzinduzi wa album yetu ya kwanzan, kukuza ushirikiano na mahusiano baina yetu na vikundi na waimbaji wengine mbalimbali.


- Mnamo 15/07/2007 tulifanikiwa kuingia studio kwa ajili ya kurekodi, kwenye studio za Morning star Radio. Lakini pia Mnamo 29/06/2008, kwa neema ya mungu, tulifanikiwa kuzindua album yetu ya kwanza pale pale kanisani MANZESE S.D.A CHURCH iliyokkua na AUDIO na VIDEO. Tukio hili liliweza kutukutanisha na watu na vikundi vingi na kukshiriki kwa pamoja.


- Lakini pia tumefanikiw kuimba katika makanisa mbalimbali, kwenye mikutano mbalimbali, pia tumeweza kufikisha ujumbe huu kwa njia ya uimbaji na pia tumeweza kualikwa katika maharusi mbalimbali.



VIKWAZO
Pamoja na mafanikio hayo muda mfupi tuliyoweza kuyapata pia tulikuwa na vikwazo mabalimbali ambavyo viliwezesha kuchelewesha ama kuzuia kabisa kazi ya ujilistu kuendelea. Vikwazo hivi vilikua ni kama:-
- Kikwazo cha kwanza ambacho kiliweza kuchelewesha na kuzuia malengo yetu kwa kiasi kikubwa kilikua ni fedha, fedha iliendelea kuwa tatizo kubwa, kwenye maendeleo yetu.
- Kikwazo kingine kilikuwa ni ukosefu wa eleimu ya kutosha juu ya suala zima la muziki. Lakini pia sisi sote tu wanafunzi wa shule za secondary hivyo tumeweza kukosa muda wa kutosha kwenye mazoezi ya uimbaji kwa ujumla.
- Kucheleweshwa kwa album kutoka studio nalo lilikuwa kati ya suala lililotuchelewesha katika malengo yetu mbalimbali.

OMBI
Tunapenda kuleta ombi letu kwenu ambao kwa namna moja ama nyingine umeweza kuisikiliza/kusoma historia hii,kwamba uweze kutusaidia kwenye maombi, ukituombea juu ya malengo yetu ya kuanga neno la Mungu Ulimwenguni kote, tuombee. Lakini pia kama waweza kutoa sapoti/msaada kwa naman yoyote juu ya malengo ambayo bado tunayo. twaweza kuwasiliana simu hizo chini.

MAWASILIANO
255 713 – 764 713 Mwenyekiti
255 712 – 743 737 Katibu
255 714 – 414 914 Mhazini
255 712 – 229 901
E – mail:
theshineaccappellagroup06@yahoo.com