Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Septemba 13, 2011

UTAMADUNI


Neno la Kilatini lenye maana ya utamaduni ni Cultura ambalo lina usuli wake katika neno colere, linalo maanisha "kulima") Neno hili lina fafanuzi nyingi. Kwa mfano, mnamo mwaka 1952, Alfred Kroeber na Clyde Kluckhohn walikusanya orodha ya vijelezi 164 vya neno "utamaduni" katika kazi yao: Culture:a Critical Review of Concepts and Definitions.  Hata hivyo, neno "utamaduni" linatumika kimsingi katika njia tatu zifuatazo:
  • Maonjo ya hali ya juu katika sanaa, vilevile hujulikana kama utamaduni wa juu
  • Mkusanyiko wa maarifa ya kibinadamu, itikadi na tabia ambao hutegemea sana uwezo wa kuwasilisha mawazo na mafunzo ya kijamii kiishara
  • Ni jumla ya mitazamo, kaida, malengo na maadili yanayotambulisha asasi, shirika au kikundi Fulani
Dhana hii ilipoibuka kwanza katika karne ya kumi na nane na kumi na tisa barani Ulaya, ilimaanisha mchakato wa kulima au kuboresha kilimo au kilimo cha mboga. Katika karne ya kumi na tisa dhana hii ilimaanisha kuboreshwa kwa mja kupitia kwa elimu na hali kadhalika ilimaanisha kutekelezwa kwa maazimio ya kitaifa au maadili. Katikati mwa karne ya kumi na tisa, wanasayansi wengine walitumia dhana ya utamaduni kurejelea uwezo wa kiubia wa binadamu.




Katika karne ya ishirini, "utamaduni" ilijitokeza kama dhana ya kimsingi katika somo la Anthropolojia. "Utamaduni" ulihusisha mambo yote yaliyomhusu binadamu ambayo hayakufungamana na matokeo ya kimaumbile. Dhana ya utamaduni katika Anthropolojia ya Kimarekani ilikuwa na maana mbili: 

(1)        Uwezo wa kibinadamu wa kuainisha na kuwasilisha tajiriba za kibinadamu kiishara na kutenda mambo kiubunifu; na

(2)        Namna mbalimbali watu wanaoishi katika sehemu mbalimbali ulimwenguni huainisha na kuwasilisha tajiriba zao za maisha na kutenda mambo kiubunifu. Kufuatia vita vya pili vya dunia, dhana hii ilipata umaarufu ingawa na fafanuzi tofautitofauti katika taaluma kama vile sosholojia, Mafunzo ya utamaduni, saikolojia ya mipangilio na mafunzo ya usimamizi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni