Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatatu, Julai 30, 2012

ULIWAHI SIKIA MAKAMBI YA MAUTI?

Wafungwa katika kambi la KZ Buchenwald wakati wa ukombozi 1945.

Makambi ya KZ ni jina la kutaja makambi ya wafungwa yaliyotumiwa hasa na Ujerumani wakati wa utawala wa Nazi miaka ya 1933 hadi 1945. "KZ" ni kifupi cha neno la Kijerumani "Konzentrationslager". Maana yake ni "Kambi la kukusanya wafungwa".

Wanazi walianzisha hayo makambi ya KZ baada ya kuteka utawala wa Ujerumani mwaka 1933. Walikamata wapinzani wao wengi, kiasi kwamba magereza hayakutosha tena. Makambi hayo hayakuwa tena chini ya wizara ya sheria bali chini ya polisi ya kisiasa na vitengo vya chama cha Nazi. Tangu mwaka 1934 yalikuwa yote chini ya kikosi cha SS.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia yalitumiwa kukusanya mamilioni ya watu waliokamatwa na Wanazi kote Ulaya, hasa vikundi viwili:

  • Wayahudi pamoja na vikundi vingine vilivyobaguliwa upande mmoja na
  • wapinzani wa utawala wa Nazi kwa upande mwingine.

    Makambi ya KZ ya kawaida

    Makambi hayo yalikuwa hasa na kusudi la kuadhibu wapinzani na kutumia wafungwa kwa ajili ya kazi za kulazimishwa. Hasa wakati wa vita Wajerumani wengi walikuwa wanajeshi na nchi ikaona uhaba wa wafanyakazi. Hivyo makambi haya yalijengwa mara nyingi karibu na viwanda.
    Idadi ya vifo ilikuwa kubwa hasa katika miaka ya mwisho ya vita kutokana na unyama wa walinzi na uhaba wa chakula pamoja na ukosefu wa matibabu. Njaa ilisababisha magonjwa na vifo vingi.

     

    Makambi ya KZ chini ya Ujerumani wa Nazi 1933-1945;
    makambi ya mauti yamepewa alama nyekundu

    Makambi ya mauti

    Baada ya azimio la Maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya makambi ya mauti yalijengwa. Makambi ya mauti ni lugha ya kutaja hasa makambi saba yafuatayo:
  • Chelmno – Kulmhof
  • Auschwitz-Birkenau
  • Belzec
  • Sobibor
  • Treblinka
  • Majdanek
  • Maly Trostinez
Yote yalijengwa nje ya eneo la Ujerumani wenyewe, sita katika Poland na moja katika Belarusi.
Mwisho wa mwaka 1941 Adolf Hitler na viongozi wengine wa Ujerumani waliamua kuwaua Wayahudi wote waliopatikana Ulaya. Majaribio ya kwanza ya kuua Wayahudi katika Ulaya ya Mashariki yalionyesha matatizo mbalimbali: uchovu kwa upande wa wanajeshi wa vikosi maalumu waliopaswa kutekeleza mauaji haya ya watu maelfu na sauti za masikitiko upande wa wanajeshi wa kawaida waliobahatika kuona mauaji haya. Azimio lilifanywa la kutumia mbinu za kisasa katika makambi maalumu ambako tendo lenyewe liliweza kufichwa vizuri zaidi.
Wayahudi na wengine waliotakiwa kuuawa walipelekwa kwa treni hadi makambi haya maalumu. Hapa wafungwa waligawiwa:
  • watu wenye afya nzuri walipelekwa kando na kupewa kazi katika viwanda vilivyojengwa pamoja na makambi haya kwa kusudi la kufanya kazi ya uzalishaji kwa ajili ya mahitaji ya uchumi wa vita. Wafanyakazi hawa walitakiwa kufanya kazi ngumu wakipewa chakula kidogo hadi kuchoka. Mara walipokuwa hawaleti tena faida walipelekwa kuuawa kwenye chumba cha gesi.
  • watoto, wazee na wagonjwa walipelekwa kando mara moja hadi vyumba vilivyoitwa "bafu". Hapo milango ilifungwa, na gesi ya sumu kuingizwa. Maiti zilichomwa katika majiko makubwa.
Kwa jumla watu milioni sita waliuawa katika makambi ya KZ hadi 1945.

Jina la "KZ"

Wanazi walitumia jina la KZ = "Konzentrationslager" kama tafsiri ya neno la Kiingereza "concentration camp". Waingereza waliwahi kutumia mbinu ya kusimamia wafungwa wengi katika kambi maalumu zilizofungwa kwa seng'enge tangu vita yao dhidi ya Makaburu katika Afrika Kusini mwaka 1899-1902; Waingereza walianzisha makambi haya kwa sababu walitaka kutenganisha familia za Makaburu na wanaume wao walioendesha vita ya porini ili kuzuia wasipate chakula na usaidizi kutoka kwa wasio wanajeshi. Makambi haya yalisababisha vifo vya makumi elfu wanawake, watoto na wazee kutokana na njaa na magonjwa ingawa hayakujengwa kwa kusudi hiyo.

Tangu kuanzishwa na Waingereza huko Afrika Kusini imeonekana ya kwamba makambi ya aina hii husababisha mara nyingi vifo hata kama wale wanaoanzisha makambi hawana nia ya kuua watu kwa njia hiyo. Matatizo ya kulisha watu wengi mahali pamoja, ya kuhakikisha usafi na matibabu ama shambani tu au katika mahema au kwenye majengo yasiyo imara, kuwalinda wafungwa dhidi ya baridi na joto na juu ya haya yote kuzuia kuambukizana kwa magonjwa ni magumu ya kushinda uwezo wa walinzi wa kambi. Hasa kama wafungwa wanatazamiwa kama maadui ambao hawapaswi kupewa uangalizi mwingi.  Kama Vipi Jihakikishie  H  A P A.


Ijumaa, Julai 27, 2012

HIVI MUZIKI NI NINI HASA?


Muziki ni sanaa kama zilivyo sanaa zingine, hivyo hatuna budi kuelewa sanaa ni nini hasa. Imeelezwa kuwa ni ufundi wa kuwasilisha mawazo yaliyomo katika fikra za binadamu ili yadhihirike na kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa walengwa-sanaa hiyoo.

**************************************************** 

 

Hivyo sanaa inabaki kuwa na malengo makuu ambayo ni kuelimisha, kuonya, kuburudisha na hata kuelekeza jamii. Sanaa pia ni utambulisho wa jamii husika. Kupitia sanaa unaweza kuifahamu jamii kuwa huu ni fulani hata kama hujawahi kuishi na jamii hiyo.

Sanaa inayo matawi mengi mno, lakini kwa leo naomba tujikite zaidi katika tawi la muziki.

Muziki ni nini hasa?
Kwa mujibu wa kamusi sanifu ya Kiswahili, muziki umeelezwa kuwa ni “mpangilio wa ala na uimbaji unaoleta athari fulani kwa kiumbe”. Hii ina maana kuwa kama msanii wa muziki hapangilii ala zake na kuimba kwa ustadi basi, anachokifanya msanii huyo si muziki bali ni kelele za kawaida.

Si nia yangu kufundisha muziki kupitia makala haya, isipokuwa ninataka tutafakari ni kwa namna gani wasanii wetu wa muziki wanavyoshiriki katika jitihada za kuleta maendeleo katika taifa letu na pia kuipotosha jamii.

Tutafanya makosa endapo tutaisahau sekta hii ya sanaa ya muziki katika ujenzi wa jamii yoyote.

Muziki una historia ndefu tena usioyumba katika ustawi wa jamii ya binadamu. Katika Biblia tunaambiwa kuwa Mfalme Sauli alipochoka na kujisikia hovyo asijue la kufanya, alipata burudani ya muziki kutoka kwa msanii chipukizi na mchunga kondoo, Daudi.

Kwa kuwa muziki wa kijana huyu ulipangiliwa vilivyo, uliweza kumliwaza Mfalme Sauli na kujisikia aliyepona na kurudia hali yake ya awali. Muziki huponya.

Ukuta mkubwa, mnene na uliojengwa kwa uimara wa hali ya juu, Yeriko, ulisambaratishwa kwa muziki pale wana wa Israeli walipopuliza tarumbeta zao kuuzunguka mji ule kwa siku saba. Ukuta ulianguka kwa kishindo kwa kusukumwa na mawimbi tu ya sauti za tarumbeta. Tukio hili linatufanya tuamini kuwa muziki una nguvu pengine hata kushinda mabomu ya B 52 NA MENGINEYO UNAYOYAFAHAMU.

Muziki umeziunganisha ndoa zilizovunjika. Muziki pia umezisambaratisha ndoa na familia nyingi. Muziki umewatoa watu machozi ya furaha ama huzuni. Muziki umevuruga na kuharibu jamii pia 

Wanasayansi bado wanakesha katika maabara kubwa duniani kutafiti ni kwa nini muziki una athari kubwa katika ubongo wa binadamu. Muziki umetumiwa kama dawa kwa wagonjwa wa akili na walio na msongo wa mawazo.



Utafiti uliofanywa miaka ya hivi karibuni na Chuo Kikuu cha Lomalinda nchini Marekani, ulionesha nguvu ya muziki pale wagonjwa 100 walipowekwa katika chumba maalumu bila kupewa dawa isipokuwa muziki na wengine 100 chumba kingine wakipewa dawa na huduma zote za tiba. Wagonjwa walioliwazwa tu kwa muziki walipona upesi kuliko waliopewa dawa.

Tafiti zote ni msukumo kwetu kuwa muziki ni sanaa yenye nguvu kubwa inayopaswa kuangaliwa kwa umakini.

Na hii inamfanya mtu yeyote anayetaka kujiingiza kwenye sanaa ya muziki sharti kujisahili na kujiridhisha kama kweli amefaulu kuwa mwanamuziki. Kujisahili ni pamoja na kusomea muziki ili kujua miiko ya sanaa hiyo. Kipaji cha muziki huwa na maana zaidi kinaposaidiwa na elimu stahiki.

Muziki ukitumiwa vizuri huwa ni baraka, na matunda yake huwa matamu kwa jamii pana. Lakini pia muziki ukitumiwa vibaya yaweza kuwa laana na kuongoza anguko la jamii inayosikiliza na kuona muziki huo.

Muziki ni uwanja huru wa kutoa mawazo na maoni chanya kwa manufaa ya jamii. Hii inamfanya mwanamuziki kujihoji anataka kuongea nini kupitia tuni ya muziki wake? Mbali na malengo yake binafsi, msanii pia anapaswa kuwa na malengo kwa jamii yake.

Hebu tuone mifano ya wasanii wa muziki waliolenga mambo fulani kwa jamii zao.

Mariam Makeba wa Afrika Kusini, alitumia muziki wake kutetea utamaduni wa Mwafrika hasa wa jamii yake ya Wazulu. Imewahi andikwa kuwa jamii yoyote ile itakayothubutu kuzipa kisogo tamaduni zake na kushadadia tamaduni pepe za watu wengine ni lazima ianguke na huenda isisimame tena.

Sote tunamkumbuka Hayati Bob Nesta Marley wa The Wailers alivyotumia muziki wake wa Reggae wenye asili ya Caribean kupinga ukandamizaji kote duniani. Nyimbo zake zililenga ukombozi kwa wanyonge hasa Waafrika. Nyimbo kama “Liberation” ulikuna hadi ndani ya masikio ya Rais wa Zimbabwe, Komredi Robert Gabriel Mugabe.

Manu Dibango wa Nigeria alitumia muziki kuhamasisha utamaduni wao wa mavazi ambao leo tunauonea gele.

Wanamuziki wenzie wakamuunga mkono. Akina Fela Anikulapo Kuti aliimba nyimbo zenye ujumbe mzito ukiwaasa Waafrika kujitambua na si kukubali kila jambo bila kuhoji. Alieleza fikra zake kwa wimbo kama “I like this gentleman”.

Hatuwezi kuwasahau akina Luambo Luanzo Makiadi, mwasisi wa rhumba ya Kizaire alivyotumia muziki kutangaza nchi yake ya Zaire kwa mataifa makubwa duniani. Alitumia muziki kutangaza utalii wa nchi yake.

Leo pombe aina ya Chibuku inauzwa hadi kwenye maduka makubwa (super markets) Ulaya. Yote ni jitihada za mwanamuziki Yvonne Chaka Chaka wa Afrika Kusini wakati sisi bado tunawafukuza mama zetu kama swala eti wanauza pombe “haramu” gongo. Wenzetu Uganda wanasindika gongo hiyo na sasa inauzwa kwenye soko moja na konyagi.

Hayati Lucky Dube; alipigania ubaguzi wa rangi na hata kutumia muziki ili mfungwa Nelson Mandela aachiwe huru. Hata mwenzie Chico Twala na kibao chake “We miss you Manelo” alipinga ubaguzi wa rangi. Neno “Manelo” ni Mandela, lakini kutokana utawala wa chuma wa Kikaburu, hakuruhusiwa kutaja jina hilo.

Hata baada ya kazi za suluba, hasa kwenye mashamba ya wazungu wa Amerika, watumwa Waafrika walikusanyika jioni kujiliwaza kwa muziki wa soul.

Maandamano makubwa yaliyoitishwa na mpigania haki za Waafrika nambari wani duniani, Martin Luther King yalitawaliwa na sauti za muziki zilizolalamika kudai haki. Kwa kuwa hawakuwa na muda wa kupangilia ala na uimbaji, ndipo walipoamua kuimba kwa kufoka-foka (Hip hop).

Hapa ndipo tunapoweza kuyakumbuka makundi kama Naught by Nature. Na pia hapa ndipo unapogundua kwa nini majina ya wanamuziki wa Kimarekani wenye asili ya Afrika yanatoa taswira ya ukorofi - Bad Boys, Gangstars Unit, Above the Law, Bad Killer na mengine unayoyajua.

Majina haya yalitoa ujumbe wa kutanua misuli kutaka kujikomboa kutoka kwenye makucha ya chuma ya ubaguzi wa rangi.

Hata wakati wa vita vya kumpiga na hatimaye kumng’oa Nduli Idd Amini, tulitumia muziki kuwahamasisha wapiganaji wetu ili waweze kusonga mbele. Kulikuwa na nyimbo kama “Yuko wapi joka huyo, fyeka pori tumkamate”.

Ndugu msomaji, natumai umegundua kuwa muziki wa kila msanii ulilenga kitu fulani mbali na kuburudisha. Wasanii walitumia sanaa yao kukomboa jamii zao. Wapo waliopoteza maisha yao kwa kutetea wanyonge kupitia sanaa ya muziki. Kifo cha Bob Marley bado kimebaki kitendawili hadi leo na Shirika la Kijasusi la Marekani (CIA) ikitajwa kuhusika.

Sasa tuna kitu kinaitwa Tanzania Music Award, eti inatoa tuzo kwa wasanii bora wa muziki ambao wanapoenda kwenye vipimo vya kimataifa hurudi kwa aibu kubwa.

Haijulikani wanatumia vigezo gani kumtambua msanii bora wa Kitanzania.

Hapa tunajiuliza ni yapi malengo ya wasanii wetu wa muziki? Wanalenga ukombozi gani?

Sasa taifa liko kwenye hatari ya kuangamia kutokana na ufisadi unaoendeshwa na tuliowapa mamlaka. Hadi watoto wadogo wanapiga kelele japo hawasikiki. Wako wapi wasanii wetu wa muziki nao watumie sauti zao kupinga na kukemea ufisadi huu? Mfano: HASA WA MUZIKI WA INJILI?.

Mbona wasanii wetu nao wanazidi kujitenga na jamii ambayo ndiyo nguzo yao kuu? Nani aliyewabadilisha wasanii wetu na kuwaambia kuwa taifa lina tatizo la mapenzi tu, nao kila wimbo ni kuimba juu ya mapenzi?. Naona sasa umeanza kupata picha namna muziki unavyobadilisha na kuharibu maadili hata uwezo wa mtu wa kiutashi.

Nani aliyewapiga upofu wasanii wetu wasione hata haja ya kuwakemea si viongozi fisadi pekee kupitia muziki bali hata wasiojali familia zao? Watanzania wanazidi kuogelea kwenye bahari ya umasikini bila kuwa na watetezi wao dhidi ya ugandamizwaji na utawala wa kidhalimu wa kujuana na viunganishi vya hapa na pale. Kwa nini hili lisiwaguse wasanii wetu nao wakapaza sauti angani kwa MUNGU ili afute hali ya ulafi na uporaji wa rasilimali za umma?



Kama lengo la sanaa ni pamoja na kuonya na kuelimisha, kwa nini wasanii wetu wasiwaelimishe na wao pia waoneshe njia sahihi ya kuenenda? Kwanini wanazidi kujikita kwenye burudani tu ilhali taifa linaangamia kwa rushwa, tena nzito nzito?

Wako wapi wasanii walio tayari kusema potelea mbali hata kama nitafungwa jela ama iwe ni kwa ajili ya MUNGU lakini nitatumia sanaa yangu kuonya watawala ambao hata hivyo historia imeonesha mara zote wamekufa kwa aibu?

Yuko wapi msanii wa aina hiyo asimame tumtambue na kumbatiza jina la mtetezi wa wanyonge?
Nani aliyewakataza kuimba nyimbo za ukombozi zisizoweza kuisha ladha? Mfano kuna wimbo wa injili unaoimbwa; NIMEKOMBOLEWA NA YESU NA SASA NIMEFURAHI KWA BEI YA MAUTI YAKE MIMI NI MTOTO WAKE.

Kwa nini wasanii wetu wanazidi tu kutekwa nyara na tamaduni za magharibi? Kwa nini wasanii wetu wanazidi kutopea kwenye utumiaji wa dawa za kulevya badala ya kuwa mabalozi wa kuupiga vita?

Wasanii wetu wanatuambia wao ni kioo cha jamii kwa mantiki kwamba tuwatizame ili tujikosoe na kisha tuenende kama wao.

Kwa maneno mengine tuvae suruali za kushuka kama wao, wanaume watoge masikio wawe kama wanawake kama wao, wanawake watembee nusu uchi kama wao, tuweke hereni hadi ulimini kama wao, hata mama zetu watembee vitovu nje kama wao, tuongee Kiingereza cha “yah”, “yu no”, “ze” na “zati” kama wao, tunywe pombe hadi kulala baa kama wao, tufikirie mapenzi muda wote kama wao, tuzisuse tamaduni zetu kama wao. Kwa kifupi tuwe makasuku na chiriku wanaopokea kila kitu kinachotoka Ulaya na Marekani kama wao.

Tuzichukie ngozi zetu kama wao, hata nywele zetu tuzichukie na badala yake tubandike za wazungu waliokufa Ulaya. Tupake midomo yetu damu tuonekane wauaji kama wao.

Eti wanataka tuamini kuwa sisi hatuna utamaduni wowote unaoweza kuigwa na wazungu isipokuwa ni sisi kuiga kila kitu chao! Huu ni utumwa wa kujitakia tena usiohitaji mijeledi.

Kwa nini wasanii wetu wasitambue vita kuu ya utamaduni inayoendelea duniani kote na msingii wake wa kihistoria?

Waarabu wana hamu ya kuona jamii yote ya binadamu inafuata tamaduni zao, Wazungu nao wanatamani watu wote wangekuwa kama wao, Wachina nao hivyo hivyo, Wanaigeria nao hawako nyuma kusambaza utamaduni wao. Kufanya dunia kuwa kijiji kimoja ni matokeo ya kila taifa kuyashawishi mataifa mengine kuwa kama wao. Nani aliyewafunga macho wasanii wetu hasa wa muziki wasiyaone haya? HII INAWAHUSU NA WA INJILI PIA.

Mbona sasa hatuna faida ya kuwa na wasanii kama hawasaidii katika ujenzi wa taifa?

Wanadai eti sanaa ni ajira hivyo maslahi yao mbele, utamaduni nyuma. Sina ugomvi juu ya hilo lakini, kinachowafurahisha ni nini hadi wacheke na kupasuka mbavu pale watakapotumia muziki huo kujinufaisha huku kundi kubwa la vijana wakipotea njia sahihi ya kuenenda kimaadili?

Kwa nini wanunuzi wa kazi zao wasigome kununua tepu zao hadi pale watakapojirekebisha kutanguliza MAADILI mbele, maslahi nyuma?


Umefika wakati wa kuwahukumu wasanii wetu kwa matendo yao. Nao pia imefika wakati wa kusimama na kuitetea jamii yetu kwa kukemea maadili yote yasiyo na asili ya Ki-MUNGU kuanzia ufisadi, uvaaji usio na heshima, ubadhirifu na mengine mengi yasiyotoa picha halisi ya JAMII BORA YENYE MAADILI Tanzania. 
 
 


Jumanne, Julai 24, 2012

Habari njema kwa wakazi wa MBEYA, MWANZA, KIGOMA na ARUSHA.



(Labda milima ambayo sijaona ikibuniwa ingawa nayo inatajwa kugunduliwa) 

Unayoyaona leo kesho unaweza usiyaone na kila linapoondoka moja jingine huja.
Hayo ndiyo maisha ya kila siku ya mwanadamu. Sasa ili uishi kwa raha kila ulipatalo sema ahsante kwa Mungu. 

Morning Star Radio imepanua wigo wa huduma ya utangazaji wa kazi za waimbaji wa nyimbo za injili hapa Tanzania, hii ni habari njema  kwa wakazi wa MWANZA sikiliza  matangazo yetu kupitia 102.1 fm, KIGOMA 103.3 fm, MBEYA 106.9 fm. ARUSHA 102.5
Na kwa wakazi walio jirani na hiyo mikoa niliyoitaja endeleeni kubarikiwa na ujio mpya wa kituo cha Radio kinacholeta.

Maisha yana kanuni moja kubwa nayo ni kubuniwa kwa vitu. 

Ukurasa ndani ya facebook BONYEZA HAPA

Jumatatu, Julai 23, 2012

WEWE, MAISHA YAKO, NDOTO ZAKO

Photo By: www.rhodayouths.wordpress.com


Ukijua unachokithamini itakusaidia kuwa mkweli kwako binafsi, hata wakati mtu mwingine
anapokulazimisha kufanya kitendo unachodhani ni makosa. Maadili yako yatakusaidia kuchagua
lililojema kwako; ambalo wakati mwingine, baada ya kuchagua, itabidi uishi nalo daima.

StaDi Za MaiSha
Unahitaji stadi za maisha pia ili uwe salama. Kusema kweli “Stadi za maisha” zinaweza kuwa stadi za kuokoa maisha, kama vile;

Kuelezea hisia zako. 
Hisia zako ni muhimu, lakini watu wengine hawawezi kujua unavyojisikia mpaka uwaeleze. Jifunze jinsi ya kuwafanya watu wengine wajue kile unachofikiri na unachokitaka kwa kusema moja kwa moja na kutumia sentensi zinazoanzia na “mimi” – “mimi ninataka” “mimi ningelipenda” “mimi ninahitaji”“mimi Sipendi” ………… .” Fanya mazoezi ya kutumia sentensi zinazoanza na “mimi” mpaka utakapozoea na kujisikia huru kuzitumia.

Tetea hoja yako. 
Una uhuru wa kufikiri na kujihisi unavyopenda. Ni vema kujifunza jinsi ya kuwasilisha
mawazo yako kwa wengine bila ya kuwaudhi au kuwafanya wajisikie vibaya, usionyeshe uadui, ugomvi wala kukosoa sana.

Tetea unachoamini bila kujali wanayosema watu wengine.
Kila mtu ana imani na yaliyo sahihi na yasiyo sahihi, mazuri na mabaya. Imani hizi zinaitwa kanuni. Wakati mwingine unaweza ukawa unajua kanuni zako lakini mambo yanaweza yasiwe wazi sana kiasi cha kukufanya utumie muda kufikiria lipi ni sahihi kwako na ni kwa nini. Iwapo unao uhakika wa usahihi wa kile unachofikiria na kwa nini unakifanya, na kwa nini hupendelei kukifanya utaweza kusimama imara na lile unaloamini. Hivyo basi msimamo wa namna hii utakupa heshima mbele za watu.

Jihadhari na yanayotokana na shinikizo.
Jinsi unavyoelekea kwenye utu uzima unatakiwa kufanya maamuzi mengi peke yako. Wakati mwingine watu wengine wanaweza kukuhimiza na kukusukuma kufanya maamuzi fulani na ukushawishika kufanya hivyo.

Lakini ufahamu kuwa kufanya maamuzi mazuri maana yake ni kupima chaguo zote zilizopo na kufikiria matokeo kwa kila chaguo.Inaweza ikawa kazi ngumu iwapo kuna mtu anakuharakisha au anakushinikiza uamue haraka. Kitu muhimu katika kufanya maamuzi bora ni kuwa na uhakika wa kanuni zako na malengo yako ya maisha kwa ujumla.
Kuwa na msimamo wa pekee ndiyo stadi za Maisha.

Jumapili, Julai 22, 2012

BADILIKO KUBWA, CHANGAMOTO KUBWA

Image By: www.imkeepingup.com

 Mahali pengi ujana umekuwa mgumu kueleweka, na hasa siku hizi vijana wanapata matatizo ambayo wazazi wao, mabibi hata babu zao hawakuwahi kuyapitia.
 
VIJANA TOKA KENYA NA GHANA WANAELEZA HIVI:
 
Patric, kutoka Kenya (Umri,miaka 16)
“Nilichokifurahia katika ujana balehe wangu ni kuwajibika katika majukumu ya nyumbani hasa wazazi wanapokuwa hawapo. Majukumau haya nayapenda kwasababu ninadhani nimeshakua na ninaweza kujidhibiti mimi mwenyewe na wadogo zangu”.

Naana, kutoka Ghana. (Umri; miaka 17)
“Yapo mambo mengi yanayomhusu kijana balehe ambayo siyapendi. Ninakumbuka nilipokiwa na umri mdogo nilikuwa na uhuru zaidi kuliko sasa.Lakini kwa sasa zipo sheria na miongozo mingi.”

TUKIANGALIA;

Mwonekano wako mpya na kujitambua kwako kunawafanya wazazi, shangazi zako na wajomba kuwa na wasiwasi kwa sababu wasingependa upate matatizo na wala wasingependa ufanye makosa makubwa kama vile kupata mimba (au kwa kumpa mimba rafiki wa kike) wakati ungali unasoma. Zaidi ya yote wanakuwa na wasiwasi kwa sababu wanafahamu kwamba umri kati ya 10-19 unaweza kuwa na athari kubwa katika ukuaji wako na aina ya maisha utakayokuwa nayo.

JE UNAFAHAMU VIJANA HUFIKIRIA KWAMBA HAKUNA JANGA LINALOWEZA KUWAPATA?

Ni tabia ya vijana duniani kote, katika nchi tajiri na maskini – kufikiria kwamba mambo mabaya
hayawezi kuwatokea. Hujiambia,

“ Haitatokea kwangu”. Wakati mwingine hujiamini sana na kuhisi wako salama mno.

Je wewe uko hivi? 
Unadhani unaweza kujaribu kitu cha hatari na lisikupate jambo? 
Kwa mfano, wewe na rafiki yako wa kike (msichana) mnafahamu kuhusu dawa za kuzuia mimba. Lakini
mnadhani kwamba ili mradi hamjamiiani mara kwa mara, msichana hawezi akapata mimba.

Au unaweza ukawa na ufahamu mkubwa kuhusu VVU, virusi vinavyo sababisha UKIMWI. Unaweza
ukafahamu kwamba maambukizi yanaweza kutokea kwa njia ya kujamiiana bila kinga, lakini unafikiri kwamba rafiki yako wa kiume hawezi kuwa na maambukizo. Unakataa kufikiri kuwa unaweza kupata maambukizo ya VVU na haiwezekani pia kwa wale watu unaowafahamu kupata ugonjwa huo.

Je haya yanakuhusu? 
Kama ndivyo, hapa kuna mambo ambayo unahitaji kuyazingatia:

Nitarejea kukwambia kuhusu: 
WEWE, MAISHA YAKO NA NDOTO ZAKO.

Jumamosi, Julai 21, 2012

Watoto Wanaoishi Katika Mazingira Magumu




Tanzania ni moja kati ya nchi nyingi barani Africa zinzokabiliwa na wimbi kubwa la watoto wanoishi katika mazingira magumu .
Utafiti ulliofanyika ulitambua makundi mbalimbali ya watoto hao ikiwa ni pamoja na:-

01. Watoto yatima ( Orphan children)
02. Watoto wenye ulemavu ( Children with disabilities)
03. Watoto wanaojilea ( Children parents)
04. Watoto wanaoishi na virusi vya ukimwi (Children with HIV/AIDS)
05. Watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albino)
06. Watoto wa mtaani (Children in/of street)
07. Watoto walioathirika kwa ubakaji (Children victim of rape)
08. Watoto wanaolelewa na wazee kupindukia (Children in eldery families)
09. Watoto walio kwenye ajira hatarishi (Children in exploitative labour)
10. Watoto walio kwenye biashara ya ngono ( Children sex workers)
11. Watoto wenye magonjwa sugu k.m. kifafa ( Chronicaly ill children)
12. Watoto waliopata mimba za mapema (Early pregnancy)
13. Watoto waliotelekezwa (Children in foster families)
14. Watoto walioathirika kwa madawa ya kulevya (Drug abuse children)
15. Watoto waliolazimishwa kuingia kwenye ndoa (Forced marriage)

HOJA.
1. Jamii inajua nini kuhusu makundi haya ya watoto?
2. Mikakati gani ifanyike ili kuhudumia makundi haya ya watoto hasa vijijini?
3. Serikali ichukue hatua zipi ili kunusuru maisha na ongezeko la watoto hawa?
4. Njia gani zitumike ili kupata takwimu zinazoonyesha tatizo hili kila wakati kitaifa?

Ijumaa, Julai 20, 2012

SABABU GANI ‘NIMHESHIMU BABA YANGU NA MAMA YANGU’?





“WAHESHIMU baba yako na mama yako.”

Kwa vijana wengi maneno hayo yanasikika kama ni jambo la zile enzi za giza.


Kijana-msichana Veda alijulisha uasi wa waziwazi dhidi ya babae kwa kufanya matembezi na mvulana aliyetumia vibaya madawa ya kulevya na alkoholi. Kwa kukaidi, angelienda pia kucheza dansi mpaka chee.


“Nilihisi kwamba yeye alikuwa mzuivu mno,” aeleza Veda.

“Nilikuwa na umri wa miaka 18, name nilifikiri mimi ni mjuzi wa yote. Nilihisi baba yangu alikuwa bahili na hakutaka kamwe nione raha, kwa hiyo mimi nikaenda nje na kufanya nililotaka kufanya.”


Yawezekana kijana; walio wengi hawatakubaliana na vitendo vya Veda. Lakini, kama wazazi wao wa masomo ya nyumbani, au wawe wamefika nyumbani saa Fulani, wengi wangechacha kwa uchungu wa moyo au, jambo baya hata zaidi, wangekaidi wazazi wake inaweza hatimaye kumaanisha si kama tu itakuwa ni vita au amani nyumbani bali pia uhai wake mwenyewe.


Kwa maana amri ya ‘kuheshimu wazazi’ inatoka kwa Mungu, na anaambatanisha motisha ifuatao na kutii amri hiyo”. (Waefeso 6:2, 3) Inaweza kumaanisha faida kubwa au hasara kubwa.


Kwa hiyo, tuangalie upya linalomaanishwa hasa na kumheshimu babako na mamako.




Alhamisi, Julai 19, 2012

Picha za Tukio la Tigo Ilivyokabidhi Fedha za TUCHANGE Kwa Hassan Majaar Trust




























HUU NI MPANGO WA MUDA MREFU ULIOUNDWA ILI KUBORESHA MAZINGIRA YA KUSOMA MASHULENI KWA KUGAWA MADAWATI KATIKA SHULE MBALIMBALI ZA WAHITAJI.

SHEREHE ZA MAKABIDHIANO ZILIHUDHURIWA NA MHESHIMIWA DK SHUKURU KAWAMBWA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI STADI, WANACHAMA WA HMT, MWANDAMIZI MTENDAJI WA TIGO NA WAFANYAKAZI.

Picha zote kwa hisani ya: Prince Ema. Hebu tembelee H A P A

UPANDE WA NYUMBANI




Hapa Tutashughulika na Washiriki wa Familia Kwa Namna hii:

“Nyumbani kuzuri.” Usemi huu unaojulikana sana unaeleza hisia ambayo siku hizi yaonekana ya kizamani na isiyofaa. Migongano yenye kuendelea ya familia inageuza nyumba nyingi kuwa kwa halisi Nyanja za mapigano. Na pengo kubwa la ukosefu wa uwasiliano mara nyingi huzuia majaribio yoyote ya kufanya suluhu.

Je! Wataka nyumba yenu iwe pumziko la amani badala ya kuwa kao lenye ugomvi unaochacha? Ni kweli, washiriki wengine wa familia lazima wafanye sehemu yao. Lakini kwa kushika kanuni chache za Biblia, kuuna mengi unayoweza kufanya ili kuchangia amani nyumbani mwenu.

Jumatano, Julai 18, 2012

YALIYO YA KUKUMBUKA


Rudolf II 
 Alizaliwa 18 Julai, 1552 na kufariki 20 Januari, 1612 alikuwa Kaizari wa Dola la Ujerumani kuanzia 12 Oktoba, 1576 hadi kifo chake. Alimfuata baba yake, Maximilian II, na kufuatiwa na mdogo wake, Matthias.


Hendrik Antoon Lorentz 
 Alizaliwa 18 Julai, 1853 na kufariki 4 Februari, 1928 alikuwa mwanafizikia kutoka nchi ya Uholanzi. Alitafiti nadharia ya elektroni. Pia alichunguza nadharia ya Albert Einstein (Relativity Theory) na ya kwanta. Mwaka wa 1902, pamoja na Pieter Zeeman alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Fizikia.


Nelson Rolihlahla Mandela 
alizaliwa tarehe 18 Julai, mwaka 1918. Ni rais wa kwanza aliyechaguliwa kidemokrasia nchini Afrika Kusini. Alikuwa mwanasheria na mwanachama wa ANC aliyepinga siasa ya Apartheid katika Afrika Kusini. Mandela alitumikia kifungo cha maisha kwa miaka 27 kutokana na harakati zake za kuupinga ubaguzi wa rangi. Alifungwa katika kisiwa cha Robben. Baada ya kuachiliwa huru mwaka 1990 alianzisha sera ya maridhiano. Mwaka wa 1993, pamoja na Frederik Willem de Klerk alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Amani.


Roald Hoffmann 
Alizaliwa 18 Julai, 1937 alikuwa mwanakemia kutoka nchi ya Marekani akiwa amezaliwa nchini Poland. Hasa alichunguza utaratibu wa athari za kikemia. Mwaka wa 1981, pamoja na Kenichi Fukui alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.


Hartmut Michel 
Alizaliwa 18 Julai, 1948. Ni mwanakemia kutoka nchi ya Ujerumani. Hasa alichunguza ugandishaji wa protini. Mwaka wa 1988, pamoja na Johann Deisenhofer na Robert Huber alikuwa mshindi wa Tuzo ya Nobel ya Kemia.


Joseph Nestroy Kizito 
Amezaliwa 27 Julai, 1982 Uganda ni mchezaji wa mpira wa miguu wa kulipwa kutoka nichini Uganda, ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya FK Vojvodona nchini Serbia tangu Januari mwaka 2005. Yeye pia ndio kapteni wa Timu ya Taifa ya Uganda. Kizito alifunga goli dhidi ya wa pinzani wao wa kuu FK Crevena Zvezda katika Ligi kuu ya Serbia katika msimu wa mwaka 2005/2006 mechi hiyo ilichezeka nyumbani kwao. Goli hilo lilivunja rekodi ya kukaa muda mrefu bila kuwafunga wapinzani wao wa jadi FK Crvena Zvezda zaidi ya miaka kumi.

Jumapili, Julai 15, 2012

Je Unafahamu Kwamba Muziki ni TIBA?




Leo ktk kipindi Morning Star Radio nimeona nikuletee jambo muhimu sana ambalo weeengi walikuwa hawafahamu. Ni suala ambalo hata wewe ukitumia muda wako kuchunguza utabaini ukweli ulio ukweli halisi.


Usikilizaji wa muziki huweza kuwasaidia wagonjwa walio na matatizo sugu ya mkandamizo wa mawazo (stress) na tiba ya kiwango fulani kwa maradhi ya moyo pale mishipa ya moyo inapoelekea kuziba. Utafiti wa kitiba uliofanyika nchini Marekani umebaini kuwa kusikiliza muziki uliotulia unaweza kupunguza ongezeko la msukumo mkubwa wa damu na kuchanganyikiwa kwa wagonjwa wa moyo.

Wataalamu hao wanasema kuwa kuishi huku ukiwa na matatizo ya moyo ni jambo linalosumbua sana kwahiyo hali hiyo inahitaji tiba mbalimbali ikiwa ni pamoja na ushauri wa matumzi ya vyakula, vinywaji , lakini pia kuufanya ubongo usipate mkandamizo bila sababu.



Lakini hata hivyo Dr. Joke Bradt wa kituo cha sanaa na ubora wa maisha katika kituo cha utafiti wa kitiba katika Chuo Kikuu huko Philadelphia nchini Marekani anasema ‘majaribio yaliyokwisha fanyika ni machache na hasa aina ya muziki unaofaa ni kwamba usikilizwe kwa muda gani na kwamba bado wanalifanyia kazi suala hilo. Tafiti zilizokwisha fanyika ni 23 kwa wagonjwa 1,461 kwa kuwapatia muziki maalum uliorekodiwa na kuungwa katika mishipa , na kazi hiyo hufanywa na wataalamu mabingwa wa masuala ya maradhi ya moyo na sanaa.

Tayari wanamuziki duniani kila mtu anakuna kichwa kufikiria kitu gani atunge na kukiweka katika muziki mororo ili uteuliwe kuwa ‘dawa’ na bila shaka atakuwa billionea ghafla. Penda kusikiliza muziki laini unapojikuta umetindikiwa na mawazo kibao…

Jumatano, Julai 11, 2012

ISHARA YA KUTAMBUA

Picha kwa hisani ya: www.telecomcircle.com

MASWALI yanaibuka. Je, kikosi kilichomteka daktari huyo na kumpeleka kwenye msitu wa Mabwepande, Dar es Salaam kimefadhiliwa na serikali au magaidi?
Dokta Steven Ulimboka, mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari alikumbana na kikosi cha watekaji, watesajii na wauaji. Kama ni magaidi walikusudia nini? Magaidi walikuwa na nongwa ipi na Dk. Ulimboka? Watekaji wametoa ujumbe wowote? Je, kuna historia ya ugaidi wa namna hii nchini?

Je, watekaji hawawezi kuwa mawakala wa serikali? Je, hakiwezi kuwa kikosi maalum cha kutesa watu kwa siri chini ya udhamini wa serikali? Jibu la maswali mawili hayo ni ndiyo, maana hiyo, ndiyo hasa ina nongwa na Dk. Ulimboka aliyeongoza mgomo wa madaktari nchi nzima kudai hali nzuri ya utumishi.

Sikia. Mtu wanayemfahamu kutoka ikulu anampigia simu Dk. Ulimboka ili wakutane kujadili ufumbuzi wa mgomo. Dk. Ulimboka na mwenzake Dk. Deogratius Michael wanakwenda eneo la kikao; wanamkuta mtu anayejiita Abeid; lakini ghafla wanatokea watu na kumchukua yeye tu.

Watekaji wanakwenda naye Mabwepande, msitu uleule ambao mwaka 2006, polisi wa serikali walitumia kuua watu wanne – wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva teksi mmoja.

Vijana wale wafanyabiashara walitekwa na polisi, wakateswa, wakaporwa mali waliyokuwa nayo kisha wakatwangwa risasi za kisogoni – wakafa. Unyama mkubwa. Mambo yalipojulikana, polisi wakadai kuwa walikuwa majambazi.

Rais Jakaya Kikwete akaunda tume; ikahoji watu, ikapata ushahidi kwamba polisi walihusika kuteka, kuwapeleka msituni na kuua. Kesi ikafunguliwa, lakini “mahakama” ikasema polisi walioteka na kuwapeleka Mabwepande na kuua hawana hatia; ikawaachia!

Wiki iliyopita, ‘mawakala’ waliokuwa na nongwa kubwa na mgomo, wakafanya juhudi usiku wa kuamkia siku ambayo serikali ilisema itatoa msimamo juu ya mgomo huo, wakatekeleza lile Waziri Mkuu, Mizengo Peter Pinda alilosema “…liwalo na liwe” wakamteka, wakampiga, wakamng’oa meno na kucha kushinikiza ametumwa na nani kuongoza mgomo. Serikali inatoka vipi hapa?

Mwaka 2008 Pinda alisema wanaoua albino wauawe, kauli inayotafsiriwa sasa kuwa hata wanaoua watu kwa njia ya mgomo wauawe. Ndiyo, waliotenda unyama huo wakawapigia simu madaktari wakachukue “mzoga” wao.

Serikali imekana kuhusika. Lakini hakuna serikali yoyote duniani iliyowahi kukiri kuhusika katika mauaji ya wanasiasa au wanaharakati au waandishi wa habari au wapinzani.

Vikosi maalum vya kuteka watu, kuwapoteza, kutesa na hata kuua, hutekeleza unyama huo kutetea au kulinda maslahi fulani, kama vile biashara haramu au ufisadi au maslahi ya kisiasa.

Mathalani magenge ya wahuni na wauzaji wa dawa za kulevya Mexico na Colombia huteka viongozi wa juu serikalini au jamaa zao na hushinikiza walipwe mamilioni ya dola kama kikombozi.

Magaidi wa Colombia waliounda jeshi linalofahamika kama Revolutionary Armed Forces of Colombia (FARC) huteka, hutesa na kuua viongozi wa serikali wanaopinga biashara ya dawa za kulevya.

Miaka ya 1970 vilikuwepo vikundi vingi vya kigaidi na kimojawapo kiliongozwa na Ilich Ramírez Sánchez “Carlos the Jackal,” raia wa Venezuela.

Matukio ya kuteka na kuua wanasiasa yakifanywa na vikundi vya watu, serikali hutumia rasilimali zake zote kuwasaka wahusika.

Hii ndiyo sababu, Carlos ambaye aliitesa sana Ufaransa na kuvamia ofisi za makao makuu ya Umoja wa Nchi za OPEC mjini Vienna, Austria mwaka 1975 na kuua mawaziri watatu na wengine 63 kutekwa wakiwemo mawaziri 11, alinaswa na sasa anatumikia kifungo cha maisha jela nchini Ufaransa.

Hata Osama bin Laden aliyetikisa dunia kuanzia miaka ya 2000, aliuawa huku kikundi cha Al-Shaabab cha Somalia kikisakwa. Ikumbukwe kila kikosi cha watu maalum kikiteka watu maarufu, hulenga ama kulipwa fedha au kushinikiza wenzao waliofungwa waachiwe kabla hawajauawa au masuala ya siasa.

Lakini huwa vigumu kuikamata serikali. Ukweli hata kama serikali itakanusha, kama ilivyofanya sasa kwa Dk. Ulimboka au kwa mkurugenzi mstaafu wa Usalama wa Taifa, Imran Kombe na kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Zanzibar, Abdullah Kassim Hanga na wengineo, ushahidi wa mazingira unathibitisha serikali inahusika.

Katikati ya mapambano dhidi ya ufisadi, Mkurugenzi wa MwanaHALISI, Saed Kubenea alipigwa ofisini na akamwagiwa tindikali machoni. Polisi wakafungua kesi; mahakama ikatupa eti ni ugomvi wa mapenzi.

Twende Kenya. Jaramogi Oginga Odinga (baba wa Raila Odinga), licha ya kuwa kiongozi katika serikali ya Kenya, alishtuka serikali kuhusika kisiri kuua watu.

Sababu za kuamini hivyo ziko wazi. Odinga ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani kabla ya mwaka 1964 kuwa Makamu wa Rais alishangaa kuona uhusiano ukibadilika haraka na marafiki zake wakiuawa.

Mwaka 1965 Odinga alishtuka mshirika wake mkuu, mwanasiasa Mkenya mwenye asili ya Asia, Pio Gama Pinto akiuawa. Serikali ilipohojiwa ilikanusha kuhusika.

Baada ya kutafakari mauaji hayo na siasa zisizo na mwelekeo, mwaka 1966 alijiuzulu na kuunda chama cha Kenya People's Union (KPU). Mwaka 1967 alitunga kitabu kiitwacho Not Yet Uhuru yaani Uhuru Bado Kidogo kilichoeleza kwa kina siasa za Kenya.

Humo alieleza kwa kina kwamba mambo yaliyokuwa yanafanywa na wakoloni dhidi ya Waafrika, wanasiasa kutekwa, kupigwa na kuuawa kwa madai ya uhaini, ndiyo yalikuwa yanafanywa chini ya serikali yao dhidi ya raia.

Mwaka 1969 aliuawa Tom Mboya (Waziri wa Uchumi na Mipango), halafu Josiah Mwangi Kariuki (1975), na mwaka 1990 akauawa Robert Ouko (Waziri wa Mambo ya Kigeni), na wanaharakati wa haki za binadamu, Oscar Kamau Kingara (2009) na John Paul Oulo (2009).

Nani alimuua Ouko? John Troon, mchunguzi kutoka Scotland Yard alitaja wanasiasa kadhaa wakiwemo Nicholaus Biwott na Hezekiah Oyugi lakini serikali iliwakingia kifua. Alipoona mazingira ya kutoa ripoti kamili yanahatarisha usalama wake, Troon alirudi Uingereza.

Baadaye Kamati ya Bunge iliyoundwa kubaini muuaji wa Ouko, ilikwenda Uingereza kuonana na Troon ambaye alisema “Ouko aliuawa kwa amri ya serikali.”

Amri hiyo ya serikali “haikutolewa na mtu mwingine yeyote isipokuwa Rais Daniel arap Moi”.

Tena ilielezwa kuwa Ouko, alitekwa shambani kwake Koru, akasafirishwa hadi Nairobi, ambako aliuawa ikulu kisha wakaurudisha mwili wake shambani na kuuchoma moto. Ukatili ulioje?

Hapa Tanzania kuna hukumu zinazotia shaka. Mwaka 1995 walimfukuza Kombe wakamtwanga risasi kwa madai eti walimfananisha na jambazi aliyeiba gari la tajiri mmoja.

Kabla ya kumiminiwa risasi, Kombe alinyanyua mikono juu akiomba wasimdhuru, lakini wapi. Ikafunguliwa kesi eti ya kuua bila kukusudia, wakafungwa na sasa wako huru.

Unatakiwa kuwa na moyo mgumu kuhoji kilichowakuta Hanga, Othman Sharrif na wengineo. Nani aliondoa uhai wao, maradhi au mkono katili wa serikali?

Ili kila mmoja aridhike kwamba serikali haihusiki, Rais Kikwete aunde TUME HURU ya kuchunguza kadhia hiyo basi.
HII KITU NIMEIPATA KTK LINK HII  H A P A