Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumapili, Mei 15, 2011

JUA NA SAYARI ZAKE

Jua letu na sayari zake

Mfumo wa jua na sayari zake ni utaratibu wa jua letu na sayari au sayari kibete zinazolizunguka pamoja na miezi yao, asteroidi, meteoridi, kometi na vumbi ya angani yote ikishikwa na mvutano wa jua.

Kwa kawaida huhesabiwa sayari 9 zinazozunguka jua. Lakini miaka ya nyuma magimba makubwa yamegunduliwa angani ambayo bado hayakukubaliwa kama yahesabiwe kuwa sayari au aina ya asteoridi.

Orodha inayofuata bado inahitaji kuangaliwa kwa sababu kuna tofauti kati ya kamusi na vitabu mbalimbali jinsi ya kutaja sayari fulani.

Sayari katika mfumo wa jua ni zifuatazo:

Namba zote zinazotaja sifa mbalimbali za sayari zinaonyesha kipimo kulingana na tabia za dunia yetu kuwa "1". Kuhusu majina ya sayari kadhaa kuna mchanganyiko katika kamusi na vitabu. Pale ambako jina au umbo tofauti la jina ni kawaida linaonyeshwa katika mabano kama (jina). Majina yanayotumiwa katika vitabu kadhaa bila kuwa na uhakika yanaonyeshwa katika mabano ya italiki pamoja na alama ya swali kama (? jina).

Jina la sayari

Kipenyo kwenye ikweta
kulingana na kipenyo cha dunia = 1

Masi

Nusukipenyo ya mzingo wa kuzunguka jua

Muda wa mzingo
(miaka)

Kuinama kwa mzingo wa kuzunguka jua
Pembenukta (°)

Muda wa siku ya sayari
(siku)

Miezi

Utaridi (Zebaki)*

0.382

0.06

0.387

0.241

7.00

58.6

0

Zuhura (Ng'andu)**

0.949

0.82

0.72

0.615

3.39

-243

0

Dunia (Ardhi)***

1.00

1.00

1.00

1.00

0.00

1.00

1

Meriki

0.53

0.11

1.52

1.88

1.85

1.03

2

Mshtarii (? Sumbula)

11.2

318

5.20

11.86

1.31

0.414

63

Zohari (Zohali) (? Sarateni)

9.41

95

9.54

29.46

2.48

0.426

49

Uranus (? Zohali)

3.98

14.6

19.22

84.01

0.77

-0.718

27

Neptun (? Kausi)

3.81

17.2

30.06

164.8

1.77

0.671

13

Pluto (? Utaridi)****

0.18

0.002

39.5

248.5

17.1

-6.5

3

Utaridi ni jina la sayari ya kwanza kutokana na lugha ya Kiarabu. Vitabu vingine hutumia neno "Zebaki" ni pia neno lenye asili ya Kiarabu linalomaanisha metali; inaonekana limepatikana kama tafsiri ya jina la Kiingereza la sayari ya kwanza "Mercury" bila kujua historia ya majina ya sayari sita ya kwanza yaliyoingia katika Kiswahili kutoka lugha ya Kiarabu.
** Zuhura - Ng'andu ni sayari lenye jina la Kibantu kwa Kiswahili pamoja na jina la asili ya Kiarabu
*** Tazama makala ya Dunia kwa ajili ya namba halisi. Neno "ardhi" hutumika na waandishi kadhaa badala ya "dunia" wakitaka kutaja sayari ya tatu.
**** Tangu 2006 Pluto imeingizwa katika kundi la "sayari kibete".

  1. Linganisha ukuasa wa majadiliano:sayari
  2. kuhusu majina ya sayari zilizojulikana kwa Waswahili na hivyo kuwa na majina ya asilia linganisha Jan Knappert, Swahili Islamic poetry, Brill 1971, Vol 1 uk 96-97 - taz google booksearch

UPO…???


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni