Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumanne, Septemba 20, 2011

Hivi Ni lazima Wazazi, Walimu na Viongozi wa Dini wawalinde vijana wakati wote?


Nchini kwangu, wazazi wangu wamefanya kazi miaka mingi, walimu na viongozi wa dini katika kuwaongoza vijana kutoka katika vitendo vya utumiaji nguvu na uhalifu kwenda katika maisha ya kuwahudumia wengine. Kwa kawaida vijana hupendelea kujitoa kikamilifu katika kutekeleza lengo fulani au kuwa sehemu ya kundi fulani. Hamasa hii inaweza kuwa jambo zuri kwa jamii pale ambapo vijana wanajitoa kikamilifu katika kuhudumia familia zao, taifa lao na imani yao na kuwahudumia masikini, wagonjwa na kuwatumikia watu kibinaadamu kwa njia nyingi tofauti.
 Hamasa ya vijana kupenda kuwa sehemu ya kundi fulani huweza kuleta matokeo mazuri pale kundi hilo linapokuwa na malengo mazuri. Hata hivyo, tabia hii ya vijana kupenda kujihusisha na lengo au kundi fulani inaweza kutumiwa vibaya na kuwafanya vijana kujitumbukiza katika vitendo viovu na uhalifu. Kuna mifano mingi duniani kote ambapo vijana wameongozwa na kuhamasishwa na wanasiasa wenye malengo mabaya na ya kibinafsi, makundi ya kihalifu au yale yenye imani kali kufanya uhalifu wa kutisha (Rwanda mwaka 1994, Kenya mwaka 2007).
------------------------------------------------
Na sasa tuelekee katika hoja ambayo ndio msingi mkuu wa kipindi hiki, pamoja na yote hayo niliyoyaeleza kwa ufupi, kuna baadhi ya vijana bado wanawaza namna ya kujikomboa kutoka katika lindi la umasikini.
------------------------------------------------


MADA

Hivi Ni lazima Wazazi, Walimu na Viongozi wa Dini wawalinde vijana wakati wote?

------------------------------------------------

Mwaka 1978 huko Marekani, Bwana mmoja aliyejiita "Mchungaji" Jim Jones alianzisha dhehebu (cult) ambalo lililokuwa likifuata baadhi ya mafundisho katika imani ya Kikristo na msimamo mkali wa kisiasa. Wafuasi wake walifanya maovu mbalimbali ikiwemo mauaji, udanganyifu wa kughushi nyaraka na wizi. Hatimaye, kwa amri yake, zaidi ya waumini 900 walijiua katika makazi yao huko Guyana.
Siwezi kabisa kulihusianisha dhehebu la Jones na Ukristo, japokuwe yeye alidai kuwa ni kiongozi wa Kikristo. Vivyo hivyo, ninakataa kuhusianisha madhehebu au viongozi wanaowatuma waumini wao kufanya mauaji na Uislamu. Viongozi na makundi haya yanatumia jina la mojawapo ya dini adhimu kabisa kwa mwanadamu yenye historia iliyotukuka ya ustaarabu, elimu na Amani na kupotosha mafundisho yake ili kuwalaghai vijana na wengine kufanya mauaji na uharibifu badala ya kutengeneza na kujenga.
------------------------------------------------

Kuna baadhi ya wasichana waliopata virusi hivyo kutokana tamaa za kutaka kuishi maisha ya gharama na fahari kubwa, kwa hiyo wakalazimika kufanya ngono na wanaume wenye fedha ambao ni waathirika.

Wapo walioathirika baada ya kufanya ngono na watu ambao hawana fedha za kutisha, bali walijiingiza katika mahusiano na watu hao pengine kwa bahati mbaya au kwa sababu ya vishawishi vidogo vidogo, huku wengine wakiwa wameathirika na Ukimwi baada ya kufanya biashara ya uchangudoa katika maeneo mbalimbali.

Baada ya kusadifu yote hayo, nahitimisha kwa kuwaomba vijana wenzagu,  na watanzania wenzangu kwamba pamoja na haraka waliyonayo kuna haja ya kusubiri na waitazame Serikali kama kweli itatekeleza na kutimiza maazimio yake hata kama itatugharimu miaka mingi.
------------------------------------------------

Katika kundi hilo kuna kila aina ya vijana; kuna waliosoma na kutunukiwa vyeti, stashahada, shahada na shahada za juu, huku wengine wakiwa ni mbumbumbu kabisa kwa maana hawakwenda shule na kuna walioishia darasa la tatu, tano na la saba.
Kimsingi, wako tofauti lakini linapokuja suala la kuukimbia umasikini fikra zao zina fanana kwa kiwango kikubwa kwani mawazo yao makuu  yanawiana kwa namna moja ama nyingine.
Kwa mfano, kuna kijana anayehitaji mtaji wa Shilingi milioni mbili ili aweze kufanya biashara zitakazomsaidia kupunguza hali ngumu ya maisha aliyonayo, na wakati huyo akiwa hivyo kuna kijana mwingine anahitaji Shilingi elfu tano tu, ili aende Tandale kununua mahindi mabichi ambayo atakuja nayo mtaani tayari kwa kuyachoma kisha ayauze.
…kama nilivyosema mwanzo kwamba fikra zao zinafanana ila michakato na michanganuo yao ndio inatofautiana, kwani mmoja anahitaji mtaji mkubwa ili aweze kuendesha shughuli zake wakati mwingine anahitaji mtaji mdogo ili naye aendeshe shughuli zake.
katika kundi lolote lile la vijana iwe wasichana au wavulana kuna ambao hawataki kusubiri, wenyewe kila wakati wana haraka, wanataka wafanikiwe na wafikie kilele kama ilivyo kwa matajiri wengine.
------------------------------------------------

Hatua Za Vitendo Zinahitajika Kuelimisha

Uchambuzi:
Tunaweza sasa kujimudu kama kila tulilokuwa tunaambiwa ni bora, ili mradi litoke magharibi, watu wengi walilikubali na kuliingiza katika mfumo. 

Ayi Kwei Armah, alisema tena linaingizwa hata kama wanasiasa hawajalielewa vizuri. Nasema hivi kwa sababu;
Jambo jipya linaletwa na nchi zilizoendelea (nchi za magharibi) Lakini wanatulazimisha sisi wananchi tulipokee. Kushinikizwa tuukubali ushoga ama na mambo mengine ni matokeo ya tabia ya kukubali kwetu kila kitu.
                                                                                                                          Hasara ya Mwafrika wa leo na Mtanzania ni kukosa anachoweza kujivunia kama itikadi yake, elimu yake, dini yake, mila na desturi yake:
                                                                                                                   Mwafrika anaonekana akiwa mbioni kuukimbia utu wake, na kila kinachofungamana na hicho eti  afananane na umagharibi. 

Wamagharibi wamefanikiwa kutufanya nusu watu!!
------------------------------------------------

Hebu fikiri kuhusu thamani, neno thamani pekee linavyosikika masikioni na hata linavyotamkika. Linganisha na kitu ama kifaa chochote chenye sifa hiyo.

------------------------------------------------

Kila siku ni ya heka heka ndani ya jiji la Dar es salaam.

Ni rahisi kufikiri kwamba wale wanaowatumikisha vijana na watoto wanawasaidia, lakini kama ni hivyo wengine wasingeishia kuchoma mishikaki na vitumbua na kuhifadhi pesa peke yao.
------------------------------------------------

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni