Hili Limeli linaitwa In Explorer of the seas,au kwa kiswahili ''Mvumbuzi
 wa bahari''.Meli hii ina kila aina ya huduma anayohiitaji mwanadamu,na 
baadhi ya huduma ni bora kuliko zinazotolewa na baadhi ya miji katika 
nchi mbali mbali.Meli hii yenye uwezo wa kubeba watu 3,100 inamilikiwa 
na kampuni ya kifalme ya kimataifa Caribbea.
 Dubwasha hii lina uzito wa 
zaidi tani 100,000,lina maduka yanayouza bidhaa mbali mbali kiasi cha 
kukufanya upate kila unachokihitaji,Lina viwanja vya michezo,kwa mfano 
uwanja wa mpira wa kikapu,mabwawa 3 makubwa ya kuogelea (swimming 
pools),kiwanja cha tenesi na gofu.
Lakini pia ukibahaitika kwenda kutanua
 kwenye dubwasha hili itakupasa kulipa kuanzia dola 400 kwa siku,na 
ndani yake utafaidi ukumbi wa sinema wa kisasa zaidi.Aidha ndani yake 
ili kukufanya ujihisi upo peponi,kuna kumbi za disko,baa za kisasa 
3,sehemu za kutereza kwenye barafu na kiwanja cha kupanda kwenye 
milima. 
 Kwa wale wanaopenda kufanya mazoezi ya kupunguza vitambi au 
kujiweka fiti ndani ya dubwasha hili kuna kiwanja malum cha Joging na 
sehemu ya kufanya mazoezi 'GIM'. Kwa upande wa hoteli ndio usiseme zipo 
hoteli za bei chee na za wenye nazo (matawi ya juu).Pia kuna 
Studio,Ukumbi wa wazi wa sinema 'Theatre',sehemu ya muziki wa 
dansi,garden kwaajili ya kupumzikia,sehemu ya kasino ya kawaida na ile 
ya maalum kwa watu wanaopenda mambo ya wakubwa.
Kuna maduka ya 
kubadilisha fedha,hospitali,kumbi za mikutano,ukumbi wa makumbusho ya 
picha za zamani,ukumbi wa michezo ya pool na darts.Katika meli hiii pia 
kuna sehemu maalum kwa wale wanaotumia internet,wanaokutana 
faragha,sehemu ya michezo ya kutereza kwenye maji.Kuna kituo cha kutoa 
ushauri nasaha wa mambo mbalimbali kimaisha,bila kukosekana kituo cha 
Polisi
.Baadhi ya watu badala ya kwenda 'Honey moon' hotelini kama 
tulivyozoea,wao hutumia muda huo wa kubembelezana kwenye meli hiyo.Cha 
kushangaza wenzetu huenda kupitisha bajeti zao ndani ya meli hii. 








 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni