Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Machi 05, 2011

...Tafakari!!. SAIKOLOJIA

Maisha yana kanuni moja kubwa nayo ni kutodumu kwa vitu. (Labda milima ambayo sijaona ikitoweka ingawa nayo inatajwa kutoweka) Unayoyaona leo kesho unaweza usiyaone kesho na kila linapoondoka moja jingine huja. Ukilia leo kesho utacheka, ukifurahi utahuzunika, ukipata utakosa, ukitajirika utafirisika pia.

Hayo ndiyo maisha ya kila siku ya mwanadamu. Sasa; ili uishi kwa raha kila ulipatalo sema litapita. Pambana na kila hali bila kuumizwa na kukata tamaa. Hayo yanayokusibu yatapita unachotakiwa kufanya ni kuishi wewe kama wewe na kutomtazama mumeo ama mkeo watoto, majirani, ndugu, rafiki, viongozi wa dini kama mkombozi wako.

LEO KWA SABABU YA UPEKEE NA UNYETI WA SIKU SIO VIBAYA TUKIBADILISHANA MAWAZO NA KUAMBIZANA YALIYOMUHIMU KTK MAISHA HASA YA KIROHO.



NA HUU UTAKUWA NI MFULULIZO KWA KILA SIKU KAMA HII LEO, NA MAANISHA JUMAMOSI.



PAMOJA NA KWAMBA WEEENGI WANAAMINI HIII NI KWELI LAKINI UKWELI HALISI JIONEE MWENYEWE HALAFU UTAFAKARI.



NAKUTAKIA SABATO RAFIKI.





...Tafakari!!.

Maoni 2 :

  1. Hiki kisebule babu kubwa. Wala sikuwa na habari nacho zaidi ya kuona jina la mtayarishaji akichangia kwenye visebule vingine. Good job keep it up.
    Nitakuwa nikikutembelea nimege hili na lile. Asante sana kwa kuwa mfuatiliaji wa blog yangu.

    JibuFuta
  2. Umenitafakarisha Mkuu! Sabato njema!



    Si unajua ingawa sijaandika komenti siku ijulikanayo kama Jumamosi kwa kalenda zetu hizi zilizobuniwa katika mikutano ya BINADAMU,..
    ... labda leo ndio JUMAMOSI kikweli aisee!:-(

    JibuFuta