Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumapili, Februari 17, 2013

TEKNOHAMA -KOMPYUTA HUTUMIA UMEME ILI IWEZE KUFANYA KAZI


Kwa kawaida vyombo vingi vinavyorahisisha kazi hutumia kazi hutumia umeme ili viweze kuleta ufanisi katika shughuli mbalimbali. Kompyuta nayo hutumia umeme katika kutekeleza majukumu yake. Umeme huu huingizwa kwa kutumia nyanya (cable) ambazo hutoa umeme kutoka katika soketi zilizopo mahali husika. Umeme huu hupitia chombo maalum kifahamikacho kama power supply

Chombo hiki huwa kimeunganishwa kuelekea motherboard na sehemu nyingine muhimu. Kwa kawaida umeme huu hubadilishwa kutoka mfumo wa kubadilika badilika (alternating current a.c) kwenda mfumo wa moja kwa moja (direct current d.c) ambao kompyuta inaweza kuutumia. Umeme huu hugawanywa katika kiwango kinachotakiwa kulingana na matumizi ya sakiti husika.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni