Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Machi 10, 2014

NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIHI YA KISWAHILI


Inkisiri

Nyimbo, kama tanzu ya fasihi yeyote ile zina majukumu mbalimbali ambayo hutekeleza katika jamii. Lengo kuu la fasihi
ni lile la kuielimisha na hata kuiburudisha jamii. Ndivyo ilivyo katika nyimbo kwa sababu kupitia kwazo wanajamii huburudika
na kuelimishwa. Ni kwa sababu hiyo ndipo makala hii inalenga kuangalia nafasi ya nyimbo zinazopendwa katika fasihi ya
Kiswahili. Huu ni utanzu ambao huwafikia watu wengi katika jamii. Kutokana na kutumia lugha ya Kiswahili, utanzu huu
unaweza kueleweka na Wakenya wengi. Nchini Kenya, vyombo vya habari vimeipa fasihi hii nafasi kubwa sana na hivyo basi
kuipanua hadhira yake. Hii ni kutokana na sababu kuwa fasihi hii inathaminiwa sana na wengi na ipewe nafasi kubwa katika
vyombo vya habari hasa katika redio kwa muda mrefu. Ni kutokana na sababu hii ndipo tunajaribu kuonesha nafasi yake katika
fasihi ya Kiswahili.

Makala

Mahusiano ya kijamii hujengwa kutokana na historia, mazingira na shughuli za watu za kila siku na imani yao pia. Watu wa
jamii moja mara nyingi husikilizana kwa lugha, mila na desturi. Misingi hiyo ya utamadununi na utamaduni wenyewe huwa
ni vigezo maalum vya kumfanya mtu aitambue nafasi yake katika jamii na vile vile kutambua wajibu wake na majukumu yake,
Mazrui (1986).

Tanzu mojawapo inayodhihirisha utamaduni wa jamii ni muziki wake. Wasanii hawa, hasa waimbaji wanaoimba kwa
lugha ya Kiswahili nyimbo ambazo twaweza kuziita nyimbo-pendwa wamechukua nafasi kubwa katika kukuza lugha hii,
utamaduni na mawasiliano...

Muziki umekuwa chombo ambacho kimewavutia wanadamu. Jambo hili limewafanya watu wa matabaka mbalimbali wakiwemo
wanafalsafa na watu wa kawaida kujru:ibu kuelewa muziki - lakini hakuna fasili ambayo imeweza kueleza muziki ni nini hasa:
Uasili wake haujulikani, kama anavyodai Schumann katika kofia (1994) kuwa:

"Sayansi hutumia hisibati na umantiki, ushaiii nao hutumia maneno teule..  muziki ni yatima ambaye babake na mamake
hawajulikani kamwe. Hata hivyo, ni huu utata wa uasili wake ambao umefanya muziki uonekane kuwa kitu bora zaidi katika
jamii" (Tafsiii yangu).

Katika kutumia nyimbo, waimbaji hawa wameweza kuhifadhi historia na utamaduni wa jamii zao. Hata hivyo, hivi sasa utaona
kuwa maendeleo ya kisayansi na teknolojia yameanza kuiingiza jamii nyingi katika fasihi ya televisheni na video na hivyo kuonekana kama kwamba jambo hili linafifisha stru:ehe inayopitikana katika nyimbo (Mlacha, 1998}.

Dhamila kuu ya makala haya ni kuangalia nafasi ya nyimbo-pendwa katika fasihi ya Kiswahili. Mabadiliko katika jamii yamesababisha mabadiliko katika nyimbo na hivyo basi nyimbo zimekuwa na maudhui na fani tofauti kutegemea namnajamii ilivyobadilika.

Uchunguzi uliofanywa juu ya nyimbo umeonyesha kuwa nyimbo ni kipengele muhimu sana katika jamii zote ulimwenguni.
Nyimbo ni utanzu uliothaminiwa sana, na zilitawala katika mifumo yote yajamii, Brandel (1959). Akuno (1999) anasema kuwa muziki ni zaidi ya sauti tu ambazo huimbwa na kuchezwa. Muziki sio wazo la dhana fulani bali ni tajriba, ni tukio ambalo huwasilisha mambo mbalimbali yenye umuhimu katika jamii husika Akuno anaona nyimbo/muziki ukiwa na uamali wa kiujozi: Kwanza ni kama kiburudisho, muziki huendeleza uhusiano wa mtu binafsi, humstarehesha na kumwezesha mtu huyu kuwasilisha hisia zake Na kama tambiko, muziki huendeleza uhusiano wa kimazingiia - kwa kuwahusisha wanadamu na viumbe vingine vinavyopatikana katika mazingiia hayo.

Katika kuangalia upande wa kijamii, Akuno anaona muziki kama chombo ambacho hutumiwa kuelezea histmia ya jamii,
hutumiwa kupasha 11iumbe maalum kwa wanajru:nii hasa kutoka kizazi kimoja hadi kingine na hutumiwa hasa kuelezea
histmia, imani, itikadi na kaida zajamii. Nyimbo ni zao la mazingiia ya jamii. Zinaweza kufananishwa na mtoto ambaye
hufinyangwa na mambo mengi katika historia ya jamii yake. Hii inamaanisha kwamba muziki hauibuki katika ombwe tupu na hauwezi vilevile kujiundia mazingira yazo yenyewe. Mabadiliko na maendeleo ya muziki yamekuwa yakifuatana na historia ya watu wenyewe. Nyimbo huathiriwa sana na mambo yanayotendeka ulimwenguni.

Umuhimu wa muziki unadhihirika katika matumizi ya nyimbo katika wakati maalum kama njia mojawapo ya kuanzisha mabadiliko katika tabia za jamii au mtu binafsi, (McAI!ester 1971). Muziki umetumika kama njia mojawapo ya kujifundisha utamaduni na aghalabu hutumiwa katika kuelezea mtu mazingira yake na jinsi anavyoweza kuyatumia na kuyatunza vilivyo Nyirnbo vi1evile
zimekuja kuchukuliwa kama chanzo cha elimu na jinsi ya kujieleza katika jamii na hasa katika sana ya ma.zllngumzo Nyimbo
humfanya mtu kumbukumbu ya vitu au tukio kwa urahisi na kumbukumbu hiyo huweza kudumu kwa muda mrefu sana.
Kwa mfano, masomo shuleni hufanikishwa kupitia nyimbo

Muziki ulioimbwa kwa Kiswahili ni sehemu muhimu sana zirrazojenga utamaduni wa Wakenya. Kwa Wakenya wengi muziki ni neno linaloeleweka kwa wananchi wengi kwa sababu watu hao huwa na upenzi wa muziki Kuhusu muziki ni nini, tunaweza kusema ni taaluma maalum ya sauti inayochanganya kwa usahihi sanaa na sayansi. Muziki ni sanaa katika matokeo na utendaji wake
na ni sayansi katika maandalizi yake na utendaji, (Sekella, 1995).

Wanamuziki wa Kenya wamegawanyika katika makundi mbalimbali:- Watendaji wa muziki wa bendi, kwaya, taarabu na watendaji wa muziki wa kiasili. Karibu kila kundi hutumia lugha ya Kiswahili linapokuwa na ujumbe maalum kwa wananchi. Muziki wa
kiasili nao huweza kugeuzwa maneno ya lugha ya kiasili ya wimbo unaohusika hadi katika lugha ya kiswahili ili ujumbe wake
uweze kueleweka kwa wasikilizaji wengi.

Kenya irnepitia hatua mbalirnbali ya mabadiliko. Hatua hizi zimeathiri nyimbo kwa njia tofauti tofauti. Tunacho kipindi kabla ya wageni au wakoloni. Huu ndio wakati ambapo nyimbo zilizoimbwa zilikuwa nyimbo za kikabila Wanajamii, kulingana na
lugha zao za mama walibuni nyimbo zao. Kipindi cha pili ni cha maajilio ya wazungu. Hiki ni kipindi ambacho mwafrika alidhalilishwa na mzungu. Hii ilikuwa dhuluma ambayo ilivuka mipaka ya uchumi na siasa ikafikia hadi kwenye hali ya kumteka mwafrika kimawazo asiweze kuonea nyimbo zake fahari. Hapa ndipo mwafrika alipojiona kwamba yeye hakuwa na uwezo wa kufanya chochote na hata nyimbo zake hazikuwa na maana yoyote. Kipindi hiki kilishuhudia nyimbo za kutoka nje na ambazo zilianza kuonewa fahari. Watu walianza kwenda katika majumba ya starehe ili kucheza densi. Lugha iliyopendelewa sana ilikuwa ni Kingereza. 

Hata hivyo nyimbo hizi hazikuwafikia watu wengi kwa sababu idadi ya watu waliokifahamu Kingereza ilikuwa ndogo nmo.
Hata hivyo, waimbaji wachache waliendelea kutumia lugha ya Kiswahili katika muziki wao. Waimbaji kama vile Fadhili William,
Daudi Kabaka, John Mwale na wengineo ni baadhi ya wanamuziki ambao bado wanasifika sana katika kuimba kwa Kiswahili..
Hawa ndio watu waliosaidia kufanikisha lugha ya Kiswahili katika miaka ya sitini, na nyimbo zao zikajulikana kama nyimbo
"zilizopendwa" hadi wa sasa. Hivi sasa kuna bendi nyingi zinazoimba kwa Kiswahili, hizi ni pamoja na "Them Mushrooms", Princess Jully", Munishi na nyingine nyingi ambazo zinapendwa na idadi kubwa ya watu. Wananchi, kwa bahati nzuri hupendelea muziki wenye ujumbe na hasa ujumbe ulio katika lugha wanayoielewa ya Kiswahili. Na nyingi ya bendi hizi hutimiza
wajibu huu.

Sanaa ya uimbaji inaonesha uwezo wa binadamu wa kusimulia au kupasha tajriba yake na ya jamii ya kila siku na kujaribu
kuleta maana katika maisha ya kila siku. Mambo haya hufanyika kwa njia ya ukawaida mno - kupitia kwenye nyimbo zilizopendwa. Nyimbo hizi huweza hata kuundwa upya na wananchi wenyewe kwa sababu mbalimbali.

Kama asemavyo Campbell (1976) nyimbo zimeundwa kru:na sanaa nyingine ili kunasa makini yetu. Sanaa hii basi ina ule ukale, uleo na hata ukesho. Kupitia nyimbo zilizopendwa, wanamuziki wa Kiswahili wanaweza kuangalia 'usasa' au dunia ya leo hapo
baadaye, usasa huu utakuwa kama ukale utakao tuelekeza kufahru:nu histmia yetu ya wakati huo. 'Usasa' huu unaweza
kutusaidia katika kutab:iii ukesho na kujua nru:nna ya kukabiliana na ulimwengu ujao.

Muziki umetumiwa katika kupinga ukandamizwaji na uonevu katika jamii. Hapa ni pale ru:nbapo mwanamuziki anaangalia mambo ya kisiasa. Jambo hili lilidhihirika wakati wa ukoloni ambapo mwafrika alitumia nyimbo kama silaha kupigania uhuru. Muziki ulitumiwa kuwahimiza watu. wapinge tamaduni za wakandamizaji. Waafrika walifanya hivi kwa kuchukua nyimbo za kisiasa na kuzipa mahadhi ya kidini ambapo kwa hakika maana ilikuwa tofauti na ile ya kidini Hivi sasa wanamuziki wa nyimbo zilizopendwa wanaimba nyimbo zinazowaelimisha na kuwahamasisha watu ili watekeleze kwa ufanisi sera na maagizo mbalimbali ya chama kinachotawala na serikali kwa jumla. 

Nyimbo nyingi zinazosikika redioni zinahusu kuwahimiza watu kuwa na uwajibikaji, kilimo cha kisasa, uzazi wa mpango, vita dhidi ya Ukimwi, kuchagua viongozi bora na kufanya kazi kwa bidii. Lugha ya Kiswahili imetumika kuimba nyimbo zenye ushauri kuhusu maisha, mapenzi, tabia nzuri na mbaya, ukulima bora na kadhalika Muziki hasa muziki wa 'zilizopendwa' ni sanaa ambayo huwafikia watu wengi kupitia vyombo vya habari hasa redio na hata
televisheni. Kwa hivyo hii ni sanaa ambayo haiwezi kupuuzwa kutokana na majukumu mbalimbali inayotekeleza. Vyombo
vya habari vimetenga masaa kadhaa ya kuwaburudisha watu kwa kutumia nyimbo mbalimbali. Balisidya (1987) anakubali
kuwa sanaa hii ni sehernu mojawapo ya fasihi ya Kiswahili na inahitaji kufanyiwa uchunguza zaidi, kwa jinsi ambavyo watu
wengi wanaweza kuipata.

Nyimbo za kisasa zinaweza kutupa mwangaza kuhusu maisha ya watu duniani.. Finnegan (1970), anasema kuwa nyimbo-pendwa zina majukumu mbalimbali ya kutekeleza hasa katika kuangalia mitazamo ya jamii kiulimwengu, na nyimbo hizi
hutekeleza majukumu haya kama zilivyo nyimbo za kijadi Mtazamo huu umeungwa rnkono na watu kama vile Kabira na
Mutahi (1988), Agovi (1989), na wengine wengi ambao wanaona muziki kuwa utanzu teule inayodhihirika katika jamii hii
inayobadilika. Nyimbo pendwa zimechukuliwa na wasomi wengi kuwa kama muingiliano wa masimulizi jadi na ukweli wa
maisha ya hivi sasa, Nyimbo hizi hushughulikia mambo kama vile ukandamizwaji, kutamauka maishani, unyimwaji wa haki
na umaskini/ubinafsi. Mambo haya ni mambo ya kisasa na huathili wanajamii kwa njia mbalimbali.

Waimbaji wa nyimbo zilizopendwa hushughulikia nyanja tofauti za maisha ya jarnii kama vile dini, uchumi na siasa. Kwa
mfano, wao wanashughulikia ndoa na mapenzi kwa kuonesha mahusiano ya jamii na migongano ya kimawazo baina
ya wazee na vijana au baina ya rnke na mume. Katika nyakati hizi za mabadiliko katika uchumi na siasa waimbaji wamekuwa
wakitunga nyimbo kwa kutuchorea picha ya jinsi mambo yalivyo. Wamekuwa katika mstari wa mbele katika kuwatahadharisha wanajamii kuhusu ugonjwa wa Ukimwi

Muziki uliopendwa katika Kiswahili ni sanaa isiyo kuwa na mipaka ya ukabila. Ni sanaa ambayo huwaunganisha watu wa
makabila mbalimbali kwa kutumia lugha inayoeleweka na kuzungumzia tajriba sawa wanazozifahamu. Nyimbo hizi pia
zimetumika kuimulika jamii kwa kuonesha maendeleo yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali Anapoikosoa jamii, mwimbaji huwa anachukuwa jukumu la kuhakiki jamii na hata kuielekeza. Nyimbo hizi pia zinatumiwa kuwazindua watu waweze kufahamu haki zao hasa pale wanaponyimwa, zinatumiwa kama ajenti wa ukombozi.

Katika nyimbo hizi, pia kuna ufasihi hasa upande wa lugha. Sifa moja ambayo hubanisha nyimbo ni matmnizi yake ya lugha hasa zile tamathali za usemi kama vile tashbihi, methali, semi, jazanda taashira na majina ya majazi. Tamathali hizo zinazotumiwa na
nyimbo huwa ama zimebuniwa katika jamii ya mwimbaji au zimebuniwa na mwimbaji mwenyewe lakini akazingatia kanuni za
uundaji wake. Hii inafanya tanzu hii iweze kuchunguzwa kwa makini kiusomi kwa kuchanganua ufani wake kupitia lugha iliyotumika. Hata hivyo, waimbaji wa nyimbo-pendwa wamekumbana na vizingiti vingi. Kutokana na sababu kuwa wao ni wahakiki wa jamii, baadhi ya nyimbo zao zimepigwa marufuku, (mwangi 1992) na hivyo basi haziwafikii watu wengi waliolengwa na haziwezi kutumiwa kama njia ya kuwazindua watu. Katika kule kuihaki jamii, wao-hulenga kuikosa, lakini mara nyingi wao huwa hawaafikiani na viongozi kuhusiana na maongozi yao.

Hitimisho

Nyimbo zinazoimbwa kwa lugha ya Kiswahili huwafikia watu wengi kutokana na sababu kuwa lugha ya Kiswahili ni lugha ya
walio wengi. Nyimbo zilizopendwa zitaendelea kukua kufuatana na mabadiliko ya kihistoria na kifani ambayo yanasababishwa
na watu wengi. Hivyo basi, nyimbo hizi hazina budi kuchukuliwa kama sehemu moja ya Fasihi ya Kiswahili kwa kuangalia mchango wake kimaudhui na kifani. Na zinahitaji kusambazwa ili ziwafikie wanajamii wote. Hii ina maanisha kuwa vyombo
vya habari vina majukumu ya kutekeleza katika kuhakikisha kwamba watu wengi wameweza kuzipata nyimbo hizi. Kwa
upande wa fasihi, haya ni mafanikio makubwa hasa kwa sababu tabia ya kupenda kusoma haijakomaa kwa wengi.

Vyombo vya habari vinatumika kusambaza fasihi hii kwa mamilioni ya watu. Hii ni kutokana na sababu kuwa kundi moja tu la waimbaji linaweza kufundisha idadi kubwa ya watu kwa wakati mmoja kupitia nyimbo zao



Mwandishi: PAMELA M. Y NGUGI


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni