Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Juni 25, 2012

USAFI WA MOYO




Hili neno hutumika mara nyingi kuelezea adili ambalo linapingana na uzinifu na kutegemea kiasi. Kwa maana hiyo unawahusu watu wanaojua kutawala maelekeo ya kijinsia yaweze kujenga maisha yao binafsi, familia na hata jamii.

Neno hilo lilivyotumiwa na Yesu katika Hotuba ya mlimani lina maana pana zaidi na kuhusisha unyofu wa dhamiri kwa jumla.

Adili, ni uzoefu wa kutenda kiutu.

Huko Ugiriki katika karne ya 5 K.K. wanafalsafa Plato na hasa Aristotle waliorodhesha maadili mengi yanayotegemea nne za msingi (maadili bawaba): busara, haki, nguvu na kiasi. Zaidi ya hayo, walionyesha kwamba haiwezekani kujipatia adili moja tu, bali uadilifu unadai mtu awe na maadili yote. Kwa mfano, haiwezekani kuwa mtu wa haki pasipo busara.

Katika Ukristo, juu ya maadili ya kiutu, mwamini anatakiwa kupokea maadili ya Kimungu yaliyoorodheshwa na mtume Paulo, yaani imani, tumaini na upendo ambayo yanaendana vilevile.

Maadili bawaba:
Ni maadili manne ya kiutu yaliyojulikana na wanafalsafa wa Ugiriki, hasa Plato na Aristotle, kuwa ndiyo yanayotegemeza maadili mengine yote ya kiutu, kama vile bawaba zinavyotegemeza mlango uweze kufanya kazi yake vizuri. Yanaitwa pia maadili ya kiutu ya msingi au fadhila za msingi, kwa kuwa ndiyo hasa yanayomfanya mtu atende kadiri ya utu wake.

Majina yake ni: busara, haki, nguvu na kiasi.
Katika Ukristo yanatofautishwa na maadili ya Kimungu, yaani imani, tumaini na upendo ambayo yanatokana na Mungu na kumlenga yeye.

Maadili ya kiutu:
Ni yale yanayotakiwa kupatikana katika binadamu yeyote ili aweze kutenda kwa uadilifu kadiri ya utu wake unaomtofautisha na wanyama, yaani hasa akili inayomwezesha kufikiria na kuelewa maana na matokeo ya matendo yake.

Kadiri ya wanafalsafa wa Ugiriki wa kale Plato na Aristotle, maadili hayo ni mengi (si chini ya 40), lakini yanategemea manne (maadili bawaba): busara, haki, nguvu na kiasi.
Katika Ukristo maadili ya Kimungu ni yale yanayotokana na Mungu na kumwezesha binadamu kuhusiana naye inavyotakiwa, yaani kwa:
Kwa maadili hayo, yale ya kiutu yanakuwa hai na bora, kwa mfano wa Yesu Kristo. Kadiri ya Kanisa Katoliki, tofauti na yale ya kiutu, maadili ya Kimungu hayawezi kupatikana kwa juhudi anazofanya mtu, bali kwa neema tu: yanamiminiwa rohoni, yaani katika akili na katika utashi.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni