Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Oktoba 22, 2012

UCHANYA WA KIMANTIKI



Wachanya wa kimantiki huuliza: Ni nini maana ya maisha? na mbona kuuliza?Kama hakuna maadili yanayolengwa, basi, hivyo ni kusema maisha hayana maana? Ludwig Wittgenstein na wachanya wa kimantiki walisema: "Linapoulizwa kilugha, swali ni la ubatili"; kwa sababu, maishani taarifa ya "maana ya x", kawaida inaashiria madhara ya x, au umuhimu wa x, au kile ambacho ni dhahiri kuhusu x na kadhalika, kwa hivyo, wakati dhana ya maana ni sawa na "x", katika taarifa ya "maana ya x", taarifa inakuwa ya kujirudia, na kwa hivyo, ya kiupuzi, au inaweza kutaja kama ukweli kwamba maisha ya kibaiolojia ni muhimu ili kuwa na maana maishani.

Mambo (watu, matukio) katika maisha ya mtu yanaweza kuwa na maana (umuhimu) kama sehemu ya uzima, lakini maana isiyobainika wazi ya maisha (hayo), yenyewe, mbali na mambo hayo, haiwezi kubainika. Maisha ya mtu yana maana (kwake mwenyewe, wengine) kama matukio ya maisha yanayotokana na mafanikio yake, urithi, familia, na kadhalika, lakini, kusema kwamba maisha, yenyewe, yana maana, ni matumizi mabaya ya lugha, kwani yoyote ya umuhimu, au ya mwisho, ni muhimu tu "katika" maisha (kwa walio hai), hivyo basi kuifanya taarifa iwe ya kimakosa. Bertrand Russell aliandika kwamba ingawa alipata kwamba chuki yake ya mateso haikuwa kama chuki yake ya mboga ya brokoli, hakupata utaratibu wowote wa kuridhisha, na wa kupimika wa kuthibitisha hili:
Tunapojaribu kuwa na uhakika, kulihusu kile tunachomaanisha tunaposema kuwa hiki au kile ndicho "Zuri," sisi hujipata katika matatizo makubwa sana. Tamko la Bentham, kwamba radhi ndiyo Zuri, lilizua upinzani mkali, na ilisemekana kuwa falsafa ya nguruwe. Yeye na wapinzani wake walishindwa kuibua hoja zozote. Katika swali la kisayansi, ushahidi unaweza kupatikana kutoka pande zote mbili, na mwishowe, upande mmoja unabainika kuwa na hoja bora - au, kama hili halitokei, swali linabaki kama halijajibiwa. Lakini katika swali, kuhusu ikiwa hili, au hilo, ndilo mwisho Mzuri, hakuna ushahidi, kwa vyovyote vile; kila mtetezi anaweza kupendekeza tu hoja kulingana na hisia zake, na kutumia vifaa vya ushawishi ambavyo vitaibua hisia sawa katika wengine. . . Maswali kuhusu "maadili" - yaani, kuhusu kile ambacho chenyewe ni kizuri kibaya , bila kutilia maanani madhara yake - yanapatikana nje ya uwanja wa sayansi, jinsi watetezi wa dini wanavyodai kwa msisitizo. Nadhani kwamba, katika hili, wako sawa, lakini, mimi napata hitimisho zaidi, ambalo hawapati, kwamba maswali kuhusu "maadili" yanapatikana kabisa nje ya uwanja wa maarifa. Hiyo ni kusema, tunaposema kwamba hili, au lile, lina "thamani", sisi tunaeleza tu hisia zetu wenyewe, si ukweli, ambao bado ungalikuwa kweli ikiwa hisia zetu za binafsi zingalikuwa tofauti.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni