Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Machi 19, 2012

Tanzania bila umasikini...Sura ya 2.


Kijitabu kinachoelezea kwa Lugha rahisi Mkakati wa Kupunguza Umasikini

 

 Tutapunguzaje Umasikini?

Mpango Mzima

Baada ya kuzungumza na watu wa kawaida na mabingwa mbalimbali; Serikali imeamua kwamba mambo matatu lazima yafanyike kama tutakuwa makini katika kupunguza umasikini.

Kuweka malengo ya kitaifa yaliyo wazi:


bullet· Badala ya kuwa na hotuba nyingi zenye nia nzuri lakini utakelezaji wake ni duni, Serikali imeamua kuweka malengo yanayoeleza yanayopaswa kutendwa. Kwa mfano, kuongeza idadi ya watoto waliochanjwa dhidi ya surua wenye umri chini ya miaka miwili na kupata chanjo ya Donda Koo, Kifaduro na Pepo Punda (DPT) toka asilimia 71% hadi kufikia 85% mwaka 2003.
bullet· Jozi ya kwanza ya malengo inawezekana isiwe sahihi. Kwa hiyo kila mmoja anapaswa kuzingatia kwa makini yanayotokea na asaidie kubadili malengo au namna ya kuyatekeleza. Matendo mengi hayawezi kutekelezeka hadi mipango ya mabadiliko ya serikali za Mitaa imetekelezeka.

Kubuni Mazingira ya Kiuchumi ya Kitaifa ambayo yatachochea Maendeleo

bulletMazingira hayo yatasaidie nchi ikue kiuchumi kwa kuimarisha masoko ya biashara ndogo na kubwa. Yataimarisha kaya zinazojishughulisha na kilimo, viwanda na viwanda vitoavyo huduma.
“Kama hujui uendako barabara yoyote itakufikisha”
[Methali ya Kiarabu]
bulletKufanya kazi pamoja na Serikali za nje na mashirika ya kimataifa
bulletkutapunguza mikopo ya nje ambayo inapaswa kulipwa.
bulletkuhakikisha kuwa wanafanya kazi pamoja katika kutusaidia tutekeleze malengo yetu.
panya-6.jpg (21103 bytes)

Zingatia mwongozo wa mawazo matatu:

Watu wengi walihusishwa katika kutayarisha makala ya Njia za Upunguzaji Umasikini. Katika siku zijazo serikali itawahusisha watu wengi zaidi katika maamuzi ya yanayopaswa kufanywa, katika kutenda, na katika kuhakikisha kuwa yaliyoamuliwa yanatekelezwa kwa kuzingatia mipango ya awali.
Kila jambo ambalo lipo katika mpango wa kupunguza umasikini linaongozwa na mawazo matatu yafuatayo:
bulletkupunguza umasikini wa kipato
bulletkuendeleza ubora wa maisha na ustawi wa jamii
bulletkupunguza dhiki za makundi ya umasikini
Je, tunawezaje kusimamia kwa ukamilifu zaidi na kuona kuwa tunatekeleza tuliyokusudia?

Haja ya kuwa na Viashirio

Tunapaswa kufahamu kuwa fedha zetu zinatumika vyema. Maana yake ni kuwa inabidi tuwe na hakika na kile tunachotaka kufanya. Aidha, tunapaswa kuangalia kama tunafaulu katika yale tunayoyafanya.
Awali tuliona kuwa malengo yaliwekwa kwa ajili ya matendo mbalimbali ya kupunguza umasikini. Kwa kila tendo tunapaswa kuwa na dalili (viashirio) zinazotuwezesha kupima kama tunatekeleza malengo yetu au hapana. Serikali imeweka njia za ushauri ili kuonyesha dalili za umasikini zinakuwaje.

Viashirio (dalili) vya aina tatu

Si rahisi kuamua mapema ni dalili zipi bora na rahisi za kutumia. Kuna aina mbalimbali zilizo katika mfumo wa kubuni viashirio. Kimsingi, kuna aina tatu za viashirio:

Dalili za athari na matokeo

Ni za msingi na zinaweza kupima kwa urahisi uthabiti wa matendo ya mara kwa mara (kwa mfano idadi ya watoto chini ya miaka miwili ambao wamechanjwa dhidi ya surua kila mwezi).

Dalili za kati

Zinapimwa katika kipindi cha muda mrefu. (Kwa mfano, idadi ya familia ambazo zinapata maji safi na salama) ·

Dalili za uwakilishi

Hupima vitu vya nje vinavyowakilisha vitu vya msingi ambavyo si rahisi kupimwa (kwa mfano, matumizi ya vifaa vya kisasa vya ujenzi wa nyumba kama njia ya mapato).
panya-7.jpg (20239 bytes)
Shabaha ni kufikiria njia rahisi na viashirio bora kwa kila malengo yaliyowekwa katika mpango. Orodha ya viashirio ambazo zimebainishwa hadi sasa zinaonyeshwa katika sura inayofuata. Zingatia kuwa ikilazimika na ikiwezekana, maelezo yaliyotolewa kwa kuzingatia viashirio yatueleze tofauti kati ya wanaume na wanawake na kati ya maeneo ya vijijini na mijini.

Kujenga Mfumo wa Usimamizi na Tathmini

Muda mwingi, nguvu na fedha vinaweza kupotea kama mfumo wa ukusanyaji taarifa utakuwa mgumu na wenye urasimu. Kazi ni kuwa watu wote wanaohusika kufikiria viashirio bora ambavyo vinaweza kupimwa mara kwa mara na kwa urahisi.
Taarifa zinaweza kukusanywa kuhusu watu binafsi, kaya, wilaya, mikoa au nchi nzima. Ukusanyaji huu unaweza kuwa wa mara kwa mara au wa kufanya mara moja. Unaweza pia kufanywa baada ya kila miaka kadhaa.
“Bila kuwa na takwimu nchi haiwezi kupanga na kusimamia maendeleo yake kikamilifu. Maamuzi yaliyotokana na taarifa potofu huharibu rasilimali adimu, hasa zile zinazowaathiri watu masikini ambao hawana uwezo wa kumudu maisha.”
[Clare Short]
Kuna njia tatu za kukusanya taarifa:
bulletTaarifa kuhusu elimu, afya na maji zinaweza kukusanywa kupitia mfumo wa utawala uliopo. Serikali za mitaa hutuma taarifa kwa ngazi ya juu ya serikali.
bulletTaarifa nyingine zitakusanywa kwa sensa au kwa ukaguzi kama vile ukaguzi wa bajeti za kaya au ukaguzi wa nguvukazi. Zinaweza kuelezea mada nyingi. ·
bulletTaarifa za kiwango cha serikali za vijiji zinaweza kukusanywa kwa ajili ya matumizi katika kiwango cha kijiji. Taarifa hizi zinaweza kukusanywa kwa kutumia rejista za vijiji na kuhoji wanajumuia. Ingawa taarifa za vijiji zitatumiwa katika kiwango cha serikali za vijiji, lakini data hizo zinaweza pia kutumiwa kwa kulinganisha na takwimu za kiserikali. Njia hii itawawezesha viongozi kujua jinsi watu, hasa watu masikini, wanavyoona hali zao.
Sababu za kukusanya taarifa ni kuzitumia ili kupata picha halisi ya jinsi ambavyo njia za upunguzaji wa umasikini zinavyotekelezwa. Itakuwa lazima kwa washika dau wote kubadili viashirio, shughuli, malengo na hata sera ambazo zinaongoza mbinu zote.
Mashirika mengi yatahusishwa katika ukusanyaji na ufafanuzi wa taarifa na pia kuelezea taarifa hizo zina maana gani katika utungaji sera kwa siku zijazo.
Takwimu ni macho ya wapanga sera.
[Keith Muhakanizi]
Majukumu ya usimamizi dhidi ya umasikini yako chini ya ofisi ya Makamu wa Rais. Ofisi hii itafanya kazi kwa ukaribu zaidi na Kitengo cha Kitaifa cha Takwimu ili kuziingiza taarifa katika kompyuta. Kompyuta hizi zinaweka takwimu katika benki ya data za kiuchumi. Data hizi zinaweza kutumiwa na mtu yeyote ambaye anataka kushirikishwa na anayetaka kuzichambua. Hali hii inafanya taarifa ziwe zimeratibiwa kikamilifu.
Kwa hiyo, ni lazima tuwe tayari kukabili changamoto hii. Bado kuna udhaifu mwingi katika kusimamia shughuli za kuondosha umasikini. Mkakati wa umasikini (PRSP) ni nafasi nzuri ya kujenga mfumo bora na madhubuti. Kama ilivyotajwa katika mkakati huo (PRSP), “Serikali inakusudia kutafuta uwakilisho wa watu masikini na washika dau wengineo katika utekelezaji, uangalizi na kufanya tathmini ya mbinu za kupunguza umasikini na baadaye Kubadili Mbinu zitumikazo”


Habari hii nimeipata...HAPA

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni