Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Aprili 09, 2011

MAJIBU YAFANYAYO KAZI..."FaMiLia Na WaJiBu Wa KuTaMbua".

UKURASA WA SIMULIZI HALISI KILA JUMAMOS

Ilikuwa ni Tarehe Aprili 08 2011 ambapo msikilizaji wangu mmoja wa kipindi cha Muziki wa Acappella aitwaye Max Martin alinitumia ujumbe ambao nimeona ni vyema pia kufahamishana kile kilichokuwa moyoni mwake kutokana na mambo anavyoyaona hasa katika tasnia ya Muziki.

Alianza katika hilo chapisho hivi:

Sabato njema kaka mcharia. Yaani kaka Mcharia ninaposikiliza kipindi chako (ACAPPELLA) huwa napata picha nyingi sana. Mojawapo kati ya picha hizo ni kwamba kama hawa wasanii wanaoimba muziki wa dunia laiti kama wangekuwa wanaimba muziki wa injili hasa wa kisabato hebu vuta picha tungekuwa na kwaya ya aina gani.

Halafu picha nyingine ni kwamba huwa naona hii acapella (christian) ina nguvu mno ya kumshawi mtu atake kuiimba hebu angalia siku hizi katika makanisa yetu karibu kila kanisa lazima kutakuwa na kikundi cha vijana wanoimba acapella, ukizingatia mtu yeyote hakuwalazimisha wala kuwaambia waimbe, ni ile tu nguvu ya ushawishi iliyopo katika muziki huu.

Na vijana hao unakuta wana umri kati ya miaka 13-19 na kuendelea, na ukija huku katika dunia vijana wenye umri kama hou hou huwa wanajishughulisha na muziki wa dunia, wengine jinsi ya kucheza muziki huo n.k. Hivyo basi vijana kati ya umri huu kutokana na mawazo yangu ni rahisi kushawishika, na picha nyingine nyingi kama hizi. Sasa kaka Yusuph huu umoja wa acapella tuliouanzisha tumuombe mungu atuwezeshe tuutumie kwa kasi zaidi kama njia mojawapo ya uinjilisti na zaidi kuliko Lusifa anavyoutumia muziki wa dunia muziki wa dunia kama moja ya njia yake ya uinjilisti.

Mi naamini umoja wa acappella utafanya kitu katika siku hizi za usoni. Tukiachana na hilo na mimi pia ni kijana ambaye huu huu muziki wa acappella ulinishawishi kuachana na muziki wa dunia. Na pia sasa najifunza kuimba acappella katika kundi la AZANIA BROTHERS pale shule ya sekondari azania. Siku moja ukipata muda njoo pale jangwani siku ya ijumaa katika jumuiya ya ASSA utatuona tukiimba. Mungu akubariki sana na sabato njema.

Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo..
.(Namaanisha JumaMosi)


Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe
ambapo

Dr. Carlton P. Byrd

anapotwambia "Don't Box Me In".



Naaam!!
Sijaondoka.., bado nipo nikiendelea kumtizama na kumuangalia Dr. Carlton P. Byrd.
Au kwa lugha nyingine
Mchungaji wetu Fesibuuku na wakati mwingine hutumia jina la Mchungaji Carlton Byrd. Mcheki katika Facebook kama nilivyoorodhesha majina yake haya.

Hivi una taarifa kwamba FAMILIA NI KITALU CHA MALEZI YA VIJANA!!?.


Makala yetu hii inawaalika wanafamilia wote kutafakari ukweli mzito uliomo katika maneno haya yote tulio yaongelea na kuzingatia umuhimu wake kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

...Kama vipi NEXT IJAYO tena.

Maoni 1 :

  1. Inapendeza,inavutia kaka Mcharia!Familiya kwanza,Ubarikiwe sana!!!!!!!

    JibuFuta