Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Mei 22, 2012

HISIA HARIBIFU NA MAHUSIANO MAPYA



Msingi wa tiba mbadala (Alternative medicine) tofauti na tiba ya jadi (traditional medicine) na tiba ya hospitalini (Converntional medicine) ni kuwa 'Mgonjwa/mtu atibiwe kwanza na ugonjwa wake ufuatie baadaye' .

Msingi hasa wa kumtibu mgonjwa unaanzia kwenye mahusiano mapya na hisia haribifu za maisha yake ya kila siku KIMATENDO.


Kitu hasa cha kufanya ni hiki: TAMBUA BILA KUKWEPA , Hisia haribifu kila zinapojitokeza: Hiyo inatosha kabisa. Utakuwa umeshamaliza wajibu wako kwa Utambuzi huo!

Hasira, woga, chuki, wasiwasi na hisia haribifu nyingine, Zikijitokeza na kurudia tena na tena, tumia NGUVU YA UTAMBUZI wako kwa kupitia machapisho yahusuyo masuala ya kiroho ama nyimbo za injili zilizotulia, mfano; Gospel Classics. Hii itasaidia kuzitambua tena na tena. Usichoke! Jenga tabia ya kudumu ya kuzitambua tena na tena, kila zikijitokeza na kuzipuuzia mara moja!

Fanya hivyo kwa utulivu na utaratibu, usigombane nazo, kuvutana wala kupambana na hisia haribifu. Zitambue, tizama, tambua-tena, TULIA! Alafu endelea na shughuli zako. Jenga mazoea hayo ya kiutu, busara na hekima. Kuzitambua, kujiachamanisha na kuzipuuzia kwa utulivu! Ikiwezekana fanya tabia hiyo kuwa mtindo wa maisha yako yaani KUMUOMBA MUNGU MARA NYINGI NYINGI!

Hisia haribifu ni nyonge na dhaifu kwa UTAMBUZI wa mtu anayezitizama na KUTAMBUA TU , zimefichuliwa, zina- AIBIKA kwa hatua ulizochokua. Udhibiti wa namna hii unaupa mwili nguvu hai iliyo msingi wa afya na tiba ya kweli kwa kizazi cha sasa!


Huu ndio ukweli na siri ya udhaifu wa hisia haribifu, Msingi wa tiba kwenye chanzo.
Tumia BIBLIA yaani soma NENO LA MUNGU 'Tulia na utambue'. Fanya zoezi la kujenga tafakari ya utambuzi na kudhoofisha hisia haribifu kwa njia hiyo MUNGU ATAKUSAIDIA.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni