Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Februari 12, 2013

TEKNOHAMA - KOMPYUTA INAFANYAJE KAZI?


Picha kwa hisani ya: http://www.macwallpapers.eu



Unaweza ukawa unajiuliza, ni vipi sasa kompyuta inafanya kazi kama ina sakiti ambazo zinaweza kufikia milioni kumi? Je si kifaa kilicho tata sana?

Kwa ujumla kompyuta haifanyi kazi vigumu kiasi hicho kama unavyoweza kudhani. Sakiti hizo zinaisaidia kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja na kwa haraka sana na ndiyo matarajio ya binadamu; kwamba ifanye kazi kwa haraka sana ili kufanya uzalishaji mali kuwa mkubwa. Maelekezo ambayo kompyuta inatoa na kufanya (baada ya kupewa na binadamu) ni rahisi kabisa: jumlisha namba moja na nyingine, toa data kutoka sehemu moja kupeleka sehemu nyingine, peleka habari kutoka kifaa kimoja kwenda kifaa kingine, punguza jotoridi la kifaa fulani endapo jotoridi hilo litazidi kiwango kilichowekwa na kadhalika. Maelekezo haya hufanyika Kwa haraka Sana kiasi kwamba unapata majibu unayoyataka papo kea papo!

Ni jambo moja tu ambalo linaifanya kompyuta kuwa tofauti Na mashine nyingine katika dunia hii: jambo hili Ni kwamba kompyuta inaweza kupangiliwa kufanya mambo kutokana na matakwa ya mtumiaji (can be programmed). Hii inamaanisha kuwa mpangilio wa maelekezo (a list of instructions) ambayo ndiyo huitwa programu ya kompyuta (computer program) huweza kuingizwa katika kompyuta na kuhifadhiwa na kuyatumia baadaye kulingana na matakwa ya mtumiaji. Ndiyo maana ukitaka kuandika barua katika kompyuta unafungua program inayohusika na kuanza kuandika barua hiyo. Ukimaliza unaifunga program hiyo na siku nyingine au mtu mwingine anaweza kuitumia.

Kuna aina kuu NNE za Kompyuta

Kompyuta hutofautiana Sana kulingana na kazi inayopaswa kufanya. Kompyuta inayotumika katika lift za majengo si sawa na kompyuta inayotumika katika mahospitali kusaidia kutibu wagonjwa. Kulingana na matumizi husika, kompyuta hutofautiana ukubwa, bei, uwezo wa kufanya kazi na hata uendeshwaji wake.

Aina ya kwanza ya Kompyuta

Kompyuta aina ya kwanza ni zile ambazo mara nyingi watu wa kawaida huzimiliki majumbani na maofisini na ndizo zilizo za bei ya chini, uwezo mdogo na umbo dogo zaidi kuliko aina nyingine ya kompyuta. Kompyuta hizi hujulikana kama personal computers au PC kwa kifupi. Ukitazama Kwa undani zaidi utagundua kuwa kompyuta hizi ni maalum kwa ajili ya matumizi binafsi ya mtu au kwa ajili ya kuendeshea mitambo midogo midogo kwa faida ya maisha ya kila siku ya binadamu. Kompyuta hizi hupatikana katika maumbo mbalimbali. Zipo desktop Na tower computers ambazo hupatikana mara nyingi maofisini katika meza; notebook computers ambayo hujulikana Sana Kama laptops; zipo palm tops (kompyuta za viganjani ambazo hujulikana Sana Kama PDA-Personal Digita Assistant). Hizi ndizo kompyuta ambazo mara nyingi tunaziona katika maduka na supermarkets zinazouza kompyuta. Tutakuwa Na sehemu kubwa ya kutazama juu ya kompyuta aina hii huko mbele Kwa sababu ndizo zinazotumika Na kuonekana zaidi Kwa sasa mionogni mwa watu wa kawaida.

Aina ya pili ya Kompyuta

ina ya pili ya kompyuta inajulikana kama miniframe computers. Aina hii ya kompyuta ina uwezo, na ukubwa zaidi ya aina ya kwanza na ni ghali zaidi. Ni kompyuta ambazo zimetengenezwa maalum Kwa ajili ya kufanyia kazi zinazohitaji nguvu kubwa na za haraka zaidi. Mitambo mingi ya kuendeshea mawasiliano ya habari katika majengo makubwa huendeshwa Kwa kutumia kompyuta hizi.

Aina ya tatu ya Kompyuta

Aina ya tatu ya kompyuta ni zile zijulikanazo kama Mainframe computers. Hizi ni kompyuta zenye uwezo mkubwa na zinazogharimu fedha nyingi. Hutumika katika utafiti katika maabara za kisayansi katika sehemu maalum hasa katika taasisi za utaiti na katika vyuo vikuu. Pia katika kuendesha mitambo ya kutafiti maswala ya hali ya hewa (weather forecast). Kwa mfano, pale mamlaka ya hali ya hewa Tanzania (TMA) makao makuu unaweza kukuta kompyuta ya namna hii.

Aina ya NNE ya Kompyuta

ina ya nne na ya mwisho ya kompyuta ni ile iitwayo super-computers. Hizi ni kompyuta ambazo ni kubwa na zenye nguvu sana na ambazo huweza kugharimu mamilion ya dolla. Ni kompyuta hizi ambazo hutumika katika kuendesha mitambo ya kinyukilia (nuclear control) na urushaji wa maroket katika kufanya utafiti katika sayari za mbali (space exploration). Hizi kompyuta zinahitaji watu wenye utaalam wa juu katika kuziendesha na kuzifanyia marekebisho.
Kompyuta aina ya Supercomputer

Kompyuta aina ya Notebook ama Laptop

Kompyuta aina ya notebook ni kama gari dogo la kuendeshea mambo nyumbani. Kila kitu kuanzia muonekano wa nje yaani hardware, mpaka katika matumizi ya nishati ya umeme kuendeshea programs ni madogo. Kwa namna hii wataalam wa masuala ya umeme katika kompyuta ya aina hii wamefanya kazi kubwa ya kupunguza matumizi ya umeme na mahitaji ya ukubwa katika sehemu zote za kompyuta hii. Ukubwa wa kompyuta hii pamoja na matumizi ya umeme yanapunguzwa kadiri inavyowezekana. Kwa mfano hard disks za notebook computer ni ndogo kuliko hard disks za desktop computers na zinaweza kupachikwa katika upande mmoja wa system unit au kuwekwa katika sehemu ya chini ya system unit.


Katika nyakati hizi CPUs za notebook computer zijulikanazo Kama Mobile CPUs zina muundo maalum unaozitofautisha na zile za zamani. Mobile CPU Ni aina maalum ya CPU kwa kompyuta aina ya Notebook ama Laptop ambayo hubadilisha mwendokasi (wa kufafanua maelekezo) na hivyo matumizi ya umeme kwa kadiri ya kupungua au kuongezeka kwa mahitaji ya kufafanua (exection of instructions) maelekezo hayo. Kwa mfano CPU ya desktop kompyuta yenye uwezo wa kufafanua maelekezo katika mwendokasi wa 1 GH (CPU speed) inatumia kati ya wati (watts) 75 mpaka 100 za umeme ilihali CPU aina ya Mobile ya Notebook kompyuta kwa mfano SpeedStep
CPU ambayo hutumia kiwango cha wati 34 za umeme wakati notebook kompyuta hii imechomekwa katika waya ya kuingizia umeme. Hii husababisha kupunguka Kwa umeme ambao CPU huhitaji na hivyo kusababisha kuzalishwa kwa kiwango kidogo cha joto ambalo husababisha feni ya kupoza joto hilo kutumia umeme mdogo.

Feni ya CPU ya notebook kompyuta huwa haifanyi kazi muda wote Kama ilivyo Kwa feni za kompyuta za aina nyingine. Feni hufanya kazi pale tu joto linapokuwa limezidi kiwango Fulani. Kumbuka kwamba Notebook kompyuta huwa Na Betri inayoweza kutunza umeme Na hivyo kukuwezesha wewe kuitumia bila kuichomeka kwenye soketi ya umeme. Ni Kama unavyoweza kuingiza umeme kwenye simu ya mkononi Na inapokuwa umejaa unaenda zako ukitumia Na unapokuwa umekwisha unarudi Na kujaza tena.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni