Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Februari 03, 2016

ENEO LENYE PWANI YA BARIDI - SVALBARD


TUNASAFIRI kwa ndege katikati ya mawingu mazito na hivyo hatuwezi kuona chochote. Kwa ghafula, ndege yetu inatoka kwenye mawingu na chini yetu tunaona eneo la Aktiki lililofunikwa kwa theluji. Mandhari hiyo inapendeza kama nini! Tunapotazama mabamba ya barafu, mikono ya bahari, na milima iliyofunikwa kwa theluji, tunastaajabu. Ni kana kwamba eneo hilo lisilo na mimea lililofunikwa kwa theluji na barafu halina mwisho. Tumekuja kutembelea Svalbard, visiwa vilivyo karibu na Ncha ya Kaskazini, kati ya digrii 74 za latitudo na digrii 81 kuelekea kaskazini!

Jina Svalbard, linalomaanisha “Pwani Baridi,” lilionekana kwa mara ya kwanza mnamo 1194 katika maandishi ya Waiceland. Lakini eneo hilo “liligunduliwa” miaka 400 baadaye, mnamo 1596 na hivyo likajulikana ulimwenguni pote. Mwaka huo kikundi cha wagunduzi Waholanzi kikiongozwa na Willem Barents kilikuwa kikisafiri kwa meli kuelekea kaskazini wakati ambapo mmoja kati yao aliona kwenye upeo wa macho yake eneo lisilojulikana, safu ya milima yenye ncha. 

Wagunduzi hao walikuwa kwenye eneo la kaskazini-magharibi mwa Svalbard, naye Barents aliita eneo hilo “Spitsbergen” jina linalomaanisha “Milima Iliyochongoka.” Hilo ndilo jina la kisiwa kikubwa zaidi kati ya visiwa hivyo. Ugunduzi wa Barents ulianzisha kipindi chenye utendaji mwingi huko Svalbard. Utendaji huo ulitia ndani kuvua nyangumi, sili, kuwakamata wanyama, kugundua maeneo mapya, kuchimba makaa ya mawe, kufanya utafiti wa kisayansi, na utalii. Kwa miaka mingi, nchi kadhaa zimeshiriki katika utendaji huo, lakini kuanzia mwaka wa 1925 visiwa hivyo vimekuwa chini ya utawala wa Norway.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni