Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Januari 01, 2013

Asili na hatma ya mwisho wa ulimwengu

Ingawa mfano wa Mlipuko Mkubwa ulipambana na mashaka mengi ulipozinduliwa kwa mara ya kwanza, shaka iliyochangiwa na uhusiano na dhana ya dini ya uumbaji, imekuja kuungwa mkono na uchunguzi kadhaa wa kujitegemea. Hata hivyo, fizikia ya sasa inaweza kuelezea tu ulimwengu wa mapema kutoka sekunde 10_"43 baada yaMlipuko Mkubwa (ambapo muda sufuri unawiana na kipimo joto kinafikia idadi isiyopimika), nadharia fulani ya mvuto wa kikwontamu huenda ikahitajika kurudi nyakati zazaidi. 

Hata hivyo wanafizikia wengi wamedadisi kuhusu nini kinachoweza kuwa kimetangulia kikomo hiki, na jinsi ulimwengu ulivyoanza. Baadhi ya wanafizikia hudhani kuwa Mlipuko Mkubwa ulitokea kiajali, na wakati kanuni ya kianthropiki inapozingatiwa, mara nyingi hutafsiriwa kama kuashiria kuwepo kwa ulimwengu maridhawa.

Hata hivyo, haijalishi jinsi ulimwengu ulikuja kuwepo, hatma ya binadamu katika ulimwengu huu ni maangamizi kwani - hata kama ubinadamu utaishi muda huo wote - maisha ya kibaiolojia hatimaye yatashindwa kujiendeleza, iwe kupitia Kuthelujika Kukubwa, Kuraruka Kukubwa au Kupasuka Kukubw]. Ni bayana kuwa njia pekee ya kuishi milele itakuwa kuuongoza mtiririko wa nishati kwenye Kiasi cha Kikosimki na kuibadilisha hatma ya ulimwengu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni