Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Machi 20, 2012

Tanzania Bila Umaskini...Sura ya 3(A-C) - 5



 

Malengo, shughuli na Viashirio

Inasemekana kuwa “kama hujui uendako basi barabara yoyote itakufikisha”. Watu ambao hutekeleza mambo wanayoyataka wana mwelekeo sahihi wa kitu wanachotaka kufanya, watakifanya vipi, na hasa, jinsi watakavyofahamu kuwa wamefaulu.
Lile lililo kweli kwa mtu binafsi ndilo lililo kweli kwa jamii, katika nyanja mbalimbali na kwa serikali. Kama uko makini kutenda jambo basi lazima uwe wazi kuhusu malengo, shughuli na viashirio.
MALENGO Wazo lililo wazi kwa lile unalotaka kulifanya litakusaidia kuamua utalitekeleza kwa kiwango gani na muda wa kukamilika.
SHUGHULI Wazo lililo wazi kuhusu shughuli utakayotekeleza litakusaidia kuorodhesha hatua mbali mbali za kufuata
VIASHIRIO (DALILI) Wazo lililo wazi kuhusu utakachopima litakusaidia kujua shughuli zinazotekelezwa zinafikia lengo au kuvuka.
Sehemu hii inaorodhesha malengo, shughuli na viashirio ambavyo vimebainishwa kwa mawazo yanayoongoza katika Mkakati wa Kuondoa Umasikini (PRSP) ambazo ni:
bulletKupunguza umasikini wa mapato
bulletKuendeleza ubora wa maisha na ustawi wa jamii
bulletKupunguza madhara yanayoweza kuwapata watu masikini
Kwa ujumla njia ya kupunguza umasikini wa mapato ni kuziwezesha shughuli za kuzalisha mapato ya aina mbalimbali zistawi ili pawe na kazi nyingi zaidi na fedha nyingi ziwepo kwenye mzunguko. Njia ya kuendeleza ubora wa maisha na ustawi wa jamii ni kuhakikisha kuwa watu wote wanapata nafasi sawa ya kupata elimu, afya bora, maji salama na chakula bora. Njia ya kwanza ya kupunguza madhara ni kuainisha watu ambao wako katika hali mbaya na kugundua matakwa yao ni yapi na kuweka bayana malengo, shughuli na viashirio.
Kupunguza Umasikini wa Kipato
Kama nchi kwa ujumla ingekuwa tajiri zaidi basi panatakiwa pawe na umasikini mdogo. Kwa hiyo inabidi tuifanye nchi iwe tajiri zaidi na tuhakikishe kuwa utajiri huo unagawanywa sawasawa na kwa haki. Aidha, makundi ya watu dhaifu wanaoathirika na mabadiliko ya hali ya kiuchumi walindwe kwa utaratibu wa tofauti.
Mpango wa miaka mitatu ijayo ni kuongeza mapato zaidi kutokana na sekta za kilimo, na viwanda na huduma.
Mpango huu utawezekana kwa sababu ya mabadiliko yanayofanywa na serikali ya kuweka mazingira bora na uchumi imara.
Tukichukulia kuwa uchumi mpya unawafikia watu masikini zaidi basi tutakuwa tumepiga hatua ya kupunguza umasikini.
Malengo
  Hadi 2003 Hadi 2010
Kupunguza sehemu ya idadi ya watu fukara Toka 48-42% Toka 48-24%
Kupunguza idadi ya watu masikini wa vijijini Hadi kufikia 7.5% Toka 57-29%
Kupunguza idadi ya watu masikini wa chakula Hadi kufikia 3.5%   Toka 27-14%
Shughuli
Shughuli ambazo ziatapunguza umasikini wa mapato zinaelezwa katika kurasa zifuatazo:
bulletKukuza maendeleo vijijini na kukua kwa biashara ya nje
bulletKusaidia kukuza sekta binafsi
bulletKufanya kazi kwa ajili ya kuboresha na kutoa madaraka zaidi ya serikali
bulletKuhakikisha kuwa uchumi unaimarika
Viashirio
bullet· Kupungua kwa umasikini wa chakula
bullet· Kupungua kwa umasikini wa mahitaji muhimu
bullet· Kupata na kumiliki vifaa kama redio, jokofu (friji), televisheni, n.k.
bullet· Kupata na kutumia vifaa vya kisasa katika ujenzi wa nyumba.
Maendeleo Vijijini na Ukuaji wa Biashara ya nje
Tanzania ina historia ndefu ya maendeleo vijijini. Juhudi za mwanzo zilidhibitiwa na taifa na kusaidiwa na mfumo mzima wa serikali kwa wazalishaji wa vijijini. Baadaye juhudi zilitawaliwa na nguvu za soko huria, huku serikali ikijiondoa polepole. Njia iliyo bora zaidi haijaeleweka. Katika miaka mitatu ijayo Serikali itamwomba kila mmoja kufanya kazi kwa ushirikiano ili kutafuta ufumbuzi na kuendeleza Mbinu za Maendeleo Vijijini.
Watu masikini na wafanya biashara binafsi wataombwa kuwa mstari wa mbele katika kutafuta njia mpya za kufaa na madhubuti.
Malengo na Shughuli
bulletMikopo itatokana na kwa wanunuzi wa mazao, benki na vyama vya ushirika badala ya kutoka serikalini
bulletWakulima watajisimamia wenyewe katika makundi au vyama vya ushirika ili kurahisisha kupata mikopo toka katika taasisi za fedha
bulletWakulima watashirikishwa kufanya utafiti wa mazao na shughuli nyinginezo ili kuongeza wingi na ubora wa mazao
bulletWanunuzi binafsi wa mazao wataendelea kutumia mpango wa vocha na mipango mingine ili kurahisisha ununuzi wa mbolea na dawa za kuulia wadudu
bulletJamii zitajishighulisha zaidi katika ujenzi na ukarabati wa barabara za vijijini na kuendeleza kilimo cha umwagiliaji maji (panapowezekana kwa msaada wa serikali)
Serikali itajishughulisha tu na kutengeneza sera za kuwasaidia wananchi wa vijijini kwa kutekeleza yafuatayo:
bulletKushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali, benki za ndani na Washirika wa Kimataifa katika kutoa mafunzo na mifumo mingine ya misaada kwa jumuiya na makundi kuhusu:
bulletUtaratibu wa stadi za uongozi na fedha
bulletKutengeneza na kukarabati barabara vijijini
bulletKuendeleza kilimo cha umwagiliaji
bulletKuweka mazingira yatakayoendeleza shughuli ndogo ndogo na za kati za biashara
bulletKuendeleza sekta isiyo rasmi
bulletkufanya utafiti unaotakiwa na kupanua huduma za mazao
bulletKuendeleza na kuboresha mazao ya kilimo hasa katika zao la korosho, pamba, kahawa n.k. kwa kutumia nguvu kazi iliyopo.
bulletKueleza mfumo wa uthibiti wa usafirishaji wa mazao ndani ya nchi na kati ya nchi na nchi
bulletKuhakikisha sheria ya ardhi inamsaidia kila mtu awe masikini au tajiri, mwanamke au mwanaume na kuhakikisha kuwa sheria nyingine zinazohusiana zinamwezesha mtu kuweka dhamana ya ardhi ili kupata mikopo.
bulletKuhakikisha kuna sehemu za nchi zilizo nyuma zinapata msaada wa ziada unaotakiwa.
panya-8.jpg (21026 bytes)
Serikali itasaidia mahali panapohusika katika kutoa mazungumzo endelevu, huduma za kilimo na kuwasaidia wawekezaji hodari. Malengo ya siku zijazo ni ongezeko la idadi na ubora wa mazao ya asili na ya sasa kwa ajili ya biashara ya nje.
Viashirio (dalili)
bulletKilomita nyingi za barabara zilizokarabatiwa
bulletOngezeko la thamani ya mazao ya kilimo
bulletUzalishaji wa msimu wa mazao ya chakula muhimu na mazao ya biashara
Uendelezaji wa Sekta Binafsi
Serikali imekuwa ikisaidia maendeleo ya biashara ya sekta binafsi tangu mwaka 1993 kwa kushughulika na:
bulletSheria ya uwekezaji Tanzania
bulletUbinafsishaji wa shughuli za biashara zilizomilikiwa na serikali
bulletUundaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC)
Hata hivyo, licha ya viwanda vya madini na Utalii, mwitikio wa Wawekezaji binafsi bado haujawa mzuri.
Malengo na Shughuli
bulletKujenga upya uwezo wa kituo cha Uwekezaji Tanzania ili kutilia mkazo ukuzaji wa uwekezaji
bulletKuwasilisha sheria mpya za makampuni Bungeni
bulletKuanzisha mfumo wa mafaili unaotumia kompyuta kwa ajili ya Mahakama
bulletKuwarahisishia wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi kuwekeza katika Tanzania (pamoja na kulindwa kikamilifu)
bulletKufanya mabadiliko ambayo yatapunguza gharama ya huduma za umma ikiwa ni pamoja na umeme katika viwanda
bulletKutekeleza kwa haraka mabadiliko muhimu ya Mbinu za Kuzuia Rushwa Kitaifa
Serikali pia itabuni Mkakati wa kuendeleza Sekta Binafsi ifikapo kwa mwaka 2003. Hii itasaida:
bulletKuendeleza uratibu mzuri kati ya serikali na michango ya Wafadhili
bulletKuweka mazingira bora yanayoimarisha biashara kubwa, ndogo, ya kati na isiyo rasmi
bulletKubadili mfumo wa kodi
Utawala Bora
Serikali nzuri ni ile ambayo inaweza kutoa huduma bora kwa wananchi wake wote kwa wakati wote. Pia ina utaratibu mzuri ambao unaiwezesha kukusanya fedha na kuzitumia kwa uwazi kwa manufaa ya wananchi wote. Kwa sababu ya matumizi ya fedha kuwa wazi na dhahiri Serikali ya aina hiyo itakuwa inawatumikia watu.
Shabaha zilizotolewa katika Mkakati wa Kuondoa Umasikini (PRSP) ni:
bulletKuendeleza utendaji kazi wa serikali katika kutoa huduma za jamii
bulletKuendeleza njia ambazo zinawapa motisha watendaji ili kuboresha kazi
“Viongozi wazuri wanapoondoka katika nafasi zao watu husema, “tulifanya sisi wenyewe””.
[Tao te Ching]
bulletKupunguza “upotevu wa fedha” na kuwa na njia ya kuwaadhibu wafanyakazi wabadhirifu.
Malengo:
bulletMfumo wa Serikali ambao ni madhubuti na unaofaa unawapa watu madaraka ya kujiamulia maendeleo yao
bulletKupunguza rushwa
bulletKustawisha ubingwa na matumizi bora ya fedha katika mfumo wa serikali
bulletKuimarisha uwezo wa utendaji kazi serikalini
bulletKuimarisha uongozi wa bajeti katika ngazi ya juu na ngazi ya chini serikalini
bulletKuunganisha Mfumo wa Taarifa za Utawala wa Fedha (IFMS) ulioundwa katika wizara zote na Hazina ndogo. Fedha zote ambazo zinatolewa katika ngazi ya wizara ya Fedha na Hazina ndogo zitapitia katika Mfumo wa Taarifa za Uongozi wa Fedha (IFM) na mipango yote ya matumizi na malipo ya nyuma yatawekwa katika kumbukumbu
panya-9.jpg (17372 bytes)
Viashirio (Dalili) Shughuli
Imarisha uaminifu na udhahiri katika uhasibu Imarisha mfumo madhubuti zaidi wa utawala wa fedha, udhibiti wa malipo na matumizi, orodha ya vifaa na rasilimali na ripoti za ukaguzi
Bajeti zitayarishwe kwa wakati katika ngazi zote  
Sekta muhimu ya utendaji kazi iliyoendelezwa na kuboreshwa  
Mipango iliyoendelezwa na kukubaliwa dhidi ya rushwa katika Wizara za Kilimo na Ushirika, Elimu na Utamaduni, Afya na Maji, ikilenga katika mbinu dhidi ya Rushwa Kitaifa Fanya ukaguzi wa Mbinu za utekelezaji zilizokubaliwa na timiza mipango dhidi ya rushwa katika Wizara za Sheria, Ujenzi, Elimu na Utamaduni, Afya, Mambo ya ndani, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, na Mamlaka ya Mapato Tanzania
  Tangaza Zabuni za Serikali katika vyombo vya Habari
Yaruhusu mashirika mbalimbali kutoa huduma za jamii Timiza majukumu chini ya Programu ya Mageuzi ya Sekta za Umma Timiza majukumu chini ya Programu ya mageuzi ya Sekta za Umma
Mfumo wa Taarifa za Utawala wa Fedha (IFM) utumike katika kutengeneza bajeti ya serikali, uhasibu na mfumo wa maelezo ya Fedha kwa ajili ya matumizi ya kawaidaBajeti ya maendeleo iliandaliwa kwa utaratibu wa GFS Panua mfumo wa Taarifa za Utawala wa Fedha kwa wizara zote, idara na wakala wa serikali Dar es Salaam na Hazina ndogo katika mikoa yote ifikapo 2002
Uchumi Mkuu Imara
Wakati uchumi imara unapokua, upandaji wa gharama za maisha unakuwa mdogo na serikali inakuwa na mlingano wa mahesabu. Serikali ya Tanzania ina rekodi nzuri ya kupunguza upandaji wa gharama za maisha na malengo kwa miaka mitatu ijayo yatajiegemeza katika hii njia.
panya-10.jpg (14223 bytes)
Malengo na Shughuli
bulletHarakisha ukuaji wa uchumi (GDP) hadi asilimia 6
bulletUpandaji wa gharama za maisha ubakie asilimia 4
bulletWeka akiba ya serikali katika kiwango cha miezi 4 ya bidhaa zinazotoka nchi za nje na huduma
bulletWeka mahesabu katika hali ya usawa (ongezeko la matumizi liwe dogo)
bulletPanua wigo wa kodi (na zuia ukwepaji wa ulipaji kodi)
bulletImarisha utawala wa mfumo wa kodi
bulletEndeleza uwezo wa mameneja wa Fedha katika ngazi ya Taifa na mitaa
Viashirio (Dalili)
bulletUkuaji wa jumla wa uchumi wa Tanzania
bulletKiasi cha upandaji wa gharama za maisha
bulletJumla ya rasilimali ya akiba ya kimataifa
bulletMabadiliko katika kima cha mabadilishano ya fedha
bulletSazo la fedha katika uchumi
bulletUgawaji wa rasilimali – ugawaji halisi wa fedha kwa ajili ya elimu, afya ya jamii, maji, barabara za vijiji, kilimo na uzuiaji wa kuenea kwa Virusi vya UKIMWI/UKIMWI
Matendo yafuatayo ambayo baadhi yameelezwa katika sehemu zilizotangulia katika kijitabu hiki yatawezesha kuwa na hali imara ya uchumi
Viashirio (Dalili) Matendo
Ukuaji wa jumla wa Uchumi wa Tanzania Imarisha uthabiti wa uchumi
Panua vitega uchumi (vya asili na vya binadamu)
bulletImarisha barabara vijijini na huduma za miundo msingi (maji, umeme, mawasiliano n.k.)
bulletElimisha watu katika stadi zinazotakiwa na katika kazi na utoaji ushauri
Imarisha vitega uchumi vya uzalishaji
bulletEndeleza nyenzo za uchumi mdogo
bulletStawisha hali nzuri ya vitega uchumi ambayo inaendana na programu
bulletkukuza sekta binafsi na thabiti
bulletkupunguza gharama za uendeshaji biashara
bulletkuunda mfumo wa sheria ambao ni thabiti na unaofaa
Endeleza Mbinu za Sekta Binafsi ifikapo mwaka 2003
bulletHakikisha uratibu mzuri kati ya serikali na mashirika ya wafadhili
bulletHakikisha kuunda mazingira yanayowezesha biashara kubwa, ndogo na ya kati. Aidha kuwa na biashara isiyo rasmi
bulletUlipaji kodi – viwango na viwango vilivyo dhibitiwa
Ukuaji wa kilimo kwa asilimia 5 ifikapo 2003
bulletEndeleza upatikanaji wa matokeo ya tafiti za kilimo
bulletRahisisha upatikanaji wa mikopo kwa ajili ya kilimo
bulletKuza upatikanaji wa fedha za maendeleo vijijini, na biashara ya mazao na futa urasimi
bulletKuza biashara ya nje ya bidhaa za kilimo ·
bulletGawa ardhi ambayo inafaa kwa umwagiliaji kwa watu masikini
Uimarishaji wa barabara za vijijini
bulletOngeza mgao wa bajeti kwa ajili ya ukarabati na uimarishaji wa barabara za vijijini
bulletEndeleza na tumia teknolojia ya nguvukazi kwa ajili ya ukarabati na uimarishaji, na tumia makandarasi wa nchini
bulletImarisha uwezo wa kudhibiti ukarabati wa barabara ambazo zinajengwa na makandarasi
 


Kuza ubora wa maisha na Ustawi wa Jamii

Umasikini wa kutokuwa na mapato unatokana na elimu ndogo, afya mbaya na ustawi wa jamii ambao ni wa mashaka. Kwa ujumla, inaonekana wazi lipi linahitaji kutendwa bali itachukua muda kugundua vipengele vyote vinavyohitajiwa. Aidha itachukua muda pia kujua gharama inayotakiwa. Mipango ifuatayo imekwisha buniwa:-

Mpango wa Taifa wa Mbinu za uendelezaji Elimu ya Msingi Ifikapo Julai 2001
Mpango wa Taifa wa Mbinu za uendelezaji Kilimo Ifikapo Juni 2001
Mpango wa Taifa wa Mbinu za uendelezaji Vijiji Ifikapo Desemba 2001
Programu ya mageuzi ya Serikali za Mitaa imekwishaanza kutekelezwa katika wilaya zote. Hii inasaidia Serikali za Mitaa kutekeleza huduma muhimu.
Mipango hii itaruhusu:
bulletMajengo chakavu na huduma dhaifu kurekebishwa (Serikali za Mitaa zitaamua mahali pa kujenga majengo mapya)
bulletMisaada mbalimbali ipatikanayo toka kwa wafadhili na hivyo kuwa nje ya bajeti (serikali itafanya kazi ya uratibu na wafadhili)
bulletUpunguzaji wa umasikini utagharimu pesa nyingi zaidi kuliko ilivyo sasa (serikali itashughulikia upatikanaji zaidi wa fedha)
panya-11.jpg (20532 bytes)
Elimu
Shabaha kuu ni kuwa na elimu zaidi na bora zaidi. Hii itajumuisha ufutaji wa ujinga ifikapo mwaka 2010. Aidha inakusudia kuleta uwiano sawa kati ya wasichana na wavulana katika shule za msingi na sekondari ifikapo mwaka 2005.
Malengo
  Hadi kufikia 2003
Uandikishaji wa wanafunzi shuleni kijumla Hadi kufikia 85%
Kiwango cha wanaoacha shule Toka 6.6% hadi 3%
Uandikishaji wa wanafunzi kihalisi Toka 57% hadi 70%
Wanafunzi wanaoshinda mtihani wa darasa la 7 Toka 20% hadi 50%
Wanafunzi wanaoingia sekondari Toka 15% hadi 21%
Mipango ya Elimu ya Watu Wazima Iongezeke
Shughuli
bulletUpimaji wa mshule na uendelezaji wa mipango utafanywa
bulletSerikali itagharimia gharama za muhimu za shule za msingi (hasa mishahara ya walimu)
bulletAda za shule zitafutwa ifikapo Julai 2001
bulletShule zitaendelezwa kwa kupatiwa vitabu, vifaa, madawati, vyoo, vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, n.k.
bulletUwiano thabiti kati ya wanafunzi – walimu utatumiwa
bulletWalimu wataendelezwa na kuhamasishwa
bulletKitengo cha ukaguzi kitaimarishwa
bulletShule binafsi na elimu ya jumuiya (ikiwa pamoja na elimu ya watu wazima) itaimarishwa.
Viashirio (dalili)
bulletOngezeko halisi la kiwango cha uandikishaji wanafunzi katika elimu ya msingi
bulletOngezeko halisi la wanafunzi wanaoanza shule
bulletOngezeko halisi la wanafunzi wanaosoma darasa la saba
bulletOngezeko halisi la wanaoshinda mtihani wa darasa la saba
“Mwanadamu anakuwa mwanadamu kwa sababu ya wanadamu wengine”
[Methali ya Kiafrika]

panya-12.jpg (17014 bytes)
Afya 
Umri wa kuishi unapungua (hasa kwa sababu ya ugonjwa wa UKIMWI). Lengo ni kuongeza umri hadi kufikia miaka 52 ifikapo 2010. Hili litawezekana kwa kuboresha lishe na kuwa na huduma bora za afya pamoja na maji salama.
Malengo

Ifikapo mwaka 2003
Kiwango cha vifo vya watoto wachanga Toka 99 hadi 85 kwa kila watoto 1000
Chini ya umri wa miaka 5 Toka 158 hadi 127 kwa kila watoto 1000
Vifo vya akina mama wakati wa kujifungua Toka 529 hadi 450 kwa kila watoto 1000
Vifo kutokana na malaria kwa watoto chini ya miaka 5 Toka 12.8 hadi 10 %
Watu wanaopata maji salama Toka 48.5 hadi 55%
Uchanjwaji wa watoto chini ya miaka 2 dhidi ya surua, dondakoo na pepopunda Toka 71 hadi 85%
Wilaya ambazo zina kampeni dhidi ya UKIMWI Hadi kufikia 75%
Punguza hali ya kudumaa Toka 43.4 hadi 20%
Punguza upotevu Toka 7.2 hadi 2%
Wafanyakazi wenye taaluma ya uzazi Toka 50 hadi 80%
Tekeleza kikamilifu sera ya maji ya mwaka 2000 kama inavyotakiwa
Shughuli
bulletOngeza kiwango na imarisha ugawaji wa fedha za serikali kwa ajili ya afya ya jamii
bulletToa afya bora karibu na mahali wanapoishi watu wote wa mijini na vijijini
bulletHakikisha misaada inatolewa kwa afya za jamii kwa kuimarisha vituo vya afya na hospitali na kubadili mfumo wa utendaji wa kazi
bulletImarisha mfumo wa kutoa misaada kwa wafanyakazi, madawa na vifaa vingine vya afya
bulletTekeleza programu ya udhibiti wa malaria kama ilivyopangwa kati ya mwaka 2000/01 hadi 2002/03
bulletKuza sekta binafsi na shirikisha makundi ya jumuiya katika utoaji wa huduma za afya
VIRUSI VYA UKIMWI/UKIMWI
Kuza utambuzi wa ugonjwa wa UKIMWI na afya ya jamii – pamoja na wanafunzi kufundishwa mashuleni
“Uchungu na huzuni huja kwa kuangalia uwapendao wakifa kwa sababu ya kukosa fedha za matibabu na hali hii ni upeo wa juu wa matatizo ya umasikini unaokuja kimya kimya”
[Deepa Narayan]

panya-15.jpg (16159 bytes)
Lishe
Kuza elimu ya lishe, hasa kwa akina mama na imarisha afya ya uzazi na mpango wa uzazi
Anzisha programu ya mfuko wa fedha wa shule
Maji
bulletOngeza matumizi ya serikali katika huduma za maji vijijini
bulletTathmini mahitaji ya makundi tofauti ya watu vijijini
bulletImarisha vianzo vya maji na data za maji salama
bulletFanya ukaguzi wa upimaji maji
bulletFanya ukaguzi wa mara kwa mara wa ubora wa huduma za maji na tumia vipimo vya shirika la Afya Duniani (WHO)
bulletKuza uvunaji maji ya mvua
bulletKarabati mipango yote ya usambazaji maji ambayo haifanyi kazi. Aidha karabati vifaa vya kutoboa udongo
bulletImarisha sheria, kanuni na taratibu za kuhifadhi maji katika vyanzo vya maji
bulletZipe uwezo Serikali za Mitaa na jumuiya kulinda vyanzo vya maji
Viashirio (Dalili)
bulletWatoto wachanga na viwango vya vifo vya watoto walio chini ya miaka mitano
bulletAsilimia ya watoto ambao wamepata chanjo kamili baada ya mwaka mmoja
bulletUwiano wa wilaya zenye kampeni za utambuzi wa UKIMWI
“Afya inahusisha mwili mzima, akili, na ustawi wa jamii na si tu kutokuwa mgojwa na kutojiweza.”
[Shirika la Afya Duniani – WHO]
bulletUwiano wa kaya ambazo zinapata maji salama
Ustawi wa Jamii – Kushiriki katika shughuli za Siasa
Kati ya vitu vingine ambavyo vinahusiana na ustawi wa jamii ni kuhusu kushiriki katika maamuzi ya kisiasa yanayohusu maisha yako, na kujiona wanalindwa na sheria na kanuni. Pametokea maendeleo mazuri katika eneo hili katika miaka mitatu iliyopita na mengi yanapangwa.
Serikali imekuwa wazi katika shughuli inazofanya na imekuwa sikivu kwa watu wa kawaida.
bulletWatu wa kawaida sasa wanaweza kujua serikali inatumiaje fedha zao na kushiriki katika mikutano inayoamua sera zipi zifuatwe na serikali
bulletMagazeti, Redio, Televisheni vinaeleza watu wa kawaida mambo yanayoendelea
bulletKuna Jumuiya hiari za Wananchi ambazo hutoa mchango na changamoto
bulletSerikali za Mitaa zitapewa uwezo zaidi wa kuamua yapi yatekelezwe katika mikoa yao baada ya kutekeleza Programu ya Mageuzi ya Serikali za Mitaa.
Linapozingatiwa suala la sheria na taratibu, watu lazima wajione salama kutembea mitaani, kuweza kutumia mahakama, na kujua kuwa mfumo wa serikali ni thabiti, wa haki na uko wazi. Mipango ifuatayo inafanywa katika kiwango cha Serikali za Mitaa:
Malengo
bulletTekeleza kikamilifu njia za Kupunguza Umasikini kama zilivyopangwa
bulletTekeleza kikamilifu Programu ya Mageuzi ya Serikali za Mitaa ifikapo mwaka 2003 katika wilaya zote
bulletHakikisha ushirikishwaji wa washika dau wote katika kuunda, kutekeleza na kutathmini mipango yote ya maendeleo
panya-13.jpg (19452 bytes)
Shughuli
bulletKuza mfumo wa usalama wa jamii
bulletKarabati majengo ya mahakama za mwanzo na vifaa vya jumuiya
bulletAjiri mahakimu ili kesi zilizoko katika mahakama za Mwanzo ziweze kuamuliwa mapema
Katika Kiwango cha Taifa:
  Hadi mwisho wa mwaka 2003
Uwiano wa vikao vilivyopangwa vya Mahakama za Rufaa na vile vilivyotimizwa Toka 50% hadi 100%
Uamuzi wa Mahakama Uharakishwe
Uwiano wa kesi zilizoamuliwa na zile zilizoletwa Toka 63% hadi 80%
Wastani wa muda uliotumiwa katika kuamua kesi za biashara Zipunguzwe hadi miezi 18
Kutakuwa pia na uchunguzi wa rushwa katika :
bulletWizara ya Sheria
bulletWizara ya Ujenzi, Elimu, Afya na Mambo ya Ndani na ofisi zao za Mikoani na Wilayani
bulletOfisi ya Mwanasheria Mkuu
bulletMamlaka ya Mapato Tanzania
Viashirio (Dalili)
Viashirio vya ushirikishwaji:
bulletIdadi ya washiriki na ushiriki katika warsha za mashauriano
bulletUshiriki wa makundi ya jumuiya
bulletUsambazaji wa ripoti za serikali
Ripoti za kila miezi minne kuhusu maendeleo ya mageuzi ya mfumo wa mahakama na uchunguzi wa rushwa.


Kupunguza Madhara katika Makundi Masikini

Serikali za Mitaa zitaombwa kupambanua makundi ambayo yamo hatarini kupata madhara zaidi na ziamue matakwa yao ni yapi na yanaweza kupatikanaje. Baadhi ya majukumu ya kutekeleza ili kusaidia makundi haya ni:
bullet
Programu za kazi za kulipwa chakula
bullet
Miradi maalum inayohusisha yatima na walemavu
bullet
Mfumo wa awali wa kugundua mabadiliko ya hali ya hewa yatakayoathiri mazao
bullet
Kutekeleza mpango wa umwagiliaji katika sehemu zenye ukame
bullet
Kuweza kufika kwa urahisi katika mikoa yenye ziada ya chakula
bullet
Kuendeleza mazao yanayohimili ukame
bullet
Kuendeleza misitu
Benki ya Dunia imetoa mkopo kwa ajili ya mradi wa mfuko wa Kuinua Jamii Tanzania (TASAF) katika ngazi ya wilaya.
Watu wengi masikini Tanzania wanategemea mazingira asilia kwa ajili ya chakula chao na pia kukabili mahitaji yao kwa kuuza kuni, mkaa, asali na matunda mwitu. Hatujui shughuli hizi kikamilifu kiasi cha kupunguza na kuweka malengo kwa ajili ya kuzuia uharibifu wa mazingira. Taarifa zitakusanywa ili zitumike katika nakala mpya ya mpango wa kusaidia Kupunguza Umasikini (PRSP).
Utaratibu utafanywa wa kuhusisha mipango mingine kama vile kuimarisha matumizi ya mazao yanayostahimili ukame na mpango wa umwagiliaji unaofanywa na jamii. Aidha upandaji miti na upunguzaji wa mifugo nao pia utahusishwa.
“Mpangilio wa maisha unaonyesha kuwa watu masikini ambao wana mali kidogo wanaweza kwa kutumia nguvu kidogo kuneemeka polepole kiuchumi, na kushtukia wamerejea tena katika ufukara wao kwa sababu ya maradhi, kuachishwa kazi, kupata mazao hafifu na wanawake kutelekezwa . Hakuna kitu kinachowazuia kuangukia katika lindi la kukata tamaa. Na wakati wanapotumbukia huko, panaweza pasiwe na mtu yeyote anayewangoja kuwadaka huko chini wanakoangukia. Aidha hakuna anayewapa mkono wa msaada ili waanze upya.”
[Deepa Narayan]
Malengo
Jenga uwezo wa jumuiya zote zinazohitaji programu za usalama.
Shughuli
bullet
Kuza programu za jumuiya za kusaidia watu ambao wanakabiliwa na matatizo mbalimbali
bullet
Unda mfuko wa kuleta usawa ili kusaidia sehemu zilizo nyuma
“Tunamsaidia mwanachama yeyote wa kundi letu anapopata matatizo; tunamliwaza yeyote yule anayepata matatizo”
[Kundi la akina mama, Tabora]

Viashirio (dalili)
Namba ya data za uchumi zinazoonyesha makundi ya watu wenye matatizo zilizoundwa katika ngazi za Serikali za Mitaa na Serikali Kuu.

panya-14.jpg (21419 bytes)

Tutagharamiaje Upunguzaji wa Umasikini?

Hatuna hakika tunahitaji fedha kiasi gani na kiasi gani cha fedha kitakuwepo katika siku zijazo. Hata hivyo ni wazi kuwa hatutakuwa na fedha za kutosha na zile ndogo tulizonazo itabidi tuzitumie kwa uangalifu mkubwa.
Hatutaweza kujua kwa hakika ni fedha kiasi gani zitapatikana hasa kwa ajili ya kupunguza umasikini mpaka mipango yote mingine iwe imekamilika.

Njia za Mapato kwa ajili ya Upunguzaji Umaskini


bulletKiasi fulani cha fedha kitatokana na bajeti ya Serikali lakini hatutaweza kujua kiasi cha fedha kitakavyokuwa hadi mfumo wa kodi utakapoboreshwa. ·
bulletKiasi cha fedha kitatoka kwa wafadhili, lakini kiasi hicho hakiwezi kujulikana katika muda mfupi na muda mrefu ·
bulletSerikali itatumia fedha zake kupata fedha zaidi kwa kutoa mikopo na michango kwa watu wa kawaida na wafanyabiashara ambao wana mawazo mazuri na miradi mizuri ·
bulletSerikali inaweza kukopa fedha kuziba pengo
Kwa kuzingatia hali hii ya mashaka, na umuhimu wa kuwa na uchumi thabiti, matarajio yaliyowekwa kwa miaka mitatu ijayo ni kuwa jumla ya bajeti ya matumizi itaongezeka toka asilimia 15.5 hadi 17-18% ya mapato yote ya serikali. Kati ya fedha hizo asilimia 70% itatoka serikalini na asilimia 30% itatoka kwa wafadhili kama misaada au mikopo. Kama Mageuzi ya Serikali yatafaulu basi Tanzania itatimiza masharti ya mpango nafuu yaliyowekwa kwa ajili ya nchi zenye madeni makubwa (HIPC) hadi kufikia katikati ya mwaka 2001.
Shughuli nyingi za upunguzaji wa umasikini zitafanywa na Serikali za Mitaa. Ufafanuzi wa shughuli hizi utafanywa katika Programu ya Mageuzi ya Serikali za Mitaa (LGRP) yanayoendelea.

Kipaumbele katika Matumizi

Katika majibu ya watu waliyotoa wakati wa kutayarisha Mkakati wa Kupunguza Umasikini (PRSP), serikali imeamua kuwa matendo muhimu katika upunguzaji wa umasikini yanapaswa kuwa; matengenezo na uimarishaji wa huduma za sekta muhimu na sehemu inyohusika. Matendo hayo ni kama yafuatayo:
 
Shilingi Milioni
Sekta Sehemu
Elimu ( Elimu ya Msingi)
182061 142424
Afya (Afya ya Msingi kwa Jamii) 65970 42314 Barabara (Vijijini)
65970 42314
Barabara (Vijijini)
50147 28849
Mfumo wa Mahakama

7855
Kilimo (Utafiti na huduma)
8213 6893
Maji

5064
VIRUSI VYA UKIMWI/UKIMWI 

4800

Upunguzaji wa Umasikini: Vipengele Muhimu vya Ziada

Ufutaji wa ada za Shule \

Serikali itaacha kutoza ada za shule ifikapo Julai 2001. Hii ni kwa sababu serikali inaamini kwamba kwa kutolipa ada watoto wengi watasoma hasa watokao katika familia masikini

Kuhimiza michango kutoka katika Jumuiya na Washika dau wengine

Jumuiya zimeshiriki kikamilifu daima katika kupunguza umasikini kwa kufanya kazi za kujitolea kama kujenga madarasa, vituo vya afya, maji, barabara za vijijini, n.k. Serikali itahimiza moyo huu kwa kuchangia gharama za miradi hii na kuwahamasisha wafadhili kufanya hivyo hivyo.

Mafunzo ya Kazi

Serikali inakusudia kutumia karibu shilingi milioni 100 kila mwaka ili kuwasaidia watu waweze kujifunza mambo yatakayowasaidia kupata kazi. Fedha hizi zitawalenga watu ambao hasa ni masikini zaidi.
panya-17.jpg (19780 bytes)
panya-14.jpg (21419 bytes)

Mipango Imebuniwaje?


Tangu wakati wa uhuru mwaka 1961 serikali imejitahidi kushughulikia tatizo la ujinga, maradhi na umasikini. Kumepatikana maendeleo kwa kutumia mipango ya serikali kuu hadi mwaka 1970 ambapo hali ya kimataifa na kitaifa ilidhoofisha juhudi hizo na kuzirudisha nyuma. Licha ya mageuzi ya kiuchumi na
“Ni vigumu kwa watu wa kawaida kuitikia kwa moyo mkunjufu kwenye wito wa kazi za maendeleo ambazo zinaweza kuwa ni za manufaa kwao, lakini ambazo zimeamuliwa na kupangwa na mamlaka ambayo iko mbali mno nao.”
[Mwalimu Julius K. Nyerere]
kisiasa tangu katikati ya mwaka 1980, nusu ya Watanzania wote wanahofiwa kuwa masikini na theluthi wanaishi katika ufukara mkubwa.
Lakini hali sasa inaweza kuwa inabadilika. Mwishoni mwa miaka ya 1990 serikali ilitoa mwelekeo wa 2025 ukionyesha malengo ya muda mrefu ya kiuchumi na kijamii. Haya yalifuatwa na Mbinu za Kitaifa za Ufutaji wa Umasikini (NPER) ambapo malengo ya ufutaji wa umasikini hadi mwaka 2010 yalifafanuliwa. Jumuiya ya Kimataifa iliiunga mkono serikali kwa kutoa Mbinu za Usaidizi wa Tanzania (TAS) ambapo ilieleza kwa muhtasari mbinu iliyoratibiwa katika utoaji wa misaada. Tangu wakati huo muundo wa matumizi ya kati (MTEF) na mapitio ya matumizi ya serikali (PER) vimetolewa. Aidha, orodha ya tathmini ya viashirio vya ustawi na umasikini (PM) imetengenezwa.
panya-18.jpg (18729 bytes)
Sasa tuna waraka wa Mkakati wa Upunguzaji wa Umasikini Tanzania (PRSP). Hii inaeleza mbinu za muda mfupi wa kupunguza umasikini na ni sehemu ya mpango wa Nchi Masikini zenye Madeni Makubwa (HIPC). Mbinu hii in maana kwamba serikali inapaswa kupunguza matumizi na huku ikiruhusu shughuli za matumizi ya kuondoa umasikini kwa bajeti ya ziada na kukuza hatua mbalimbali zisizo ingiza gharama ambazo zaweza kuondoa umasikini.
Watu wengi walihusika katika kuandaa Mkakati wa Kupunguza Umasikini Tanzania (PRSP) na watu watahusika katika utekelezaji wake. Mpango unaorodhesha sababu zinazowafanya watu wawe masikini na kutoa mapendekezo ya njia za kuuondoa umasikini huo.
“Kama watu elfu moja watapiga risasi wakilenga shabaha moja tu na kwa wakati mmoja, hakuna sehemu ya shabaha ambayo haitapigwa.”
[Methali ya Kichina]
Baadhi ya ufumbuzi huihusisha serikali na mashirika ya wafadhili na ufumbuzi mwingine huwahusisha watu wa kawaida.
Watu hawaendelezwi ila wanajiendeleza wenyewe. [Mwl. Julius K. Nyerere]
Mpango wa Mkakati wa Kupunguza Umasikini Tanzania (PRSP) ni tofauti na mipango ya awali kwa sababu unatoa malengo thabiti na unawashirikisha watu wa kawaida. Watu wa kawaida walihusishwa katika kutengeneza mpango huo na watahusishwa katika kuutekeleza. Na hasa lililo muhimu ni kuwa watahusishwa katika kuhakikisha kwamba malengo yaliyobainishwa katika mpango huo yanapatikana.

Mpango huu Uliandaliwaje?

Mwezi Oktoba 1999 kamati ya mawaziri kumi na wawili na Gavana wa Benki ya Tanzania iliundwa kuandaa waraka wa mpango wa Mkakati wa Kupunguza Umasikini (PRSP). Kamati hii ilisaidiwa na kamati ya wataalamu (iliratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais) ambayo iliwahusisha maofisa kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, Tume ya Mipango, Wizara Kuu na Benki Kuu ya Tanzania.
Waraka wa msingi (waraka wa awali) wa Mpango wa Mkakati wa Kupunguza Umasikini Tanzania (PRSP)) ulitolewa kama muswada wa kwanza mwanzoni mwa mwezi Januari 2000. Waraka huu ulijadiliwa katika mkutano wa mashauriano ambao uliwahusisha wawakilishi wa serikali na watu waliotoka katika jumuiya ya wafadhili na makundi ya kijamii.
Waraka ulihakikiwa na kuidhinishwa na baraza la mawaziri mwanzoni mwa mwezi Februari 2000. Aidha, waraka huo ulijadiliwa na Shirika la Fedha Duniani mjini Washington mwezi Machi 2000. Hili liliiwezesha Tanzania kuendelea na kutoa waraka kamili wa Mbinu za Kupunguza Umasikini.
Mwezi Machi mwaka 2000 kamati ya wataalamu ilitayarisha vidokezo vya waraka wa mwanzo kwa ajili waraka kamili wa mpango wa Mkakati za Kupunguza Umasikini Tanzania (PRSP). Waraka huu ulijadiliwa katika warsha za kanda saba kati ya tarehe 11-12 Mei 2000. Warsha hizi zilihudhuriwa na washiriki 804 na zilihusisha vijiji 426, madiwani 215, Wakurugenzi wa Halmashauri 110 na watu 53 waliotoka katika mashirika yasiyo ya kiserikali. Chini ya robo ya washiriki walikuwa wanawake. Ripoti za kila kanda zilitolewa kwa kamati ya wataalamu tarehe 16 Mei 2000.
Mkutano wa mashauriano kati ya serikali na wafadhili uliofanywa tarehe 22 Mei 2000 na ulifuatwa na kamati ya wataalamu ambayo ilitengeneza waraka wa mwanzo wa Mbinu za Upunguzaji wa Umasikini Tanzania. Waraka huu ulitumia taarifa zilizotoka katika tafiti zilizotangulia, waraka za sera na matokeo ya warsha za kanda. Tarehe 30 Juni waraka ulijadiliwa katika mkutano ambao uliwashirikisha jumuia ya wafadhili kutoka Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani. Tarehe 1 Julai 2000 Wabunge walijulishwa juu ya maendeleo yaliyokwisha fikiwa na waliombwa kutoa mawazo yao.
Tarehe 3-4 Agosti 2000 kulifanyika warsha ya kitaifa ikiwa na washiriki 25 ili kupata maoni zaidi kuhusu malengo, na kutathmini mambo muhimu ya kufanya ambayo yalikuwa yameainishwa katika waraka wa awali. Waliohudhuria warsha hiyo ni pamoja na Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa, Wawakilishi na Wafadhili, Mashirika ya Kimataifa, sekta binafsi, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, vyombo vya habari na wawakilishi wa sekta zisizokuwa rasmi. Aidha tarehe 3 - 4 Agosti 2000 waraka wa awali ulijadiliwa na Makatibu Tawala wa Mikoa (RAS) huko Lobo, Serengeti.
Waraka uliorekebishwa uliidhinishwa na Baraza la Mawaziri tarehe 31 Agosti 2000. Marekebisho zaidi yalifanywa na Serikali na Shirika la Fedha Duniani/Benki ya Dunia na Waraka wa mwisho uliidhinishwa na Bodi za Shirika la Fedha Duniani na Benki ya Dunia mwezi Oktoba 2000.

Mipango ya baadaye itafanywaje?

Tafiti mbalimbali zinafanywa ili kupata takwimu bora za kusaidia mipango ya baadaye. Hizi ni pamoja na: · Ukaguzi mpya wa bajeti za kaya zaidi ya 24,000 · Ukaguzi wa nguvu kazi ili kuanzisha msingi wa soko la kazi · Sensa ya idadi ya watu na nyumba katika mwaka 2002 · Ukaguzi wa taarifa za uzazi na vifo pamoja na afya katika mwaka 2003
Shirika la Fedha Duniani/Benki ya Dunia inashauri kutengenezwa upya kwa mahesabu ya kijamii ili kupima kama mapato na matendo ya sera yana matokeo yoyote juu ya upunguzaji umasikini
“Watu masikini ndio wataalamu wa umasikini”
[Deepa Narayan]
Kuna umuhimu wa haraka wa kuimarisha uwezo wa watu wa aina mbalimbali ili kutathmini shughuli ambazo zimeanzishwa pamoja na waraka wa Mkakati wa Upunguzaji wa Umasikini Tanzania (PRSP). Watu wanahitaji pia kufasili taarifa ambazo zinakusanywa na kubainishwa, taarifa hizo zina maana gani katika masuala ya sera.
Inategemewa kuwa vikao mbalimbali vitafanywa ili kuanzisha utaratibu wa uoanishaji wa shughuli mbalimbali katika ngazi tofauti. Aidha vikao hivi vitatafuta njia za kuhusisha sera na ushirikishwaji wa watu. Kama ilivyoelezwa katika Mkakati wa Upunguzaji wa Umasikini Tanzania (PRSP), “Serikali imekusudia kuendeleza ushirikishaji wa watu masikini na washika dau wengine katika utekelezaji, usimamizi na tathmini ya mbinu za upunguzaji umasikini, na kisha kurekebisha waraka huo”. 


Maana za Baadhi ya Maneno

Uchumi Mkuu: (macroeconomics) ni elimu juu ya picha kamili ya uchumi, yaani njia ambayo utajiri unapatikana na unagawanywa. Inaweza kuwa elimu kuhusu nchi maalum au dunia nzima na jinsi tofauti zinavyoingizwa katika picha nzima ya dunia. Kuna majadiliano kama ya:

bulletMatajiri wanazidi kutajirika na masikini wanazidi kuwa masikini zaidi. Tufanye nini kuhusu jambo hili?
bulletSerikali ijiingize kiasi gani katika uendeshaji wa soko huru?
bulletKwa kuzingatia na uharibifu wa mazingira, je, ukuaji wa uchumi usiodhibitiwa unatakiwa?
panya-19.jpg (19321 bytes)
Uchumi Mkuu Imara (Macroeconomic Stability) ni matokeo ya kuwa na kodi ya hazina, sera za fedha na kiwango cha kubadilishana fedha inayokusudia kufikia malengo ya uchumi mkuu kama vile ukuaji wa uchumi, kupanda kwa gharama za maisha, madeni ya nje na akiba halisi ya kimataifa.
Uchumi Mdogo (Microeconomics) ni elimu kuhusu jinsi viwanda, sekta fulani, biashara au kaya zinavyofanya kazi.
Jumla ya Pato la Taifa (Gross Domestic Product - GDP) ni kipimo cha jumla ya pato la utajiri ambalo linapatikana nchini katika muda maalum. Kwa maneno mengine Pato la Taifa ni tathmini ya bidhaa zote na huduma ambazo zinaundwa na zinabadilishwa kwa fedha. Kama jumla ya thamani ya bidhaa na huduma mwaka huu ni asilimia 1% zaidi kuliko ya mwaka jana basi ukuaji wa pato la utajiri ni asilimia 1%. Lakini jumla ya pato la taifa (GDP) huacha kazi zingine za thamani ambazo zingeweza kujumuishwa – kwa mfano, uendeshaji wa kaya na familia kwa kupata nishati rahisi na maji, na pia watu kujenga nyumba zao kwa kutumia vifaa vya asilia na ustawishaji wa vyakula kwa ajili ya matumizi yao.
Jumla ya Pato la Taifa (GNP) ni sawa na jumla ya pato la taifa lakini unaongezea biashara ya ndani na biashara ya nje.
Ukuaji Halisi (Real Growth): Kwa vipengele vyote viwili jumla ya pato la utajiri (GDP) na ukuaji wa pato la utajiri (GNP), kama ukuaji ni asilimia 7% kwa mwaka, lakini mfumuko wa bei umekuwa asilimia 5% basi Ukuaji Halisi ungekuwa asilimia 2% tu kwa mwaka.
Mfumuko wa Bei (Inflation): Kipimo cha kupanda kwa bei kati ya mwaka mmoja na mwaka unaofuata – hasa ukizingatia wazo la kupata vifaa vya madukani/sokoni.
Mtaji wa jamii (Social Capital) ni kama “gundi” inayounganisha pamoja familia, makundi na jumuiya. Inahusisha imani, desturi na tabia za jamii ambazo husaidia kufanya kazi pamoja kwa uthabiti katika makundi yaliyo rasmi na yasiyo rasmi.
Vyama vya Jumuiya (Civil Society Organisation):Inahusisha vyama rasmi ambavyo vimesajiliwa na serikali na vile visivyo rasmi. Vyama hivyo ni pamoja na vile vya hisani, dini, vya shughuli maalumu, kundi shawishi, kitaaluma, na vyama vya makundi maalumu kama vile vyama vya wafanyakazi na vyama vya wanafunzi. Vyama visivyo rasmi ni pamoja na Upatu, vyama vya makabila, mpira wa miguu ambavyo vinaundwa na vijana wa kiume na netiboli vinavyoundwa na vijana wa kike.
Matayarisho Ya Bajeti inayozingatia maskini (Pro-poor Budgeting): na usimamizi wa matumizi (and expenditure monitoring). Fedha zinatengwa katika bajeti kwa ajili ya programu zinazowalenga watu masikini. Lakini fedha hizi zinapaswa kupitia Hazina, wizara inayohusika, serikali za Mikoa na Halmashauri za Wilaya/ Miji na kitengo cha huduma (k.m. shule au hospitali) kabla ya mtu masikini kupata faida. Kwa usimamizi thabiti fedha hizi zinaweza kutumika vizuri.
Mapitio ya Matumizi ya Serikali (Public Expenditure Review). Timu ya Matumizi ya Serikali hukutana mara moja kila baada ya majuma mawili ili kutafakari jinsi serikali inavyopata na kutumia fedha zilizo kwenye bajeti. Timu hii iliundwa mwaka 1997 inawajumuisha viongozi wakuu wa serikali na wawakilishi kutoka katika jumuiya ya wafanyabiashara, makundi ya jumuiya na makundi ya wafadhili wa nje.
panya-20.jpg (17638 bytes)
Bajeti za Serikali (Government Budgets). Serikali ni kama familia ambayo inapaswa kuweka uwiano kati ya fedha zinazoingia na fedha zitumikazo. Kama hakuna fedha zinazoingia serikali inapaswa kuamua itumie kiasi gani na isitumie kiasi gani. Utaratibu wa kukusanya taarifa hii na kufanya uamuzi ndiyo huitwa Bajeti
Njia za Mapato ya Serikali (Source of government income):
bulletKodi ya moja kwa moja k.m. kodi ya mapato, kodi ya mali
bulletKodi isiyo ya moja kwa moja k.m. kodi ya ushuru wa forodha, kodi ya mauzo
bulletMapato yasiyo na kodi k.m. liseni na ada
bulletMikopo k.m. toka Mashirika ya Fedha Duniani na Benki ya Dunia ·
bulletMisaada k.m. toka serikali nyinginezo na toka mashirika yasiyo ya kiserikali
Kuongeza kodi ni jambo lisilopendwa na baadhi ya kodi nyingine ni mzigo mkubwa kwa watu masikini kuliko watu matajiri. Mikopo ni mizuri kuziba mapengo ya muda mfupi na kuanzisha biashara mpya, lakini lazima mikopo hiyo ilipwe. Misaada inakaribishwa bali hatuwezi kupata misaada wakati wote.
panya-21.jpg (18491 bytes)
Mishahara na Gharama Nyinginezo (Personal Emoluments (PE) and other charges (OC)): Wizara inatumia sehemu ya bajeti yake kwa mishahara na sehemu nyingine kulipia gharama nyinginezo. Kama sehemu ya kutekeleza waraka wa Upunguzaji wa Umasikini (PRSP), Serikali itaongeza bajeti ambayo inatengwa kwa ajili ya gharama za matumizi mengine – kwa mfano, kati ya mwaka 1999/2000 hadi 2002/2003 bajeti itaongezwa toka asilimia 2 hadi 3.8% kwa ajili ya elimu ya msingi na toka asilimia 2.1 hadi 3.8% kwa ajili ya Afya ya Jamii.


Vifupisho

BoT Bank of Tanzania – Benki Kuu (ya Tanzania)
CAS Country Assistance Strategy – Mbinu za Kusaidia Nchi
CSO Civil Society Organisation – Jumuiya Hiari za Wananchi
DED District Executive Director – Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya
ELCT Evangelical Lutheran Church of Tanzania – Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania
ESAF Enhanced Structural Adjustment Facility – Uharakishaji Mabadiliko ya Kimuundo
GDP Gross Domestic Product – Pato Ghafi la Ndani
GNP Gross Nationa Product – Jumla ya Pato la Taifa
HBS Household Budget Survey (1991/92) – Mapitio ya Bajeti za Kaya (1991/92)
HIPC Highly Indebted Poor Countries – Nchi Masikini zenye Madeni Makubwa
HRDS Human Resource Development Survey (1993) – Ukaguzi wa Maendeleo ya Nguvu kazi (1993)
HRS Human Resource Survey (1983) – Ukaguzi wa Nguvu kazi
IBRD International Bank for Reconstruction and Development (World Bank) – Benki ya Dunia ya Urekebishaji na Maendeleo
IFMS Integrated Financial Management Information System – Mfumo wa Pamoja wa Taarifa za Uendeshaji wa Fedha
IMCI Integrated Management of Childhood Illness – Uendeshaji wa Pamoja wa Magonjwa ya Watoto
IMF International Monetary Fund – Shirika la Mfuko wa Fedha Duniani
LGRP Local Government Reform Programme – Mpango wa Mageuzi wa Serikali za Mitaa
M & E Monitoring and Evaluation – Usimamizi na Tathmini
MDF Multilateral Development Fund – Mfuko wa Shughuli mbali mbali za Maendeleo
MSME Micro, Small and Medium Enterprises – Viwanda Vidogo na vya Kati
MTEF Medium-term Expenditure Framework - Muundo wa Matumizi ya Muda wa Kati
NBS National Bureau Statistics – Kitengo cha Taifa cha Takwimu
NGO Non-Government Organisation – Shirika lisilo la Kiserikali
NPES National Poverty Eradication Strategy – Mpango wa Taifa wa Mkakati waKupunguza Umasikini
OPM Oxford Policy Management – Manejimenti ya Oxford kuhusuSera ya Uongozi
PER Public Expenditure Review – Mapitio ya Matumizi ya Serikali
PL Poverty Line – Mstari wa Umasikini
PMI Poverty and Welfare Monitoring Indicators – Viashirio vya Uratibishaji wa Umasikini na Usawa
PPA Participatory Povery Assessment (1995) – Tathmini ya Ushirikishwaji juu ya Umasikini
PRGF Poverty Reduction and Growth Facility – Mfumo wa Ukuaji na Upunguaji wa Umasikini
PRSC Poverty Reduction Support Credit – Mikopo ya Kusaidia Kupunguza Umasikini
PRSP Poverty Reduction Strategy Paper – Mkakati wa Mbinu za Upunguzaji Umasikini
PSAC-I Programme Structural Adjustment Credit – Programu ya Mikopo ya Urekebishaji Miundo
PSRP Public Service Reform Programme – Programu za Mageuzi ya Huduma za Umma
RAS Reginal Administrative Secretaries – Makatibu Tawala wa Mikoa
SME Small to Medium Enterprises – Viwanda Vidogo hadi vya Kati
TAS Tanzania Assistance Strategy – Mbinu za Kusaidia Tanzania
TIC Tanzania Investment Centre – Kituo cha Uwekezaji Tanzania
TIPER Tanzania-Italian Petroleum Refinery – Mtambo wa Kusafisha Mafuta Tanzania na Italia
TRCHS Tanzania Reproductive and Child Health Survey (1999) - Mpango wa Uzazi na Afya ya Watoto
TSED Tanzania Socio-Economic Database – Mfumo wa Utunzaji wa Taarifa za Jamii na Uchumi
TTC Teacher Training College – Chuo cha Ualimu
VPO Vice President's Office – Ofisi ya Makamu wa Rais
 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni