Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Agosti 09, 2016

Taarifa...UZINDUZI WA TRENI STESHENI PUGU DAR ES SALAAM.

 

Leo kampuni ya reli Tanzania TRL  kwa kushirikiana na wadau mbali mbali ikiwemo CHAMA CHA KUTETEA ABIRIA (Chakua), kwa pamoja tumezinduwa treni ya abiria itakayofanya safari zake kuanzia stesheni ya dsm kwenda pugu.

 

Katibu idara ya reli,, Godfrey Mali, kulia,, Mkurugenzi wa Kanda ya Mashariki, Wilson Sylvester na muheshimiwa waziri wa uchukuzi Makame Mbarawa wakiwa kwenye uzinduzi wa treni ya abiria ya kwenda pugu leo.
 

 Katika Uzinduzi hua Chama Cha Kutetea Abiria (Chakua) iliwakilishwa na mkurugenzi wa kanda ya mashariki, Wilson na katibu idara ya reli, Godfrey Mali.



 Pongezi kwa Katibu mkuu idara ya reli, hiyo ni kazi nzuri sana.



 Ni safari  ambayo itaanza saa 10:45 alfajiri kwenda pugu tripu ya kwanza na tripu ya mwisho 4:20 asubuhi hiyo routi ya asubuhi.

Routi nyingine itaanza saa 09 :55 alasiri kuekea pugu mwisho wa routi za jioni ni saa 4:15 usiku. Nauli kwa mkubwa Tsh 400 mwanafunzi Tsh 100. Hizi zitakuwa nauli za majaribio mpaka hapo sumatra watakapotoa muongozo wa nauli.


Uzinduzi wa treni ya abiria ya kwenda Gongolamboto Pugu  tayari umezindiliwa na walielekea pugu  viongozi mbali mbali akiwemo waziri wa uchukuzi pia mea wa jiji halikadhalika   mkuu wa mkoa,, na viongozi wa shirika la reli Tanzania.


 Kama unavyoona kwenye Picha hapo Juu Mh.Makame Mbarawa akiwa Na Mkuu Wa Mkoa Wa Dar es salaam Mh.Paul Makonda.

 
 Kesho (Jumatano) Chakua itafanya mazungumzo na mkurugenzi mtendaji wa shirika la reli Tanzania TRL  ofisini kwake makao makuu ya reli tanzania kuanzia saa tisa kamili.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni