Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Februari 14, 2014

MPIGAJI MZURI WA PIANO


Eldar Nebolsin wa nchi ya Uzbekistani ni mpigaji wa piano mwenye kujulikana katika mataifa mengi. Alicheza piano katika vikundi vya wanamuziki huko Londres, Moscow, Saint Petersburg, New York, Paris, Roma, Sydney, Tokyo, na Vienna.

Eldar alikulia katika Muungano wa Kisovieti na hakuamini kwamba kuna Mungu. Lakini baadaye alikubali kwamba wanadamu waliumbwa na Muumbaji mwenye upendo.

KISA CHA AJABU...

Sikuzote nyumba yetu ilijaa vitabu ambavyo baba yangu alinunua katika mji wa Moscow. Kuna kitabu ambacho kilinivutia sana ni kitabu kilichokuwa na habari za Mungu. Biblia ilieleza kuhusu mwanzo wa mwanadamu na mambo ambayo yaliwapata Waisraeli.

Nilipohamia Hispania katika mwaka wa 1991 ili kujifunza muziki, nilibeba kitabu hicho na nikakisoma mara nyingi. Nilivumbua imani ambayo haitegemei tu namna mtu anavyojisikia moyoni lakini pia mambo yenye kupatana na akili na yenye nguvu ya kiroho.

Fundisho ambalo lilinivutia kabisa ni ahadi ya Biblia kwamba wanadamu wanaweza kuishi milele. Fundisho hilo lilikuwa lenye kueleweka bayana kabisa!

USHAURI WAKE...

Biblia ni kama muziki mzuri sana wa PIANO wenye mpangilio wa ajabu, na ina ujumbe wenye kuchochea kwa ajili ya wanadamu wote.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni