Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Mei 12, 2012

PETE YA NDOA WALA HAINA CHIMBUKO LA KIDINI

“Fuatana nami katika historia hii fupi na yenye ukweli juu ya chanzo cha Pete ya ndoa”.
Historia 

Kumekuwa na maswali mengi juu ya chanzo hasa cha pete hiyo inayotumiwa katika harakati za ndoa’.
Wale walio na matazamo hasi juu ya matumizi ya pete, wamekuwa na sababu mbalimbali za kutetea msimamo huo hasa ni ile sababu kuwa “pete inafanya wazo la upendo kuwa la kinadharia” na ushahidi wa nje kuliko kuwa na chimbuko halisi la upendo wa ndani ya moyo. Lakini katika makala hii tutaona kwa kina juu ya historia halisi pete.

Pete ya ndoa ilianzishwa na watu wa Farao” Firauni” nchini Misri.
Historia inaonyesha kuwa karne ya 14, BC (kabla ya kristo), katika nchi hiyo ya Misri iliyo kaskazini mwa Afrika, watu wanchi hiyo chini ya mfalme wao Farao’ walianzisha utamaduni wa kuwekeana viapo vya uaminifu katika mahusiano yao ya kimapenzi na ndoa kwa kutumia pete.
Wananchi walilazimika kwenda kwenye ukingo wa Mto Nile ambapo huko walifanya matambiko ya kipagani na kuwekeana viapo vya uaminifu. Sherehe hiyo iliambatana na kuvalishana pete yenye umbo la duara baina ya mke na mume kwenye vidole vyao vya mkono wa kushoto.

Lengo, Maana yake’
Kwa kufanya hivyo wapagani wa Misri waliamini kuwa wameweka kiapo na ahadi ya kuto salitiana ambapo pia ilifuatiwa na kumvalisha mwanamke mkufu wa fedha na dhahabu au chuma kiunoni.
Umbo la duara la pete liliundwa hivyo kuashiria kuwa kifungo hicho cha ndoa ni cha milele kwa maisha yote.

Umbo la duara la pete na upagani’
Umbo hilo la duara la pete liliashiria imani kuwa viapo hivyo vilishuhudiwa na miungu miwili ya wamisri yaani mungu Jua’ na Mwezi ambao alama zake zilikuwa ni umbo hilo la duara la pete.
Pia uwazi huo wa pete “duara ya kati” ilimaanisha kuwa ndiyo mlango wa kuingilia katika maisha ya ndoa” na yakuwa ndoa hiyo na familia ijayo vinalindwa na miungu hiyo Jua’ na Mwezi daima.

Eneo la kuvaa pete na chimbuko lake’
Uamuzi wa kuvaa pete kwenye “kidole” kinachoitwa cha “Pete” ulifanyika kutokana na ushauri wa watalamu wa Sanyansi ya maumbile ya mwanadamu.
Wataalamu hao waliamini kuwa mshipa mkuu wa damu unaogawa damu mwilini toka moyoni (vein) unaunganika moja kwa moja na kidole hicho, hivyo pamoja na elimu ya kinajimu iliyotawala wakati huo bado ilishauriwa kuwa pete hiyo ivaliwe katika kidole hicho.

Kuenea kwa tendo hilo la uvaaji pete
Utamaduni huu wa kuvaa pete ulianza kuenea duniani baada mfalme Alexander, kuvamia nchi ya Misri, ambapo mambo yalovutia utawala huo ni pete ya ndoa.
Baadae Wagiriki walichukua utamaduni huo na kuubadilisha kidogo huku wakiwa na hofu ya kuwaudhi miungu hao Jua na Mwezi.

Miongoni mwa mambo yalofanywa kuhamasisha matumizi ya pete hiyo ni tendo la kuibadilisha jina na kuiita pete hiyo jina la kigiriki “evena amoris” yaani mshipa wa penzi” na kuruhusu itengenezwe kwa matirio tofauti kama pembe za ndovu, mifupa ya miguu, ngozi za wanyama nk.

SWALI:
Leo hii watoto wa Mungu wamechukua ibada hiyo’ na kuiweka katika maisha yao??????

“Unapovaa pete’ fanya ukijua kuwa haina chimbuko takatifu’

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni