Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Mei 07, 2011

MAJIBU YAFANYAYO KAZI..."MTAKATIFU".

Kwa Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki

Makanisa ya Kiorthodoksi yanamuita mtakatifu hasa anayesadikiwa yuko katika paradiso, kuanzia Adamu na Eva, Mose na manabii wengine, lakini pia malaika. Ni Mungu anayefunua watakatifu wake kwa kuitikia sala anazotolewa kwa kuwapitia na kwa kutenda miujiza. Wakristo wanaanza kuwatambua lakini uamuzi wa mwisho unachukuliwa na sinodi ya maaskofu.

Waorthodoksi wanawatendea watakatifu kama watu hai, kwa sababu wanaishi mbinguni pamoja na Kristo mfufuka, ingawa miili yao haijaungana tena na roho zao. Kila mtu anapobatizwa anapewa jina la mtakatifu fulani kama msimamizi kwa maisha yake yote.

Katika Uprotestanti

Madhehebu mengi hayakubali mawazo hayo, yakipenda kusisitiza kwamba wokovu unamtegemea Mungu tu. Hata hivyo mara nyingi waamini bora wanakumbukwa kwa heshima na kuchukuliwa kama mfano (taz. Confessio augustana art. 21). Hasa Waanglikana wanakaribia msimamo wa Wakatoliki na kuadhimisha sikukuu za watakatifu kadiri ya kalenda maalumu.

Katika Uislamu

Ingawa dini hiyo haikubali tofauti kati ya watu, Waislamu wengi wanapenda kuheshimu kwa namna ya pekee marafiki wa Mungu (wali), wakisadiki wana uwezo wa kutabiri, kuombea na kuponya.

Ndugu msomaji: MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...

(Namaanisha JumaMosi)

Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo

Dr. Carlton P. Byrd

Anapotwambia: “Devil Is Alive




Kwa kuwa bado upo nikuongezee nahii kutoka kwa Take 6 katika moja ya nyimbo zao za LIVE wanaposisitiza kuwa Fly Away.


Maoni 1 :

  1. Mkuu Mtayarishaji nashukuru sana kwa maelezo haya hasa kuhusu mtakatifu na utakatifu. TUPO PAMOJA MKUU

    JibuFuta