Mtayarishaji

Morning Star Radio

Alhamisi, Januari 24, 2013

YASABABISHAYO MSONGO WA MAWAZO FAMILIANI



Family stressors

Kuzidiwa na majukumu
Mmoja kutoyaelewa majukumu yake 
Mgongano katika kuyatimiza majukumu ya kifamilia (rule conflict) 
Mapungufu katika kuyatekeleza majukumu ya mmoja 
Ukosefu wa kupeana zawadi au vichochezi pale mmoja anapofanya vema, (suprises and motivators)  
Mahusiano mabovu 
Ukosefu wa fedha 
Kutotoshelezeshwa katika tendo la ndoa

Tabia binafsi ambazo zaweza kuchangia katika kuleta msongo wa mawazo 

Mmoja kujisikia au kujithamini zaidi ya mwezake 
Kiwango cha juu cha hasira 
Mmoja kuchukulia kazi yake kuwa ya muhimu zaidi ya ile ya mwenzake 
Mapungufu katika mbinu za mahusiano, Mfano; mmoja hana tabia yakusema asante, au kutoa zawadi au hata kusema neno “nakupenda” 
Udhaifu katika afya ya mmoja

Dalili za kukuonyesha kuwa misongo ya mawazo ipo ndani ya familia 

Mahusiano nje ya ndoa 
Muda mwingi kazini hata kama hakuna kinachofanywa huko 
Malumbano kuzidi 
Mmoja kutokuwa tayari kumhudumia mwenzake katika tendo la ndoa “sexual withdrawal” 
Kuanza au kuzidi kwa matumizi ya vilevi 
Hali ya mmoja kupooza na kukosa raha wakati mwingi 
Uadui baina ya wanandoa

Matokeo ya kuzidi kwa dalili hizi 

Talaka au kutengana 
Mmoja kunyanyasika au wote kunyanyasana 
Unyanyasaji wa watoto (child abuse) nk. 
Visababishi toka nje ya familia (extrafamily stressors) 
Kazi 
Mahangaiko ya maisha 
Familia kubwa (extended family) 
Kukosa kazi 
Mshahara mdogo kazini 
Matatizo ya shule (hasa kwa wale wanaosoma wakiwa ndani ya ndoa) 
Kukosa elimu (kwa wale ambao hawakubahatika kusoma)

Matokeo ya misongo hii kiafya baina ya wanandoa 

Kuongazeka kwa matatizo ya shinikizo la damu 
Kuongezeka kwa matatizo ya misuli (muscle tention) 
Kuongezeka kwa mapigo ya moyo 
Kuongezeka kwa kasi ya mfumo mzima wa upumuaji (breathing system)

Hali hii inapozidi kwa wanandoa tunategemea yafuatayo 

Magonjwa ya moyo 
Shinikizo la damu 
Vidonda vya tumbo (ulcers) 
Maumivu makali na ya mara kwa mara ya kichwa 
Maumivu ya mara kwa mara ya mgongo 
Hypertension 
Saratani (cancer) 
Hofu kubwa katika baadhi ya vitu ( allergic reaction)

Msongo wa mawazo juu ya masuala ya uzazi wa mpango
 

Pangeni ninyi wawili kukutana na kuzungumza na mshauri, hili sio jambo la mmoja wenu bali wote. Fanyeni chaguzi fasaha ni njia ipi ya uzazi wa mpango mtaiweza na mtaipenda. Tafuteni taarifa Muhimu za kuhusu uzazi wa mpango toka kwa wataalamu, marafiki, ndugu, vitabu, na vujarida husika, msitegemee taaria za uzushi zisizoweza kuaminika. Yamkini njia nyingine zitakingana na imani au misimamo yako binafsi, basi pata ushauri toka kwa kiongozi wako wa dini. Katika kuyatimiza haya yote shirikianeni kwa upendo katika kuelekezana na kukumbushana juu ya ushauri mlioupata.

Msongo wa mawazo unaosababishwa na mzazi mmoja kuwa mbali na familia 

Panga kuitembelea familia yako kila upatapo nafasi zaidi ya kwenda maeneo mengine. Wasiliana nao kwa simu mara kwa mara, hii inaruhusu muda wa maongezi na kujuliana hali. Njia nyingine isiyo ya gharama sana ni kutumiana barua, hapa ninatia msisitizo katika barua na sio kadi. Kadi kama za siku za kuzaliwa na nyingine hazina uzito mkubwa wa mawasiliano kama ule uliopo katika barua. Lazima familia yako ijue kuwa unatumia jitihada zako zote katika kuwasiliana nao hii itawajengea haja moyoni ya kutaka kukujibu.

Misongo ya mawazo inayoletwa na masuala ya fedha 

Stress zinazisababishwa na masuala ya fedha ni mbaya sana, zaweza kuvunja mahusiano baina ya wanafamilia, zaweza kuleta matatizo kiafya hasa pale matibabu yanapocheleweshwa mpaka mgonjwa azidiwe sana, kwasababu ya ukosefu wa fedha. Hali hii huwafanya wanafamilia kuwa na hisia mbaya, kutojithamini, na kutojipenda, hali ya kujitawala kwao hushuka maana hamna mwenye uhakika na maisha.

Jinsi ya kukabiliana na misongo hii.

Jifunzeni kuwa na bajeti ya mapato na matumizi ya familia, bajeti hii itawasaidia kupunguza madeni, ambayo kama yasipolipwa huleta stress zaidi na maranyingine kushitakiwa kisheria. Bajeti pia itawasaidia ninyi kutawala fedha zenu zaidi ya fedha zenu kuwatawala ninyi. Namna nzuri ya kuandaa bajeti ni kupiga picha nyuma, nijinsi gani mlitumia fedha mwakajana, au mwezi uliopita. Angalia vyanzo vyenu vya mapato, vile vikubwa na vile vidogovidogo. Wakati wote jitahidi sana matumizi yasije yakawa ya kasi kubwa kuliko kasi ya kuingiza. Fahamu ni vitu vipi hutumia fedha zenu zaidi, matumizi haya yawe ya lazima na yakishatimizwa yote ndio mwaweza kufikiria matumizi mengine ya anasa.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni