Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Julai 20, 2012

SABABU GANI ‘NIMHESHIMU BABA YANGU NA MAMA YANGU’?





“WAHESHIMU baba yako na mama yako.”

Kwa vijana wengi maneno hayo yanasikika kama ni jambo la zile enzi za giza.


Kijana-msichana Veda alijulisha uasi wa waziwazi dhidi ya babae kwa kufanya matembezi na mvulana aliyetumia vibaya madawa ya kulevya na alkoholi. Kwa kukaidi, angelienda pia kucheza dansi mpaka chee.


“Nilihisi kwamba yeye alikuwa mzuivu mno,” aeleza Veda.

“Nilikuwa na umri wa miaka 18, name nilifikiri mimi ni mjuzi wa yote. Nilihisi baba yangu alikuwa bahili na hakutaka kamwe nione raha, kwa hiyo mimi nikaenda nje na kufanya nililotaka kufanya.”


Yawezekana kijana; walio wengi hawatakubaliana na vitendo vya Veda. Lakini, kama wazazi wao wa masomo ya nyumbani, au wawe wamefika nyumbani saa Fulani, wengi wangechacha kwa uchungu wa moyo au, jambo baya hata zaidi, wangekaidi wazazi wake inaweza hatimaye kumaanisha si kama tu itakuwa ni vita au amani nyumbani bali pia uhai wake mwenyewe.


Kwa maana amri ya ‘kuheshimu wazazi’ inatoka kwa Mungu, na anaambatanisha motisha ifuatao na kutii amri hiyo”. (Waefeso 6:2, 3) Inaweza kumaanisha faida kubwa au hasara kubwa.


Kwa hiyo, tuangalie upya linalomaanishwa hasa na kumheshimu babako na mamako.




Maoni 1 :