Mtayarishaji

Morning Star Radio

Jumatano, Februari 06, 2013

WAJIBIKA KUTAFUTA FURAHA KATIKA UHUSIANO ULIONAO


Kila Mmoja Bila Kutegeana.


Inawezekana kuwa na furaha na amani katika ndoa au uhusiano ulionao kama wote wawili mtawajibika bila kutegeana,kwani ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha uhusiano alionao unakuwa na furaha wakati wote,haiwezekani katika muungano wa watu wawili kama mke na mume mmoja akaonekana kufaidi zaidi ya mwingine tupeane haki sawa kila mmoja amfurahishe mwenzie.




Inapendeza kuwa na amani na furaha kwa wote wawili kwani kila mmoja anajua jukumu lake kwa mwenzi wake ikiwa ni baba au mama alimradi kuwepo na maelewano baina yao,na kama utafahamu nini mwenzio anakipenda naye pia akawa anatambua kipi unapenda ni rahisi kudumu katika ndoa hata mahusiano kutokana na maelewano mazuri






Kama itatokea mahusiano yana mapungufu ya mmoja kukosa kujituma ili  kutimiza mahitaji ya ndoa kwasababu zilizo ndani ya uwezo,,basi uwezekano wa kuwepo na migogoro ni mkubwa,na katika hali kama hii haitashangaza suala la uaminifu kukosekana kutokana na kwamba mmoja anaona hapati mahitaji ya msingi kutoka kwa mwenzake mume au mke.maisha ya ndoa yanaitaji mawasiliano ya mara kwa mara,kwani kwa kufanya hivyo inaleta ushirikiano ,na uwazi ukiwa ni silaha ya kujenga zaidi..usinyamaze kimya kwa matatizo yanayojitokeza kwani kwa kufanya hivyo ni kuhatarisha mahusiano yenu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni