Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumapili, Novemba 10, 2013

DARASA LA UIMBAJI



John Shabani akiwa na baadhi ya wanafunzi wenzake wa sauti

(SIFA NA MBINU ZA KUWA MWIMBAJI BORA)

SINGING COURSE 

Jinsi ya kuponya na kutunza Sauti yako
 
Weka  sauti yako katika afya nzuri ili uweze kuendelea kuimba!
Kila mtu anaweza kutumia sauti yake, lakini si kila mtu anajua jinsi ya kutunza afya ya sauti yake, au nini cha kufanya kunapotokea tatizo katika sauti. Makala hii itasaidia kila mtu kujifunza jinsi ya kuponya sauti zao  na pia kutoa ushauri wa jinsi ya kutunza afya yake na kuwa nguvu ile ile kwa ajili ya siku zijazo.
Mambo  unayo hitaji au ya kuzingatia kama mwimbaji
  • maji kwa uwingi
  • ngumu pipi, mints, nk
  • mvuke (moto oga)
  • Koo kanzu chai
  • asali
  • limao
Maelekezo
o    1 Kama sauti yako imejeruhiwa,  jambo muhimu zaidi la kufanya hivi sasa ni kuacha kutumia kwa muda. Sauti inahitaji kupumzika pia. Punguza mazungumzo yako na hasa kupayuka na kupaza sauti, kujifunza kuzungumza zaidi kwa ufupi, na kutumia zaidi kidogo muda katika ukimya.

o    2  Jambo jingine kubwa ambalo husaidia sauti iliojeruhiwa ni  chai ya moto pamoja na limau kidogo na asali. chai nzuri ni ile iliyo shauriwa ki afya na si kila chai ni bora. Unaweza kupata na dawa za mitishamba katika duka la dawa,  ambazo ni maalumu kwa ajili ya sauti, Kunywa angalau kikombe asubuhi na kikombe wakati wa usiku.

Mwl. John akielekeza matumizi ya asali

 
MAFUNZO YA SAUTI

By John Shabani
Mobile: 0716560094, 0754818767
Facebook: John Shabani



Mambo ya msingi yanayofunzishwa katika program hii:
Ø  Historia ya uimbaji
Ø  Tofauti ya mwimbaji na mwanamuziki
Ø  Vyakula na vinywaji vinavyofaa na visivyofaa
Ø  Sifa na mbinu za kuwa mwimbaji bora
Ø  Jinsi ya kuitunza na kuiponya sauti yako
Ø  Amri 10 za sauti
Ø  Matumizi ya kipaza sauti (Microphone technique)
Ø  Utunzi wa nyimbo
Ø  Mazoezi ya viungo yanayofaa kwa mwimbaji na faida zake
Ø  Ushauri kwa wanaotaka kurekodi nyimbo

Kuimba ni kutamka maneno katika hali ya ki-muziki au pia twaweza kusema ni kutamka maneno moja baada ya jingine kwa sauti yenye lahani (sauti ya ala ya muziki, tuni) au ghani

Kama vile tulivyo na ala za aina mbalimbali, mwimbaji naye pia anazo ala mbili muhimu:
·         Mdomo wenye uwezo wa kutoa sauti ya uimbaji
·         Mwili
Kumbuka moja ya vitu vya msingi katika uimbaji ni nguvu (energy) “As you sing higher, you must need more energy, as you sing lower, you must useless”. Zipo nguvu za kiroho na za kimwili. Ili kuwa na nguvu za kimwili unahitaji maji ya kutosha, chakula kizuri pamoja na  mazoezi ya viungo. 

MAZOEZI NA FAIDA ZAKE
 
 
Pamoja na faida nyingi za mazoezi lakini pia mazoezi huchangamsha mwili, hulainisha koo, husaidia kuwa na pumzi ya kutosha, hukuhepusha au kupunguza baadhi ya magonjwa kama kisukari, presha n.k, hung’arisha ngozi, na kusaidia mfumo wa mzunguko wa damu, MAZOEZI HUSAIDIA KATIKA MFUMO WA USAGAJI CHAKULA KUWA MZURI , KUKUPA NGUVU NA KUWEZA KUFANYA KAZI KWA NGUVU ZAKO BILA KUJISKIA UMECHOKA NA MWISHO WA SIKU HUPUNGUZA MAFUTA MWILINI,  HUPUNGUZA UZITO, KUNYOOSHA NA KUIMARISHA MISULI YA MWILI, HUSAIDIA MAPIGO MAZURI YA MOYO KWA KUONGEZA KASI YA MAPIGO YAKE WAKATI WA MAZOEZI, UNGUZA MRUNDIKO WA DAMU KWENYE MISHIPA, HII NI MUHIMU KWA SABABU MGANDO WA DAMU HUSABABISHA MAGONJWA YA MOYO PAMOJA NA KUPOTEZA FAHAMU, MAZOEZI HUIMARISHA MIFUPA YA MWILI, HUBORESHA USINGIZI.

Fikiria mwenyewe kama mwanamichezo au mtu wa fani fulani na jifunze kuwa mtu wa kula na kunywa kulingana na fani yako: Aina ya chakula na kinywaji na muda  wa kutumia ni jambo la kuzingatia sana. Kula na kunywa ni muhimu lakini Jiepushe na ulafi kwani huleta uchovu, mfumo wa kupumua kuathirika na wakati mwingine kusababisha magonjwa.


Kuna misimu fulani kama msimu wa vumbi au baridi kali au alegi au matatizo mengine kibao, wakati mwingine aina fulani ya dawa kwa ajili ya ugonjwa fulani, Wakati mwingine husababisha mafua au kutokwa na kamasi mara kwa mara au kukausha koo kabisa, hivyo husumbua sana na kuathiri mfumo wako wa kuimba. Wakati mwingine mazingira ya shughuli au kazi tuzifanyazo au pia mazingira ya makazi huweza kuathiri sauti zetu. Hivyo masomo ya utunzaji wa sauti ni ya muhimu sana.

Vilaji na vinywaji visivyofaa Kabla ya kuimba

Kuhusu chakula, ni muhimu ili kuepuka kuimba  tumbo likuwatupu kabisa. Kuimba ni kama riadha, inahitajika nguvu kwa ajili ya utendaji wako. Hata hivyo, ni muhimu pia kuepuka kuimba tumbo likiwa limeshiba sana. Yapo madhara mengi yanayotokana na shibe. Unaweza ukawasiliana na mwalimu wa sauti ili kujua madhara hayo. Kumbuka kuimba ni kazi ngumu, unahitaji mafuta (you need fuel), hivyo inashauriwa kuwa na mlo wa kawaida wa saa moja au mbili kabla ya uimbaji ni bora zaidi.

Kulingana na mazoea yetu vipo vyakula na vinywaji ambavyo ni vigumu kuachana navyo ghafla, mengine huchukua muda. Lakini hata hivyo kwa ajili ya kutunza koo (Mashine inayozalisha sauti) pamoja na kujihepusha na madhara yanayoweza kujitokeza unapokuwa na shughuli nzito ya uimbaji, ni muhimu ujihepushe navyo. Nitakuambia kwa ufupi kuhusu vyakula visivyofaha unapokuwa na shughuli za uimbaji. Kwasababu za msingi si rahisi kukutajia kwa undani madhara ya baadhi ya vyakula au vinywaji, wasiliana na mwalimu kwa wakati wako.

Baadhi ya vyakula na vinywaji vya kuepuka kabla ya kuimba ni kama vile:

  • Vinavyoleta mwasho au kukera koo (throat irritants): vyakula au vinywaji vinavyochangamsha, kusisimua au kulewesha (Overly spicy foods) ,  kama vile kahawa na pilipili, vinywaji baridi sana, sukari iliyosafishwa, chocolate.
  • Jamii ya vitu vyenye alkoholi, Sigara, tumbako, bangi, ugoro na aina yoyote ya madawa ya kulevya
·         Vyakula vinavyoongeza mucous (sehemu ya kiwambo cha seli inayozunguka mfereji wa chakula): maziwa, koni, malai/maziwa yenye ubarafu (ice cream), maziwa mgando na aina nyingine ya maziwa (dairy products)
  • Vyakula vinavyofanya koo kuwa kavu: matunda jamii ya machungwa, pombe
  • Soda na aina ya vinywaji vinavyochemsha au vinavyojaza gesi au hewa katika tumbo
  • Vyenye ubaridi sana au barafu: husababisha koo kubana, kuminywa au kunyongwa.
·         Vyakula vinywaji vyenye ubarafu na pombe (ikiwa ni pamoja na mvinyo na bia). Kuna baadhi ya watu pia huwa na alegi (kwa mfano, baadhi ya waimbaji wana shida na matunda jamii ya machungwa, ngano, karanga, samakigamba au soya).
·         Vyakula vyenye mafuta mengi

Ili kuwa na afya nzuri katika mwili na katika uimbaji wako zingatia :
·         Punguza  matumizi mengi ya sukari, ongeza matumizi ya matunda
·         Punguza kula nyama nyekundu, ongeza matumizi ya mbogamboga
·         Punguza matumizi ya soda, ongeza matumizi ya maji
·         Punguza kuendesha, ongeza kutembea kwa miguu
·         Punguza kupoteza muda wa kulala, Zingatia kulala kwa wakati
·         Punguza msongo wa mawazo, ongeza kupumzika

Zingatia :
·         Maji ya moto au aina ya chai mitishamba (herbal tea) ni bora, Mwimbaji mzuri hutumia class 8 za maji kwa siku, wapo ambao hutumia hadi lita 4 pia yapo maji ya ziada kutoka katika vyakula.
·         Kupasha sauti kwa kukohowa kohowa sio njia ya kukusaidia kuimba vizuri, badala yake hukata sauti
·         Pamoja na umuhimu wa maji, lakini acha matumizi ya maji mengi saa moja au mbili kabla ya kuanza uimbaji badala yake asali ni bora zaidi. Lakini pia sauti ikipatwa na tatito unaruhusiwa kupata maji ya moto pamoja na asali
·         Angalizo kuhusu mazoezi: Mazoezi huwa yana ugumu wake hasa pale unapokuwa unaanza, usikate tamaa wala usikubali uvivu au maumivu yakakurudisha nyuma. Jitengee muda maalum kwa ajili ya kufanya mazoezi na usianze kwa kufanya mazoezi magumu bali anza na mepesi mepesi ili kuupa mwili nafasi ya ku-adopt mabadiliko

koo hupendezwa, hutulizwa, huburudishwa, hutengenezwa na:

Aina fulani ya pipi, asali, mvuke, chai fulani ya mitishamba au mchaichai, kusafisha koo kwa maji chumvi, baadhi ya dawa kwa ushauri wa daktari n.k

Jinsi ya kulinda na kuiponya Sauti yako

 

 

Kila mtu anawezakuitumia sauti yake, lakini si kila mtu anajua jinsi ya kuitunza au kuiponya inapopatwa na tatizo. afya yake, au nini cha kufanya wakati si tu kufanya kazi haki. Makala hii itasaidia kila mtu kujifunza jinsi ya kuponya sauti  na pia kutoa ushauri wa jinsi ya kuitunza na kuifanya kuwa na afya na nguvu kwa ajili ya siku zijazo
Masomo haya yanawafaha walimu, wainjilisti, wanasiasa, wazazi, wanasheria, madaktari, na waimbaji, na kila mtu ambaye shughuli zake hulazimi kakuongea sana.

·         Kama sauti yako  imejeruhiwa vibaya, basi jambo muhimu zaidi la kufanya sasa hivi ni kuacha kutumia hiyo Sauti,  ipumzishe. Punguza pia kuzungumza kwa muda mrefu na hasa kwa kupaza sauti kubwa na kutumia muda kidogo zaidi katika ukimya.
·         Jambo jingine kubwa ambayo husaidia sauti iliyojeruhiwa ni chai ya moto (Kama vile coat tea). Unaweza kupata pia  dawa za mitishamba zilizohifadhiwa kitaalam katika maduka ya dawa, lakini ikiwa dini yako au tamaduni yako haina shida katika hili. Kunywa angalau kikombe asubuhi na kikombe wakati wa usiku.
·         kama kuna kitu ambacho kinaweza kusaidia kuponya sauti yako na pia inaweza kutumika kulinda kwa haraka  ni unywaji wa maji ya kila siku. Maji husaidia na sauti yako katika afya nzuri
 
Source:http://johnshabani.blogspot.com

 


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni