Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Septemba 17, 2011

INJILI...MAJIBU YAFANYAYO KAZI.

Injili ni neno lenye asili ya Kigiriki linalotafsiriwa Habari Njema, yaani habari ya Yesu Kristo kufa na kufufuka.
Jina hilo linatumika pia kuhusu vitabu vinavyoeleza maisha na mafundisho ya Yesu kufuatana na kile cha Mtakatifu Marko ambacho kwa wataalamu wengi ndiyo Injili iliyowahi kuandikwa (65-70 B.K.)
Kati ya vitabu vyote vya namna hiyo, Ukristo tangu karne II unakubali vile vinne vya kwanza tu, ambavyo viliandikwa wakati wa Mitume wa Yesu.
Hivyo vinashika nafasi ya kwanza katika orodha ya vitabu vya Agano Jipya kama ifuatavyo: Injili ya Mathayo, Injili ya Marko, Injili ya Luka na Injili ya Yohane.
Injili tatu za kwanza zinafanana kwa kiasi kikubwa katika mpangilio, habari na maneno yenyewe, na kwa sababu hiyo zinaitwa Injili-Ndugu. Kadiri ya wataalamu wengi mfanano unatokana na kwamba Injili ya Marko ilitumiwa na waandishi wa zile nyingine.
Ile ya Mtume Yohane ni ya pekee na inategemea ushahidi wa Mtume ambaye alipendwa zaidi na Yesu akamfuata kiaminifu hadi msalabani.
Vinahesabiwa na Wakristo kuwa moyo wa Maandiko Matakatifu yote (Biblia) yanayotunza ufunuo wa Mungu, kwa kuwa ndivyo shuhuda kuu juu ya Neno aliyefanyika mwili.
Vile vingi vilivyoandikwa kuanzia karne II havitumiwi na Kanisa katika kufundisha imani na katika liturujia. Vinaitwa kwa kawaida apokrifa yaani za bandia.
Waislamu wanakiri Injili kuwa iliteremshwa toka mbinguni kwa nabii Isa, lakini hawakubali vitabu 4 vya Wakristo kama vilivyo.

Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.
Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...
(Namaanisha JumaMosi)
Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo

Golden Gate Quartet

Wanapotwambia: 

Early Songs

 

Au tufanye jambo mbadala kwa ujumbe huu usemao: "Nobody knows the troubles I've seen" kutoka kwa hawa waimbaji waitwao Negro spiritual (1982)







Maoni 1 :

  1. Along with the snoring products above, here are a few additional methods you can use in conjunction to assist you eliminate snoring:
    my web site: Sleep Study

    JibuFuta