Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Februari 25, 2012

Majibu Yafanyayo Kazi...SINAGOGI vs KANISA.


Sinagogi ni nyumba ya dini na ya jamii ya Wayahudi inayotumika hasa kusali.

Etimolojia

Neno linatokana na Kigiriki  sinagoge likimaanisha "mkutano"; ni tafsiri ya Kiebrania  beit knesset yaani "nyumba ya mkutano". Wayahudi hutumia pia neno la Kiyiddish "shul" (=shule) kutajia sinagogi.

Muundo

Chumba kikuu ni ukumbi wa sala lakini mara nyingi kipo pamoja na vyumba vya pembeni kama vile madarasa, ofisi na vingine. 

Historia

Katika Israeli ya Kale (kabla ya maangamizi ya Yerusalemu mwaka 587 KK) inaonekana hakukuwa na sinagogi: walau halitajwi kabisa katika Agano la Kale.
Hakuna uhakika kamili lakini inaonekana ya kwamba masinagogi yalianzishwa baada ya hekalu ya Yerusalemu kubomolewa pamoja na kuanza uhamisho wa Wayahudi kwenda nchi mbalimbali.
Tangu kuharibiwa kwa Hekalu la Pili mwaka 70 Wayahudi wana masinagogi tu kufanyia ibada.



Kanisa

Kwanza kabisa neno Kanisa linamaanisha "mkusanyiko wa waamini" kama ule wa Waisraeli chini ya Musamlima Sinai walipopewa Amri za Mungu. kwenye
Neno hilohilo lilitumiwa na Wakristo wa kwanza kwa ajili yao wenyewe kusema wameshika nafasi ya Israelitaifa la Mungu hata wasipokuwa Wayahudi bali watu wa mataifa mengine. kama
Jina hilo lilitumika kwa jumuia mama ya Yerusalemu, kwa kila mojawapo ya jumuia za Kikristo zilizotokana na umisionari wa wafuasi wa Yesu Kristo, na kwa umoja wao wa kimataifa uliotazamwa na Mtume PauloMwili wa Kristo, ukiwa na Yesu kama kichwa chake. kuwa

Kanisa kama jengo


Wakristo walipoanza kujenga mahali pa ibada, pakaja kuitwa vilevile "kanisa" kwa sababu ndani yake lilikusanyika Kanisa hai.
Hivyo mara nyingi neno hilo linatumika kwa maana ya jengo, ambalo ni mfano mwingine uliotumiwa na Paulo kuhusu umoja wa Wakristo, ukiwa na Yesu kama jiwe kuu la msingi.
Majengo hayo ya ibada yanaweza kuwa na ubora tofauti hata upande wa sanaa; baadhi yake yanatembelewa na watalii na kuhifadhiwa kwa bidii kwa sababu hiyo.
Kwa namna ya pekee ni muhimu Kanisa kuu la kila jimbo (dayosisi), halafu Basilika na Patakatifu.


 

Madhehebu

Baada ya umoja wa Wakristo kuanza kuvunjika, kwa kawaida madhehebu yaliyotokea yaliendelea kujiita makanisa, ingawa kwa maana mbalimbali: hasa Kanisa Katoliki na Waorthodoksi wanadai kuwa la kwao ndilo linaloendeleza Kanisa pekee la kweli; kumbe Waprotestanti hawatii maanani sana umoja wa Wakristo upande wa miundo, bali ule wa kiroho.
Ndani ya Kanisa Katoliki, linalokubali uongozi wa Papa wa Roma, neno Kanisa linatumika pia kumaanisha kila jimbo na makundi ya majimbo yanayochanga mapokeo yaleyale upande wa teolojia, liturujia, maisha ya kiroho, sheria n.k.
Kwa msingi huo Kanisa la Kilatini, ambalo lilienea kwanza upande wa magharibi wa Dola la Roma (Kanisa la Magharibi), linatofautishwa na Makanisa ya Mashariki yaliyoenea kwanza upande wa mashariki wa dola hilo na nje ya mipaka yake.

Mfumo  wa Waadventista Wasabato

 

Agizo la utume wa Mwokozi kwa kanisa kupeleka injili ulimwnegunu mwote (Mat. 28:19-20; Marko 16:15) halikumaanisha tu kuhubiri ujumbe bali kuhakikisha ustawi wa wale walioupokea ujumbe ule. Hii ilhusisha kuchuga na pia kulipatia kundi makazi, na pia kukabiliana na matatizo ya mahusiano. Hali kama hiyo ilihitaji mfumo (Oganaizaisheni).

Mwanzoni mitume wao wenyewe waliunda baraza ambalo liliongoza shughuli  katika kila kanisa (Mdo.14:23).Kanisa lile changa kutoka Yerusalemu (Mdo. 6:2; 8:14). Pale kundi la jijini lilipokuwa kubwa kiasi kwamba uendeshaji wa shughuli zao za dhati ukawa tatizo,mashemasi waliteuliwa kusimamia shughuli za kanisa (Mdo. 6:2-4). Pia inaonekana wazi kutokana na kumbukumbu za Mungu kwamba upanuzi wa kazi katika majimbo mbalimbali ya Dola ya Kirumi ulihitaji mfumo wa kanisa katika kile mabacho kinaweza kuitwa konferensi. Zilijumuisha makanisa katika ,jimbo mahsusi, kama vile makanisa ya Galatia(Waga.1:2); likawa na mfumo(oganaizesheni). Kadri mahitaji yalivyojitokeza Mungu aliwaongoza na kuwaelekeza viongozi wa kazi yake.

Madaraja katika mfumo wa kiutawala wa Waadventista Wasabato

Miongoni mwa Waadventista wasabato kuna madaraja manne ya uwakilishi kuanziamuumini mmoja hadi mfumo(oganaizesheni)mzima wa kazi ya kanisa ulimwenguni pote.

1. Kanisa moja;
Jamii iliyoungana katika mfumowa kundi la waumini mmoja mmoja.

2. Konferensi, fildi au misheni ya sehemu moja
Muungano wa jamii ya makanisa katika nchi, mkoa au eno la nchi.

3. Union inayojitegmea
Hii ni jamii ya muungano wa koferensi, fildi au misheni kadhaa ndani ya eneo kubwa la nchi.

4. Halmasahuri kuu
Ambayo ni sehemu kubwa ya mfumo wa utawala, unaounganisha union zote pande zote za ulimwengu. Divisheni ni shemu ya Halmashauri kuu, zikiwa na mamlaka katika maeneo maalumu yaliyotengwa
kijiografia.

Kila mshiriki wa kanisa ana sauti katika kuchagua maofisa wa kanisa. Kanisa huchagua maofisa wa fildi au konferensi. Wajumbe waliochaguliwa na fildi au konferensi huwachagua maofisa wa union zilizo konferensi au union misheni, na wajumbe waliochaguliwa na union konferensi au union misheni huwachagua maofisa wa halmashauri kuu. Kwa mpangilio huu kila konferensi au fildi, kila taasisi, kila kanisa na kila mshiriki binafsi, aidha moja kwa moja au kupitia wawakilishi, ana sauti kwa uchaguzi wa watu wanaobeba majukumu makubwa katika halmashauri kuu.

Halmashauri kuu , Mamlaka ya Juu Zaidi

Halmashauri kuu katika kikao rasmi cha kila miaka mitano,na Kamati ya Utendaji ikutanikayo katikati ya vikao rasmi, ndicho chombo cha juu zaidi katika utawala wa shuguli za kanisa uimwenguni kote, na chombo hicho kimepewa mamalaka na katiba yake kuunda mashirika yalio chini yake ili kuendeleza maslahi mahsusi katika sehemu mbalimbali za ulimwengu. Kwa hiyo basi imeeleweka wazi kwamba mashirika yote madogomadogo na taasisi ulimwenguni kote zitatambua Halmashari kuu kama mamalaka iliyo juu zaidi, chini ya Mungu miongoni wa Waadventista Wasabato. “Mara kwa mara nimeagizwa na Bwana ya kwamba maamuzi ya mtu yasisalimishwe kwa maamuzi ya mtu mwingine yeyote. Kamwe nia ya mtu mmoja au nia za watu wachache zisichukuliwe kama zatosha kwa hekima na uwezo kudhibiti kazi na kusema ni mipango ipi ndo itakayofuatwa. 

Lakini katika kikao rasmi cha halmashauri kuu, wakati maamuzi ya ndugu waliokusanyika pamoja kutoka sehemu zote za kazi ulimwenguni yanapotolewa, basi ushupavu binafsi na maamuzi binafsi ya pekee yasishiikiliwe kwa ukaidi, ila sharti yasalimishwe. Kamwe mtenda kazi asichukulie kuwa ni sifa kushikilia kwa ushupavu msimamao wake wa kutoambilika, kinyume cha uamuzi wa watu wote kwa ujumla. Nyakati nyingine kikundi, wakati ambapo kikundi kidogo cha watu kwa jumla waliokabidhiwa kusimamia kazi, kwa jina la Halmashauri kuu, wamejaribu kuendesha mipango isiyo ya busara nahivyo kuzuia kazi ya Mungu, hapo nimesema kuwa nisingeweza tena kuendelea kuheshimu sauti ya Halmashauri kuu iliyowakilishwa na watu hao wachache, kama sauti ya Mungu. Lakini hii siyo kusema kwamba maamuzi ya halmashauri kuu yenye wajumbe waliochaguliwa rasmi kutoka sehemu zote za kazi ulimwenguni hayapaswi kuheshimiwa. Mungu ameagiza kwamba wawakilishi wa kanisa lake kutoka sehemu zote za kazi duniani, wanapokusanyikakatika kikao cha Halmashauri kuu, watakuwa na mamlaka"-EG White

  ********************************

Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...
(Namaanisha JumaMosi)

Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo

Doug Batchelor  

a n a p o t w a m b i a    k u h u s u:

Who are the Seventh-day Adventists?

(AmazingFacts)



KARIBU TENA

Maoni 1 :

  1. mbona ujaniambiwa jibu la who are seventh day adventist???///?/?

    JibuFuta