Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumamosi, Oktoba 29, 2011

UWEZO WA NENO

Ngoja nikwambie msomaji wangu jambo hili, kwamba:
MAJIBU YAFANYAYO KAZI ni kipengele kinachoongelea masuala ya kiroho zaidi.


****************************************



****************************************

“Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu

makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu

awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” 2 Timotheo 3:16-17. Katika

Neno la Mungu kimo kila kitu cha muhimu kiwezacho kumkamilisha mtu wa Mungu. Ni

kama nyumba ya hazina iliyojaa bidhaa bora sana na za thamani.

“Lenye pumzi ya Mungu,” “ambayo yaweza kukuhekimisha hata upate wokovu”

(fungu la 15), na kumfanya mtu wa Mungu, “awe kamili, amekamilishwa apate kutenda

kila tendo jema,” Kitabu hiki kipitacho vitabu vyote kina madai ya juu kabisa kwetu ili

tupate kukiangalia kwa kicho. Kukisoma kwa juu juu tu hakuwezi kukidhi [kutosheleza]

madai ambayo kinayo juu yetu, wala kutupatia sisi manufaa yanayoahidiwa humo.

Tungejitahidi kujifunza maana kamili ya lile Neno la kweli, na kuinywa kwa kina roho

ile iliyomo ndani ya Mausia hayo Matakatifu. Kusoma kila siku idadi fulani ya sura, au

kukariri kiasi fulani cha Maandiko kilichowekwa , bila kutafakari kwa makini maana ya

fungu hilo, kutaleta faida ndogo sana. Kujifunza kifungu cha maneno kimoja mpaka

maana yake imekuwa wazi mawazoni mwako, na uhusiano wake kwa mpango ule wa

wokovu uwe unaonekana wazi, kuna manufaa sana kuliko kusoma sura nyingi bila kuwa

na lengo lo lote linaloeleweka, wala kupata mafundisho yo yote yanayokujenga.

Hatuwezi kupata hekima toka katika Neno la Mungu bila kuwa na bidii ya dhati na

maombi katika kujifunza kwetu. Ni kweli kwamba sehemu fulani za Maandiko zi wazi

mno kuweza kukosewa; lakini ziko nyingine nyingi ambazo maana yake haiwezi

kuonekana upesi kwa kuziangalia kwa haraka, maana ile kweli haiwi juu. Ili kuelewa

maana ya vifungu vya maneno kama hivyo, ni lazima kulinganisha andiko na andiko; ni

lazima pawepo na utafiti wa makini na kutafakari kwa moyo wa maombi. Kujifunza

kama huko kutalipwa maridhawa. Kama mchimba machimbo anavyozigundua tabaka za

thamani za madini zilizofichwa chini ya uso wa nchi, ndivyo yule anayeendelea kwa bidii

kulichunguza Neno la Mungu kama hazina iliyositirika, atakavyoweza kuziona kweli zile

za thamani sana, ambazo zimefichwa kwa mtafutaji mzembe.

Lakini mafundisho hayo matakatifu ya Neno la Mungu usipoyafanya kuwa kanuni na

mwongozo wa maisha yako, kweli hiyo itakuwa si kitu kwako. Kweli inafaa tu wakati

ule inapotekelezwa kwa matendo katika maisha yako. Kama Neno la Mungu

linaishutumu tabia yako moja unayoipenda, hisia yako unayoitunza moyoni mwako, roho

uliyoidhihirisha, basi, wewe usigeuke na kumpa kisogo mshauri wako huyo mtakatifu

[Neno la Mungu], bali uupe kisogo uovu ule unaoufanya na kumruhusu Yesu kukusafisha

na kukutakasa moyo wako. Ungama makosa yako, na kuachana nayo kabisa na kwa nia

thabiti, ukiziamini ahadi za Mungu, na kuonyesha imani yako kwa matendo yako. Kama

kweli za Biblia zinafumwa pamoja na matendo ya maisha yako, basi, zitaweza kuyainuamawazo yako toka katika hali yake ya kuipenda dunia pamoja na upotovu wake. Wale

wanaoyajua sana Maandiko watakuwa ni wanaume na wanawake ambao mvuto wao una

nguvu ya kuwainua watu. Katika kuzichunguza kweli hizo za Mbinguni zilizofunuliwa,

Roho wa Mungu huunganishwa na moyo wako kwa karibu sana.

Kuyaelewa mapenzi ya

Mungu yaliyofunuliwa huukuza ubongo, huupa mawazo bora, na kuupa nguvu mpya,

kwa kuuleta uwezo wake mbalimbali katika mgusano na ile kweli kubwa mno ajabu.

Hakuna somo liwezalo kuupa ubongo nguvu yake na kuiimarisha akili kama kulivyo

kujifunza Neno la Mungu. Hakuna kitabu kinginecho chote chenye uwezo mkubwa mno

katika kuyaadilisha mawazo, kuupa nguvu uwezo wa akili, kama ilivyo Biblia, ambayo

inazo kweli bora kabisa. Kama Neno la Mungu lingesomwa linavyopaswa kusomwa,

basi, tungeweza kuuona upana wa mawazo, uthabiti wa nia, ubora wa tabia, kama ule

unaoonekana kwa nadra sana katika nyakazi hizi.

Walakini, kujifunza Biblia kunapewa nafasi ya pili katika mawazo yetu, na kwa ajili

hiyo, hasara kubwa inapatikana. Ufahamu wetu unafuata usawa wa mambo yale

unayoyazoea. Kama wote wangeifanya Biblia kuwa somo lao, tungeweza kuwaona watu

waliokua vizuri, wenye uwezo wa kufikiri kwa kina zaidi, ambao wangeonekana kuwa na

ujuzi mkubwa kuliko wale waliosoma kwa bidii sayansi mbalimbali pamoja na historia

za ulimwengu huu, ambao wanaiacha Biblia. Biblia humpa mtafutaji wa ile kweli

nidhamu ya hali ya juu kiakili, naye anapotoka katika kutafakari mambo hayo ya Mungu,

nguvu zake za akili zikiwa zimesitawishwa; nafsi yake inanyenyekezwa, wakati Mungu

na kweli yake iliyofunuliwa kwake inapotukuzwa. Ni kwa sababu watu hawazifahamu

historia za thamani zilizo katika Biblia, ndiyo maana kuna hali ya kumtukuza mno

mwanadamu na heshima ndogo mno hutolewa kwa Mungu.

Biblia inacho kile kiwezacho kumfanya Mkristo kuwa na nguvu ya kiroho na kiakili.

Mtunga Zaburi asema hivi, “Kuyafafanusha maneno yako kwatia nuru, na

kumfahamisha mjinga.” Zaburi 119:130. Biblia ni kitabu cha ajabu. Ni historia

inayotufunulia sisi mambo ya karne zile zilizopita. Pasipo kuwa na Biblia, sisi

tungekuwa tumeachwa kufuata dhana mbalimbali na hadithi za uongo kwa habari ya

matukio ya vizazi vile vilivyopita.

Ni unabii unaolifunua pazia la siku zijazo. Ni Neno la

Mungu, liufunualo mpango ule wa wokovu, ambalo linatuonyesha njia ile ambayo kwayo

sisi tunaweza kuikwepa mauti ile ya milele, na kujipatia wema wa milele na uzima wa

milele. Katika vitabu vyote vinavyoigharikisha [vinavyoijaza] dunia hii, haidhuru viwe

vya thamani ilioje, Biblia ni Kitabu kipitacho vitabu vyote, inastahili kabisa kuwa somo

letu na kupewa heshima. Haitupatii sisi historia ya ulimwengu huu tu, bali maelezo ya

ulimwengu ule ujao. Ina mafundisho yahusuyo maajabu ya malimwengu mbalimbali;

inatufunulia katika ufahamu wetu tabia ya Mwasisi yule wa mbingu na nchi. Ndani yake

umo ufunuo wa Mungu kwa mwanadamu.

Kuvichunguza vitabu vya falsafa na sayansi hakuwezi kuiletea akili na maadili kile

ambacho kujifunza Biblia kunaweza kutuletea, mradi tu kiwekwe katika matendo yetu.

Yule anayejifunza Biblia anaongea na wazee wa zamani pamoja na manabii. Anagusana

na ile kweli iliyovikwa mavazi ya lugha ya heshima, ambayo ina mvuto wenye nguvu

unaoupendeza moyo, na kuyainua mawazo toka katika mambo ya dunia hii kwenda

kwenye utukufu ule wa maisha ya baadaye ya milele.

Ni hekima gani ya mwanadamu

inayoweza kulinganishwa na ufunuo wa utukufu wa Mungu. Mwanadamu mwenye

maisha mafupi, asiyemjua Mungu, anajitahidi kuipunguza thamani ya Maandiko, akidaikwamba, maarifa yake ya sayansi anayodhania kuwa anayo, hayawezi kupatana na

Neno la Mungu; lakini Neno la Mungu ni taa ya miguu yetu na mwanga wa njia yetu.

Wale wanaojigamba kwamba wanayo hekima nyingi kuliko ile ifundishwayo katika

Neno la Mungu wanahitaji kunywa kwa kina zaidi katika chemchemi hiyo ya maarifa, ili

wapate kuuona ujinga wao ulivyo hasa.

Wanadamu hujisifu wenyewe kwa hekima

waliyo nayo, wakati hekima hiyo ni upumbavu mtupu. Hebu na asiwepo mtu awaye yote

anayejidanganya mwenyewe. “Mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu

katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. Maana hekima ya

dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye

wenye hekima katika hila yao.” 1 Wakorintho 3:18-19. Ujinga mkubwa mno

unaowaletea laana wanadamu hivi sasa ni ujinga wa kukosa kuyajua masharti ya

Sheria ya Mungu [Amri Kumi – Kut. 20:3-17] ambayo yanawafunga wanadamu wote;

na ujinga huo ni matokeo ya kudharau kulichunguza Neno la Mungu. Ni mpango wake

Shetani kuyashughulisha mno mawazo kiasi cha kuwafanya wanadamu kukiacha Kitabu

hicho Kikuu cha Mwongozo, na hivyo kuwafanya waongozwe katika njia ile ya uasi

[uvunjaji wa Amri Kumi – Yak. 2:10-12] na maangamizi.

Biblia haipewi heshima na kuwekwa mahali pake inapostahili miongoni mwa vitabu

vya ulimwengu huu, japokuwa kuisoma kuna umuhimu usio na kifani kwa roho za

wanadamu. Katika kuzichunguza kurasa zake mawazo yetu huziona mandhari [picha]

zile tukufu za milele. Twamwona Yesu, Mwana wa Mungu, akija katika dunia yetu, na

kuingia katika pambano la ajabu ambalo limezivunjilia mbali nguvu zile za giza. Lo!ni

ajabu jinsi gani, ni jambo ambalo karibu halisadikiki kabisa kwamba Mungu yule wa

milele angeweza kukubali Mwana wake apate kudhalilishwa kiasi kile, ili sisi tupate

kuinuliwa juu na kuketi pamoja naye katika kiti chake cha enzi!Hebu kila mwanafunzi

wa Maandiko na atafakari ukweli huo mkuu, ndipo hatatoka katika kujifunza Biblia

pasipo kutakaswa, kuinuliwa juu na kuadilishwa.

Ile kweli itafunuliwa akilini mwake na

kutumiwa na Roho wa Mungu katika moyo wake. Kwa njia ya kuunganishwa na Mungu,

Mkristo atakuwa na mawazo safi na mapana zaidi, yasiyopendelea kufuata maoni yake

mwenyewe aliyokuwa nayo hapo kwanza. Uwezo wake wa kupambanua mema na

mabaya utapenya ndani zaidi, uwezo wake wa akili utakuwa na uwiano mzuri zaidi.

Akili yake, ikitumika katika kuzitafakari zile kweli tukufu, itapanuka, na katika kujipatia

maarifa yale ya mbinguni ataweza kuujua vizuri zaidi udhaifu wake alio nao, naye atakua

katika imani na katika unyenyekevu wake wa moyo. Usikivu mdogo tu ukitolewa kwa

Neno la Mungu, mashauri ya Mungu huwa hayazingatiwi, maonyo yanayotolewa huwa

kazi bure, neema na hekima ya mbinguni haitafutwi ili dhambi zile zilizopita zipate

kuepukwa na kila waa la ufisadi lipate kusafishwa katika tabia yetu.

Daudi aliomba,

akasema, “Unifahamishe njia ya mausia yako [yaani, amri zako – KJV].” “Unifumbue

macho yangu niyatazame maajabu yatokayo katika Sheria yao [Amri Kumi].” Zaburi

119:27,18.

Ipo kazi kubwa ya kufanywa na mwanafunzi wa Biblia mwenye bidii; kwa sababu

vito vya thamani vya ile kweli vinatakiwa kukusanywa na kuletwa juu, kisha vinapaswa

kutengwa mbali na urafiki wo wote na makosa [mafundisho potofu]. Ingawa Biblia ni

ufunuo utokao mbinguni, hata hivyo, wengi hawayaelewi mafundisho yake ya mbinguni.

Tunapaswa kugundua maono mapya ya ile kweli katika Agano la Kale na Agano Jipya,

hatuna budi kukiona kina na upana upitao kiasi wa zile kweli tunazofikiri kwamba

tunazijua, lakini ambazo sisi tuna ujuzi wake wa juu juu tu. Yule anayeyachunguzaMaandiko kwa bidii ataona kwamba mwafaka upo kati ya sehemu mbalimbali za Biblia;

atagundua uhusiano wa kifungu kimoja cha maneno na kile kingine, na thawabu ya taabu

yake [ya kujitahidi kukichunguza] itakuwa ya thamani kubwa mno.

Katika eneo lote la ufunuo huo zimetawanyika chemchemi za furaha, amani na

shangwe za ile kweli ya mbinguni. Chemchemi hizo za furaha zinaweza kufikiwa na kila

mmoja atafutaye. Maneno yale ya Uvuvio, yakifikiriwa sana moyoni, yatakuwa kama

vijito vinavyotiririka kutoka katika mto ule wa maji ya uzima. Mwokozi wetu aliomba

kwamba akili za wafuasi wake zipate kuzinduliwa ili kuyaelewa Maandiko hayo. Kila

tunapojifunza Biblia kwa moyo wa maombi, Roho Mtakatifu huwa karibu nasi

kutufunulia maana ya maneno yale tusomayo. Mtu yule ambaye akili yake imetiwa nuru

kwa kulifafanua Neno la Mungu, hatajisikia tu kuwa anapaswa kutafuta kwa bidii ili

apate kulielewa Neno lile, bali kwamba anapaswa kuwa na ujuzi bora wa sayansi zile

nyingine. Atajisikia kwamba ameitwa kwa mwito ule mkuu katika Kristo Yesu. Kadiri

mwanadamu anavyounganishwa kwa karibu sana na lile Chimbulo la maarifa yote na

hekima, ndivyo kadiri atakavyojisikia kwamba hana budi kusonga mbele katika kujipatia

mambo yale ya kiakili na kiroho. Roho Mtakatifu, kwa njia ya ile kweli ya Mungu,

huuhuisha uwezo ule wa kiroho uliokufa na kuuvuta moyo kuelekea mbinguni.

Basi, chukua Biblia yako na kujiweka mbele za Baba yako wa Mbinguni, ukisema,

“Unitie nuru; unifundishe kweli ni nini.” Bwana ataifikiria sala yako, na Roho Mtakatifu

ataitia kweli hiyo moyoni mwako. Katika kuyachunguza Maandiko wewe mwenyewe,

utakuwa umejiimarisha katika imani. Ni jambo la maana sana kwamba uweke moyoni

mwako akiba ya kweli hizo za Mungu. Unaweza kujikuta uko mahali ambako hutapata

nafasi ya kukutana na watoto wa Mungu. Unahitaji kuzificha hazina za Neno la Mungu

moyoni mwako, ili upinzani utakapokuja dhidi yako, upate kulipima kila jambo kwa

Maandiko hayo.

Kweli ni ya milele, na kupambana kwake na uongo [mafundisho potofu]

kutaudhihirisha tu uwezo wake. Kamwe tusikatae kuyachunguza Maandiko pamoja na

wale ambao tunayo sababu ya kuamini kwamba wanataka kujua kweli hiyo ni nini.

Tuseme ndugu mmoja anashikilia maoni yaliyo tofauti na yako, naye anakuja kwako, na

kupendekeza kwamba wewe uketi chini pamoja naye na kulichunguza jambo lile katika

nuru ya Maandiko; je!ungesimama ukiwa umejazwa na chuki bila sababu na

kuyashutumu mawazo yake, na wakati uo huo ukiwa unakataa kumpa usikivu wako

usiopendelea upande wo wote? Njia pekee sahihi kwetu sisi kama Wakristo ingekuwa ni

ile ya kuchunguza msimamo uliotolewa katika nuru ya Neno la Mungu, ambalo litaifunua

kweli na kuufichua uongo.

Kuyadhihaki mawazo yake kusingeweza kuudhofisha

msimamo wake, ingawa [yale usemayo] yangekuwa ni ya kweli. Hebu kilete kila kitu

kwenye Biblia; kwa maana hiyo peke yake ndiyo kanuni ya imani na mafundisho ya

dini. Hatuna budi kujifunza ile kweli sisi wenyewe; tusimtegemee mtu awaye yote

kufikiri kwa niaba yetu, haidhuru awe ni nani au awe na cheo gani. Hatupaswi

kumwangalia mwanadamu ye yote kama kiongozi mkamilifu [asiye na dosari]

aliyewekwa kwa ajili yetu. Tunapaswa kushauriana pamoja na kunyenyekeana; lakini

wakati uo huo hatuna budi kumwangalia Mungu kwa ajili ya kututia sisi nuru ile ya

mbinguni, ili kila mmoja wetu apate kukuza tabia ile itakayoweza kushinda katika jaribio

la siku ile kuu.

Sisi tunaishi katika siku za mwisho, wakati makosa [mafundisho ya uongo] yaliyojaa

udanganyifu wa hali ya juu yanapokelewa na watu na kusadikiwa, wakati ile kweli [Nenola Mungu – Yn. 17:17] inapotupiliwa mbali. Wengi wanachukuliwa na mkondo wa maji

na kuingia katika giza [la ujinga] na ukafiri, wanaikosoa Biblia, wanaleta mavumbuzi ya

kishirikina [uchawi], wanaleta nadharia zisizoungwa mkono na Maandiko, pamoja na

dhana zinazotokana na falsafa ya kipumbavu; lakini ni jukumu la kila mmoja wetu

kujitahidi kupata ujuzi kamili wa Maandiko. Umuhimu na faida ya kujifunza Biblia

haviwezi kusifiwa mno. Katika kuyachunguza Maandiko mawazo yetu huongozwa

katika kuifikiria sana ile kafara ya Kristo isiyo na kikomo katika kutupatanisha sisi.

Tunapouona upendo wake, tunapotafakari juu ya kujidhili kwake na mateso yake, roho

ile ile ya kujikana nafsi na kujitoa mhanga kwa faida ya wengine inaamshwa ndani ya

mioyo yetu. Tunapomtazama Yesu kwa jicho la imani, tuta“badilishwa tufanane na

mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, kama vile utukufu utokao kwa Bwana, aliye

Roho.” 2 Wakorintho 3:18.

Bibi E. G. White, The Power of the Word, au Kichwa cha makala ya awali ni

“Apples of Gold Library No. 10.”

***********************************************

Kwa sababu ya upekee na unyeti wa siku, Sio vibaya tukibadilishana mawazo na kuambizana yaliyomuhimu katika maisha hasa ya kiroho.
Na huu utakuwa ni mfululizo kwa kila siku kama hii ya leo...

(Ninamaanisha JumaMosi)

Pamoja na kwamba weeengi wanaamini hii ni kweli, lakini kweli halisi jionee mwenyewe ambapo Walter Pearson anajambo la kutwambia.




AMANI KWAKO.

Maoni 2 :

  1. Amani kwako pia NGULI na asante kwa SHULE hii!


    Ila nasikia UWEZO wa NENo ni siri ya mafanikio ya hata WANAMAZINGAOMBWE ,...
    ... na pia hata UCHAWI kwa WACHAWI ni jambo la KIROHO!

    Ni angalizo tu hili MKUU!

    JibuFuta