Mtayarishaji

Morning Star Radio

Ijumaa, Oktoba 26, 2012

Chenjiagou, sehemu ya chimbuko la mchezo wa Wushu wa Taiji


Wushu ya Taiji ilianzishwa nchini China, na ni kiini cha Wushu ya China. Taiji ni yenye vitendo vyenye nguvu na vitendo laini kwa pamoja, licha ya kuweza kutumika kujilinda, pia inaweza kutumika kuimarisha afya ya mwili. Chenjiagou, ambayo ni sehemu ya chimbuko la Wushu ya Taiji, iko kwenye mlima Qingfeng, wilaya ya Wen, sehemu ya kati ya China. Chenjiagou ni kijiji kimoja kidogo, mtu akitaka kwenda huko kwanza anapaswa kufika Jiaozuo kwa garimoshi au kwa gari kutoka mji wa Zhengzhou, halafu anaweza kupanda teksi na kufika huko. Mto Manjano unapita kusini mwa kijiji hicho, kijiji hicho kina familia 600 hivi na wakazi zaidi ya 2,500. 

Jua linapoanza kuzama, watu wanafanya mazoezi ya wushu. Ingawa Chenjiagou haina mlima maarufu na mto mkubwa, lakini ni mahali penye mabingwa wengi. Tangu Chen Wangting, ambaye ni kizazi cha 9 cha nasaba ya ukoo wa Chen kwenye mji wa Chenjiagou kubuni Wushu ya Taiji mwishoni mwa enzi ya Ming na mwanzoni mwa enzi ya Qing, mabingwa wengi walijitokeza katika vizazi mbalimbali.
Kwenye ukumbi wa kuwekea michoro ya vielelezo vya Wushu ulioko kwenye sehemu ya kuingilia katika kijiji hicho, zimewekwa sanamu za mwanzilishi wa Wushu ya Taiji Chen Wangting, pamoja na mabingwa wa vizazi mbalimbali wa Wushu ya Taiji waliotoa mchango mkubwa kwa maendeleo ya Wushu. Kwenye kando mbili za sanamu yameandikwa maneno ya "Taiji ya Kidao inakusanya maendeleo ya makundi mbalimbali, undani wa Taiji ni astrotech". Mwongoza watalii Bi. WangJingyu alisema,
"Maneno hayo yanaeleza sayansi ya chanya na hasi ya Taiji, Wushu ya Taiji ni Wushu inayounganisha ubora wa utamaduni mbalimbali, dini ya Kidao na falsafa ya meridian." 

Michoro miwili mikubwa iliyotundikwa kwenye ukuta wa ukumbi wa kuwekea vitabu vya Wushu, inawavutia sana watalii, michoro hiyo miwili ni ya mabingwa wawili wa Wushu waliotofautiana kabisa, mmoja mwenye uso wa kutisha, nywele zimesimama kutokana na hasira, na mwingine ni mpole mwenye uso wa kutabasamu, mikono mingi isiyohesabika yenye nguvu ilinyooshwa kutoka katika miili ya mabingwa hao wawili. Mwongoza watalii Bi. Wang Jingyu alisema,
"Mtu akifanya mazoezi ya Wushu, baada ya kufika kiwango cha juu, kama ana mikono mingi sana mwilini mwake isiyoonekana, anaweza kuangusha kitu chenye uzito wa kilo elfu kumi akitumia nguvu ya nusu kilo moja tu." 

Mtu akitembea kwenye mitaa ya Chenjiagou, anaweza kuhisi jadi kubwa ya Wushu. Kuna msemo mmoja unaosema, "baada ya mtu kunywa maji ya Chenjiagou, anajua kupiga teke la Wushu."
Mazingira maalumu ya Taiji yanafanya kijiji hiki kidogo cha Chenjiagou kionekana kuwa na mambo mengi yasiyofahamika, mashabiki wengi wa Wushu wa nchi za nje wanafika huko kwa kuvutiwa na sifa zake. Daktari wa Marekani Bw Bob mwenye umri wa zaidi ya miaka 50, alianza kufanya mazoezi ya Wushu ya Taiji toka alipokuwa na umri wa miaka 15, mwaka 2004 alipata nafasi ya kufika Chenjiagou, na kujifunza Wushu ya Taiji kutoka kwa bingwa Wang Xian, ambaye ni mmoja kati ya mabingwa wa Wushu wa huko. Bw Bob alisema
"Ingawa anaonekana hakutumia nguvu sana, lakini ngumi yake ni yenye nguvu kubwa. Hii ni tofauti na michezo mingine inayotumia nguvu za misuli, michezo mingine inafanya misuli ya mchezaji iwe mikubwa, lakini Taiji inafuatilia kutojikaza mwilini. Hii ndiyo sababu inayoifanya itumike katika kujilinda, vilevile inafaa kwa kuimarisha afya." 

Kuna mashabiki wengi waliofika Chenjiagou kujifunza Wushu ya Taiji kama alivyo Bw Bob. Toka mwaka 1981, Chenjiagou imeshayapokea makundi zaidi ya 100 ya Wushu kutoka nchi na sehemu zaidi ya 50. Mwezi Mei mwaka 1983, bingwa Wang Xian alitembelea Japan na kufanya maingiliano na wana-wushu wa nchi za nje. Kiongozi wa taasisi ya utafiti wa Wushu ya Wang Xian, Bi Yan Sujie toka muda mrefu uliopita amekuwa akifuatana na bingwa Wang Xian kutoa mafunzo ya Wushu katika nchi za nje, alisema,
"Mashabiki wa Wushu ya Taiji wa nchi za nje hawajabadilisha Wushu waliyoichagua toka mwanzo. Bw Noguti Atsuko kutoka Japan amejifunza Wushu kwa miaka 28 kutoka kwa Wang Xian. Kwa sababu undani wa Taiji una mambo mengi sana, hivyo mtu akifanya mazoezi atakuwa kama anafanya usingaji kwenye viungo vyake mwilini, na anasikia raha sana."

SOURCE INGIA:  H A P A

Alhamisi, Oktoba 25, 2012

UMUHIMU WA KISAIKOLOJIA NA THAMANI KATIKA MAISHA




Kwamba sayansi inaweza kutusaidia kuelewa zaidi kuhusu masuala ya msingi kama vile maana ya maisha ni suala linalozua mabishano mengi katika jamii za sayansi na falsafa ya kisayansi.
Hata hivyo, sayansi inaweza kutupa muktadha fulani na huiweka baadhi ya mipaka ya mazungumzo kuhusu mada zinazolingana.
 
Sayansi huenda ikashindwa kutuambia nini ni cha thamani muhimu maishani, lakini baadhi ya masomo hugusia maswali yanayohusiana: watafiti katika saikolojia chanya (na, mapema na bila umakini mwingi, katika saikolojia ya binadamu) hufanya utafiti kuhusu sababu zinazoleta kuridhika na maisha, kujihusisha vikamilifu katika shughuli, kufanya mchango zaidi kwa kutumia vipawa vya kibinafsi, na maana iliyo na msingi wa kuwekeza katika jambo kubwa kuliko mtu binafsi.

Aina moja ya mfumo wa thamani uliopendekezwa na wanaelimunafsia wa jamii, uitwayo kwa upana Nadharia ya Kupambana na Mambo ya Kutisha, inasema kwamba maana yote ya binadamu inatokana na hofu ya kimsingi ya kifo, ambapo maadili yanachaguliwa yanapotusaidia kuepukana na kumbukumbu ya kifo.

Sayansi ya niurolojia imetunga nadharia ya malipo, raha na msukumo katika masuala ya kimwili kama shughuli za kupitisha ujumbe za kiniuro, hasa katika mfumo wa kilimbi na haswaeneo la kiventrali tegimentali. Ikiwa mtu anaamini kwamba maana ya maisha ni kufanya raha iwe nyingi iwezekanavyo, basi nadharia zinatoa utabiri unaozidi kuongezeka, kuhusu jinsi ya kufanya ili kufanikisha hili.

Somo la kijamii linapima thamani katika ngazi ya kijamii kwa kubuni nadharia kama vile nadharia ya thamani kanuni, anomi, n.k.

Jumatano, Oktoba 24, 2012

Kolonia Santita: RIWAYA YA KISWAHILI YA KIJASUSI INAYOSISIMUA..

 

546935
Kolonia Santita ni shirika la madawa ya kulevya. Panthera Tigrisi ni mfanyabiashara wa madawa ya kulevya, katili kuliko wote katika Hemisifia ya Magharibi. Kitabu hiki Kinahusu Ujasusi, Madawa ya kulevya na ugaidi wa kimataifa. Ukianza kukisoma hutakiweka chini kamwe unless kimeisha… 

Kitabu hiki kimetungwa na mtunzi anayekuja juu akiwa ni mjomba kabisa wa mtunzi maarufu wa Riwaya za Kijasusi Marehemu Elvis Musiba ambaye alitamba na kitabu chake cha kwanza cha Njama.
Enock Maregesi ambaye anaishi na kufanya shughuli zake kwa Malkia Elizabeth anasema kitabu hiki amekifanyia kazi kwa umakini na kitaleta mapinduzi kwenye uandishi wa Riwaya za Kiswahili za Kijasusi.

“Kolonia Santita ni tofauti na hadithi zingine kwa sababu ya wapelelezi wake. Wapelelezi wake ni makomandoo-wapelelezi-wanajeshi.” 

Kwa wapenzi wa vitabu kaeni mkao wa kula kwani kiko njiani na kitapatikana kwenye Bookstores zote.

Jumatatu, Oktoba 22, 2012

UCHANYA WA KIMANTIKI



Wachanya wa kimantiki huuliza: Ni nini maana ya maisha? na mbona kuuliza?Kama hakuna maadili yanayolengwa, basi, hivyo ni kusema maisha hayana maana? Ludwig Wittgenstein na wachanya wa kimantiki walisema: "Linapoulizwa kilugha, swali ni la ubatili"; kwa sababu, maishani taarifa ya "maana ya x", kawaida inaashiria madhara ya x, au umuhimu wa x, au kile ambacho ni dhahiri kuhusu x na kadhalika, kwa hivyo, wakati dhana ya maana ni sawa na "x", katika taarifa ya "maana ya x", taarifa inakuwa ya kujirudia, na kwa hivyo, ya kiupuzi, au inaweza kutaja kama ukweli kwamba maisha ya kibaiolojia ni muhimu ili kuwa na maana maishani.

Mambo (watu, matukio) katika maisha ya mtu yanaweza kuwa na maana (umuhimu) kama sehemu ya uzima, lakini maana isiyobainika wazi ya maisha (hayo), yenyewe, mbali na mambo hayo, haiwezi kubainika. Maisha ya mtu yana maana (kwake mwenyewe, wengine) kama matukio ya maisha yanayotokana na mafanikio yake, urithi, familia, na kadhalika, lakini, kusema kwamba maisha, yenyewe, yana maana, ni matumizi mabaya ya lugha, kwani yoyote ya umuhimu, au ya mwisho, ni muhimu tu "katika" maisha (kwa walio hai), hivyo basi kuifanya taarifa iwe ya kimakosa. Bertrand Russell aliandika kwamba ingawa alipata kwamba chuki yake ya mateso haikuwa kama chuki yake ya mboga ya brokoli, hakupata utaratibu wowote wa kuridhisha, na wa kupimika wa kuthibitisha hili:
Tunapojaribu kuwa na uhakika, kulihusu kile tunachomaanisha tunaposema kuwa hiki au kile ndicho "Zuri," sisi hujipata katika matatizo makubwa sana. Tamko la Bentham, kwamba radhi ndiyo Zuri, lilizua upinzani mkali, na ilisemekana kuwa falsafa ya nguruwe. Yeye na wapinzani wake walishindwa kuibua hoja zozote. Katika swali la kisayansi, ushahidi unaweza kupatikana kutoka pande zote mbili, na mwishowe, upande mmoja unabainika kuwa na hoja bora - au, kama hili halitokei, swali linabaki kama halijajibiwa. Lakini katika swali, kuhusu ikiwa hili, au hilo, ndilo mwisho Mzuri, hakuna ushahidi, kwa vyovyote vile; kila mtetezi anaweza kupendekeza tu hoja kulingana na hisia zake, na kutumia vifaa vya ushawishi ambavyo vitaibua hisia sawa katika wengine. . . Maswali kuhusu "maadili" - yaani, kuhusu kile ambacho chenyewe ni kizuri kibaya , bila kutilia maanani madhara yake - yanapatikana nje ya uwanja wa sayansi, jinsi watetezi wa dini wanavyodai kwa msisitizo. Nadhani kwamba, katika hili, wako sawa, lakini, mimi napata hitimisho zaidi, ambalo hawapati, kwamba maswali kuhusu "maadili" yanapatikana kabisa nje ya uwanja wa maarifa. Hiyo ni kusema, tunaposema kwamba hili, au lile, lina "thamani", sisi tunaeleza tu hisia zetu wenyewe, si ukweli, ambao bado ungalikuwa kweli ikiwa hisia zetu za binafsi zingalikuwa tofauti.

Jumapili, Oktoba 21, 2012

BREAKING NEWS

Photo Credit By: spectrummagazine.org

Wapendwa Viongozi wa Kanisa,

Kufuatia tamko la Serikali la kupiga marufuku mihadhara yote ya dini kwa siku thelathini kuanzia leo Oktoba21,2012, Uongozi wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Tanzania Unioni,unaelekeza kwamba tuzingatie maelekezo hayo kwa kuahirisha Mahubiri yote ya hadhara au kuyahamishia makanisani, pale itakapowezekana, mpaka marufuku hiyo itakapoondolewa. Tafadhali fikisheni ujumbe huu makanisani. Tunawasihi tumlilie Mungu ili Hali ya Amani na Utulivu irejee mapema na marufuku hii iondolewe.
 
*********************************  
Dear Adventist Church Leaders,

Following the Statement of the government to ban all religious public meetings for thirty days with effect from today October 21, 2012, Tanzania Union Administration of the Seventh Day Adventist Church Directs that we adhere to this directive by canceling all public evangelistic meetings which were falling within these thirty days from today. Kindly pass this message to all churches today. We shall let you know the moment the ban is lifted.

Pr. Mussa Daniel Mika
Director of Communication- 

TANZANIA UNION OF SEVENTH DAY ADVENTIST CHURCH

Alhamisi, Oktoba 18, 2012

KAMPUNI YABUNI PROGRAMU YA WAZAZI KUDHIBITI SIMU ZA WATOTO WAO!!.

Picha ya mtandaoni ikionesha mtoto akitumia simu.



Hatimaye kilio cha wazazi kote duniani kuhusiana na matumizi ya mabaya ya simu ambayo yamekuwa yakifanywa na watoto wao kwa ajili ya kufanikisha michongo isiyo na tija kwao kimepatiwa tiba, baada ya kampuni moja ya teknolojia kugundua mfumo utakaowawezesha kufuatilia mwendendo wa simu za watoto wao.

Mfumo huo unaojulikana kwa jina la Belimo, ambao kwa kuanzia utaweza kufanya kazi kupitia mtandao wa Vodafone, unatoa fursa kwa wazazi kudhibiti muda wa watoto wao kuweza kuwa hewani, kutuma ujumbe mfupi wa maandishi au hata kupiga simu.

Tofauti na mifumo mingine inayojulikana kwa lugha ya kiingereza kama Application, mfumo huu umetengenezwa katika namna ambayo mtoto anayedhibitiwa hawezi kuukataa kwa namna yoyote ile kwani anayekuwa na uwezo wa kuuendesha na kuuamuru ni mzazi anayeamua kuutumia.

Tayari mfumo huu umeshapata umaarufu hata kabla haujaanza kutumika ambapo asasi moja ya nchini Uingereza yenye kujihusisha na masuala ya uzazi na malezi, imeweka bayana mtazamo wake juu ya kuukubali mfumo huu huku ikisema kuwa “utawawezesha wazazi kudhibiti vijana wao kujihusisha na masuala ya kipuuzi”
Chini ya mfumo huu, mzazi ataweza kununua kifurushi ambacho kinajumuisha kadi ya simu ya kawaida tu kama zilivyo zinazotumika kwenye simu hivi sasa, lakini ikiwa imeunganishwa kwenye mfumo huo, na huduma hiyo itakuwa ya kulipia kwa kadiri mtumiaji anavyopenda kuendelea kuitumia.

“Mfumo huu utawawezesha wazazi kudhibiti kwa mfano, namba zipi ambazo hawapendi ziwe zinawasiliana na mtoto wao, muda wa kupiga simu, kutuma ujumbe na huduma zingine za simu. Lakini pia, wazazi watakuwa na uwezo wa kusoma ujumbe mfupi wa maneno ulioko kwenye simu za watoto wao, bila kuwa na simu za watoto hao” amesema msemaji mmoja wa kampuni inayoandaa mfumo huo.

Hatua hii imekuja ikiwa ni katika zama ambazo taasisi kadhaa za kiutafiti zimetanabaisha kuwa, watoto hasa wa kike barani Ulaya, wamekuwa katika shinikizo la kutuma kwa njia mbalimbali, mambo yenye kuhusu maisha yao ya kimapenzi, jambo ambalo limekuwa likiwakwaza wazazi wao huku maadili pia yakizidi kupotea watoto wao simu kwa watoto wao.

CHANZO CLICK:  H A P A

Jumatano, Oktoba 17, 2012

NI KWA NINI UHALALI KWA UKABILA, UDINI, UKANDA NK?



Wapendwa katika Bwana,

NDUGU Wakristo umefika wakati tumeonelea kuwa ipo haja ya kuwaelezeni machache ili kuona maendeleo yetu na mafanikio tuliokwisha yapata hapa Zanzibar, yanaendelezwa na hayarudi nyuma kwa namna yoyote. Hapana shaka kuwa munaelewa kuwa idadi yetu hadi sasa ni ndogo sana na wengi wetu tungali katika kiwango na hadhi ya wahamiaji na sio Wazanzibar kama wanavyosema wenyewe.


MAFANIKIO YETU


KABLA kugusia yale ambayo tunahisi ndio lengo la waraka huu hapana budi kuwatajieni mambo machache ambayo tumefanikiwa kuyapata hadi sasa. Pamoja na jitihada zetu za muda mrefu bado tunapaswa tumsifu Bwana kwa msaada wake mkubwa kwetu dhidi ya maadui zetu. Tunaamini kuwa kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu, Bwana atatupa ushindi na mafanikio makuu zaidi ya haya na atawafumba macho maadui zetu wazidi kulala ili mipango yetu yote ya kuibadilisha Zanzibar kidemografia ifanikiwe katika kipindi kifupi kijacho. 


Mafanikio yetu yameenea katika kila upande - katika uchumi, siasa, huduma za jamii, umiliki wa ardhi, ujenzi, elimu na kadhalika ili kupata picha kamili ni vyema tuorodheshe kwa ufupi mafanikio hayo:
Nafasi yetu kwa upande wa elimu imekuwa ya kuridhisha kupitia nafasi za serikali. Hivi sasa ni rahisi na limekua jambo la kawaida katika kila matangazo ya wito wa masomo kusikia majina ya Wakristo. Kati ya vijana 7 hadi 10 ni lazima upate vijana wawili hadi watatu kutoka katika makanisa yetu.


Sambamba na matangazo ya elimu, vijana wetu wamekuwa wanapata nafasi nyingi za ajira katika serikali ya Zanzibar. Hali ya kutoelewana kisiasa baina ya Wazanzibari imetoa mwanya kwetu kuingiza vijana wa Kikristo wenye asili ya bara kwa wingi kwani wamekuwa wanaaminika zaidi kuliko vijana wa Zanzibar. Hali tulioieleza juu imetuwezesha kuwa na Wakristo wengi katika nafasi za juu serikalini na katika chama tawala. Hali hii ni lazima iendelezwe katika ngazi zote kwani ndiko kunako mambo mengi ya kila siku.


Tumepata fursa ya kutumia 


Taasisi za serikali kwa uendeshaji wa ibada zetu. Hali hii imefanya tuzidi kukubaliwa na Waislamu na kuvumiliwa na inaweza kutupa nafsi ya kuwavuta katika NENO LA BWANA Kwa upande wa mashamba (vijijini) tumepata wasaa mzuri wa kununua ardhi toka kwa Waislamu ambao hadi sasa bado hawajashtuka. Ardhi hizi zimetuwezesha kujenga makanisa kadhaa ambayo hapo awali hayakuwepo. Idadi ya skuli na vituo vyetu (ambavyo licha ya picha ya juu kuwa haviendeshwi kwa misingi ya Kikristo lakini kiukweli ni vituo vya kimisionari) vimeongezeka kwa hali ya kuridhisha. Skuli hizi ni kuanzia kwa watoto wadogo hadi vituo kama hichi kilichopo mji mkongwe (Stone Town Youth Centre) na zinafanya kazi vizuri katika kupandikiza mila za Kikristo.

Sera zilizopo hivi sasa kwa upande wa uingiaji na utokaji 


Zanzibar imetusaidia sana katika uingizaji wetu (Wakristo) kutoka Bara na hivyo kusaidia kufuta ile imani ya kuwa Zanzibar ni kisiwa cha Waislamu eti Wazanzibari kwa zaidi ya asilimia 99 ni Waislamu.  Ujaji wa Wakristo kwa wingi kutoka Bara umewezesha kuongezeka kwa idadi ya mabaa na kilabu za pombe. Hivi sasa ni jambo la kawaida kuona magari ya aina mbalimbali yanayomilikiwa na eti Waislamu yamebeba kreti za bia na pombe kali.

Kujiingiza kwetu katika taasisi za dola katika ngazi za mitaa kumetuwezesha kupata nafasi ya kutangaza Ukristo kwa njia ya mihadhara na wakati huo huo kudhibiti mihadhara ya wazi ya Waislamu kwa kutumia madai ya kashfa na kutatanisha maelewano mazuri baina ya watu wa dini tofauti. Tumefanikiwa kupata viwanja vingi katika maeneo ya mjini ambayo yangali mapya. Maeneo haya ni kama Tomondo, Mombasa,
Mwanakwerekwe na kadhalika ambayo tayari tumeshajenga makanisa yetu ingawaje kwa sasa hayajawa na waumini wengi wa kuyatumia na bado yanaonekana ni matupu.


Ndugu wapendwa katika Bwana,  


Mafanikio hayo yasitufanye tukalewa na kusahau jukumu la kanisa la kuona kuwa utawala wa Bwana unashuka Zanzibar haraka iwezekanavyo. Kosa lolote utakalofanya hivi sasa litaweza kuturudisha hatua kadhaa na huenda nafasi hii tuliyonayo hivi sasa tusiipate kwa karne
mpya ijayo. Mambo ya kufanya yanayotukabili ili kuimarisha nafasi yetu ni kuona yale tuliyokwisha yapata hayatutoki na kuyafanya dira kwa karne ijayo ni haya yafuatayo:


Tusahau tofauti zetu dhidi ya adui  


Ingawaje tupo madhehebu nyingi lakini tunawajibika kuelewa kuwa Waislamu na Uislamu wao ni adui yetu namba moja ambaye hatutofaulu kupambana nae mmoja mmoja. Uislamu hapa Zanzibar ni dini iliofungamana na mila na utamaduni hivyo kila itakavyowezekana tusahau tofauti zetu ndogo ndogo na hata kubwa kukabiliana nao, vingienvyo tutarudi kama wakati wa Karume.

Tuhakikishe tunapata ardhi  


Hii ni mbinu kongwe katika usambazaji wa Ukristo. Wazee wetu walipoleta Ukristo Zanzibar na katika Afrika, jitihada waliyofanya ni kupata ardhi kuwa kwa ajili ya ujenzi wa maeneo yetu, majengo ya hospitali, shule, zahanati na vituo vya chekechea, makanisa na kadhalika. Tunahitaji ardhi kubwa ili kuziweka huduma hizo mahala pamoja kwa ajili ya kueneza injili ya Bwana na Muokozi wetu.

Tununue nyumba na viwanja kwa ujenzi wa Makanisa 


Inaonekana Waislamu wenye siasa kali na baadhi ya watendaji kwenye serikali wameanza kushtuka na ongezeko kubwa la makanisa katika kisiwa cha Unguja. Kuna dalili kuwa tunaweza kupata ugumu katika kupata viwanja kwa ajili ya makanisa. Njia tunayoweza kuitumia kwa muda huu ni kununuwa viwanja vitupu au nyumba za Waislamu kwa bei kubwa itakayowashawishi kuziuza na baadaye tukaweza kuvijenga au kugeuza nyumba hizo kuwa makanisa.

Tujenge shule na hospitali kwa wingi  


Hizi ni taasisi ambazo tunaweza kueneza neno la Bwana kwa Waislamu walio wengi hapa Zanzibar. Kwa kutumia umaskini unaowakabili wengi ya Wazanzibari na uchache wa huduma hizo tunaweza kujitangaza vizuri, tujitahidi kutoa huduma nzuri kuweka vifaa vya kisasa kuweka bei ndogo, kuweka upendo ili vituo vya Waislamu au hata vile vya serikali visiweze kuvikaribia vyetu. Shule ni sehemu muhimu ya kupandikiza mafundisho yetu zaidi kwa watoto wadogo (Nursery).

Tunadai muda zaidi katika vyombo vya habari (TV na Radio) 


Kwa muda mrefu sasa Uislamu na Waislamu wamehodhi vyombo hivi vya habari mbali na kuwa siku ya Ijumaa ambayo yote humilikiwa na vipindi vya Kiislamu vyombo hivyo hutenga siku nyingine kadhaa kwa vipindi vya Kiislamu na hata kuthubutu kutia adhana kila wakati wa sala hali hii inaudhi na inatoa picha ya wazi ya serikali kupendelea Uislamu ingawaje inadai kuwa haina dini. Wakati wa kusherehekea miaka 25 ya TVZ tulizungumzia suala hili lakini halikupata mtu wa kulifanyia kazi. Sasa tuhakikishe kuwa Ukristo unapata muda zaidi katika vyombo hivyo au Uislamu nao upunguziwe nafasi.

Tuongeze mhadhara wa wazi  


Wakati Waislamu wamezuiliwa kufanya mihadhara ya wazi, sisi tujitahidi kuhakikisha kuwa mihadhara yetu inaongezeka kwa kiwango kikubwa. Kwa kuwa Waislamu hawahudhurii mihadhara hiyo, lazima tuone Wakristo wa mjini na mashamba wanahamasishwa na kupatiwa nyenzo ili kuhudhuria. Vipaza sauti vitumike kuhakikisha kuwa neno la Bwana linafika kila pahala. Mihadhara ifanyike karibu na nyumba, Misikiti na kwenye viwanja vya wazi.

Tuendelee kutumia shule na sehemu za umma  


Ili kuwafanya Waislamu watuzoee na kuondosha chuki yao kwetu ni lazima kuendelea kutumia mashule na sehemu za umma zilizo wazi kwa mambo yetu ya ibada kwa kipindi kirefu hali hii inaweza kuwafanya washindwe kuona tofauti yetu na wao. 

Tufanye suala la uhamiaji Zanzibar kuwa jepesi 

Uzoefu unaonesha kuwa ni jambo gumu kuwabatiza Wazanzibari Waislamu. Hali hii inafanya ongezeko la Wakristo kuwa dogo au halipo kabisa ukitoa wale wanaozaliwa katika familia za Kikristo.  Njia pekee ya kuhakikisha ongezeko la makanisa na taasisi zetu ni kuongezeka kwa Wakristo. Jambo hili litawezekana kwa kuingiza Wakristo wengi kutoka Tanzania Bara au wapagani ambao tutaweza kuwabatiza kwa kutumia udugu wetu wa kikabila au asili ya Bara. Kwa kuwatumia ndugu zetu waliomo serikalini (SMZ au SMT) tuhakikishe kuwa suala la uhamiaji linabakia wazi na rahisi na linaendelea kwa kila hali.

Tuzuie jaribio lolote la kadi za uraia au vitambulisho 


Wakrsito tunapaswa kuelewa kuwa iwapo serikali ya Zanzibar itaamua kufanya chochote ili, kuwa na vitambulisho au kadi za uraia kwa Wazanzibari basi jambo hilo litaathiri sana mipango yetu ya muda mrefu kwa Zanzibar. Jitihada zozote za kuiimarisha Zanzibar kama Zanzibar na nje ya Utanzania ni lazima tuelewe kuwa Uislamu utapata nguvu na kuwa tishio kwa hapa Zanzibar na hata Bara. Iwapo tutawajibika kuunga mkono ni kadi za Uraia na vitambulisho vya Watanzania kwa ujumla na sio Zanzibar peke yake.

Tujipenyeze na kushika nafasi muhimu  


Lazima tuelewe kuwa chama chochote cha siasa kinalenga kukamata serikali ili kiweze kutekeleza yale yanayoaminika kuwa mazuri kwa chama hicho. Tunapozungumzia vyama vya siasa kwa Zanzibar tunahusisha zaidi kwenye CCM na CUF. Watu wetu wamefaulu kuingia kwa wingi katika chama tawala na katika jumuiya zake.

Tuunge mkono sera za utalii 


Hadi sasa wengi wa watalii wanaoingia Zanaibar hutokea nchi za Kikristo. Desturi za watalii hupingana na zile za Kizanzibari na hata za Kiislamu. Watalii wanasaidia kuongezeka kwa mabaa na vivazi ambavyo Waislamu wanataka visivaliwe hasa na wanawake. 

Uwafuate Wakristo waliosilimu ili warudie Ukristo 
Watu wa aina hii wanakuwa bado hawajatulia na mara nyingi huwemo katika matatizo. Pana haja ya kuwalenga watu hawa ili kuwarudisha kabla hawajatulia au kupata elimu nzuri. Matatizo yao ndipo mahala pa kuanzia ili Bwana atawateremshie roho ya utulivu. Uzima wa Ukristo ni kuwa na wafuasi wengi kadiri iwezekanavyo. Tuwafuate wanawake kwa misaada  Jumuiya zisizo za kiserikali zinaungwa mkono duniani kote na hasa zile za wanawake na watoto tujiweke pamoja ili tuweze kuwavutia kwa jina la kuwasaidia.

Tuongeze vituo vya mafunzo ya Kikristo 


Kituo cha vijana cha mji mkongwe (Stone Town Youth Center) kimekuwa kikifanya kazi yake vizuri kwani hadi sasa lengo lake la ndani bali halijaeleweka na vijana wanaohudhuria hapo kwa shughuli mbalimbali, jitihada zifanyike ili kuwa na vituo vya aina hii katika maeneo mengine. Lengo kuu liwe ni vijana na wanawake bila ya kuonesha dalili za kidini. Tuwaoe wanawake wao kwa kusilimu kimajina  Jitihada za makusudi zifanyike ili kila itakapowezekana kuwaoa wanawake wa Kiislamu ili tuweze kuwabatiza baadae, njia nzuri iwapo patakuwa na ugumu ni kusilimu kiuongo ili kuruhusiwa kuwaoa wanawake wao.

Tuanzishe NGOs na sisi tuwe viongozi  


Kwa kuwa hivi sasa wafadhili wengi wameonesha hamu ya kuzisaidia NGOs moja kwa moja badala ya serikali ni lazima tujitahidi kuunda jumuiya zetu ambazo zitawashirikisha Waislamu lakini uongozi wa juu ni lazima uwe mikononi mwetu. Hii itatuwezesha kuona sera zetu na malengo yanatelekezwa kwa kivuli hicho. 

Tujenge ukaribu na viongozi ili kuwadhibiti 

Waislamu  Mambo yetu mengi yamekuwa yanakwenda vizuri katika maeneo mbalimbali baada ya wenzetu kuwemo katika kamati za masheha, na matawi ya vyama, na kamati za maendeleo za maeneo mbalimbali. Hali hii ni lazima iongezeke ili udhibiti wa shughuli za Waislamu uwe mzuri zaidi na wakati huo huo kuona kuwa mambo yetu yanakwenda yakiwa na baraka ya vyombo vya dola na vyama vya siasa.

Tuwachonganishe Mashehe wenye msimamo mkali  


Mashehe wenye misimamo mikali wamekuwa ni tatizo kwa Ukristo kwani wana wafuasi wengi na wamekuwa wakisema wazi na kushutumu maendeleo yetu. Mashehe hao ni lazima wachonganishwe na serikali ili hali ikiruhusu wazuiliwe kuendesha shughuli zao. Wakati tukifanya hivyo hatuna budi kuwaunga mkono Mashehe wote ambao wamekuwa wakitusaidia kwa njia mbalimbali. 

Tulenge kuifuta Tabligh  

Pamoja na kuwa na Tabligh sio hatari moja kwa moja kwa Ukristo lakini bado inastahili kupigwa vita kwa sababu ina aina pekee ya mihadhara ya Waislamu inayoruhusiwa humu Zanzibar. Tabligh inaweza kuwazindua baadhi ya Waislamu ambao ni vema kubaki bila ya kuzinduliwa.

Tudai turudishiwe taasisi zetu  


Serikali ya Zanzibar bado inaonekana kuwa ngumu katika milki ya makanisa, ardhi na taasisi zetu. Dalili za huko nyuma zilionekana nzuri kwani tulifanikiwa kupata hospitali yetu Walezo na eneo la Kiugani hata hivyo panakuwepo na ugumu wa kurudishwa shule zetu. Kwa kuwatumia wenzetu waliomo serikalini na baraza la wawakilishi tuzidishe harakati na madai ya taasisi zote zilizobaki.  

Tulete waumini kutoka mashamba kuanza makanisa

Hivyo sasa pameibuka wasi wasi kuhusiana na wingi wa makanisa ambayo hayajapata waumini wa kuyajaza. Ili kuficha dosari hii na hoja kadhaa utaratibu uliopo hivi sasa chini ya baadhi ya makanisa ni lazima uungwe mkono. Wakristo wahamiaji wengi hufikia mashamba hivyo pawekwe na utaratibu wa kuwaleta mjini ili kujaza makanisa.


Neno la mwisho


Wapendwa katika Bwana.  


Miongozi hii ni mikubwa na inaweza kuwatisha baadhi ya waumini wa Kikristo hasa wale ambao bado hawajampokea Roho Mtakatifu vizuri. Hata hivyo, kwa uwezo wa Bwana Mungu wetu ni mpango rahisi. Suala la muhimu ni haya kufahamika na kila Mkristo apendae kumtumikia Bwana. Pia hatuna budi kuishukuru awamu ya nne ya serikali ya Mapinduzi ambao imefungua milango kwa Ukristo na kushuhudia ongezeko la makanisa. Bwana awe nasi!
--
SOURCE:  Jukwaa la www.mwanabidii.com

 

Jumatatu, Oktoba 15, 2012

INAUMIZA SANA

 
Jamii ni namba moja (kaya na wakazi ktk eneo) cha pili ni serikali. Kwani serikali ni nani? Hata vijijini porini watu hutumia video kama kipato na burudani nako kuna uovu pamoja na kuwa na wazee wa mila.Nishati mbadala (solar power) kwa sasa, betri na generator za umeme zimefanikisha haya.Machimboni ndio balaa watoto huona makubwa maana video na mapombe huko hatari.  
Ukiwa vijijini, ukiuliza matatizo makuu ya wananchi kijijini hapo linakuwa mojawapo kati ya makubwa ni 'watu wazima na watoto wadogo kuangalia video za mapenzi (matusi)'. Pamoja na za kuonyesha mpira za mapenzi ni mojawapo. Uliza kwa nini huwa hivyo, wazee wa mila wapo? Viongozi jee, watumishi wa umma.....? Kama watu wana mila zao na dini zao za maadili na wanafanya hivyo, utahitaji polisi na social welfare workers wangapi kukagua nyumba hadi nyumba mtaani, kitongojini maporini kijijini haya yasitokee. 
Kama madhara wanayajua na wanaona ni tatizo-wazazi, wazee wa mila wapo wapi? Apangishaye nyumba na kuweka bar mtaani na vilabu vya pombe ktk makazi na dangulo ni mzazi. Na akataae kuchanga hela 500 kwa wiki au kulipia uchafu 100/= directly kwa gari la uzoaji taka ni yule mwenye bar au mama ntilie, saluni ya nywele ambae hutupa malundo ya uchafu usiku mtaroni au barabarani au mwenye hoteli anayekataa kuunganisha katika sewer line anaunganisha usiku kiwizi mtaro wazi. yanajaa, yananuka na matakataka yanajazana kisha unaona ktk TV-serikali ije izibue, ituondolee huu uchafu unanuka, unatusumbua, unazalisha mbu. Mmefanya nini kuondoa tatizo-tumeita serikali haiji, tunateseka!! 
Ukienda na kampuni hapo kuvunja maunganisho ya mambomba hayo kuziba yamwakigie huko yatokako-atatiririsha barabarani, atakayemfuatilia kumshitaki-atatolewa bastora baada ya muda ataokotwa maiti mtaroni. Ya video na vilabu mtaani nyumba hadi nyumba ni sisi, uchafu na chuki za visafi sheria inapochukua mkondo wake-ni sisi, rushwa na njia za mkato ni sisi-tutabadilika lini watanzania? 
Inaumiza sana.
Mungu atusaidie tubadilike.

Ijumaa, Oktoba 12, 2012

USIKU WA MWISHO DUNIANI

Photo by: lolamouse.

 
(SOMA DANIELI 5 YOTE)

Moyo wa mwanadamu umejaa upumbavu. "Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu; Wametenda uovu wa ufisadi na kuchukiza, Hakuna atendaye mema" (Zab.53:1). Watu wanaopenda kufanya
dhambi huamua kumfutilia mbali Mungu katika mawazo yao, mafundisho yao, na maisha yao. Biblia inasema huo ni upumbavu. Kwa sababu Mungu yuko kweli, na watu kama hao watawajibika kwa vitendo vyao viovu. Lakini jambo la kusikitisha ni kwamba hatujifunzi kutokana na yale yaliyowapata watangulizi wetu.
Tunataka kujionea wenyewe.

Siku moja mfalme Belshaza (mjukuu wa Nebukadreza) alifanya karamu kubwa ya ulevi kwa ajili ya wakuu wake elfu. Hakujua kwamba karamu yake hiyo ilikuwa ya mwisho, na ya kwamba Mungu wa
mbinguni alikuwa ameiona hata kabla haijafanywa (Yer. 51:37-40,57-58). Na usiku ule karamu ile ikawa ya aina yake; lakini wahusika hawakuweza kuamka asubuhi yake; walikuwa maiti. Belshaza hakujifunza kutokana na mambo yaliyompata babu yake Nebukadreza (Dan. 5:18-23). Alikuwa anajua yote hayo lakini kwa kiburi kabisa akafanya yaliyomchukiza Mungu wa Mbinguni. Makosa makubwa aliyoyafanya ni haya:

Kosa lake la kwanza ni kutumia vyombo vitakatifu kunywea pombe (Dan. 5:1-3). Hakuweka tofauti kati ya vyombo vya kawaida vya kutumia na vyombo vitakatifu vinavyotumika kwa kazi maalum ya Mungu. Jinsi gani siku hizi wachungaji hawawafundishi washiriki wao kuweka tofauti hiyo? "Makuhani [wachungaji] wake
wameihalifu sheria yangu [Amri Kumi], wametia unajisi vitu vyangu vitakatifu; hawakuweka tofauti ya vitu vitakatifu na vitu vya kutumiwa sikuzote; wala hawakuwafundisha watu kupambanua vitu vichafu [kama nguruwe, panya, na kadhalika] na vitu vilivyo safi [kama ng'ombe, mbuzi, kondoo], nao wamefumba macho yao, wasiziangalie Sabato zangu, nami nimetiwa unajisi kati yao" (Eze. 22:26). 

Kutokutambua vitakatifu ni kosa la kufisha. Sabato [Jumamosi] ni takatifu (Mwa.2:2,3; Kut. 20:11; Isa. 58:13,14). Jumapili si takatifu; ni siku ya kazi (Eze. 46:1). Siku ya ibada aliyoiweka Mungu kwa wanadamu wote ni Sabato [Jumamosi] na itakuwa hivyo milele zote (Isa. 66:22,23). Zaka (sehemu ya kumi ya mapato yetu) ni takatifu (Law. 27:30-33). Kuitumia kwa matumizi yetu ya kawaida ni kumwibia Mungu (Mal.3:8-11). Wevi hawataurithi ufalme wa Mungu (1 Kor. 6:9,10). Kumtegemea mchungaji wako badala ya kusoma Biblia mwenyewe ni hatari kubwa!

Kosa lake la pili ni kunywa divai [pombe] (Dan. 5:4a). Tulijifunza katika somo la kwanza lililohusu vyakula na vinywaji kwamba pombe inaudhuru sana mwili wetu, na ya kwamba wale wanaouharibu mwili wao kwa pombe au kwa njia nyingine yo yote wataharibiwa (1 Kor. 3:16,17). Pombe ina sumu ya alkoholi
ambayo inaathiri mishipa ya fahamu, ubongo, moyo, nyama za mwili, na kadhalika. Sio suala tu la kulewa linalohusika, bali ni ile sumu iliyomo. Wengi hata wakinywa pombe nyingi hawalewi; lakini sumu inafanya kazi miilini mwao na kuiharibu. Hivyo wale wasemao kunywa pombe kidogo tu wasingeweza kusema hivyo kuhusu sumu ya panya. Sumu kidogo tu yatosha kuua mtu au kuuathiri mwili (Mithali 23:29-35). Biblia inailinganisha sumu iliyomo katika pombe na sumu ya nyoka aitwaye "fira" (Mithali 23:31,32).
 
Ni sumu mbaya sana. Biblia inasema walevi [wanaolewa na wasiolewa] hawataurithi ufalme wa mbinguni (1 Kor. 6:9,10). Kosa la tatu la Belshaza ni lile la kuisifu miungu badala ya Mungu wa mbinguni (Dan. 5:4b). Neno lasema, "BWANA asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni BWANA, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema BWANA" (Yer. 9:6).

Si kwamba Belshaza alikuwa hamjui Mungu wa mbinguni alipokuwa anaisifu miungu yake pamoja na wakuu wake, kilikuwa ni kiburi chake sugu kilichomfanya afanye hivyo. Je! wewe unamsifu nani? Wakati sherehe imefikia kilele chake, wamelewa na kuanza kusifu wanawake na miungu yao, kiganja cha mkono kisichotoka
damu kikaanza kuandika ukutani. Jasho jembamba likawatoka. Pombe yote ikayeyuka kichwani. Hofu kuu ikawashika, wasijue la kufanya. Wataalam wakaitwa ili wayasome maandiko yale; hawakuweza. Ndipo malkia, mke wa Nebukadreza, akaingia na kuwaambia habari za Danieli jinsi alivyomtafsiria ndoto babu
yake. 

Danieli akaitwa. Akamshutumu Belshaza kwa kiburi chake, licha ya kujua fika yaliyompata babu yake. Akasoma maandiko yale ukutani: "MENE (HESABU), MENE (HESABU), TEKELI (MIZANI), NA PERESI (MGAWANYO). Na tafsiri ya maneno hayo ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. TEKELI, Umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. PERESI, Ufalme
wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi" (Dan.5:25-28). Ilikuwa imetabiriwa mapema kwamba milango ya kuingilia mjini itaachwa wazi na maji ya mto yatakaushwa (Isa. 45:1; 44:27). Hivyo ndivyo alivyofanya Koreshi aliyeyaongoza majeshi ya Wamedi na Waajemi usiku ule. Milango ya mto
haikufungwa usiku ule. Wakaingia na kumwua mfalme na viongozi wake waliokuwamo mle. Ulikuwa ni usiku wa mwisho kwao.

Mungu anayapima mataifa katika mizani na kukomesha ufalme wao kama apendavyo. Vile vile anampima mtu mmoja mmoja katika mizani ile ya mbinguni (Amri Kumi) na kuandika mbele ya jina lake "umepunguka" au "umetimilika katika yeye" (Kol. 2:10). Hiyo ndiyo kazi anayofanya Kuhani wetu Mkuu, Yesu Kristo, mbinguni tangu mwaka wa 1844. Karibu sana kesi ya kila mmoja wetu itakatwa kwa milele. Akimaliza kazi yake ya upatanisho au hukumu atatamka maneno haya ya kutisha: "Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi
kutakaswa" (Ufu.22:11). Hukumu hiyo itakatwa kabla ya kuanguka mapigo yale 7 ya Ufunuo 16. Katika pigo la mwisho atakuja kuwachukua watu wake na kuwaangamiza waovu wote.

Mkulima yule tajiri aliyevuna mavuno mengi asijue pa kuyaweka, alifikiri kwamba atakuwa na maisha marefu sana ya raha mbele yake (Luka 12:16-21). Usiku ule akajiambia mwenyewe, "Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi" (Luka 12:19). Maskini
yule, alipolala usiku ule hakuamka, aliuawa. Yule mlinzi mtakatifu asiyeonekana aliyeandika ukutani Babeli, akatamka kwa tajiri huyo maneno haya, "Usiku huu wa leo wanataka roho yako!

Vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?" (Luka 12:20). Ndugu yangu, leo ndiyo siku ya wokovu (2 Kor. 6:2). Kesho si yako (Yak. 4:13-16). Amua leo kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wako. Achana na ulevi na dhambi zote. Ukimpokea atakupa uwezo wa kushinda dhambi (l Kor. 15:57; Yuda 24,25).
Usiku wa mwisho duniani kwako na kwangu unaweza kuwa ni usiku huu wa leo. "Basi jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi na masumbufu ya maisha haya, siku ile ikawajia kama mtego unasavyo; kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia" (Luka 21:34,35). Siku moja ulimwengu wote unaojifurahisha katika anasa mbalimbali za dhambi hautaweza kuiona asubuhi; watakuwa maiti, hawatazikwa, wala kuliliwa (Yer. 25:32-37). Itakuwa karamu ya mwisho Mungu atakayowafanyia ndege (Ufu. 19:17,18).

Jumapili, Oktoba 07, 2012

Mkutano wa Berlin wa 1885 na "Dola huru la Kongo".





Kisiasa hakuwa na umuhimu sana kwa sababu nchi yake ilikuwa ndogo tena nafasi ya mfalme katika Ubelgiji haikuwa na mamlaka kubwa. Lakini Leopold II alifaulu kama mwanabiashara aliyetafuta kila njia ya kuongeza mali yake. Kwa njia hii alianza kujihusisha na habari za Afrika na hasa Kongo.

Leopold ailifaulu kujipatia utawala juu ya maeneo makubwa ya beseni ya Kongo kama mali ya kampuni ya binafsi ambamo yeye mwenyewe alikuwa na hisa nyingi. Leopold alishirikiana na mpelelezi Henry Morton Stanley aliyeweka misingi kwa yote yaliyotokea baadaye. Kwa njia hii alielekea kufanya Kongo kuwa mali yake ya binafsi. Baada ya kutawala sehemu za Kongo alitafuta utambulizi wa utawala wake kutoka nchi mbalimbali. 

1884 Marekani ilitambua "Dola huru ya Kongo". Sasa athira yake ilikuwa kubwa kiasi ya kusababisha mashindano kati ya mataifa mengine ya Ulaya juu ya athira katika Afrika. Mkutano wa Berlin wa 1885 ilikubali "Dola huru la Kongo" kama nchi ya kujitegemea iliyokuwa mkononi mwa shirika la Leopold.

Leopold mwenyewe hakukanyaga ardhi ya Kongo. Nia yake ilikuwa utajiri pekee. Alifaulu kijitajirisha lakini bei kali ililipiwa na watu wa Kongo.

Badala ya kulinda wenyeji dhidi ya biashara ya watumwa jinsi alivyotangaza kote duniani alikodi malighafi za Kongo kwa watu na makampuni waliompa pesa. Makampuni haya yalipewa mamlaka ya kulazimisha wenyeji kuwafanyia kazi ya lazima kama kubeba mizigo na kukusanya mpira msituni. Leopold alitajirika kwa sababu teknolojia mpya ya matairi ilihitaji kiasi kikubwa cha mpira iliyopatikana pekee katika misitu ya nchi za tropiki kama Kongo. Baadaye mashamba ya mipira ilianzishwa lakini wakati ule viwanda vilitumia mpira asilia.

Wakala wa Leopold walidai kila kijiji kilete kiasi fulani cha mpira. Kama hakikuletwa walitoa adhabu kali kwa kusudi ya kutisha wengine. Watu maelfu walikatwa mikono yao. Unyama ulisababisha watu kujitetea kwa silaha. Upinzani huu ulikandamizwa kwa ukali zaidi. Kuna makadirio ya kwamba chini ya utawala wa Leopold idadi ya wakazi wa Kongo ilipungukiwa kutoka watu milioni 20 kubaki milioni 10 tu

Habari za unyama wa utawala wa Leopold ulienea kwa sababu wamisionari walipeleka barua na picha kwenda marekani na Ulaya. Tangu 1903 kamati za bunge la uingereza zilifanya utafiti kuhusu hali ya utawala wake Leopold. Upinzani ulikuwa pia ndani ya Ubelgiji na watu wengi waliona aibu kuhusu matendo ya mfalme wao.

Baada ya upinzani kukua mwaka 1908 Leopold alikabidhi Kongo kwa serikali ya Ubelgiji ikawa Kongo ya Kibelgiji. Leopold alipokufa mwaka uliofuata watu barabarani walikashifu maiti yake ilipopita wakimwita aibu ya taifa.

Leopold II alikuwa mfalme wa Ubelgiji tangu 10 Desemba 1865 hadi 17 Desemba 1909. Alimfuata babake Leopold I aliyekuwa mfalme wa kwanza wa nchi baada ya kuanzishwa kwa taifa hili.