Ndugu mpendwa, ni vyema sana kuwa nawe tena katika eneo hili. 
Tuko
 hapa duniani katika kipindi cha ajabu katika historia yake. Nafasi zetu
 karibu hazina kipimo, na bado tunakumbana pia na changamoto nyingi, 
baadhi yazo za kipekee kwa wakati wetu.
Tunaishi
 katika ulimwengu ambapo maadili yametupiliwa mbali kwa kiasi kikubwa, 
ambapo dhambi imeanikwa wazi, na ambapo majaribu kupotoka kutoka kwenye 
njia nyembamba na iliyosonga yanatuzunguka. Tunakabiliwa na mashinikizo 
yasiyokoma na ushawishi wa kudanganya unaoharibu kile ambacho ni cha 
heshima na kujaribu kukibadilisha na falsafa na utamaduni duni.
Kwa
 sababu hizi na changamoto zingine, maamuzi daima yako mbele yetu ambayo
 yanaweza kuamua hatima yetu. Ili kwetu sisi kufanya maamuzi sahihi, 
ujasiri unahitajika---ujasiri wa kusema hapana wakati tunapaswa, ujasiri
 wa kusema ndio wakati inafaa, ujasiri wa kufanya jambo la haki kwa 
sababu ni la haki.
Kwa
 sababu viwango vya jamii hivi sasa kwa haraka vinaachana kwa mbali na 
maadili na kanuni ambazo Bwana ametupa, sisi bila shaka tutaitwa kutetea
 kile ambacho tunaamini. Je, tutakuwa na ujasiri wa kufanya hivyo?
Rais
 J. Reuben Clark Jr., ambaye kwa miaka mingi alikuwa mshiriki wa Urais 
wa Kwanza, alisema: “Zinajulikana kesi ambapo [wale] wa imani ya 
kudhaniwa … wamehisi kwamba, kwa sababu ya kudhibitisha imani yao kamili
 huenda wakajiitia kejeli ya wenzao wasioamini, lazima aidha warekebishe
 au kuelezea vyema imani yao, ama kuizimua kiuangamizi, ama hata 
kujifanya kuitupilia mbali. Watu kama hao ni wanafiki.” Hakuna yeyote miongoni mwetu angependa kuitwa mnafiki, na bado tunasita kutangaza imani yetu katika hali fulani. ?
Tunaweza
 kujisaidia katika hamu yetu ya kufanya mema tukijiweka katika maeneo na
 kushiriki katika shughuli ambapo mawazo yetu yanashawishiwa kwa ajili 
ya mema na ambapo Roho wa Bwana atasikia vizuri kuwa.
Nakumbuka
 nikisoma hapo awali ushauri ambao baba alimpa mwanawe wakati akienda 
shule: “Ukiwahi kujipata mahali ambapo haupaswi kuwa, ondoka!” Nawapa 
kila mmoja wenu ushauri huo huo: “Ukijikuta wakati wowote mahali ambapo 
haupaswi kuwa, ondoka!”
Sote
 tunahitaji kila mara kuwa na ujasiri. Kila siku ya maisha yetu ujasiri 
unahitajika---si tu kwa ajili ya matukio makubwa, lakini mara nyingi 
zaidi tunapofanya maamuzi ama kutenda kwa ajili ya hali zilizo karibu 
nasi. Mshairi na mwandishi Mskoti Robert Louis Stevenson alisema: “Kila 
siku ujasiri una mashahidi wachache. Lakini ujasiri wako bado una 
heshima hata kama hakuna anayekutia moyo na hakuna umati unaokusifu.”
Ujasiri
 huja kwa njia nyingi. Mwandishi Mkristo Charles Swindoll aliandika: 
“Ujasiri hauko tu kwenye uwanja wa vita … ama kwa kumshika kiushujaa 
mwizi katika nyumba yako. Vipimo halisi vya ujasiri ni kimya sana. Ni 
majaribio ya kindani, kama vile kubaki mwaminifu wakati hakuna mtu 
anayeangalia, … kama kusimama peke yako wakati watu hawaelewi imani 
yako.” 
Ningeongezea kwamba ujasiri huu wa ndani pia unajumuisha kufanya jambo 
la haki hata kama huenda kuwa unahofia, kutetea imani yetu katika hatari
 ya kudharauliwa , na kudumisha imani hizo hata baada ya kutishwa na 
kupoteza marafiki ama hadhi ya kijamii. Yule ambaye anasimama dhabiti 
kwa yale ambayo ni ya haki lazima ahatarishe kuwa wakati mwingine 
hakubaliwi na kukosa umaarufu.
Mtu mmoja alipokuwa akihudumu katika Jeshi la Majini la Marekani alikuja kujua kuhusu 
matendo ya ujasiri, matukio ya ushujaa, na mifano ya ujasiri. Mmoja 
ambao kamwe hakuwahi sahau ilikuwa ujasiri usio wazi wa mwana maji wa 
umri wa miaka 18---sio wa imani yetu---ambaye hakuogopa kusali. 
Kwa watu
 250 katika kitengo chetu, alikuwa ndiye peke yake ambaye kila usiku 
alipiga magoti kando ya kitanda chake, wakati mwingine akiwa anakejeliwa
 na kuchekwa na wasioamini. Akiwa ameinamisha kichwa, alimwomba Mungu. 
Kamwe hakuogopa kuomba. Kamwe hakuyumba. Alikuwa na ujasiri.
Muda
 mfupi uliopita, nilisikiliza mfano wa mtu ambaye hakika alionekana 
kukosa ujasiri huu wa ndani. Rafiki alisimulia kuhusu mkutano wa kiroho na wa kukuza imani ambao yeye na mumewe walikuwa 
wamehudhuria katika kata yao. 
Mvulana aliyekuwa katika ofisi ya mkuhani 
katika Ukuhani wa Haruni aligusa mioyo ya mkusanyiko mzima 
alipozungumzia kweli za injili na furaha za kutii amri. Alishuhudia kwa 
dhati akisimama kwenye mimbari, akionekana kuwa msafi na nadhifu akiwa 
amevaa shati yake nyeupe na tai.
Baadaye
 siku hiyo hiyo, mwanamke huyu na mumewe walipokuwa wanaondoka kule, 
walimuona mvulana yule yule ambaye alikuwa amewavutia sana saa chache tu
 awali. Sasa, hata hivyo, alionekana kubadilika kabisa akitembea 
barabarani akiwa amevaa nguo chafu---na anavuta sigara. 
Rafiki yangu na 
mumewe hawakuwa wamesikitishwa sana na kuhuzunika tu, lakini pia 
walichanganyikiwa na jinsi angeweza kusadikisha kuonekana kuwa mtu mmoja
 katika mkutano wa kiroho na kisha haraka hivyo kuonekana kuwa mtu 
mwingine kabisa.
Ndugu,
 je, wewe ni mtu yule yule popote ulipo na katika chochote 
unachofanya---mtu Baba yetu wa Mbinguni anataka uwe na mtu unajua 
unapaswa kuwa?
Katika
 mahojiano yaliyochapishwa katika gazeti la kitaifa, mchezaji 
aliyejulikana wa mpira wa kikapu wa NCAA Mmarekani anayeitwa Jabari 
Parker, mshiriki wa Kanisa, aliombwa ashiriki ushauri bora kabisa 
aliokuwa amepokea kutoka kwa baba yake. Jabari alijibu, “[Baba Yangu] 
alisema, kuwa mtu yule yule unapokuwa peke yako na vivyo hivyo unapokuwa
 mbele ya watu.” Ushauri muhimu, ndugu zangu, kwetu sisi sote.
Maandiko
 yetu yamejaa mifano ya aina ya ujasiri unaohitajika na kila mmoja wetu 
leo. Nabii Danieli alionyesha ujasiri mkuu kutetea aliyoyajua kuwa ya 
haki na kwa kuonyesha ujasiri wa kuomba, ingawa alitishwa na kifo kama 
angefanya hivyo.
Abinadi aliishi maisha ya ujasiri, ilivyoonyeshwa na kukubali kifo badala ya kukana ukweli.
Sisi
 sote tunavutiwa na maisha ya vijana askari 2,000 wana wa Helamani, 
waliofundisha na kuonyesha umuhimu wa kuwa na ujasiri wa kufuata 
mafundisho ya wazazi, kuwa waadilifu na wasafi?
Pengine
 kila moja ya hadithi hizi za maandiko zimepambwa na mfano wa Moroni, 
ambaye alikuwa na ujasiri wa kustahimili katika haki hadi mwisho
Katika
 maisha yake yote, Nabii Joseph Smith alitoa mifano isiyohesabika ya 
ujasiri. Mojawapo wa mfano mkubwa zaidi ulitokea wakati yeye na ndugu 
wengine walifungwa minyororo pamoja---fikiria, kufungwa minyororo 
pamoja---na kufungiwa katika nyumba ambayo haijamalizika karibu na jumba
 la mahakama kule Richmond, Missouri. Parley P. Pratt, ambaye alikuwa 
miongoni mwa wale waliofungwa, aliandika kuhusu usiku mmoja: 
“Tulikuwa 
tumelala ni kama tuko usingizini mpaka saa ya usiku wa manane kupita, na
 tulikuwa tumehuzunika sana, wakati tulikuwa tumesikiliza kwa masaa 
kejeli mbaya, maneno mabaya, kashfa kubwa na lugha chafu ya walinzi 
wetu.”
Mzee Pratt aliendelea:
“Nilikuwa
 nimesikiliza hadi nikachukizwa, nikasikitika, nikahudhika , na kujawa 
na roho ya haki ya kukasirika kwamba ilikuwa vigumu kwangu kujizuia 
kusimama na kuwakemea walinzi, lakini [mimi] sikuwa nimemwambia Joseph 
chochote, ama mtu yeyote mwingine, ingawa nilikuwa nimelala karibu naye 
na nilijua kwamba alikuwa macho. Ghafla, alisimama na kuzungumza kwa 
sauti ya nguvu kama mgurumo wa simba, akisema, vyema ninavyoweza 
kukumbuka, maneno yafuatayo:
“‘NYAMAZENI.
 ... Katika jina la Yesu Kristo nawakemea ninyi, na kuwaamurisha mtulie;
 sitaishi dakika ingine na kusikia lugha kama hiyo. Komeni kuongea 
hivyo, ama ninyi au mimi nife SAA HII!’”
Joseph
 “alisimama wima katika enzi ya kutisha,” kama ilivyoelezwa na Mzee 
Pratt. Alikuwa amefungwa kwa minyororo, bila silaha, na bado alikuwa 
mtulivu na mwenye heshima. Aliwaangalia walinzi waliohofia, ambao 
walikuwa wanarudi nyuma kwenye kona wakijikunyata miguu. Watu hawa 
walioonekana kutorekebishika waliomba msamaha kwake na wakabaki kimya.
Si
 vitendo vyote vya ujasiri huleta matokeo ya kuvutia kama hayo ama ya 
mara moja, na bado yote huleta amani akilini na maarifa kwamba haki na 
ukweli umetetewa.
Ni
 vigumu kusimama wima wakati mtu anapanda mizizi yake kwenye changarawe 
inayonyong’onyea ya maoni na idhinisho linalobobea. Ujasiri kama ule wa 
Danieli, Abinadi, Moroni ama Joseph Smith unahitajika ili tubaki imara 
na dhabiti kwa yale tunayojua ni mema. Walikuwa na ujasiri wa kufanya 
kile ambacho akikuwa rahisi, bali kile kilichokuwa sahihi.
Sote
 tutakumbana na hofu, tutakejeliliwa, na kukutana na upinzani. Acheni 
sisi —sisi sote—tuwe na ujasiri kushinda yanayopendelewa na wengi, 
ujasiri wa kutetea kanuni zetu. Ujasiri, si kuridhisha, hutuletea 
tabasamu ya idhini ya Mungu. Ujasiri unakuwa sifa ya uwezo na ya kuvutia
 wakati unachukuliwa si tu kama nia ya kufa kidume lakini pia kama 
uamuzi wa kuishi kwa heshima. 
Tunavyosonga mbele, tukijitahidi kuishi 
kama tunavyopaswa, hakika tutapokea msaada kutoka kwa Bwana na tunaweza 
kupata faraja katika maneno Yake. Naipenda ahadi Yake katika kitabu cha 
Yoshua: “Sitakupungukia wala sitakuacha. …
“...Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.”
Ndugu yangu mpendwa, kwa ujasiri wa imani yetu, tutangazeni, pamoja na Mtume Paulo, “Siionei haya Injili ya Kristo.”Kisha,
 kwa ujasiri huo huo, tufuateni ushauri wa Paulo : “Uwe kielelezo kwao 
waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo, na katika roho na 
imani na usafi.”
Migogoro
 ya janga huja na kwenda, lakini vita vinavyopigwa kwa nafsi za watu 
vinaendelea bila kukoma. Kama mwito linakuja neno la Bwana kwenu, kwangu
 mimi, na kwa wenye ukuhani kila mahali: 
“Kwa sababu hiyo, sasa acha 
kila mtu na ajifunze wajibu wake, na kutenda kazi katika ofisi ambayo 
ameteuliwa, kwa bidii yote.” Kisha tutakuwa, kama vile Mtume Petro alivyotangaza, hata “ukuhani wa kifalme,”na umoja katika kusudi na kubarikiwa na nguvu kutoka mbinguni.
Acha
 kila mmoja wetu aondoke siku ya leo akiwa na dhamira na ujasiri wa 
kusema, pamoja na Ayubu wa kale, “Kwa kuwa uhai wangu ukali mzima ndani 
yangu,...sitajiondolea uelekevu wangu.” 
Naomba kwa unyenyekevu kwamba hii iweze kuwa hivyo katika jina la Yesu Kristo, Bwana wetu, Amina.

 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni